Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kwa Nini Tujiache Kuongozwa na Roho ya Mungu?

Kwa Nini Tujiache Kuongozwa na Roho ya Mungu?

Kwa Nini Tujiache Kuongozwa na Roho ya Mungu?

‘Wewe ni Mungu wangu. Roho yako ni nzuri; na iniongoze katika inchi ya unyoofu.’—ZAB. 143:10.

1. Toa mufano unaoonyesha kwamba nguvu isiyoonekana inaweza kumwongoza mutu.

 JE, UMEKWISHA kutumia dira (boussole) ili kujua mahali unapokwenda? Dira ni kifaa kilicho kama saa ambacho kina mukuki moja; mukuki huo wenye nguvu ya sumako unaonyesha tu upande wa kaskazini. Dunia ina nguvu yenye sumako inayovuta kila kitu, nguvu hiyo ndio inayotembeza mukuki wa dira. Kwa muda wa miaka mingi, watu wametumia dira ili iwaonyeshe njia ya kufuata wanaposafiri katika bahari ao inchi kavu.

2, 3. (a) Ni nguvu gani ya ajabu ambayo Yehova alitumia wakati wa uumbaji? (b) Kwa nini tunapaswa kutazamia nguvu ya utendaji ya Mungu isiyoonekana iongoze maisha yetu leo?

2 Ni nguvu gani nyingine isiyoonekana ambayo ni ya maana sana ili kutuongoza? Ni nguvu inayozungumuziwa katika mistari miwili ya sura ya kwanza ya Biblia. Kitabu cha Mwanzo kinatuelezea mambo ambayo Yehova alifanya zamani sana, kinaeleza hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” Tunajua kwamba alitumia nguvu ya ajabu ili kufanya hivyo, kwa kuwa Biblia inaendelea kusema: “Nguvu za utendaji za Mungu zilikuwa zikienda huku na huku.” (Mwa. 1:1, 2) Ni nguvu gani ambayo Mungu alitumia ili kuumba? Ni roho takatifu, yaani nguvu yake ya utendaji. Ikiwa tunaishi ni kwa sababu Yehova alitumia roho hiyo ili kuumba kila kitu.—Ayu. 33:4; Zab. 104:30.

3 Kwa kuwa tunaishi na kupumua, je, tunapaswa kutazamia tena nguvu hiyo ya utendaji ya Mungu iongoze maishani yetu? Yesu, mwana wa Mungu, alijua kwamba mambo yanapaswa kuwa hivyo, kwa kuwa aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Roho . . . atawaongoza ninyi ndani ya kweli yote.” (Yoh. 16:13) Roho hiyo ni nini, na kwa nini tunapaswa kujiacha tuongozwe nayo?

Roho Takatifu Ni Nini?

4, 5. (a) Watu wanaomini Utatu wanafikiri roho takatifu ni nini? (b) Lakini, roho takatifu ni nini? Eleza.

4 Unapohubiri, labda unakutana na watu wanaoita nguvu hiyo ya utendaji ya Mungu kuwa Roho Mutakatifu. Biblia zingine zinafanya hivyo pia, kama vile La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo. Wale wanaoamini Utatu wanafikiri kwamba roho takatifu ni mutu aliye sawa na Mungu Baba. (1 Kor. 8:6) Lakini mutu anaweza kuona kwa vyepesi kwamba fundisho la Utatu halipatane na Maandiko.

5 Basi, roho takatifu ni nini? Maelezo ya chini kwenye andiko la Mwanzo 1:2 katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kifaransa (Rbi8-F) yanasema: “Neno la Kiebrania rouah linatafsiriwa na neno ‘roho,’ lakini pia na neno ‘upepo’ ao na maneno mengine yanayomaanisha nguvu ya utendaji isiyoonekana.” (Linganisha na maelezo ya chini katika andiko la Mwanzo 3:8; 8:1.) Upepo hauonekani, lakini tunaweza kuona nguvu yake ikitenda, vivyo hivyo, roho takatifu haionekani lakini inatenda. Roho hiyo si mutu lakini ni nguvu ambayo Mungu anatumia juu ya wanadamu ao vitu ili kutimiza mapenzi yake. Je, ni vigumu kuamini kwamba nguvu ya ajabu kama hiyo inatokana na chanzo kitakatifu, yaani Mungu Mweza Yote? Hapana!—Soma Isaya 40:12, 13.

