Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka

Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka

Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka

“Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii.”​—2 TIM. 4:2.

JE, UNAWEZA KUELEZA?

Ni nini iliyochochea Wakristo wa kwanza waone uhitaji wa kuhubiri kwa haraka?

Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunatambua uhitaji wa kutenda kwa haraka?

Kwa nini leo ni jambo la maana sana kuhubiri kupita wakati mwingine wowote.

1, 2. Amri ya ‘kuhubiri kwa bidii,’ inatokeza maulizo gani?

 KWA kawaida watu wanaofanya kazi ya kuokoa maisha, wanatenda kwa haraka. Kwa mufano, wazima​-moto wanatenda kwa haraka wanapoitwa, kwa kuwa wanajua kwamba maisha ya watu yako katika hatari.

2 Sisi Mashahidi wa Yehova tunatamani kuwasaidia watu ili waokolewe. Kwa hiyo, tunachukua kwa uzito kazi yetu ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Lakini, hatufanye kazi hiyo haraka-haraka bila kufikiri. Hivyo basi, mutume Paulo alimaanisha nini alipotoa shauri hili: “Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii”? (2 Tim. 4:2) Namna gani tunaweza kuhubiri tukitambua uhitaji wa kufanya hivyo kwa haraka? Na kwa nini tunapaswa kufanya kazi yetu kwa bidii?

KWA NINI KAZI YETU YA KUHUBIRI NI YA HARAKA?

3. Ni nini litawapata watu wanaokubali ujumbe wa Ufalme na wale wanaoukataa?

3 Wale wanaokubali ujumbe wa Ufalme wataokolewa na wale wanaoukataa wataharibiwa. Kuchunga hilo akilini kutatusaidia tuone kuwa ni jambo la haraka kuhubiria watu habari njema. (Rom. 10:13, 14) Neno la Mungu linasema hivi: ‘Ninapomuambia muovu: Hakika utakufa, naye kwa kweli anageuka na kuiacha zambi yake na kuendelea kutenda haki na uadilifu, hakika ataendelea kuishi. Yeye hatakufa. Hakuna yoyote kati ya zambi zake alizozitenda itakayokumbukwa juu yake.’ (Ezek. 33:14-16) Ndiyo sababu, sisi tunaohubiri Ufalme, Biblia inatuambia hivi: “Utajiokoa wewe mwenyewe na [kuokoa] wale wanaokusikiliza pia.”​—1 Tim. 4:16; Ezek. 3:17-21.

4. Kwa nini uasi-imani ulifanya mitume wahubiri kwa haraka?

4 Ili kuelewa kwa nini mutume Paulo alimushauria Timotheo kuhubiri kwa bidii, fikiria maneno yanayozunguka andiko letu la musingi. Tunasoma hivi: ‘Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii katika majira yanayofaa, katika majira yenye taabu, karipia, kemea, himiza, kwa ustahimilivu wote na ufundi wa kufundisha. Kwa maana kutakuwa na kipindi cha wakati ambapo hawatalivumilia fundisho lenye afya, bali, kwa kupatana na tamaa zao wenyewe, watajikusanyia walimu kwa ajili yao wenyewe ili masikio yao yafurahishwe; nao watageuza masikio yao kutoka kwenye kweli.’ (2 Tim. 4:2-4) Yesu alitabiri kwamba uasi​-imani ungetokea. (Math. 13:24, 25, 38) Kwa kuwa uasi-imani ulikaribia kutokea, lilikuwa jambo la lazima Timotheo ‘alihubiri neno’ hata katika kutaniko ili Wakristo wasivutiwe na kudanganywa na mafundisho ya uongo. Maisha ya watu yalikuwa katika hatari. Tuseme nini kuhusu wakati wetu?

5, 6. Katika mahubiri, tunaweza kukutana na watu walio na mawazo gani yenye kuenea sana?

