Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mufano wa Mitume wa Yesu wa Kuendelea Kukesha Unatufundisha Nini?

Mufano wa Mitume wa Yesu wa Kuendelea Kukesha Unatufundisha Nini?

Mufano wa Mitume wa Yesu wa Kuendelea Kukesha Unatufundisha Nini?

“Mwendelee kukesha pamoja nami.”​—MT. 26:38.

UNAWEZA KUJIFUNZA NINI KUHUSU:

Kukesha kwa kukubali mwongozo kuhusu mahali pa kuhubiri?

Kuendelea kukesha kuhusiana na sala?

Kutoa ushahidi kamili ijapokuwa magumu?

1-3. Ni nini kinachoonyesha kwamba mitume hawakuendelea kukesha usiku wa mwisho wa maisha ya Yesu hapa duniani, na ni nini kinachoonyesha kwamba walijifunza kutokana na kosa lao?

 WAZIA mambo yaliyotokea usiku wa mwisho wa maisha ya Yesu hapa duniani. Yesu amefika mahali alipopenda sana; bustani ya Gethsemane, upande wa mashariki wa Yerusalemu. Amefika hapo na mitume wake waaminifu. Yesu anasumbuliwa akilini na moyoni, kwa hiyo anatafuta mahali ambapo atakuwa peke yake ili kusali.​—Mt. 26:36; Yoh. 18:1, 2.

2 Mitume wake watatu, Petro, Yakobo, na Yohana, wanamusindikiza Yesu ndani zaidi katika bustani. Yesu anawaambia: “Kaeni hapa na mwendelee kukesha pamoja nami,” na kisha anawaacha, anaenda kusali. Anaporudi anawakuta wanafunzi wake wamelala. Anawasihi tena: “Endeleeni kukesha.” Hata hivyo, mara mbili tena anawakuta wamelala! Baadaye, usiku huohuo, mitume wote wanashindwa kukesha. Jambo la kushangaza, wanamwacha hata Yesu na kukimbia!​—Mt. 26:38, 41, 56.

3 Bila shaka, mitume walisikitikia uzaifu huo. Wanaume hao waaminifu walijifunza mara moja kutokana na kosa lao. Kitabu cha Matendo kinatuonyesha kwamba baadaye mitume wa Yesu wakawa mufano muzuri kuhusu kuendelea kukesha. Bila shaka, mufano wao uliwachochea Wakristo wengine waendelee kukesha. Sasa, huu ndio wakati wa kuendelea kukesha. (Mt. 24:42) Acheni basi tuzungumuzie mambo matatu tunayoweza kujifunza kutoka kitabu cha Matendo ambayo yanaweza kutusaidia ili tuendelee kukesha.

WALIKESHA KWA KUKUBALI MWONGOZO KUHUSU MAHALI PA KUHUBIRI

4, 5. Namna gani mutume Paulo na wenzake walijionea mwongozo wa roho takatifu?

4 Kwanza, mitume walikesha kwa kufuata muongozo kuhusu mahali pa kuhubiri. Katika habari moja, tunajifunza jinsi Yesu alivyotumia roho takatifu, ambayo Yehova alimutolea, ili kuongoza mutume Paulo na wenzake katika safari zao zisizo rahisi. (Mdo. 2:33) Acheni tuzungumuzie safari hizo.​—Soma Matendo 16:6-10.

5 Paulo, Sila, na Timotheo waliondoka Listra, muji ulio sehemu ya kusini mwa Galatia. Baada ya siku fulani, walifika kwenye barabara kubwa ya Roma inayoongoza kwenye sehemu ya mangaribi ya Asia yenye watu wengi. Waliifuata ili watembelee miji ambamo watu wengi walihitaji kusikiliza habari kuhusu Kristo. Hata hivyo, kuna kitu fulani kilichowazuia. Mustari wa 6 unasema hivi: ‘Zaidi ya hayo, wakapitia Frigia na inchi ya Galatia, kwa sababu walikatazwa na roho takatifu wasiseme lile neno katika wilaya ya Asia.’ Kwa njia isiyozungumuziwa waziwazi katika Biblia, roho takatifu iliwazuia wasafiri hao wenye bidii, wasihubiri katika Asia. Ni wazi kwamba Yesu kupitia roho ya Mungu, alitaka kuongoza Paulo na wenzake mahali tofauti.