6. Daudi alimwomba Yehova nini?

6 Je, Yehova anaweza kuendelea kutumia roho yake ili kutuongoza maishani? Alimwahidi Daudi hivi: “Nitakufanya uwe na ufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea.” (Zab. 32:8) Je, Daudi alitaka kweli Mungu amuongoze? Ndiyo, kwa kuwa alimwomba Yehova hivi: “Unifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ni Mungu wangu. Roho yako ni nzuri; na iniongoze.” (Zab. 143:10) Tunapaswa kuwa na nia hiyo na kuwa tayari kuongozwa na roho ya Mungu. Kwa nini? Acheni tuzungumuzie sababu ine.

Hatuna Uwezo wa Kujiongoza

7, 8. (a) Kwa nini hatuwezi kujiongoza sisi wenyewe bila Mungu? (b) Toa mufano ili kuonyesha kwa nini hatupaswi kujaribu kujiongoza katika ulimwengu huu mwovu.

7 Sababu ya kwanza: Tunapaswa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu kwa kuwa hatuwezi kujiongoza sisi wenyewe. “Kuongoza” kunamaanisha ‘kuonyesha mutu njia ya kufuata.’ Yehova hakumuumba mwanadamu na uwezo wa kujiongoza yeye mwenyewe; na kwa kuwa hatukamilike, inakuwa vigumu hata zaidi. Nabii Yeremia aliandika: ‘Ninajua vema, Ee Yehova, kwamba njia ya mutu wa udongo haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.’ (Yer. 10:23) Kwa nini? Kupitia Yeremia Mungu alifunua sababu hiyo, yaani kile kinachotuzuia tusiweze kujiongoza wenyewe. Yehova alisema: “Moyo ni wenye hila kuliko kitu kingine chochote nao ni hatari. Ni nani anayeweza kuujua?”—Yer. 17:9; Mt. 15:19.

8 Fikiria mutu asiyeijua vizuri njia fulani, lakini anasafiri akiwa peke yake, bila mwongozi mwenye kuijua vizuri njia hiyo, ao bila dira. Ikiwa anapitia katika jangwa kubwa, je, huo haungekuwa upumbavu? Kwa kuwa hajue namna ya kupita katika jangwa na kwa kuwa yeye mwenyewe hawezi kuiona njia inayofaa inayoweza kumupeleka mahali anapokwenda na kufika salama, akijaribu kufanya hivyo atakuwa ameiweka maisha yake katika hatari. Vivyo hivyo, mutu akifikiri kwamba anaweza kujiongoza katika ulimwengu huu mwovu bila kukubali Mungu amwonyeshe njia anayopaswa kufuata, mutu huyo anatia maisha yake katika hatari. Ikiwa tunataka kuvuka ulimwengu huu kwa usalama ni lazima tumwombe Yehova kama Daudi alivyofanya aliposema: “Hatua zangu na zishike njia zako, ambamo hatua za miguu yangu hakika hazitatikiswa.” (Zab. 17:5; 23:3) Namna gani tunaweza kupata uongozi kama huo?

9. Kulingana na picha kwenye ukurasa wa 17, namna gani roho takatifu inaweza kuongoza hatua zetu vizuri?

9 Ikiwa sisi ni wanyenyekevu na ikiwa tunamutegemea Yehova, atatupatia roho yake nayo itaongoza hatua zetu vizuri. Namna gani nguvu hiyo ya utendaji itatusaidia? Yesu aliwaelezea wanafunzi wake: ‘Musaidizi, roho takatifu, ambayo Baba atatuma katika jina langu, hiyo itawafundisha ninyi mambo yote na kuwakumbusha mambo yote niliyowaambia.’ (Yoh. 14:26) Ikiwa tunasali na kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida, kutia ndani mafundisho yote ya Kristo, roho takatifu itaongeza uelewaji wetu kuhusu hekima ya Yehova ili tufuate mapenzi yake kwa ukaribu. (1 Kor. 2:10) Pia, ikiwa katika njia inayoongoza kwenye uzima kuna mambo yanayotufikia bila kutazamia, roho takatifu itatusaidia ili tujue jambo tunalopaswa kufanya. Itatukumbusha kanuni za Biblia ambazo tumekwisha kujifunza na kutusaidia tuelewe jinsi ya kuzitumia ili kuongoza hatua zetu.

Yesu Aliongozwa na Roho ya Mungu

10, 11. Mwana muzaliwa pekee wa Mungu alitazamia nini kuhusiana na roho takatifu, nayo ilimusaidia namna gani?

10 Sababu ya pili: Tunapaswa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu kwa kuwa Mungu aliitumia ili kumwongoza Mwana wake. Mbele ya kuja duniani, Mwana wa pekee wa Mungu alijua unabii uliosema hivi: “Na roho ya Yehova itatua juu yake, roho ya hekima na ya uelewaji, roho ya shauri na ya nguvu, roho ya ujuzi na ya kumwogopa Yehova.” (Isa. 11:2) Wazia jinsi Yesu alivyotazamia sana musaada wa roho ya Mungu ili aweze kupambana na hali mbaya alipokuwa duniani!