5 Waasi-imani wanaotoka katika ibada ya kweli wameongezeka na kueneza mafundisho yao. (2 Thes. 2:3, 8) Ni mafundisho gani yanayofurahisha masikio ya watu leo? Mahali pengi, fundisho la mageuzi limeenezwa kwa bidii kama fundisho la kidini. Hata ikiwa mageuzi ni fundisho la sayansi, limekuwa kama fundisho la kidini, na limewafanya watu wawe na maoni yasiyofaa juu ya Mungu na watu wengine. Fundisho lingine linalojulikana sana ni lile linalosema kwamba Mungu hatuhangaikie, kwa hiyo sisi pia si lazima tujiangaishe juu yake. Kwa nini watu wengi wanavutiwa sana na mafundisho hayo yanayowafanya wasinzie kiroho? Mafundisho hayo mawili yanachochea watu wafikiri hivi: ‘Uko huru kufanya jambo lolote unalotaka kwa kuwa hakuna yule atakayekuuliza lolote.’ kwa kweli, mafundisho hayo yamefurahisha masikio ya watu wengi.​—Soma Zaburi 10:4.

6 Kuna mafundisho mengine pia yanayofurahisha masikio ya watu. Watu fulani ambao bado wanaenda kanisani wanapenda walimu wanaowaambia, ‘Ufanye mema ao mabaya, Mungu anakupenda.’ Mapadiri na mapasta wanafurahisha masikio ya waamini wao kwa kuwaambia kwamba kuhuzuria misa, kusherehekea sikukuu fulani za kidini, na kuwa na sanamu vitawaletea baraka ya Mungu. Waamini hao hawaoni kabisa hatari ya mafundisho hayo. (Zab. 115:4-8) Lakini, wanaweza kufaidika na Ufalme wa Mungu ikiwa tu tunawaamusha katika usingizi wa kiroho kupitia ujumbe wa kweli wa Biblia.

KUTAMBUA UHITAJI WA KUHUBIRI KWA HARAKA KUNAMAANISHA NINI?

7. Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunatambua uhitaji wa kutenda kwa haraka?

7 Muganga anayefanya upasuaji anapaswa kufanya kazi yake kwa uangalifu bila kukengeushwa kwa kuwa maisha ya mugonjwa yamo katika hatari. Katika mahubiri, tunaweza kuonyesha kwamba tunatambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kwa kufanya kazi yetu bila kukengeushwa, yaani, kufikiria mambo, maulizo ao habari zilizo katika vichapo vyetu zinazoweza kuwapendeza watu tunaohubiria. Kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kunaweza pia kutuchochea tubadili programu yetu ili kuwatembelea watu wanapoweza kuwa na wakati wa kutusikiliza.​—Rom. 1:15, 16; 1 Tim. 4:16.

8. Kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kunamaanisha pia nini?

8 Kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kunamaanisha pia kujua mambo ya kutia pa nafasi ya kwanza. (Soma Mwanzo 19:15.) Kwa mufano, wazia kisha kuchunguza hali ya afya yako muganga anakuita katika chumba chake cha kazi na kukuambia hivi: “Hali yako ya afya inaomba kutenda kwa haraka. Unabaki tu na mwezi mumoja ili kufanya jambo fulani kuhusu ugonjwa wako.” Labda hautatoka kwa haraka katika chumba chake cha kazi kama muzima​-moto anayeitwa. Labda utasikiliza kwanza mapendekezo yake, utarudi nyumbani, na kufikiria kwa uzito mambo ya kufanya kwanza kuhusu afya yako.

9. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Paulo alitambua uhitaji wa kutenda kwa haraka alipokuwa Efeso?

9 Maneno ambayo Paulo alizungumuza pamoja na wazee wa Efeso kuhusu kuhubiri habari njema katika wilaya ya Asia, yanaonyesha kwamba alitambua uhitaji wa kutenda kwa haraka. (Soma Matendo 20:18-21.) Inaonekana kwamba, mara tu alipofika, alianza kuhubiri habari njema nyumba kwa nyumba kwa bidii. Pia, kwa muda wa miaka miwili aliendelea na programu yake ya ‘kutoa kila siku hotuba nyingi katika jumba la shule ya Tirano.’ (Mdo. 19:1, 8-10) Kwa kweli, kwa kuwa Paulo alitambua uhitaji wa kutenda kwa haraka jambo hilo lilikuwa na uvutano juu ya programu yake. ‘Kuhubiri kwa bidii’ hakumaanishi kwamba kazi yetu inapaswa kutulemea. Hata hivyo, tunapaswa kutia kazi yetu ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza maishani.

