Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Endelea Kuwa na Moyo Usiogawanyika Kumuelekea Yehova

Endelea Kuwa na Moyo Usiogawanyika Kumuelekea Yehova

Endelea Kuwa na Moyo Usiogawanyika Kumuelekea Yehova

‘Mwanangu, umujue Mungu wa baba yako, umutumikie kwa moyo kamili.’​—1 NYA. 28:9.

TAFUTA MAJIBU YA MAULIZO HAYA:

Moyo wa mufano unamaanisha nini?

Tunaweza kutumia njia gani ili kuuchunguza moyo wetu?

Namna gani tunaweza kuendelea kuwa na moyo usiogawanyika kumuelekea Yehova?

1, 2. (a) Ni sehemu gani ya mwili ambayo inatajwa mara nyingi kwa njia ya mufano katika Biblia kuliko sehemu zingine? (b) Sababu gani ni jambo la lazima tuelewe maana ya moyo wa mufano?

 MARA nyingi Biblia inataja sehemu za mwili wa mwanadamu ili kuzungumuzia jambo fulani. Kwa mufano, Ayubu alisema hivi: “Hakuna jeuri mikononi mwangu.” Mufalme Sulemani naye alisema hivi: “Habari ambayo ni njema inaifanya mifupa inone.” Yehova alimuhakikishia Ezekieli hivi: “Nimelifanya paji la uso wako gumu kuliko jiwe gumu.” Na watu fulani walimuambia mutume Paulo hivi: “Unaanzisha mambo yaliyo mageni masikioni mwetu.”​—Ayu. 16:17; Met. 15:30; Eze. 3:9; Mdo. 17:20.

2 Hata hivyo, moyo ndio sehemu ya mwili wa mwanadamu inayotajwa zaidi kwa njia ya mufano katika Biblia kuliko sehemu nyingine zote. Mwanamuke mwaminifu Hana, alitaja sehemu hiyo katika sala yake aliposema: “Moyo wangu unafurahi katika Yehova.” (1 Sam. 2:1) Kwa kweli, waandishi wa Biblia wanataja moyo karibu mara elfu, zaidi sana kwa njia ya mufano. Ni jambo la lazima sana tuelewe maana ya moyo wa mufano kwa sababu Biblia inasema kama tunapaswa kulinda moyo wetu.​—Soma Methali 4:23.

MOYO HUO WA MUFANO NI NINI?

3. Namna gani tunaweza kuelewa maana ya moyo wa mufano katika Biblia? Eleza.

3 Ijapokuwa Neno la Mungu halitoi maelezo yote juu ya moyo wa mufano, hata hivyo linatusaidia kwa kiasi fulani kuelewa maana ya neno hilo. Namna gani? Tuchukue mufano, fikiria picha nzuri iliyofanyizwa kwa maelfu ya mawe madogo​-madogo ambayo yaliunganishwa​-unganishwa pamoja. Ili kuelewa namna picha hiyo ilivyo kabisa, inakuomba urudi nyuma kidogo na kutazama vizuri namna mawe hayo madogomadogo yalivyopangwa ili kufanyiza picha hiyo nzuri. Vile vile, ikiwa tunachunguza vizuri sana maandiko mengi yanayozungumuzia moyo wa mufano, jambo hilo linaweza kutusaidia kuelewa vizuri maana ya neno hilo.

4. (a) Moyo wa mufano unamaanisha nini? (b) Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 22:37 yanamaanisha nini?

4 Waandishi wa Biblia wanatumia neno “moyo” ili kuonyesha mutu wote wa ndani; yaani, tamaa zetu, mawazo yetu, furaha ao huzuni, mutazamo, uwezo mbalimbali, nia, na mipango ya mutu. (Soma Kumbukumbu 15:7; Methali 16:9; Matendo 2:26.) Kitabu kimoja kinaonyesha kwamba “moyo” ni ‘yule mutu wote wa ndani.’ Lakini wakati mwingine neno “moyo” halichukui maana hiyo yote. Kwa mufano, Yesu alisema: ‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’ (Mt. 22:37) Katika andiko hilo, neno “moyo” linamaanisha tamaa ya mutu, furaha ao huzuni, na namna mutu anavyojisikia kabisa kindani. Yesu alitofautisha moyo na nafsi, na akili, kwa sababu alipenda kukazia kama upendo wetu kwa Mungu unapaswa kuonyeshwa na yale yaliyo moyoni mwetu, yaani, namna tunavyojisikia kabisa kindani, na pia kupitia namna tunavyojiendesha katika maisha na namna tunavyotumia uwezo wetu wa kufikiri, yaani, akili. (Yoh. 17:3; Efe. 6:6) Lakini wakati neno “moyo” linatumiwa peke yalo, linamaanisha mutu wote wa ndani.

