Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Nilivutiwa Sana na Ndugu na Dada Wenye Kuzeeka

Nilivutiwa Sana na Ndugu na Dada Wenye Kuzeeka

Masimulizi Kuhusu Maisha ya Watu

Nilivutiwa Sana na Ndugu na Dada Wenye Kuzeeka

Elva Gjerde Anaeleza Maisha Yake

Mugeni mumoja alifika kwetu na kumuambia baba yangu maneno fulani ambayo yemefanya maisha yangu yote yabadilike. Kumepita karibu miaka 70 tangu jambo hilo litendeke. Kuanzia siku hiyo ya maana, watu wengine wengi wamefanya maisha yangu yabadilike. Watu hao wamenisaidia kuwa na rafiki wa maana sana katika maisha yangu. Acha niwaelezee.

NILIZALIWA Australie katika muji wa Sydney, mwaka wa 1932. Wazazi wangu waliamini kama Mungu yuko, lakini hawakuwa wakienda kanisani. Mama yangu alinifundisha kama kila siku Mungu ananitazama na kwa hiyo, yuko tayari kunipa malipizi ninapofanya makosa. Hilo lilinifanya niwe na uoga sana juu ya Mungu. Hata hivyo, nilikuwa naipenda sana Biblia. Shangazi yangu alipokuja kututembelea kila Siku ya Posho ao Siku ya Yenga, alinielezea hadisi nyingi za Biblia zenye kufurahisha. Siku zote, nilimungojea kwa hamu.

Nilipokuwa kijana, baba alinisomea vitabu ambavyo mama alipokea kutoka kwa mwanamuke fulani muzee aliyekuwa Shahidi wa Yehova. Baba alifurahia sana mambo aliyosoma katika vitabu hivyo vyenye kufasiria Biblia na kisha akakubali kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi. Mangaribi moja baba alipokuwa akijifunza Biblia, alinikuta nikisikiliza kwa siri mazungumuzo yao. Alitaka niende kulala, lakini ndugu aliyekuwa akijifunza pamoja naye, akasema: “Kwa nini usimuache Elva naye asikilize?” Shauri hilo lilibadilisha maisha yangu na lilinisaidia kuanza urafiki pamoja na Mungu wa kweli, yaani, Yehova.

Kisha siku fulani, baba na mimi tulianza kuhuzuria mikutano. Mambo aliyojifunza yalimuchochea kufanya mabadiliko katika maisha yake. Hata akaanza kuzuia hasira yake alipochokozwa. Hilo liliwachochea mama yangu na kaka yangu, Frank, waanze kuhuzuria mikutano. * Sisi wote, watu ine, tulifanya maendeleo na kisha tukabatizwa. Tangu wakati huo, ndugu na dada wengi wazee walinisaidia kubadilisha maisha yangu kwa njia inayofaa kadiri nilivyokuwa nikikomaa.

KAZI YA UTUMISHI WA WAKATI WOTE

Nilipokuwa kijana, nilivutiwa sana na ndugu na dada wazee wa kutaniko letu. Mumoja wao aliitwa Alice Place, ni yeye aliyekuja kutembelea familia yetu kwa mara ya kwanza. Yeye alikuwa kama nkambo ao tate yangu. Alice alinizoeza katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba na alinitia moyo ili nifikie ubatizo. Nilipokuwa na miaka 15, nilibatizwa.

Pia, nilifanya urafiki sana na wenzi wawili wa ndoa wazee, yaani, Percy na Madge [Margaret] Dunham. Kuwa rafiki yao kulinisaidia sana katika siku za mbele. Kwa kweli, nilipenda hesabu (mathématiques), na nilipenda siku moja niwe mwalimu wa hesabu. Percy na Madge walikuwa wamisionere katika inchi ya Lettonie katika miaka ya 1930. Vita ya Pili ya Ulimwengu ilipoanza katika Ulaya, walienda kutumikia kwenye Beteli ya Australie, iliyopatikana kando kando ya Muji wa Sydney. Percy na Madge walinifurahia sana. Walieleza mambo mengi yenye kupendeza waliyojionea walipokuwa wamisionere. Kwa hiyo, nilitambua kama kufundisha Biblia kungeniletea furaha nyingi kuliko kufundisha hesabu. Basi, nikajiwekea muradi wa kuwa misionere.