10. Kwa nini tunaweza kufurahi kwa kuwa Wakristo walitambua uhitaji wa kutenda kwa haraka miaka 100 iliyopita?

10 Mufano wa kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia ambao mbele ya mwaka wa 1914 walianzisha kazi ya kuhubiri habari njema, unatusaidia tuelewe kinachomaanisha kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka. Ijapokuwa walikuwa wachache, walikuwa wenye kuazimia na walielewa kwamba waliishi kipindi kilichowaomba kutenda kwa haraka, na kwa hiyo walijitoa ili kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii. Walichapisha hotuba katika magazeti mengi na kuonyesha watu filme ya “Photo-drame de la création.” Filme hiyo ilikuwa ya rangi na picha za watu wenye kusema. Kwa njia hiyo, walihubiria watu wengi habari njema. Ikiwa hangewangetambua kwamba walipaswa kutenda kwa haraka, ni wangapi kati yetu leo ambao wangesikia ujumbe wa Ufalme?​—Soma Zaburi 119:60.

FANYA ANGALISHO ILI USISAHAU KWAMBA UNAPASWA KUTENDA KWA HARAKA

11. Nini kilichowafanya ndugu fulani wasahau kwamba walipaswa kutenda kwa haraka?

11 Mambo ya kukengeusha akili yanaweza kumufanya mutu asione umaana wa kazi ya kuhubiri. Ulimwengu wa Shetani unatuchochea ili tufuatie tu faida zetu wenyewe na mambo yasiyo ya lazima. (1 Pet. 5:8; 1 Yoh. 2:15-17) Kuna ndugu ambao wakati fulani walitia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza, kisha wakasahau kwamba walipaswa kutenda kwa haraka. Kwa mufano, Mukristo mumoja aliyeishi wakati wa mitume anayeitwa Dema alikuwa ‘mufanyakazi’ pamoja na Paulo, lakini akakengeushwa na mambo ya ulimwengu usiomuogopa Mungu. Kuliko kuendelea kumutia nguvu ndugu yake Paulo wakati wa taabu, Dema akamuacha Paulo.—Filem. 23, 24; 2 Tim. 4:10.

12. Ni nini iliyo kazi ya maana sana leo, na tutakuwa na nafasi ya kufurahia nini milele?

12 Ikiwa tunataka kuendelea kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka, ni lazima tupigane na tamaa ya kupenda kuwa na mambo fulani katika maisha. Tunapaswa kushika “imara uzima ulio wa kweli.” (1 Tim. 6:18, 19) Tunajua vizuri kwamba tutakapokuwa katika ulimwengu mupya tutakuwa na nafasi za kufurahia milele mambo mengi yenye kupendeza. Lakini kwa sasa, kazi ya kuwasaidia wengine ili wasiharibiwe kwenye Har-magedoni ndio kazi ya maana sana ya wakati wetu.

13. Kwa kuwa sasa sisi ni Wakristo, namna gani tunaweza kuendelea kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka?

13 Kwa kuwa watu wengi wanaotuzunguka leo ni wenye kulala usingizi wa kiroho, ni nini kitakachotusaidia tusisahau uhitaji wa kutenda kwa haraka? Tukumbuke kwamba wakati fulani sisi pia tulikuwa wenye kulala katika giza. Lakini tuliamushwa, na Kristo akatuangazia, kama Paulo alivyoonyesha. Sasa tuna pendeleo la kuwa wachukuaji wa nuru. (Soma Waefeso 5:14.) Kisha kuzungumuzia jambo hilo Paulo aliandika hivi: ‘Endeleeni kuangalia sana kwamba jinsi munavyotembea si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima, mukijinunulia wakati unaofaa, kwa sababu siku hizi ni zenye uovu.’ (Efe. 5:15, 16) Kwa kuwa tunapatikana katika ulimwengu huu muovu, acheni ‘tujinunulie wakati’ ili kufanya mambo yanayoweza kutusaidia tukae macho kiroho.