6, 7. (a) Walipokaribia Bithinia, Paulo na wenzake walipatwa na nini? (b) Walichukua uamuzi gani, na matokeo yalikuwa nini?

6 Walienda wapi? Mustari wa 7 unaeleza hivi: “Tena, walipofika Misia wakafanya jitihada za kuingia Bithinia, lakini roho ya Yesu haikuwaruhusu.” Walipozuiwa kuhubiri katika Asia, Paulo na wenzake walijielekeza kaskazini, wakikusudia kuhubiri katika miji ya Bithinia. Lakini, walipokaribia Bithinia, Yesu alitumia tena roho takatifu iwazuie. Ni wazi kwamba jambo hilo liliwavuruga sana. Walijua watahubiri nini na jinsi gani watafanya hivyo, lakini hawakujua ni wapi watahubiri. Kwa njia nyingine, tunaweza kusema: Walijaribu kugonga mulango wa Asia, lakini haukufunguka. Walijaribu ule wa Bithinia, haukufunguka pia. Je, walivunjika moyo? Hata kidogo!

7 Wakati huo, wanaume hao wakachukua uamuzi ambao yaelekea haukutazamiwa. Mustari wa 8 unasema hivi: “Kwa hiyo wakapita Misia na kushuka mupaka Troa.” Wakaenda sehemu ya mangaribi na kutembea kilomita 550, wakipitia muji baada ya muji mupaka walipofika kwenye bandari ya Troa, njia iliyofaa ili kuingia Makedonia. Walipofika huko, kwa mara ya tatu, Paulo na wenzake walijaribu kugonga mulango, mara hiyo mulango ulifunguliwa wazi kabisa. Mustari wa 9 unaeleza jambo lililotokea: “Na usiku maono yakamutokea Paulo: mwanamume fulani Mumakedonia alikuwa amesimama akimusihi na kusema: ‘Vuka uingie Makedonia utusaidie.’” Mwishowe, Paulo akajua ni wapi atahubiri. Bila kuchelewa, wakachukua mashua kwenda Makedonia.

8, 9. Safari ya Paulo inaweza kutufundisha nini?

8 Habari hiyo inaweza kutufundisha nini? Ona kwamba roho ya Mungu ilimwonyesha Paulo mahali pa kuhubiri kisha tu Paulo kuanza safari ya kwenda Asia. Paulo alipokaribia tu Bithinia ndipo Yesu alimutolea maagizo. Na mwishowe, kisha tu Paulo kufika Troa ndipo Yesu alimwongoza Makedonia. Kwa kuwa Yesu ndiye Kichwa cha kutaniko, anaweza kutuongoza kwa njia hiyo hiyo leo. (Kol. 1:18) Kwa mufano, labda umekwisha kufikiria kutumikia kama painia ao kuhamia katika eneo lililo na lazima sana ya wahubiri. Lakini inawezekana Yesu atakuongoza kupitia roho ya Mungu ukisha tu kuchukua hatua fulani ili kufikia muradi huo. Fikiria mufano huu: Shofere anaweza kuongoza gari lake upande wa kushoto ao wa kuume ikiwa tu gari hilo ni lenye kutembea. Vivyo hivyo, Yesu anaweza kutuongoza ili tupanue utumishi wetu ikiwa tu tunachukua hatua na kujikaza kufikia muradi wetu.

9 Itakuwa namna gani ikiwa nguvu unazofanya hazizae matunda mara moja? Je, utavunjika moyo na kufikiri kwamba roho ya Mungu haikuongozi tena? Hapana, kumbuka kwamba Paulo pia alikutana na vizuizi. Lakini, aliendelea kutafuta na kugonga mupaka akapata mulango uliofunguka. Wewe pia, ikiwa unaendelea kutafuta ‘mulango mukubwa unaoongoza kwenye utendaji,’ utabarikiwa.​—1 Kor. 16:9.

WALIENDELEA KUKESHA KUHUSIANA NA SALA

10. Ni nini inayoonyesha kwamba ili kuendelea kukesha ni lazima kukesha kuhusiana na sala?

10 Tuzungumuzie sasa jambo la tatu ambalo tunaweza kujifunza kutoka kwa Wakristo wa kwanza kuhusu kukesha: Waliendelea kukesha kuhusiana na sala. (1 Pet. 4:7) Ni jambo la maana kudumu katika sala ili kuendelea kukesha. Kumbuka kwamba katika bustani ya Gethsemane, Yesu aliwaambia mitume wake watatu hivi: “Endeleeni kukesha na kusali sikuzote.”​—Mt. 26:41.