TUNAPASWA KULINDA MOYO WETU

5. Sababu gani ni vizuri tufanye yote tuwezayo ili kumutumikia Yehova kwa moyo usiogawanyika?

5 Mufalme Daudi alizungumuza juu ya moyo, naye alimukumbusha Sulemani hivi: ‘Mwanangu, umujue Mungu wa baba yako, umutumikie kwa moyo kamili na kwa nafsi yenye shangwe; kwa maana Yehova anaichunguza mioyo yote, naye anatambua kila mwelekeo wa fikira.’ (1 Nya. 28:9) Kwa kweli, Yehova anaichunguza mioyo yote, anaichunguza mioyo yetu pia. (Met. 17:3; 21:2) Na yale anayoona katika mioyo yetu yanaonyesha ikiwa tuna uhusiano muzuri pamoja naye ao hapana na ikiwa tutapata uzima ao hapana. Kwa hiyo, tunapaswa kusikiliza shauri la Daudi lenye kuongozwa na roho ya Mungu kwa kufanya yote tuwezayo ili kumutumikia Yehova kwa moyo usiogawanyika.

6. Ni nini inayoweza kuregeza tamaa yetu ya kumutumikia Yehova?

6 Sisi Mashahidi tunamutumikia Yehova kwa bidii, na hilo linaonyesha kweli kama tunatamani sana kumutumikia kwa moyo usiogawanyika. Lakini tunapofanya hivyo, tunajua kama magumu ya ulimwengu huu muovu wa Shetani na tamaa mbaya ya mwili wetu wenye zambi vina nguvu, na kwa hiyo vinaweza kuturegeza ili tusimutumikie Mungu kwa moyo wetu wote. (Yer. 17:9; Efe. 2:2) Kwa hiyo, tunapaswa kila mara kuuchunguza moyo wetu ili kuhakikisha kama tungali na tamaa ya kumutumikia Mungu na kama tunafanya angalisho ili tusianguke. Namna gani tunaweza kuuchunguza moyo wetu?

7. Ni nini inayoonyesha hali ya moyo wetu?

7 Kama vile sehemu ya ndani ya muti haionekani, mutu wetu wa ndani pia haonekani. Hata hivyo, katika Mahubiri yake ya Mulimani Yesu alisema kama matunda ya muti yanaonyesha ikiwa muti ni muzuri ao hapana, ni hivyo pia juu ya maisha yetu, mambo tunayofanya yanaonyesha hali ya moyo wetu. (Mt. 7:17-20) Acheni tuzungumuzie matendo hayo.

TUUCHUNGUZE MOYO WETU

8. Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 6:33 yanatusaidia namna gani kujua yale yaliyo katika moyo wetu?

8 Mbele ya hapo katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu aliwaambia wasikilizaji wake mambo ambayo walipaswa kufanya ili kuonyesha kama walikuwa na tamaa kabisa ya kumutumikia Yehova kwa moyo wao wote. Aliwaambia: ‘Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, nanyi mutaongezewa hivi vitu vingine vyote.’ (Mt. 6:33) Kwa kweli, mambo tunayotia pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu ndiyo yanayoonyesha yale tunayotamani katika moyo wetu, yale tunayowaza katika moyo wetu, na mipango iliyo ndani kabisa ya moyo wetu. Kwa hiyo, njia nzuri ya kujua ikiwa tunamutumikia Mungu kwa moyo usiogawanyika ni kuchunguza tu yale tunayotia pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu.