Ndugu Percy na dada Madge walinitia moyo nianze upainia ili kujitayarisha kwa ajili ya kazi ya misionere. Kwa hiyo, katika mwaka wa 1948, nikiwa na miaka 16, nilianza kufanya kazi ya upainia pamoja na vijana wengine waliokuwa wamefurahia kazi ya upainia katika kutaniko letu la Hurstville, Sydney.

Kwa kipindi cha miaka ine, nilikuwa painia katika miji mingine 4 iliyopatikana katika Nouvelle​-Galles ya Kusini na Queensland. Mutu wa kwanza ambaye nilijifunza pamoja naye Biblia alikuwa Betty Law (sasa anaitwa Remnant). Alikuwa mukubwa kwangu miaka miwili, na alinipenda sana. Baada ya muda fulani, Betty naye akawa painia na tukatumika pamoja katika muji wa Cowra, uliopatikana kilometa 230 katika sehemu ya mangaribi ya Sydney. Ijapokuwa tulifanya kazi ya upainia kwa kipindi kifupi tu, Betty na mimi tungali marafiki mupaka leo.

Nilipokubaliwa kuwa painia wa pekee, nilitumwa katika muji wa Narrandera uliopatikana kilometa 220 kusini-mangaribi mwa Cowra. Nilianza kufanya upainia pamoja na dada Joy Lennox (sasa anaitwa Joy Hunter), painia mwenye bidii, yeye pia alikuwa mukubwa kwangu miaka miwili. Ni sisi wawili tu ndio tulikuwa Mashahidi katika muji huo. Mimi na Joy tuliishi katika familia ya Ray na Esther Irons, waliokuwa wenzi wa ndoa. Wao pamoja na kijana wao na binti zao watatu walipendezwa na kweli ya Biblia. Katika juma, Ray na kijana wao walifuga kondoo na kulima ngano katika shamba lao lililokuwa mbali na muji, naye Esther pamoja na binti zao watatu walisimamia hoteli yao ndogo. Kila Siku ya Yenga, mimi na Joy tulipika chakula kingi kwa ajili ya familia ya Ray, na wanaume 12 waliopanga katika hoteli yao ndogo; wanaume hao walikuwa wakitumika kwenye njia ya treni, na wote walikuwa na njaa sana. Kazi hiyo ilitusaidia kulipia nusu ya pesa kwa ajili ya chumba chetu. Kisha kusafisha vitu, tuliwapatia Ray na familia yake chakula cha kiroho, yaani, tulijifunza nao Munara wa Mulinzi wa juma hilo. Ray, Esther, na watoto wao wane walikubali kweli na wakawa Mashahidi wa kwanza wa Kutaniko la Narrandera.

Katika mwaka wa 1951, nilihuzuria mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika muji wa Sydney. Kwenye mukusanyiko huo, nilihuzuria mukutano wa pekee kwa ajili ya mapainia wanaopendezwa na kazi ya misionere. Watu zaidi ya 300 walihuzuria mukutano huo uliofanywa katika hema kubwa. Ndugu Nathan Knorr kutoka Beteli ya Brooklyn alitutolea hotuba na akaonyesha kama kuna uhitaji mukubwa wa kupeleka habari njema kila sehemu ya dunia. Tulimusikiliza kwa uangalifu sana. Siku zilizofuata, mapainia wengi waliohuzuria mukusanyiko huo walienda kuhubiri katika sehemu ya Pacifique ya Kusini na maeneo mengine. Nilifurahia sana kuwa mumoja wa wanaume na wanawake 17 walioalikwa kutoka Australie ili kuhuzuria somo la 19 la Masomo ya Gileadi katika mwaka wa 1952. Ndoto yangu ya kuwa misionere ikatimia. Wakati huo nilikuwa na miaka 20.

NILIHITAJI KUBADILISHA MAONI YANGU

Mambo tuliyojifunza na uhusiano niliokuwa nao na wanafunzi wengine kwenye Masomo ya Gileadi viliongeza ujuzi wangu wa Biblia na imani yangu, lakini pia vilinisaidia sana nibadili tabia zangu. Nilikuwa bado kijana na nilipenda kila kitu ninachofanya kiwe kikamilifu, na nilitazamia ukamilifu kwa wengine pia. Nilikuwa mutu mugumu sana. Kwa mufano, nilipomuona Ndugu Knorr akicheza kabumbu pamoja na Wanabeteli vijana, jambo hilo lilinikwaza kabisa.

