Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunayoweza Kufanya ili Kulinda Roho Nzuri ya Kutaniko Letu

Tunayoweza Kufanya ili Kulinda Roho Nzuri ya Kutaniko Letu

Tunayoweza Kufanya ili Kulinda Roho Nzuri ya Kutaniko Letu

‘Fazili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo ziwe pamoja na roho munayoonyesha.’​—FLP. 4:23.

NAMNA GANI TUNAWEZA KULINDA ROHO NZURI KATIKA KUTANIKO . . .

tunaposhirikiana na ndugu zetu?

kupitia bidii yetu katika mahubiri?

kwa kuwaelezea wazee zambi nzito iliyofanywa?

1. Kwa nini makutaniko ya Filipi na ya Thiatira yalipongezwa?

 WAKRISTO wa Filipi wa wakati wa mitume walikuwa maskini. Hata hivyo, walikuwa wakarimu na walionyesha ndugu zao Wakristo upendo. (Flp. 1:3-5, 9; 4:15, 16) Kwa hiyo katika maneno ya kumalizia ya barua yake kwao, mutume Paulo aliandika: ‘Fazili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo ziwe pamoja na roho munayoonyesha.’ (Flp. 4:23) Kwa kuwa Wakristo wa Thiatira walionyesha roho hiyohiyo, Yesu aliyetukuzwa aliwaambia hivi: “Mimi nayajua matendo yako, na upendo wako na imani na huduma na uvumilivu wako, na kwamba matendo yako ya hivi karibuni yanazidi yale ya zamani.”​—Ufu. 2:19.

2. Namna gani roho ambayo kila mumoja wetu anajikaza kuonyesha inaweza kusaidia kutaniko letu liwe na roho nzuri ao roho isiyofaa?

2 Leo, kila kutaniko la Mashahidi wa Yehova linaonyesha roho fulani ao sifa fulani inayotawala katika kutaniko. Makutaniko fulani yanajulikana kuwa yenye shauku ao roho ya upendo. Mengine yanajulikana kwa sababu ya bidii ya ajabu katika kazi ya kuhubiri Ufalme na yanapenda sana utumishi wa wakati wote. Wakati kila mumoja wetu anajikaza kuwa na roho nzuri, jambo hilo litasaidia kutaniko liwe na umoja na litakuwa na maendeleo ya kiroho. (1 Kor. 1:10) Lakini, wakati ndugu wana roho ao mawazo yasiyofaa, hilo linaweza kufanya wengine katika kutaniko wasimutumikie Yehova kwa bidii, wawe na hali ya kutokuwa moto ao baridi, na hata kuachilia matendo mabaya katika kutaniko. (1 Kor. 5:1; Ufu. 3:15, 16) Kutaniko lenu lina roho gani? Wewe unaweza kufanya nini ili uendeleze roho nzuri katika kutaniko?

CHOCHEA ROHO NZURI KATIKA KUTANIKO

3, 4. Namna gani tunaweza ‘kumusifu [Yehova] katika kutaniko kubwa’?

3 Daudi alimwimbia Yehova hivi: “Nitakusifu [Yehova] katika kutaniko kubwa; nitakusifu kati ya kikundi cha watu wengi.” (Zab. 35:18) Daudi hakujizuia kumusifu Yehova alipokuwa na watumishi wengine wa Mungu. Mikutano ya kila juma, kutia ndani Funzo la Munara wa Mulinzi, inatutolea nafasi za kuonyesha bidii yetu na imani yetu tunapotoa maelezo. Kila mumoja wetu anaweza kujiuliza: ‘Je, ninatumia kabisa pendeleo la kutoa maelezo kwenye mikutaniko? Je, ninatayarisha mikutano vizuri na kutoa maelezo yenye kujenga? Baba wa familia anaweza kujiuliza, je, ninasaidia watoto wangu kutayarisha maelezo mbele ya wakati na kuwafundisha jinsi ya kujibu kwa maneno yao wenyewe?’

4 Jinsi tunavyoimba kwenye mikutano kunaonyesha kwamba tuna moyo ulio imara, yaani moyo unaoazimia kufanya yaliyo sawa ao hapana. Daudi alisema hivi: “Moyo wangu uko imara, Ee Mungu, moyo wangu uko imara. Nitaimba na kupiga muziki.” (Zab. 57:7) Nyimbo tunazoimba kwenye mikutano ya Kikristo zinatutolea nafasi ya ‘kumwimbia na kumupigia [Yehova] muziki’ kwa moyo imara. Ikiwa hatujui nyimbo fulani, kwa nini tusijizoeze kuimba nyimbo hizo wakati wa Ibada yetu ya Familia ya mangaribi? Kama mutunga​-zaburi, acheni basi tuazimie ‘kumwimbia Yehova katika maisha yetu na kumupigia Mungu wetu muziki maadamu tupo.’​—Zab. 104:33.

