Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari zilizozungumuziwa hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Basi, jaribu kujibu maulizo yanayofuata:

Namna gani mufano wa Sulemani unaweza kuwa onyo kwetu?

Mungu alimubariki Mufalme Sulemani na kumutumia. Hata hivyo, wakati wa utawala wake, Sulemani aliacha kufuata shauri la Mungu. Alimuoa binti mupagani wa Farao, alichukua wanawake wengi, na aliwaacha wanawake wapagani wamuongoze pole pole katika ibada ya uongo. Tunapaswa kuepuka kukomalisha pole pole mawazo ao mielekeo isiyofaa. (Kum. 7:1-4; 17:17; 1 Fal. 11:4-8)​—15/12, ukurasa wa 10-12.

Sababu gani Sara alikuwa kweli mwanamuke aliyemuogopa Mungu na sababu gani alipendwa sana?

Wakati Mungu alimuamuru Abrahamu atoke Uru, hilo lilimaanisha kuacha familia yake, marafiki, na kwenda mahali ambapo hakujua. Hata hivyo, Sara alimuunga mukono na kuwa hakika kama Mungu atamubariki. Alimuheshimu Abrahamu, na kuonyesha sifa nzuri.​—1/1, ukurasa wa 8.

Sababu gani Yehova alimuomba Abrahamu amutoe mwana wake mupendwa kuwa zabihu?

Ni jambo la maana kukumbuka kama Mungu hakumuacha Abrahamu amutoe Isaka kuwa zabihu. Hiyo ilikuwa njia tu ya kuonyesha namna Mungu angemutoa Mwana wake Yesu kuwa zabihu, hata ikiwa kufanya hivyo ilikuwa garama kubwa.​—1/1, ukurasa wa 23.

Ni nini kinachoonyesha kama kuanzia wakati wa mitume na kuendelea, Wakristo watiwa-mafuta fulani wa kweli wamekuwapo duniani?

Katika mufano wa Yesu wa “ngano” na “magugu,” “mbegu nzuri” ilimaanisha “wana wa ufalme.” (Mt. 13:24-30, 38) Ngano ingeendelea kukua ao kukomaa pamoja na magugu mupaka wakati wa mavuno. Kwa hiyo, ijapokuwa hatuwezi kusema kwa uhakika ni nani kabisa waliofananishwa na ngano, lakini sikuzote kumekuwa na watu walio mufano wa ngano mupaka wakati wetu.​—15/1, ukurasa wa 7.

Ni matukio gani yatakayoongoza moja kwa moja kwenye Har-Magedoni?

Mataifa yatatoa tangazo la maana la “Amani na usalama!” (1 Thes. 5:3) Serikali zitashambulia dini za uongo. (Ufu. 17:15-18) Waabudu wa kweli watashambuliwa, jambo litakaloongoza kwenye mwisho.​—1/2, ukurasa wa 9.

Namna gani tunaweza kushinda wivu?

Hatua zinazofuata zinaweza kutusaidia: Ujikaze kuonyesha upendo na shauku ya kindugu, shirikiana na watu wanaomuogopa Mungu, tenda mema, ‘shangilia pamoja na watu wanaoshangilia.’ (Rom. 12:15)​—15/2, ukurasa wa 16-17.

Ni nani wanaozungumuza luga ya Nahuatl, na ni jambo gani linalofanywa kwa ajili yao?

Ilikuwa luga ya Waazteke wa zamani, na luga hiyo ingali inazungumuziwa na watu zaidi ya milioni moja na nusu katika Mexique. Mashahidi wanahubiri katika Nahuatl, na vichapo vyetu fulani vinapatikana katika luga hiyo.​—1/3, ukurasa wa 13-14.

Tunapotolea mutu mashauri, ni kanuni gani tunazopaswa kukumbuka?

Jua hali ya mutu anayeomba shauri. Epuka kujibu haraka. Onyesha unyenyekevu kwa kutumia Neno la Mungu. Inapowezekana, tumia vitabu vya Kikristo. Epuka kuchukulia wengine maamuzi.​—15/3, ukurasa wa 7-9.

Yesu alitia wasikilizaji wake moyo kwenda kilometa ya pili. (Math. 5:41) Alipenda kufundisha nini?

Wakati huo katika Israeli, Waroma walikaza watu kufanya kazi. Kwa kutia moyo wasikilizaji wake waende kilometa ya pili, Yesu alimaanisha kama bila kuchunga kinyongo walipaswa kufanya kazi hizo ambazo watu wenye mamlaka waliwaomba wafanye.​—1/4, ukurasa wa 9.