11, 12. Kwa nini Herode aliwatesa Wakristo na Petro, na jinsi gani alifanya hivyo?

11 Petro, aliyekuwa katika bustani ya Gethsemane, baadaye alifaidika na nguvu inayotokana na sala inayofanywa kwa bidii. (Soma Matendo 12:1-6.) Mistari ya kwanza-kwanza ya andiko hilo, inaonyesha kwamba ili Herode akubaliwe na Wayahudi, alianza kuwatesa Wakristo. Labda Herode alijua kwamba Yakobo alikuwa mutume wa Yesu aliyekuwa rafiki wake wa karibu. Kwa hiyo, mustari wa 2 unasema kwamba Herode “alimuua kwa upanga Yakobo.” Hivyo, kutaniko lilipoteza mutume mupendwa. Hilo lilikuwa jaribu kubwa kwa ndugu!

12 Herode alifanya nini kisha hapo? Mustari wa 3 unasema hivi: “Alipoona kuwa jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akamukamata Petro pia.” Lakini hapo mbele, mitume fulani, kutia ndani Petro walifunguliwa kwa njia ya muujiza. (Mdo. 5:17-20) Labda Herode alijua vizuri jambo hilo. Herode alifanya yote awezayo ili Petro asitoroke. Mustari wa 4 unaeleza kwamba Herode aliamuru Petro alindwe na ‘vikundi vine vya askari-jeshi, kila kikundi kikiwa na askari wanne, kwa kuwa alikusudia kumuleta mbele ya watu baada ya pasaka.’ Wazia jambo hilo! Herode aliamuru kwamba Petro afungwe munyororo akiwa kati ya walinzi wawili; walinzi 16 walikuwa wakigomboana muchana na usiku ili Petro asitoroke. Nia ya Herode ilikuwa kumuleta Petro mbele ya watu kisha Pasaka. Alikusudia kumua ili kufurahisha watu. Katika hali ngumu kama hizo, Wakristo wengine wangefanya nini kwa ajili ya Petro?

13, 14. (a) Kutaniko lilifanya nini Petro alipotiwa gerezani? (b) Wakristo walisali kwa ajili ya Petro, mufano wao unaweza kutufundisha nini kuhusiana na sala?

13 Kutaniko lilijua vizuri jambo la kufanya. Kwenye mustari wa 5 tunasoma hivi: “Kwa hiyo Petro alikuwa gerezani; lakini kutaniko lilikuwa likisali kwa Mungu kwa juhudi nyingi kwa ajili yake.” Ndiyo, walisali sana na kusihi kwa ajili ya ndugu yao mupendwa. Kifo cha Yakobo hakikuwafanya wakose tumaini; wala kuwafanya wafikiri kwamba kusali si jambo la lazima. Lakini, walijua kwamba sala za waabudu waaminifu ni za maana sana kwa Yehova. Ikiwa sala hizo zinapatana na mapenzi yake, yeye yuko tayari kuzijibia.​—Ebr. 13:18, 19; Yak. 5:16.

14 Kwa kuwa Wakristo walisali sana kwa ajili ya Petro, jambo hilo linaweza kufundisha nini? Kuendelea kukesha hakumaanishe kuomba tu kwa ajili yetu wenyewe, lakini pia kwa ajili ya ndugu na dada wengine. (Efe. 6:18) Je, unajua ndugu na dada ambao wanapambana na majaribu? Labda wengine wanavumilia mateso, wengine wako katika inchi ambamo serikali inakataza kazi yetu, wengine wanapatwa na misiba. Kwa nini usiwatie katika sala zako? Unaweza kuwajua ndugu wengine ambao wanapambana na taabu bila watu kujua; matatizo ya familia, kuvunjika moyo, ao matatizo ya afya. Unaweza kufikiria watu fulani ambao unaweza kutia katika sala zako ukiwataja kwa majina unapozungumuza na Yehova ‘Musikiaji wa sala.’—Zab. 65:2.

15, 16. (a) Eleza jinsi malaika wa Yehova alivyomufungua Petro katika gereza. (Ona picha hapa chini.) (b) Kwa nini ni jambo lenye kufariji kufikiria jinsi Yehova alivyomwokoa Petro?