Walimu wa Masomo ya Gileadi, wenye hekima, walitambua kama nilihitaji musaada. Walipendezwa nami na walinisaidia kubadilisha maoni yangu yasiyofaa. Siku baada ya siku, nikaanza kutambua kama Yehova si Mungu mugumu, na hatazamie ukamilifu kwetu. Wanafunzi wenzangu walinisaidia pia. Nakumbuka mumoja wao akiniambia hivi: “Elva, Yehova hakutazame ili akupe malipizi. Usijitese.” Maneno hayo yaliyo wazi yaligusa moyo wangu.

Tulipomaliza Masomo ya Gileadi, mimi na wanafunzi wenzangu, watu ine, tulitumwa Afrika katika inchi ya Namibie. Kisha muda fulani, tulianza kuongoza mafunzo 80 ya Biblia. Nilifurahia inchi hiyo na maisha yangu ya umisionere. Lakini, tulipendana na ndugu mumoja tuliyesoma naye masomo ya Gileadi, yeye alitumwa Suisse na tukachumbiana. Baada ya kuishi mwaka mumoja katika Namibie, nilienda Suisse kumuona muchumba wangu. Kisha kufunga ndoa, nilikuwa pamoja na bwana yangu katika kutembelea makutaniko, kwa sababu alikuwa mwangalizi wa muzunguko.

MAGUMU NILIYOPATA

Baada ya kufurahia miaka mitano katika kazi ya muzunguko, tulialikwa kwenye Beteli ya Suisse. Nilipokuwa Beteli, nilifurahia sana kutumika pamoja na ndugu na dada wengi wenye kukomaa kimwili na kiroho.

Kisha muda fulani, nilipatwa na huzuni sana. Nilivumbua kama bwana yangu hakuwa mwaminifu kwangu na kwa Yehova. Basi, aliniacha. Nilivurugika sana. Ikiwa marafiki wangu waliokomaa wa familia ya Beteli hawangenitegemeza na kunionyesha upendo, sijui ningeishia wapi. Walinisikiliza nilipotaka kuongea na waliniacha nipumuzike nilipohitaji kutuliza akili. Maneno yao yenye kutia moyo na matendo yao ya upendo yalinisaidia nivumilie uchungu huo mukubwa, na yalinisaidia nimukaribie Yehova zaidi.

Nilikumbuka pia maneno ambayo ndugu na dada wazee walinielezea miaka mingi iliyopita, magumu waliyopambana nayo na namna yalivyoimarisha imani yao. Kwa mufano, nilikumbuka maneno ya dada Madge Dunham. Siku moja aliniambia hivi: “Elva, utakutana na majaribu mengi unapomutumikia Yehova, labda hata wale unaowapenda sana ndio watakaokuletea magumu zaidi. Wakati kama huo, umukaribie Yehova zaidi. Usisahau kama ni Yehova unayetumikia, wala si wanadamu!” Shauri la Madge lilinisaidia wakati wote wa magumu hayo. Niliamua kama sitaacha hata kidogo makosa ya bwana yangu yavunje urafiki wangu na Yehova.

Kisha muda fulani, niliamua kurudi Australie ili nifanye kazi ya upainia karibu na jamaa yangu. Tulipokuwa tukisafiri katika Bahari, nilianzisha mazungumuzo ya Biblia pamoja na watu fulani tuliosafiri nao. Kati yao kulikuwa mwanaume mumoja mutulivu kutoka Norvège aliyeitwa Arne Gjerde. Alifurahia mambo aliyosikia. Muda fulani baadaye, Arne alikuja kuniona mimi na jamaa yetu katika muji wa Sydney. Alifanya maendeleo ya haraka na akawa Shahidi. Katika mwaka wa 1963, tulioana na kisha miaka miwili nikazaa mutoto mwanaume anayeitwa Gary.

MAGUMU MENGINE

Arne, Gary, na mimi tulikuwa na maisha ya familia yenye furaha. Siku zilizofuata, Arne alipanua nyumba yetu ili wazazi wangu waliozeeka waje kuishi pamoja nasi. Kisha miaka sita ya ndoa, tulipatwa na tatizo kubwa sana. Arne alipatwa na ugonjwa wa kansere ya ubongo. Nilifika kwenye hospitali kila siku ili kumuona alipokuwa akitiwa katika mashini ya kutunza kansere. Alijisikia vizuri kwa wakati fulani, kisha hali yake ikawa mbaya zaidi na akaanza kupoteza ufahamu. Muganga aliniambia kama bwana yangu ataishi tu kwa majuma machache. Lakini, alipona. Kisha alirudi nyumbani; niliendelea kumushugulikia na kisha akajisikia vizuri kabisa. Akaanza kutembea na akawa tena muzee wa kutaniko. Kwa kuwa alikuwa mutu mwenye furaha sikuzote na alipenda kuchekesha sana, hilo lilimusaidia apone na ilikuwa rahisi kwangu kuendelea kumutunza.