5, 6. Namna gani tunaweza kuwaonyesha wengine ukaribishaji na ukarimu, na kufanya hivyo kutachochea roho gani katika kutaniko?

5 Kuonyesha ndugu na dada ukaribishaji ni njia nyingine ya kuchochea roho ya upendo katika kutaniko. Katika sura ya mwisho ya barua yake kwa Waebrania, Paulo anawahimiza hivi: ‘Upendo wenu wa kindugu na uendelee. Musisahau ukaribishaji-wageni.’ (Ebr. 13:1, 2) Kuwaalika waangalizi wenye kusafiri na wake zao ao watumishi wa wakati wote wa kutaniko ili kula pamoja nao ni njia nzuri ya kuonyesha ukaribishaji. Fikiria pia wajane, familia zilizo na muzazi mumoja, ao watu wengine wanaoweza kufaidika kwa kushirikiana nasi wakati wa chakula ao wakati wa ibada yetu ya familia.

6 Paulo alimuagiza Timotheo awashaurie wengine ‘wafanye mema, wawe matajiri katika matendo mazuri, wawe wakarimu, tayari kushiriki, wakijiwekea wenyewe kwa usalama hazina ya musingi muzuri kwa ajili ya wakati ujao, ili waushike imara uzima ulio wa kweli.’ (1 Tim. 6:17-19) Paulo alitaka waabudu wenzake wajikaze kuonyesha roho ya ukarimu. Hata wakati ni vigumu kupata feza, tunaweza kuendeleza roho ya ukarimu. Kwa mufano ikiwa una motokari, unaweza kuwasaidia wengine kwa kuwapeleka katika mahubiri ao kwenye mikutano. Sasa hao wanaosaidiwa hivyo kwa upendo wanaweza kufanya nini? Wao pia wanaweza kuchochea roho nzuri ya kutaniko kwa kushukuru, labda ikiwa wana feza kidogo wanaweza pia kusaidia kwa kulipia garama ya essence inayozidi kuongezeka na kutengenezesha motokari. Zaidi ya hilo, kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu kunawafanya wajione kuwa wanahitajiwa na kupendwa. Tunapotendea ndugu zetu mambo mema, yaani “wale ambao katika imani ni jamaa zetu,” na kuwa tayari kupitisha wakati pamoja nao na kuwatolea zawadi fulani, tunaongeza upendo wetu kwao, pia tunasaidia kufanya kutaniko liwe na roho nzuri na ya shauku.​—Gal. 6:10.

7. Namna gani kuendelea kuchunga mambo ya siri kuhusu mambo ya kipekee ya wengine kunasaidia kulinda roho nzuri katika kutaniko?

7 Kufanya urafiki na kuchunga siri vinafanya kifungo cha upendo kati ya ndugu kiwe nguvu. (Soma Methali 18:24.) Rafiki wa kweli wanachunga siri. Wakati ndugu fulani anatufunulia mawazo yake ya ndani na jinsi anavyojisikia na kuwa hakika kwamba hatutayafunulia watu wengine, hivyo kifungo cha upendo kinachotuunganisha kitakuwa nguvu zaidi. Acheni tuwe marafiki wenye kutumainika ambao wanaweza kuchunga mambo ya siri na kusaidia kutaniko liwe kama familia yenye upendo.​—Met. 20:19.

UWE MWENYE BIDII KATIKA MAHUBIRI

8. Walaodikia Walipewa shauri gani, na kwa nini?

8 Yesu aliambia kutaniko la Laodikia hivi: ‘Mimi nayajua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala si moto. Laiti ungalikuwa baridi ao moto. Kwa hiyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu na si moto wala si baridi, nitakutapika kutoka kinywani mwangu.’ (Ufu. 3:15, 16) Wakristo wa Laodikia hawakuwa na bidii katika mahubiri. Inaelekea kwamba, jambo hilo lilifanya wasiwe na uhusiano muzuri kati yao. Kwa hiyo, Yesu aliwashauri hivi kwa upendo: ‘Wale wote ninaowapenda, mimi huwakaripia na kuwatia nizamu. Kwa hiyo uwe mwenye bidii na utubu.’​—Ufu. 3:19.

