Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Ya Wasomaji Wetu

Maulizo Ya Wasomaji Wetu

Maulizo Ya Wasomaji Wetu

Je, Mukristo aliye na zoezi la kutazama ponografia (picha ao habari za ngono) anaweza kufikia kutengwa na ushirika?

▪ Ndiyo. Hilo linaonyesha kwa nini ni lazima kuepuka kabisa kila namna ya ponografia. Hilo linatia ndani kusoma vitabu, magazeti, kutazama filme, video, na programu za internet zinazoonyesha ponografia.

Ponografia inaenea mahali pote ulimwenguni. Hesabu ya watu wanaotazama ponografia inaongezeka kwa kuwa internet inafanya iwe rahisi kutazama ponografia. Watu fulani, vijana na wazee, wameona mambo ya ponografia bila kukusudia wanapofungua internet. Wengine wanafungua kwa makusudi programu ya internet iliyo na mambo ya ponografia, wanajisikia kuwa huru zaidi kwa kuwa wanaweza kusoma ao kutazama mambo hayo kwa uficho nyumbani ao katika biro kazini. Kwa nini Wakristo hawapaswi kuona ponografia kuwa jambo la muchezo?

Sababu inapatikana katika onyo hili la Yesu: ‘Kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.’ (Math. 5:28) Ni kweli kwamba mume na muke waliooana wanaruhusiwa kufanya ngono, na hilo linawaletea furaha. (Met. 5:15-19; 1 Kor. 7:2-5) Lakini ponografia inakusudi lingine. Ponografia inakazia ngono isiyoruhusiwa inayoamusha mawazo mabaya ambayo Yesu alituonya tuepuke. Kwa kweli, kusoma ao kutazama mambo ya ponografia ni kinyume na muongozo huu wa Mungu: ‘Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye mazara, na kutamani, ambako ni ibada ya sanamu.’​—Kol. 3:5.

Namna gani ikiwa Mukristo alitazama ponografia mara moja ao mara mbili tu? Hali yake inaweza kufananishwa na hali ya hatari ambayo wakati fulani mutunga​-zaburi Asafu alipatikana ndani: “Mimi nami karibu miguu yangu igeuke kando, hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.” Namna gani Mukristo aliyeangalia kwa muda mambo ya ponografia, yaani, picha za wanawake ao wanaume walio uchi ao watu wenye kufanya uasherati, anaweza kuwa na zamiri safi na kuwa na amani pamoja na Mungu? Asafu alikosa amani, yeye alisema: ‘Nami nikapata mapigo muchana kutwa, na rekebisho langu ni la kila asubuhi.’​—Zab. 73:2, 14.

Mukristo anayetazama ponografia anapaswa kuamuka kiroho na kutafuta musaada. Musaada huo unapatikana katika kutaniko: ‘Hata mutu akijikwaa katika kosa fulani kabla ya yeye kulijua, ninyi mulio na sifa za kustahili kiroho jaribuni kumurekebisha upya mutu huyo katika roho ya upole, huku kila mumoja wenu akiendelea kujiangalia.’ (Gal. 6:1) Muzee mumoja ao wazee wawili wanaweza kumutolea musaada. Wanaweza kutoa ‘sala ya imani inayoweza kumuponya huyo asiyejisikia vizuri, na zambi yake inaweza kusamehewa.’ (Yak. 5:13-15) Wale waliotafuta musaada ili kuondoa uchafu wa ponografia katika maisha yao wametambua kama Asafu, kwamba ni jambo la lazima sana kufanya hivyo ili kumukaribia Mungu.​—Zab. 73:28.

Hata hivyo, mutume Paulo alisema kwamba watu fulani waliotenda zambi hawakutubu ‘kutokana na unajisi wao na uasherati na mwenendo mupotovu.’ * (2 Kor. 12:21) Profesa Marvin R. Vincent alisema kwamba neno la Kigiriki lililotumiwa hapo ili kutafsiri neno “unajisi,” ni uchafu wenye kuchukiza sana.” Ni jambo la huzuni sana kuona kwamba picha zingine za ponografia zinaonyesha mambo machafu sana kupita picha za wanawake walio uchi ao mwanaume na mwanamuke wakifanya uasherati. Ni ponografia yenye kuchukiza sana, yenye kinyaa, inayotia ndani ngono ya wanaume kwa wanaume ao wanawake kwa wanawake, kikundi cha watu wenye kufanya ngono ao kulalana kwa kubadilishana, kufanya ngono na wanyama, kufanya ngono na watoto wadogo, wanawake wakilalwa kinguvu na kikundi cha watu wengi, kuwatesa wanawake kingono, ao kuwatesa kinyama. Wakati wa mutume Paulo watu fulani waliokuwa ‘katika giza kiakili waliishiwa ufahamu wote wa maadili na wakajitoa wenyewe ili kuwa na mwenendo mupotovu na kufanya ukosefu wa usafi wa kila namna kwa pupa.’​—Efe. 4:18, 19.

Mutume Paulo alizungumuzia pia neno “uchafu” kwenye Wagalatia 5:19. Mutu fulani mwenye elimu ya Biblia alionyesha kwamba neno hilo linaweza kumaanisha zaidi sana “tamaa ya ngono isiyo ya kawaida.” Ni Mukristo gani anayeweza kukataa kwamba mambo hayo machafu ya ponografia yanayotajwa hapo juu ni ‘tamaa ya ngono isiyo ya kawaida’ na ni yenye kuchukiza sana? Katika andiko la Wagalatia 5:19-21 Paulo alimalizia kwa kusema kwamba “wale walio na mazoea” ya kufanya mambo hayo machafu ‘hawatauriti Ufalme wa Mungu.’ Kwa hiyo, ikiwa mutu fulani amekuwa na zoezi la kutazama mambo machafu na yenye kuchukiza ya ponografia, labda mara nyingi, na hatubu na kugeuka, ataondolewa katika kutaniko. Anaweza kutengwa ili kulinda usafi na hali nzuri ya kutaniko.​—1 Kor. 5:5, 11.

Ni vizuri kujua kwamba ndugu fulani waliotazama mambo yenye kuchukiza ya ponografia waliwaendea wazee na kupokea musaada wa kiroho waliohitaji ili kufanya mabadiliko makubwa. Yesu aliwasihi Wakristo katika kutaniko la Sardi hivi: ‘Uyatie nguvu mambo yanayobaki yaliyokuwa tayari kufa, endelea kukazia akilini jinsi ulivyopokea na jinsi ulivyosikia, nawe uendelee kulishika, na utubu. Hakika usipoamuka, nawe hautajua hata kidogo saa nitakayokuja juu yako.’ (Ufu. 3:2, 3) Inawezekana kutubu na kunyakuliwa kutoka katika moto.​—Yuda 22, 23.

Kwa hiyo, itakuwa vizuri kabisa ikiwa kila mumoja wetu anaazimia kutokukaribia hatari hiyo. Ndiyo, tunapaswa kuepuka kabisa kila namna ya ponografia!

[Maelezo ya chini]

^ Ili kutofautisha maneno “unajisi, uasherati na mwenendo mupotovu,” ona Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 7, 2006, ukurasa wa 29-31.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 30]

Mukristo anayetazama ponografia anapaswa kuamuka kiroho na kutafuta musaada