Baadaye, katika mwaka wa 1986, Arne akaanza tena kujisikia vibaya. Wakati huo wazazi wangu walikuwa wamekufa, kwa hiyo tulihamia eneo nzuri la milima inje ya muji wa Sydney, karibu na marafiki wetu. Kisha wakati fulani, Gary, mutoto wetu, alioa dada mwenye sifa za kiroho aliyeitwa Karin, nao walipenda tuishi katika nyumba moja. Kisha miezi fulani, sisi wote tukahamia katika nyumba moja karibu tu na mahali ambapo Arne na mimi tulikuwa tunaishi.

Kwa kipindi cha miezi 18 kilichotangulia kifo chake, Arne hakutoka kitandani na alihitaji matunzo kwa uangalifu. Kwa kuwa nilipitisha wakati wote nyumbani, nilijifunza kila siku Biblia na vitabu vyetu kwa muda wa saa mbili. Nilipokuwa nikijifunza, nilipata mashauri mengi kuhusu namna ya kupambana na magumu yangu. Pia, wengi kati ya ndugu na dada wazee wa kutaniko letu waliopambana na magumu kama yangu, walikuja kututembelea. Ziara zao zilinituliza. Mwezi wa 4, 2003, Arne alikufa akiwa na tumaini kama siku moja ataweza kufufuliwa.

MUTEGEMEZAJI WANGU MUKUBWA ZAIDI

Nilipokuwa kijana, nilitazamia kila kitu kifanyike kama ninavyopenda. Lakini, nilikuja kutambua kama katika maisha mambo hayatokei tu kama tunavyotazamia. Nimepata baraka nyingi na nimevumilia majaribu mawili makubwa: Kupoteza wenzi wawili wa ndoa; mumoja kwa sababu hakuwa mwaminifu na mwingine kwa sababu ya magonjwa. Miaka yote hiyo, nimepata muongozo na faraja kupitia njia nyingi. Hata hivyo, Yehova Mungu, anayeitwa ‘Muzee wa siku’ ndiye amekuwa mutegemezaji wangu mukubwa zaidi. (Dan. 7:9) Mashauri yake yamebadilisha tabia zangu na yamenisaidia kupata baraka nyingi katika kazi ya umisionere. Nilipopata magumu, ‘fazili za Yehova zenye upendo zilinitegemeza na faraja zake ziliikumbatia nafsi yangu.’ (Zab. 94:18, 19) Nimefurahia pia upendo na utegemezo wa jamaa yangu na wa ‘marafiki wa kweli waliozaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.’ (Met. 17:17) Wengi wao walikuwa ndugu na dada wazee wenye hekima.

Yobu aliuliza hivi: ‘Je, hekima haimo katikati ya wazee na uelewaji katika wingi wa siku?’ (Ayu. 12:12) Ninapofikiri juu ya maisha yangu ninaweza kusema kabisa kuwa maneno hayo ni ya kweli. Mashauri ya ndugu na dada wazee wenye hekima yamenisaidia, na faraja yao imenitegemeza. Kweli kabisa, urafiki wao umeniletea baraka nyingi. Mimi ni mwenye shukrani kwao kwa sababu nilivutiwa nao.

Sasa mimi pia nimezeeka, nina miaka 80. Mambo ambayo nimejionea yamenifanya mimi pia niwahangaikie sana ndugu na dada wazee. Ningali ninapenda kuwatembelea na kuwasaidia. Lakini, ninafurahia pia kuwa rafiki ya vijana. Nguvu yao inasisimua, na ninapendezwa kabisa na shauku yao. Vijana wanapokuja kuniomba muongozo na musaada, ninafurahi sana kuwasaidia.

[Maelezo ya chini]

^ Frank Lambert, kaka yake na Elva, alikuja kuwa painia mwenye bidii katika vijiji vya Australie. Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1983, kwenye ukurasa wa 110-112, kinaeleza safari zake zenye kusisimua za mahubiri.

[Picha katika ukurasa wa 14]

Nilipokuwa painia pamoja na dada Joy Lennox katika muji wa Narrandera

[Picha katika ukurasa wa 15]

Elva na familia ya Beteli ya Suisse katika mwaka wa 1960

[Picha katika ukurasa wa 16]

Ninamushugulikia Arne alipokuwa mugonjwa