9. Namna gani bidii yetu katika mahubiri inasaidia kulinda roho nzuri ya kutaniko?

9 Ili kulinda roho nzuri ya kutaniko, ni lazima tujiangalie ikiwa tuna bidii katika mahubiri. Kusudi la kutaniko ni kutafuta watu walio mufano wa kondoo katika eneo na kuwajenga kiroho. Kwa hiyo, tunahitaji kushiriki kazi ya kufanya wanafunzi kwa bidii, kama Yesu alivyofanya. (Mt. 28:19, 20; Luka 4:43) Kadiri tunavyohubiri kwa bidii ndivyo tutakuwa na umoja zaidi tukiwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu.” (1 Kor. 3:9) Tunapoona jinsi wengine wanavyotetea imani yao katika mahubiri na jinsi wanavyopendezwa na mambo ya kiroho, hilo linatuchochea kuwapenda na kuwaheshimu zaidi. Pia, kutumika “bega kwa bega” katika mahubiri kunatokeza roho ya umoja katika kutaniko.​—Soma Zefania 3:9.

10. Kufanya namna yetu ya kuhubiri iwe nzuri zaidi kunakuwa na matokeo gani juu ya wengine katika kutaniko?

10 Tunapojikaza kufanya namna yetu ya kuhubiri iwe nzuri zaidi, hilo linakuwa na matokeo mazuri kwa wahubiri wengine. Ikiwa tunapendezwa na watu tunaokutana nao katika mahubiri na kujikaza ili kugusa mioyo yao, bidii yetu kwa ajili ya mahubiri inaongezeka. (Mt. 9:36, 37) Ikiwa tunaonyesha bidii, wengine wanaweza pia kutuiga. Yesu aliwatuma wanafunzi wake wakiwa wawili wawili ili kuhubiri, hakuwatuma mumoja​-mumoja. (Luka 10:1) Hilo liliwatolea nafasi ya kutiana moyo na kuzoezana, na pia kufanya hivyo kuliongeza bidii yao katika mahubiri. Tunafurahi kutumika pamoja na wahubiri wa Ufalme wenye bidii, sivyo? Bidii yao inatutia moyo na inatuchochea kuhubiri.​—Rom. 1:12.

EPUKA KUNUNGUNIKA-NUNGUNIKA NA USIFICHE ZAMBI NZITO

11. Waisraeli fulani katika siku za Musa walionyesha roho gani, na hilo lilikuwa na matokeo gani juu yao?

11 Majuma fulani tu kisha Yehova kuwafanya Waisraeli kuwa taifa, walianza kuonyesha roho ya kukosa kutosheka ao ya kunungunika. Hivyo walimuasi Yehova na waakilishi wake Musa na Haruni. (Kut. 16:1, 2) Ni hesabu chache tu ya Waisraeli waliotoka Misri ndio waliingia katika Inchi ya Ahadi. Hata Musa hakuruhusiwa kuingia katika Inchi ya Ahadi kwa sababu ya jinsi alivyojiendesha wakati kutaniko la Israeli lilionyesha roho isiyofaa! (Kum. 32:48-52) Tunaweza kufanya nini leo ili sisi pia tusiangukie katika mutego wa roho isiyofaa kama hiyo?

12. Namna gani tunaweza kuepuka roho ya kunungunika​-nungunika?

12 Tunapaswa kuepuka roho ya kunungunika-nungunika. Kuonyesha unyenyekevu na kuwaheshimu wale wanaotuongoza kutatusaidia, lakini pia ni lazima tuwe waangalifu kuhusiana na wale tunaoshirikiana nao. Kuchagua viburudisho visivyofaa ao kupitisha wakati mwingi sana pamoja na wafanyakazi wenzetu ao wanafunzi wenzetu wasioheshimu kanuni za Biblia kunaweza kuwa na matokeo mabaya. Ni jambo la hekima kutokushirikiana sana na watu wanaosema tu vibaya kuhusu kila jambo ao wanaoendeleza roho ya kujitegemea.​—Met. 13:20.

13. Kunungunika​-nungunika kunaweza kuongoza kwenye matatizo mengine gani ya kiroho katika kutaniko?

13 Kunungunika​-nungunika katika kutaniko kunaweza kuongoza kwenye matatizo mengine ya kiroho. Kwa mufano, kunungunika​-nungunika kunaweza kuhatarisha amani na umoja wa kutaniko. Zaidi ya hilo, kusema​-sema vibaya kuhusu waamini wenzetu kunaweza kuwaumiza moyoni na hata kutuongoza katika zambi ya kusingizia wengine na kuwatukana. (Law. 19:16; 1 Kor. 5:11) Wakati wa mitume, watu fulani wenye kunungunika-nungunika ‘walipuuza mamlaka na kuwatukana watukufu.’ (Yuda 8, 16) Bila shaka, Mungu hakukubali zoea hilo la kunungunika kuhusu ndugu wenye madaraka katika kutaniko.