9. Ni aliko gani ambalo Yesu alitolea wanaume fulani, na majibu yao yalionyesha nini?

9 Kisha Yesu kuwatia wafuasi wake moyo ‘waendelee kutafuta kwanza ufalme,’ kulitokea jambo fulani linaloonyesha kama mambo ambayo mutu anatia pa nafasi ya kwanza maishani ndiyo yanaonyesha hali ya moyo wake. Luka, mumoja wa waandikaji wa Injili, alianza kuzungumuzia jambo hilo kwa kusema kwamba Yesu “aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu” ijapokuwa alijua vizuri mambo yatakayomupata huko. Wakati yeye na mitume wake “walipokuwa wakienda barabarani,” Yesu alikutana na wanaume fulani, na alitolea kila mumoja wao aliko hili: ‘Uwe mufuasi wangu.’ Wanaume hao walikuwa tayari kukubali mwaliko wa Yesu, lakini walimuomba Yesu awaache kwanza watimize jambo fulani. Mumoja wao alimujibu Yesu hivi: ‘Niruhusu kwanza niondoke nikamuzike baba yangu.’ Mwingine akasema: “Nitakufuata, Bwana; lakini kwanza niruhusu niwaage watu wa nyumbani mwangu.” (Luka 9:51, 57-61) Tofauti ilionekana wazi kati ya Yesu na wanaume hao. Yesu hakuacha kitu chochote kimuzuie kumutumikia Mungu kwa moyo wote lakini wanaume hao walitoa visababu visivyofaa juu ya mwaliko! Kwa kutia mahangaiko yao mbele ya faida za Ufalme, walionyesha kama hawakuwa tayari kumutumikia Mungu kwa moyo wote.

10. (a) Namna gani tuliitikia mwaliko wa Kristo wa kuwa wafuasi wake? (b) Yesu alitoa mufano gani mufupi?

10 Tofauti na hao wanaume, sisi tumekubali kwa hekima mwaliko wa Yesu wa kuwa wafuasi wake na tunamutumikia Yehova kila siku. Kwa njia hiyo, tunaonyesha namna tunavyojisikia katika moyo wetu kumuhusu Yehova. Hata ikiwa sisi tunaendelea leo kumutumikia Yehova, tunapaswa kila mara kukumbuka kama kuna mambo mengi yanayoweza kugawanya moyo wetu. Ni mambo gani? Katika mazungumuzo hayo hayo pamoja na wale wanaume waliokataa kuwa wanafunzi wake, Yesu alifunua mambo hayo, alipotoa mufano huu: ‘Hakuna mutu ambaye ameweka mukono wake kwenye jembe la ngombe na kutazama mambo yaliyo nyuma anayefaa kwa ajili ya ufalme wa Mungu.’ (Luka 9:62) Mufano huo unatufundisha nini?

JE ‘TUNASHIKAMANA NA MEMA’?

11. Katika mufano wa Yesu, kazi ya mulimaji ilipatwa na nini, na kwa sababu gani?

11 Acheni tuongeze maelezo mengine kwenye mufano huo wa Yesu ili tuuelewe vizuri. Tuwazie mutu anayelima. Ijapokuwa si vibaya, mutu anayelima anaweza kuwaza juu ya watu wa familia yake, marafiki, chakula, muziki, kujifurahisha, na mahali pa kujikinga jua. Kufanya hivyo kunaonyesha kama anatamani sana vitu hivyo. Lakini sasa, kisha tu kulima sehemu fulani ya shamba, tamaa yake juu ya vitu hivyo vyenye kuvutia inakuwa nguvu sana hivi kwamba anageuka ili kutazama “mambo yaliyo nyuma.” Ijapokuwa kungali mengi ya kufanya katika shamba hilo, mulimaji huyo anakengeushwa, na kazi inaharibika. Kwa kweli, bwana wake atakasirika kwa sababu mulimaji huyo alikosa uvumilivu.

12. Mulimaji wa mufano wa Yesu na Wakristo fulani leo wanalingana namna gani?

12 Sasa tulinganishe mufano huo na hali yetu leo. Mulimaji huyo anaweza kufananishwa na Mukristo yeyote anayeonekana kufanya mambo mazuri lakini aliye katika hatari ya kiroho. Kwa kulinganisha, tufikirie ndugu anayepitisha wakati mwingi katika mahubiri. Hata ikiwa anakusanyika na kuhubiri, lakini anaendelea kuwaza sana juu ya mambo fulani ya maisha yenye kuvutia ambayo ulimwengu unatolea . . . watu. Kwa kuwa anawaza sana mambo hayo, kwa hiyo, moyo wake unafikia kuyatamani sana. Mwishowe, kisha kufanya kazi ya kuhubiri kwa miaka mingi, tamaa yake juu ya mambo fulani ya ulimwengu huu inaanza kuwa nguvu sana hivi kwamba anageuka na kutazama “mambo yaliyo nyuma.” Ijapokuwa kungali kazi nyingi ya kufanya katika mahubiri, haendelei tena “kulishika sana neno la uzima,” na utendaji wake wa kiroho unaharibika. (Flp. 2:16) Yehova, “Bwana wa mavuno,” anahuzunishwa sana na hali kama hiyo ya kukosa uvumilivu.​—Luka 10:2.