TUNAISHI NYAKATI ZA HATARI

14-16. Kwa nini kazi ya kuhubiri Ufalme inaombwa kufanywa haraka sana leo kuliko wakati mwingine wowote?

14 Sikuzote wahubiri wametambua uhitaji wa kutenda kwa haraka, lakini sasa ndiyo wakati wa kufanya hivyo zaidi. Kuanzia mwaka wa 1914, ile ishara yenye matukio mengi ni yenye kuonekana waziwazi. (Math. 24:3-51) Maisha ya wanadamu yako katika hatari sasa kuliko wakati mwingine wowote. Ijapokuwa makubaliano ya hivi karibuni ya mataifa yenye nguvu ulimwenguni, mataifa hayo yangali na mabombe ya nyukilia 2 000 hivi ambayo yanaweza kufyatuliwa wakati wowote. Inaripotiwa kwamba vifaa vingi vya kutengeneza mabombe ya nyukilia ‘vimepotea.’ Je, inawezekana vitu hivyo viwe katika mikono ya wateroriste? Watu wenye kujifunza matukio ya ulimwengu wanasema kwamba wanadamu wanaweza kuangamizwa kupitia vita ambayo wateroriste wanaweza kuanzisha. Lakini si vita tu inayotia maisha ya wanadamu katika hatari.

15 Kulingana na ripoti moja ya mwaka wa 2009, ‘mabadiliko ya hali ya hewa yanatia maisha ya watu katika hatari kubwa katika siku zetu.’ Ripoti hiyo inaongeza hivi: ‘Katika miaka inayokuja mabadiliko ya hali ya hewa yatakuwa na matokeo mabaya juu ya afya ya watu wengi na yatatia maisha ya watu wengi sana katika hatari.’ Hatari hiyo yenye uharibifu mukubwa inaweza kusababishwa na kupanda sana kwa maji ya bahari, ukosefu wa mvua kwa muda murefu, maji ya mitoni inayofurika, magonjwa ya kuambukiza, upepo mukali, na vita kwa sababu ya upungufu wa chakula. Bila shaka, vita na misiba yenye kutokana na hali ya hewa vinatia maisha ya wanadamu katika hatari.

16 Watu fulani wanafikiri kwamba vita ya nyukilia inaweza kuongoza kwenye utimizo wa “ile ishara.” Lakini pia watu wengi hawaelewi umaana kabisa wa ile ishara. Ishara hiyo ni yenye kuonekana wazi tangu miaka mingi sasa, hilo linaonyesha kwamba Yesu ameanza kutawala na kwamba mwisho wa ulimwengu huu uko karibu sana. (Math. 24:3) Leo, sehemu nyingi za ishara hiyo zimeonekana wazi kupita wakati mwingine wowote. Sasa ndiyo wakati wa kuamuka kiroho. Kazi yetu ya kuhubiri inaweza kusaidia watu waamuke.

17, 18. (a) Namna gani kujua “majira” kunatuchochea? (b) Ni nini kitakachowachochea watu wabadili maoni yao na kukubali ujumbe wa Ufalme?

17 Wakati huu mudogo unaobaki, unatutolea nafasi ya kuonyesha kwamba tunamupenda Yehova na kumaliza kazi aliyotutolea katika siku hizi za mwisho. Maneno ambayo Paulo aliwaandikia Wakristo wa Roma ni ya maana sana hata leo: ‘Munayajua majira, kwamba tayari ni saa ya ninyi kuamuka kutoka katika usingizi, kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko wakati tulipokuwa waamini.’​—Rom. 13:11.

