Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kufanya Wakati wa Funzo Uwe Wenye Kufurahisha Zaidi na Wenye Faida Zaidi

Kufanya Wakati wa Funzo Uwe Wenye Kufurahisha Zaidi na Wenye Faida Zaidi

Kufanya Wakati wa Funzo Uwe Wenye Kufurahisha Zaidi na Wenye Faida Zaidi

Namna gani tunaweza kufurahia zaidi funzo la Biblia? Namna gani tunaweza kufanya wakati wa funzo uwe wenye kufaidi zaidi? Acheni tuchunguze kwa kifupi hatua tatu za maana zitakozotusaidia tufaidike kabisa na funzo la pekee la Biblia.

1 KUSALI: Hatua ya kwanza ni kusali. (Zab. 42:8) Kwa nini? Tunapaswa kuona funzo la Neno la Mungu kuwa sehemu ya ibada yetu kwake. Kwa hiyo, ni lazima tumwombe Yehova atusaidie ili akili na mioyo yetu vifurahie kabisa funzo na tumwombe atupatie roho yake takatifu. (Luka 11:13) Barbara, misionari wa muda murefu anasema hivi: “Sikuzote ninasali mbele ya kusoma ao kujifunza Biblia. Kisha hapo, najisikia kwamba Yehova yuko pamoja nami na kwamba anapendezwa na funzo langu.” Kusali mbele ya kuanza funzo kunafanya akili na mioyo yetu vifurahie kabisa chakula kingi cha kiroho kilicho mbele yetu.

2 KUTAFAKARI: Kwa kuwa hawana wakati, wengine wanasoma neno la Mungu kijuujuu tu. Hivyo hawafaidike kabisa na funzo la Biblia. Ndugu Carlos, ambaye amemutumikia Yehova kwa muda wa zaidi ya miaka 50, amefikia kutambua kwamba kuwa na wakati wa kutafakari ni jambo la maana sana ili kufanya funzo lake liwe lenye kufaidi zaidi. Anasema hivi: “Sasa ninasoma kurasa fulani za Biblia kwa wakati mudogo​—karibu kurasa mbili kila siku. Kwa hiyo, ninaweza kuchukua wakati zaidi ili kutafakari kuhusu mambo niliyosoma ili kujua jinsi ya kuyatumia.” (Zab. 77:12) Tunapochukua wakati wa kutafakari, tunaongeza ujuzi na uelewevu wetu kuhusu mapenzi ya Mungu.​—Kol. 1:9-11.

3 KUTUMIKISHA YALE UNAYOJIFUNZA: Tunafaidika zaidi na jambo fulani ikiwa tunaona faida ya jambo hilo. Ndivyo ilivyo pia kuhusiana na funzo la Biblia. Gabriel, ndugu kijana aliye na programu ya kujifunza Biblia kwa ukawaida anasema hivi: “Funzo linanisaidia nipambane na matatizo ya kila siku, na linanitayarisha kuwasaidia wengine.” Anaongeza hivi: “Ninajikaza kutumikisha katika maisha yangu kila jambo ninalojifunza.” (Kum. 11:18; Yosh. 1:8) Ndiyo, Mungu ana ujuzi mwingi ambao tunaweza kuendelea kujichukulia na kutumikisha katika maisha.​—Met. 2:1-5.

KURUDILIA: Ni pendeleo kama nini kutafuta​-tafuta katika ujuzi ambao Yehova, Mutoaji wa hekima, anatutolea! (Rom. 11:33) Kwa hiyo, kwenye funzo lako la pekee linalofuata, hakikisha kwamba umeanza kwa kutoa sala kwa Yehova na umwombe akusaidie ili akili na moyo wako vifurahie kabisa funzo na umuombe akupatie roho takatifu. Kisha, wakati fulani-fulani tua ili kutafakari kuhusu mambo unayosoma. Pia, endelea kufikiria mambo hayo na uyatumikishe katika maisha yako ya kila siku. Ikiwa unafuata hatua hizo za lazima, utaona kwamba funzo lako la Biblia linakuwa lenye kufurahisha zaidi na lenye kufaidi zaidi.