13. Ili kumutumikia Yehova kwa moyo usiogawanyika haitoshi tu kufanya nini?

13 Somo tunalopata kutokana na mufano huo liko wazi. Kukusanyika kwa ukawaida, na kuhubiri ni mambo yenye kusifiwa. Lakini ndugu ao dada anaweza kufanya mambo hayo bila kumutumikia Yehova kwa moyo wote. (2 Nya. 25:1, 2, 27) Ikiwa Mukristo anaendelea kupenda “mambo yaliyo nyuma” katika moyo wake, yaani, anaendelea kupenda mambo fulani ya maisha ya ulimwengu huu, Mukristo kama huyo anapatikana katika hatari ya kukataliwa na Mungu. (Luka 17:32) Tutakuwa watu wenye ‘kufaa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu’ ikiwa tu ‘tunachukia mabaya, na kushikamana na mema.’ (Rom. 12:9; Luka 9:62) Kwa hiyo, sisi wote tunapaswa kuhakikisha kama tunatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza na kama haturuhusu jambo lolote katika ulimwengu huu wa Shetani liturudishe nyuma na kutuzuia tusimutumikie Yehova kwa moyo wote, hata kama jambo hilo linaonekana kuwa la lazima ao lenye kuvutia.​—2 Kor. 11:14; soma Wafilipi 3:13, 14.

ENDELEA KUKAA MACHO!

14, 15. (a) Namna gani Shetani anajaribu kuharibu hali ya moyo wetu? (b) Toa mufano unaoonyesha kwa nini njia hiyo ya Shetani ni hatari.

14 Ni upendo kwa Yehova ndio uliotuchochea tujitoe kwake. Wengi kati yetu, tangu walipojitoa kwa Mungu, wameonyesha kwa miaka mingi kama wana tamaa ya kuendelea kumutumikia Yehova kwa moyo usiogawanyika. Hata hivyo, tusiwaze kama Shetani amekwisha kuchoka. Angali anavizia moyo wetu. (Efe. 6:12) Kwa kweli, labda anaona kuwa hatuwezi kumuacha Yehova kwa mara moja. Kwa hiyo, anajikaza kwa ujanja kutumia ‘mufumo huu wa mambo’ ao mahangaiko ya mambo ya dunia ili kuregeza polepole bidii yetu kumuelekea Mungu. (Soma Marko 4:18, 19.) Kwa nini amefikia kuangusha wengine kwa kutumia njia hiyo?

15 Ili kujibu ulizo hilo, wazia mufano huu: Unatumia kifagio ili kufagia nyumba yako. Unapomaliza, unaweka kifagio hicho mahali fulani. Kisha wewe kuondoka, mutu mwingine anachukua kifagio hicho na anaondoa miti kumi. Utakapotumia tena kifagio hicho ili kufagia nyumba, je, utajua mara moja kama mutu fulani aliondoa miti fulani? Labda hautajua. Mutu huyo akija tena na kuondoa miti mingine katika kifagio hicho, tuseme miti kumi ao kumi na tano, je, utajua kama aliondoa miti hiyo? Hautajua! Sababu gani? Kwa sababu alikuwa akiondoa kidogo-kidogo. Hivyo hivyo, ulimwengu wa Shetani unaweza kupunguza bidii yetu polepole. Mukristo asipokuwa macho hawezi hata kutambua badiliko hilo linalofanyika polepole.​—Mt. 24:42; 1 Pet. 5:8.

SALA NI YA LAZIMA SANA

16. Namna gani tunaweza kujilinda na njia za udanganyifu za Shetani?

16 Namna gani tunaweza kujilinda na njia hizo za udanganyifu za Shetani na kuendelea kuwa na moyo usiogawanyika kumuelekea Yehova? (2 Kor. 2:11) Sala ni ya lazima sana. Paulo aliwatia moyo waamini wenzake ‘wasimame imara ili kupinga hila za Ibilisi.’ Kisha akawasihi hivi: ‘Kwa kila namna ya sala na dua muendelee kusali kila wakati katika roho.’​—Efe. 6:11, 18; 1 Pet. 4:7.