11 Maneno ya Yehova yalitimia. Masimulizi ya Injili yanaonyesha mambo yaliyotokea mara moja kisha kubatizwa kwa Yesu: “Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akarudi kutoka Yordani, naye akaongozwa na roho huku na huku nyikani.” (Luka 4:1) Huko, Yesu alipokuwa akifunga, akisali na kutafakari, inaelekea kwamba Yehova alimutolea maagizo na kumujulisha mambo ambayo yangemupata. Nguvu ya Mungu ya utendaji ilichochea akili, na moyo wa Yesu, iliongoza mawazo na maamuzi yake. Ndiyo sababu, Yesu alijua jambo la kufanya katika kila hali, na alitenda kabisa kulingana na mapenzi ya Baba yake.

12. Kwa nini ni jambo la maana tumuombe Mungu roho yake ili ituongoze?

12 Kwa kuwa alijua faida ya roho ya Mungu katika maisha yake, Yesu aliwatia wanafunzi wake moyo kwamba ni jambo la maana waombe roho hiyo na wajiache kuongozwa nayo katika maisha yao. (Soma Luka 11:9-13.) Kwa nini hilo ni jambo la maana sisi pia tuombe roho takatifu? Kwa kuwa inaweza kubadili akili yetu, na kutusaidia tuwe na akili ya Kristo. (Rom. 12:2; 1 Kor. 2:16) Kwa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu, tunaweza kufikiri kama Kristo na kufuata mufano wake.—1 Pet. 2:21.

Roho ya Ulimwengu Inaweza Kutupoteza

13. Roho ya ulimwengu ni nini, na inachochea watu wafanye nini?

13 Sababu ya tatu: Tunapaswa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu kwa kuwa bila roho hiyo roho mbaya ya ulimwengu inayoongoza maisha ya watu wengi leo inaweza kutupoteza. Ulimwengu una roho yenye nguvu, inayochochea watu wafanye mambo yanayopingana na yale ambayo roho takatifu inatuchochea tufanye. Kuliko kuwasaidia watu wawe na akili ya Kristo, roho ya ulimwengu inafanya mawazo na matendo ya watu yawe kama ya Shetani, mutawala wa ulimwengu huu. (Soma Waefeso 2:1-3; Tito 3:3.) Mutu anapoacha roho ya ulimwengu imuongoze na kuanza kufanya matendo ya mwili, atapatwa na matokeo mabaya, na hawezi kuriti Ufalme wa Mungu.—Gal. 5:19-21.

14, 15. Namna gani tunaweza kushinda roho ya ulimwengu?

14 Yehova ametutolea musaada ili tushinde roho ya ulimwengu. Mutume Paulo alisema hivi, ‘endeleeni kujipatia nguvu katika Bwana na katika uwezo ili muweze kupinga katika ile siku ya uovu.’ (Efe. 6:10, 13) Kupitia roho yake, Yehova anatupatia nguvu ya kushindana na Shetani anapojikaza kutudanganya. (Ufu. 12:9) Ni kweli kwamba roho ya ulimwengu ni yenye nguvu, na hatuwezi kabisa kuiepuka. Hata hivyo, hatupaswi kujiacha itupotoshe. Roho takatifu ni yenye nguvu zaidi, na itatusaidia kushinda roho ya ulimwengu!

15 Katika wakati wa mitume kuna wale walioacha Ukristo; mutume Petro aliandika juu yao hivi: “Wameiacha njia iliyo nyoofu, wamepotoshwa.” (2 Pet. 2:15) Sisi ni wenye shukrani kwa kuwa tumepokea, “si roho ya ulimwengu, bali roho inayotoka kwa Mungu”! (1 Kor. 2:12) Kwa musaada wa roho hiyo na kwa kufaidika na mipango yote ambayo Yehova anatutolea ili tuendelee kufuata njia nzuri, tunaweza kushinda roho ya ulimwengu huu mwovu.—Gal. 5:16.

Roho Takatifu Inatusaida Tuwe na Sifa Nzuri

16. Roho takatifu inaweza kutusaidia tuwe na sifa gani?

16 Sababu ya ine: Tunapaswa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu kwa kuwa inatusaidia tuwe na sifa nzuri katika maisha yetu. (Soma Wagalatia 5:22, 23.) Bila shaka, sisi wote tungependa kuwa wenye upendo zaidi, wenye furaha, na wenye amani na wengine, sivyo? Sisi wote tungependa kuwa wenye ustahimilivu zaidi, wenye fazili na wema zaidi, sivyo? Pia, lingekuwa jambo nzuri ikiwa sisi wote tuna imani kubwa, upole na kujizuia, sivyo? Roho takatifu inatusaidia tuwe na sifa hizo nzuri ambazo zitatuletea faida sisi wenyewe, watu tunaoishi nao, na mashahidi wenzetu. Tunapaswa kuendelea kufanya nguvu ili kukomalisha sifa hizo maishani mwetu. Tunda la roho linatia ndani mambo mengi na tunaweza pia kufanya mambo mengi ili kuonyesha kwamba tuna tunda hilo.