18 Matukio ya siku za mwisho yaliyotabiriwa yanaweza kusaidia watu waone kwamba wanahitaji kuamuka kiroho. Wengine wanatambua kwamba mwanadamu ana lazima ya musaada wanapoona jinsi serikali za wanadamu zinavyoshindwa kutengeneza mambo ya uchumi, kumaliza hatari za mabombe ya nyukilia, jeuri, ao kulinda mazingira yasiharibiwe. Wengine wanafikia kupendezwa na ujumbe wa Ufalme wanapopatwa na mambo fulani katika familia zao, kama vile ugonjwa, ndoa kuvunjika, ao kufiwa na mutu waliyemupenda. Tunapohubiri, tunaweza kukutana na watu kama hao ili kuwasaidia.

UHITAJI WA KUTENDA KWA HARAKA UNATUCHOCHEA

19, 20. Namna gani kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kumechochea wahubiri wengi wabadili namna yao ya kuishi?

19 Kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kumesaidia wahubiri wengi waongeze bidii yao katika mahubiri. Kwa mufano, ndugu mumoja na bibi yake wa inchi inayoitwa Équateur waliamua kurahisisha maisha yao kisha kuhuzuria mukusanyiko wa pekee wa siku moja wa mwaka wa 2006, uliokuwa na kichwa, “Uwe na Jicho Rahisi.” Waliandika kwenye karatasi vitu ambavyo hawakuhitaji, na katika miezi mitatu walitoka katika nyumba yao yenye vyumba vitatu vya kulalia na kuhamia katika nyumba yenye chumba kimoja, waliuzisha vitu fulani, na kubaki bila deni ya mutu. Baada ya muda kidogo walianza kazi ya upainia musaidizi na kukubali pendekezo la mwangalizi wa muzunguko la kwenda kutumikia katika kutaniko lililokuwa na lazima sana ya wahubiri.

20 Ndugu mumoja wa huko Amerika ya Kaskazini anasema hivi: “Wakati muke wangu nami tulipohuzuria mukusanyiko wa 2006, kulikuwa kumekwisha kupita miaka 30 tangu tubatizwe. Kisha programu ya mukusanyiko, tulipokuwa tukirudi nyumbani katika motakari yetu, tulizungumuzia jinsi ya kutumia katika maisha yetu mashauri yaliyotolewa kuhusu kuwa na maisha rahisi. (Math. 6:19-22) Tulikuwa na nyumba tatu, shamba, motokari nzuri, mashua, na vitu vingine. Tulijisikia kuwa sisi ni Wakristo wasio na akili, kwa hiyo tuliamua kuwa na muradi wa kufanya kazi ya utumishi wa wakati wote. Katika mwaka wa 2008 tukawa mapainia wa kawaida kama binti yetu. Tulifurahi kabisa kutumika pamoja na ndugu zetu kwa ukaribu! Tulikuwa na uwezekano wa kutumikia mahali ambapo kulikuwa lazima sana ya wahubiri. Pia, kwa sababu ya kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Yehova kulitufanya tumukaribie zaidi. Zawadi kubwa ambayo ndugu huyo na muke wake wamepata ni kuona jinsi watu wanavyofurahi wanapoelewa ukweli kutoka katika Neno la Mungu.”

21. Ni ujuzi gani unaotuchochea kuhubiri kwa bidii?

21 Sisi tunajua jambo litakaloupata ulimwengu huu muovu hivi karibuni—“siku ya hukumu na ya kuangamizwa kwa watu wasiomuogopa Mungu.” (2 Pet. 3:7) Kujua Neno la Mungu kunatuchochea kutangaza kwa bidii ziki kubwa inayokuja na kuhubiri kuhusu ulimwengu mupya. Tuendelee kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka ili kutolea wanadamu tumaini la kweli. Kwa kufanya yote tuwezayo ili kuhubiri kwa ukamili, tunaonyesha kwamba tunamupenda kabisa Mungu na tunawapenda wanadamu wenzetu.

[Maulizo ya Funzo]