14, 15. (a) Kuficha zambi kunaweza kuwa na matokeo gani juu ya kutaniko lote? (b) Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunajua kwamba mutu fulani amefanya zambi nzito?

14 Basi tutafanya nini ikiwa tunajua kwamba mutu fulani amefanya zambi kwa siri, labda alilewa, alitazama ponografia, ao anaishi maisha ya uasherati? (Efe. 5:11, 12) Kuficha zambi nzito kunaweza kuzuia utendaji wa roho takatifu ya Yehova na kuharibu amani ya kutaniko lote. (Gal. 5:19-23) Wakristo wa kwanza katika Korintho walipaswa kuondoa ubaya, leo pia watu wenye kuingiza uvutano mubaya wanapaswa kuondolewa katika kutaniko ili kulinda roho nzuri ya kutaniko. Unaweza kufanya nini ili kusaidia kutaniko liendelee kuwa na amani?

15 Kama tulivyoona hapo juu, ni lazima kulinda siri katika mambo fulani ya kipekee, zaidi sana wakati wengine wanatufunulia mawazo yao ao jinsi wanavyojisikia. Ni vibaya kabisa na inaumiza kufunua mambo ya siri kuhusu mutu fulani! Hata hivyo, wakati mutu fulani anatenda zambi nzito, wazee wa kutaniko ambao kulingana na Maandiko ndio wanaoruhusiwa kushugulikia jambo hilo, wanapaswa kujulishwa. (Soma Walawi 5:1.) Kwa hiyo, tukijua kwamba ndugu ao dada fulani amefanya zambi nzito, tunapaswa kumutia moyo awaendee wazee ili kupata musaada. (Yak. 5:13-15) Tutamuachia wakati wa kutosha ili afanye hivyo, ikiwa hafanyi hivyo katika wakati huo, basi, tunapaswa kuwaelezea wazee.

16. Kwa nini kuwaelezea wazee zambi nzito iliyofanywa kunasaidia kulinda roho ya kutaniko?

16 Kutaniko la Kikristo ni kimbilio la kiroho, kwa hiyo, tunapaswa kuwajulisha wazee ikiwa zambi nzito imefanywa ili kusaidia kulilinda. Ikiwa wazee wanamusaidia mukosaji kukubali uzito wa kosa lake, naye anatubu, na kukubali karipio, hatahatarisha tena roho nzuri ya kutaniko. Lakini itakuwa namna gani ikiwa mutu aliyefanya zambi nzito hatubu na hakubali mashauri ambayo wazee wanamutolea kwa upendo? Kutengwa kwa mutu huyo ‘kunaharibu’ ao kunaondoa uvutano mbaya wa mutu huyo katika kutaniko na kunalinda roho ya kutaniko. (Soma 1 Wakorintho 5:5.) Kwa kweli, ili kulinda roho ya kutaniko kila mumoja anapaswa kutimiza daraka lake: kushirikiana na baraza la wazee, na kulinda hali ya kiroho katika kutaniko.

CHOCHEA “UMOJA WA ROHO”

17, 18. Ni nini kitakachotusaidia “kuushika umoja wa roho”?

17 Kwa ‘kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume,’ wafuasi wa kwanza wa Yesu walisaidia kulinda umoja katika kutaniko. (Mdo. 2:42) Waliheshimu mashauri ya Maandiko na mwongozo waliopata kutoka kwa wanaume wazee. Kwa kuwa leo wazee wanaunga mukono mutumwa mwaminifu na mwenye busara, ndiyo sababu sisi wote katika kutaniko tunatiwa moyo na kusaidiwa ili kuendelea kuwa na umoja. (1 Kor. 1:10) Tunapoheshimu maagizo ya Biblia ambayo tengenezo la Yehova linatutolea na kufuata mwongozo wa wazee, tunaonyesha kwamba “tunajitahidi sana kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.”​—Efe. 4:3.

18 Kwa hiyo, acheni basi tufanye yote tuwezayo ili kuendelea kulinda roho nzuri ya kutaniko. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuwa hakika kwamba ‘fazili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo zitakuwa pamoja na roho tunayoonyesha.’​—Flp. 4:23.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 19]

Je, unasaidia kulinda roho nzuri katika kutaniko kwa kutayarisha maelezo yenye kujenga?

[Picha katika ukurasa wa 20]

Saidia kulinda roho nzuri kwa kuzijua nyimbo zetu