17. Namna gani tunaweza kujikaza sana kuonyesha tunda la roho?

17 Ni jambo la hekima kujichunguza sisi wenyewe ili kuhakikisha kwamba maneno na matendo yetu yanaonyesha kwamba sisi tunaongozwa na roho takatifu na kwamba tunaonyesha tunda la roho hiyo katika maisha yetu. (2 Kor. 13:5a; Gal. 5:25) Tutafanya nini ikiwa tunatambua kwamba tuna lazima ya kufanyia maendeleo sifa fulani? Tunaweza kujikaza sana na kujiacha tuongozwe na roho takatifu ili tuwe na sifa hiyo. Tutafikia jambo hilo kwa kujifunza kila sehemu ya tunda hilo jinsi linavyoelezwa katika Biblia na katika vichapo vyetu. Kwa hiyo tunaweza kufikiria jinsi tunavyoweza kuonyesha tunda la roho katika maisha yetu ya kila siku na kisha kufanya nguvu ili kulionyesha zaidi. * Tunapoona jinsi roho ya Mungu inavyotenda juu yetu na juu ya Wakristo wenzetu, bila shaka tunaelewa kwa nini ni lazima tujiache kuongozwa na roho ya Mungu.

Je, Unajiacha Uongozwe na Roho ya Mungu?

18. Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Yesu alivyojiacha aongozwe na roho ya Mungu?

18 Mungu alipoumba ulimwengu wote muzima, Yesu alikuwa ‘stadi wake wa kazi.’ Kwa hiyo, yeye alijua habari zote kuhusu nguvu ya sumako ya dunia inayovuta vitu, na inayotembeza mukuki wa dira, chombo ambacho wanadamu wanatumia wanaposafiri. (Met. 8:30; Yoh. 1:3) Lakini, hakuna andiko katika Biblia linaloonyesha kwamba Yesu alitumia nguvu hiyo ili imuongoze kufuata njia fulani alipokuwa duniani. Biblia inasema kwamba alipokuwa mwanadamu, aliongozwa na roho takatifu, yaani nguvu ya utendaji ya Mungu. Alijiacha imuongoze, na ilipomuchochea kufanya jambo fulani, alikubali na kutenda. (Marko 1:12, 13; Luka 4:14) Je, wewe pia unajiacha uongozwe na roho hiyo?

19. Tunapaswa kufanya nini ili roho takatifu ituongoze katika maisha yetu?

19 Leo, nguvu ya utendaji ya Mungu inaendelea kuchochea akili na mioyo ya watu wanaojiacha kuongozwa nayo. Namna gani unaweza kuiruhusu roho takatifu ikuongoze katika njia inayofaa? Sali kwa Yehova kila siku ili akupatie roho yake na akusaidie ili ujiache kuongozwa na roho hiyo. (Soma Waefeso 3:14-16.) Tenda kulingana na sala zako kwa kutafuta mashauri yaliyo katika Biblia, Neno la Mungu, iliyoongozwa na roho takatifu. (2 Tim. 3:16, 17) Fuata maagizo yenye hekima ambayo Biblia inakutolea na uwe tayari kukubali mwongozo wa roho takatifu. Kwa kufanya hivyo, utaonyesha kwamba unaamini Yehova ana uwezo wa kukuongoza kwa njia inayofaa zaidi katika ulimwengu huu mwovu.

[Maelezo ya chini]

^ Ili kupata habari zaidi kuhusu kila sehemu ya tunda la roho, ona habari “Fruit de L’esprit de Dieu” na kichwa “Liste par facette” katika Index des publications Watch Tower.

Je, Unakumbuka Mawazo Makuu?

• Namna gani roho takatifu inaweza kutusaidia katika maisha?

• Toa sababu ine zinazoonyesha kwa nini tunapaswa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu.

• Tunaweza kufanya nini ili tufaidike kabisa na uongozi wa roho takatifu?

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 15]

Roho ya Mungu ilikuwa ndio nguvu iliyoongoza maisha ya Yesu

[Picha katika ukurasa wa 17]

Roho ya Mungu inachochea akili na mioyo ya wale wanaojiacha kuongozwa nayo