15 Sasa, mambo yalikuwa namna gani kwa Petro? Usiku wa mwisho katika gereza, Petro alikuwa katika usingizi muzito katikati ya walinzi wawili, Petro alijionea mambo ya ajabu. (Soma Matendo 12:7-11.) Kwa gafula, mwangaza ulionekana katika chumba cha gereza alimokuwa. Malaika alisimama, lakini walinzi hawakumwona, na alimuamusha Petro kwa haraka. Na minyororo hiyo iliyofunga mikono yake ilijifungua yenyewe! Malaika akamutosha Petro katika chumba cha gereza, akapita mbele ya walinzi waliokuwa inje, na kupitia mulango mukubwa wa chuma, ambao ‘ulifunguka wenyewe.’ Walipokuwa inje ya gereza, malaika hakuonekana tena. Petro alikuwa amefunguliwa!

16 Tunapofikiri sana jinsi Yehova anavyotumia nguvu yake ili kuwaokoa watumishi wake, hilo linatia imani yetu nguvu, sivyo? Ni kweli kwamba leo Yehova haokowe watumishi wake kwa njia ya muujiza. Lakini tunaamini kabisa kwamba anatumia nguvu yake kwa faida ya watu wake leo. (2 Nya. 16:9) Kupitia roho takatifu anaweza kutupatia nguvu ya kushinda kila jaribu tunalopata. (2 Kor. 4:7; 2 Pet. 2:9) Pia, karibuni Yehova atamutolea Mwana wake uwezo wa kufufua mamilioni ya wafu ambao wamefungwa katika magereza ya kifo. (Yoh. 5:28, 29) Imani yetu katika ahadi za Yehova inaweza kututia nguvu tunapopata majaribu leo.

MAGUMU HAYAKUWAZUIA KUTOA USHAHIDI KAMILI

17. Paulo alituachia mufano gani muzuri kuhusu kuhubiri kwa bidii na kuona kwamba hatuna wakati wa kupoteza?

17 Jambo la tatu ambalo tunaweza kujifunza kwa kuwa mitume waliendelea kukesha ni hili: Jambo hilo liliwasaidia waendelee kutoa ushahidi kamili ijapokuwa magumu. Ni jambo la maana kuhubiri kwa bidii na kuona kwamba hatuna tena wakati wa kupoteza; hilo litatusaidia tuendelee kukesha. Mutume Paulo alituachia mufano muzuri kuhusu jambo hilo. Alihubiri kwa bidii, alitembelea maeneo mengi na kuanzisha makutaniko mengi. Alivumilia taabu nyingi, lakini hakupoteza bidii yake na aliona kwamba hana wakati wa kupoteza.—2 Kor. 11:23-29.

18. Namna gani Paulo aliendelea kutoa ushahidi alipokuwa katika kifungo huko Roma?

18 Tufikirie sehemu ya mwisho inayozungumuzia mutume Paulo, katika kitabu cha Matendo sura ya 28. Mutume Paulo alifika Roma mahali ambapo ilimufaa akutane na Mufalme Nero. Aliwekwa katika kifungo, labda akifungwa munyororo ambao ulimushikanisha na askari-mulinzi. Hata hivyo, hakuna munyororo ambao ungemuzuia asihubiri kwa bidii. Paulo alipata nafasi ya kutoa ushahidi (Soma Matendo 28:17, 23, 24.) Kisha siku tatu, Paulo aliwaita watu walio wakuu kati ya Wayahudi ili kuwatolea ushahidi. Kisha, siku fulani waliyosikilizana, Paulo aliwatolea ushahidi mukubwa zaidi. Ona jinsi mustari wa 23 unavyosema: ‘Wakapanga siku fulani ya kuwa pamoja naye, nao wakaja kwake wakiwa hesabu kubwa zaidi katika makao yake. Naye akawaelezea jambo hilo kwa kutoa ushahidi kamili kuhusiana na ufalme wa Mungu na kwa kutumia ushawishi kwao kuhusu Yesu kutoka katika sheria ya Musa na pia Manabii, tangu asubuhi mupaka jioni.’

19, 20. (a) Ni nini kilichomusaidia Paulo hivi kwamba alikuwa na matokeo mazuri alipotoa ushahidi? (b) Paulo alifanya nini, hata ikiwa si kila mutu aliyekubali habari njema?