17. Sala za Yesu zinatufundisha nini?

17 Ili kupambana na Shetani, ni jambo la hekima kumuiga Yesu. Yeye alikuwa akisali kwa ukawaida, na hilo lilionyesha kama alitamani sana kuendelea kuwa na moyo usiogawanyika kumuelekea Yehova. Ona kwa mufano, yale ambayo Luka alisema kuhusu namna Yesu alivyosali usiku mbele auawe: “Akaingia katika maumivu makali, akaendelea kusali kwa bidii zaidi.” (Luka 22:44) Hata mbele ya hapo Yesu alisali kwa bidii, lakini wakati huu, kwa sababu alikuwa akipambana na majaribu makali, alisali “kwa bidii zaidi” na Mungu alijibu sala yake. Mufano wa Yesu unaonyesha kama sala fulani zinaweza kuwa nzito ao za bidii zaidi kuliko zingine. Kwa hiyo, kadiri majaribu yanavyoongezeka na kadiri njia za Shetani zinazidi kuwa za udanganyifu, tunapaswa kusali “kwa bidii zaidi” ili Yehova atulinde.

18. (a) Tunapaswa kujiuliza ulizo gani juu ya sala, na kwa nini? (b) Ni mambo gani yanayoweza kutusaidia ili tulinde moyo wetu? Eleza. (Ona  kisanduku kwenye ukurasa wa 16.)

18 Namna gani sala kama hizo zinaweza kutusaidia? Paulo alisema: “Katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu.” (Flp. 4:6, 7) Ili kuendelea kuwa na moyo usiogawanyika kumuelekea Yehova ni jambo la lazima kusali mara kwa mara. (Luka 6:12) Basi ujiulize, ‘Je, ninasali mara kwa mara na ninafanya hivyo kwa bidii?’ (Mt. 7:7; Rom. 12:12) Jibu lako litaonyesha kama unatamani kabisa kumutumikia Mungu ao hapana.

19. Utafanya nini ili kuendelea kuwa na moyo usiogawanyika kumuelekea Yehova?

19 Kulingana na habari hii tumejifunza kama mambo tunayotia pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu yanaweza kutusaidia sana tujue hali ya moyo wetu. Tunapenda kuhakikisha kama hatuache kitu chochote kiregeze bidii yetu ya kutumikia Yehova kwa moyo usiogawanyika, iwe vitu tulivyoacha nyuma wala njia za udanganyifu za Shetani. (Soma Luka 21:19, 34-36.) Kwa hiyo, kama Daudi, tutaendelea kumusihi Yehova hivi: “Unganisha moyo wangu.”​—Zab. 86:11.

[Maulizo ya Funzo]

[Sanduku katika ukurasa wa 16]

MAMBO MATATU YANAYOWEZA KUTUSAIDIA ILI TULINDE MOYO WETU

Ili moyo wetu wa kawaida uwe na afya nzuri ni lazima kuchukua hatua fulani, ni hivyo hivyo juu ya moyo wetu wa mufano. Tuone mambo matatu ya lazima yanayoweza kutusaidia:

1 Chakula: Moyo wetu unahitaji kulishwa kwa ukawaida na chakula chenye kujenga na kizuri. Vilevile tunapaswa kula chakula cha kutosha na kizuri kupitia funzo la pekee la kawaida, kutafakari, na kuhuzuria mikutano.​—Zab. 1:1, 2; Met. 15:28; Ebr. 10:24, 25.

 2 Mazoezi: Ili kuwa na afya nzuri, wakati mwingine moyo wetu unahitaji kusukuma damu kwa nguvu. Vilevile, kuhubiri kwa bidii—labda kwa kuongeza bidii yetu katika kazi hiyo​—kunafanya moyo wetu wa mufano uwe katika hali nzuri.​—Luka 13:24; Flp. 3:12.

3 Mahali tunapoishi ao kutumika: Kuishi katikati ya watu wasiomuogopa Mungu kunaweza kuharibu moyo wetu wa kawaida na moyo wetu wa mufano. Lakini, tunaweza kuepuka hatari hiyo kwa kuwa pamoja na ndugu na dada zetu mara nyingi iwezekanavyo, wao wanatuhangaikia kabisa na wana mioyo isiyogawanyika kumuelekea Mungu.​—Zab. 119:63; Met. 13:20.