19 Kwa nini Paulo alipata matokeo mazuri alipotoa ushahidi? Mustari wa 23 unaonyesha mambo yaliyomusaidia. (1) Alikazia Ufalme wa Mungu na Yesu Kristo. (2) Alijikaza kuvutia wasikilizaji wake ‘kwa kutumia usadikisho.’ (3) Alifikiri na watu akitumia Maandiko. (4) Alikuwa mwenye kujinyima mambo fulani; alitoa ushahidi “tangu asubuhi mupaka jioni.” Paulo alitoa ushahidi wenye nguvu, lakini si kila mutu aliyekubali ujumbe wake. Mustari wa 24 unasema hivi: “Wengine wakaanza kuamini mambo yaliyosemwa; wengine hawakuamini.” Kukawa hali ya kutoelewana, na watu wakaondoka na kumwacha.

20 Je, Paulo alivunjika moyo kwa kuwa si kila mutu aliyekubali habari njema? Hata kidogo! Matendo 28:30, 31 inasema hivi: ‘Akakaa miaka miwili kamili katika nyumba yake mwenyewe ya kukodiwa, naye akawa akiwakaribisha kwa fazili wale wote walioingia ndani kwake, akiwahubiria ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yanayohusu Bwana Yesu Kristo kwa uhuru wa kusema ulio mukubwa zaidi, bila kizuizi.’ Kitabu cha Matendo kilichoongozwa na roho ya Mungu kinamalizia kwa maneno hayo yenye kufariji.

21. Mufano wa Paulo alipokuwa katika kifungo unatufundisha nini?

21 Mufano wa Paulo unatufundisha nini? Alipokuwa katika kifungo, Paulo hakuwa na wakati wa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Lakini, hakuwazia wengine vibaya; alitoa ushahidi kwa kila mutu aliyekuja kumwona. Vivyo hivyo, watumishi wa Mungu wengi leo wanalinda furaha yao na kuendelea kuhubiri ijapokuwa wamefungwa kwa sababu ya imani yao. Ndugu na dada zetu fulani wanabaki nyumbani, labda hata katika nyumba za kuwachunga watu kwa sababu ya uzee ao ugonjwa. Wanapokuwa na uwezo, wanawahubiria waganga, wale wanaotembelea wagonjwa, na wengine wanaokuja kuwaona. Tamaa ya moyo wao ni kutoa ushahidi kamili kuhusu Ufalme wa Mungu. Tunapendezwa kabisa na bidii yao, sivyo?

22. (a) Ni kitabu gani kinachotusaidia tufaidike na kitabu cha Matendo ya Mitume? (Ona kisanduku hapo juu.) (b) Wewe umekusudia kufanya nini unapongojea mwisho wa ulimwengu huu mwovu?

22 Kwa kweli, mufano wa mitume na Wakristo wengine wanaozungumuziwa katika kitabu cha Matendo unaweza kutufundisha mambo mengi. Tunapongojea mwisho wa ulimwengu huu mwovu, acheni tukusudie sana kuwaiga Wakristo wa wakati wa mitume kwa kuhubiri kwa bidii na kwa ujasiri. Hakuna pendeleo lingine kubwa tunaloweza kuwa nalo isipokuwa lile la “kutoa ushahidi kamili” kuhusu Ufalme wa Mungu!​—Mdo. 28:23.

[Maulizo ya Funzo]

[Sanduku katika ukurasa wa 13]

“Nimeelewa Sasa Vizuri Kitabu Cha Matendo ya Mitume”

Mwangalizi mumoja wa muzunguko alieleza jinsi alivyojisikia alipomaliza kusoma kitabu “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu. Alisema hivi: “Nimeelewa sasa vizuri kitabu cha Matendo ya Mitume. ‘Nimesoma’ kitabu hicho cha Biblia mara nyingi lakini ilikuwa kama nilikisoma nikiwa mwenye kuvaa lunete isiyoona vizuri katika mwangaza wa buji. Sasa najisikia nimebarikiwa kwa kuwa ni kama kwamba ninaona mambo mazuri yaliyo katika kitabu hicho kwa musaada wa mwangaza wa jua.”

[Picha katika ukurasa wa 12]

Malaika alimwongoza Petro kupitia mulango mukubwa wa chuma