Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Ni wakati gani Uingereza na Amerika ilikuja kuwa Serikali Kubwa ya saba ya ulimwengu kulingana na unabii wa Biblia?

▪ Sanamu kubwa ambayo Mufalme Nebukadneza alilota haifananishe serikali zote za ulimwengu. (Dan. 2:31-45) Sanamu hiyo inafananisha tu serikali kubwa tano zilizotawala tangu siku za Danieli na kuendelea, na zilizowatesa watu wa Mungu kwa njia fulani ya pekee.

Maelezo ya Danieli ya sanamu kubwa hayaonyeshe kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ingeshinda Roma, lakini yanaonyesha kama serikali hiyo ingetokana na Roma. Danieli aliona chuma ikianzia sehemu ya juu kidogo ya magoti mupaka kwenye vidole vya miguu. (Katika sehemu hiyo chuma inachangana na udongo.) * Hiyo inaonyesha kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ingetokana na miguu ya chuma. Jambo hilo linahakikishwa na namna mambo yalivyotokea katika historia ya wanadamu. Mwishoni mwa miaka ya 1700, Uingereza, iliyokuwa sehemu ya Utawala wa Roma ilianza kupata nguvu. Baadaye, Amerika ikapata uhuru na kuanza kutegemewa. Hata hivyo, serikali ya saba ya ulimwengu, ilikuwa haijatokea. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu serikali za Uingereza na Amerika zilikuwa hazijaanza kutumika pamoja kwa njia ya pekee. Zilianza kutumika pamoja wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu.

Wakati huo, “wana wa ufalme” walikuwa wakihubiri zaidi sana katika Amerika, na makao yao makuu yalikuwa katika Brooklyn, New York. (Mt. 13:36-43) Wakristo watiwa​-mafuta waliendelea kuhubiri kwa bidii katika inchi zilizotawaliwa na Utawala wa Uingereza. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali za Uingereza na Amerika zilifanya mapatano ya pekee ili kupigana na maadui wao. Tena, kwa sababu kila mutu alipaswa kuonyesha roho ya kuipenda sana inchi yake wakati huo wa vita, serikali hizo zilianza kuwachukia wale waliokuwa sehemu ya uzao wa ‘mwanamuke’ wa Mungu. Zilikataza vitabu vyao visichapishwe na kugawanywa na ziliwafunga wale waliokuwa wakisimamia kazi ya kuhubiri.​—Ufu. 12:17.

Unabii wa Biblia unaonyesha kama serikali kubwa ya ulimwengu ya saba haikuanza kutawala mwishoni mwa miaka ya 1700, wakati serikali ya Uingereza ilipoanza kupata nguvu. Lakini, serikali hiyo ilitokea mwanzoni mwa siku ya Bwana. *

[Maelezo ya chini]

^ Udongo unaochangana na chuma unafananisha sehemu ao mambo mengine yenye kuleta mugawanyiko mahali pote ambapo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika, iliyo kama chuma, inapotawala. Kwa miaka mingi, udongo huo umefanya Serikali hiyo ipoteze uwezo wake wa kutenda.

^ Mafasiriyo haya ni maelezo mapya yakilinganishwa na yale yaliyo katika kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli ukurasa wa 57, paragrafe ya 24, na picha kwenye ukurasa wa 56 na 139.

[Picha katika ukurasa wa 19]

Katika mwezi wa 6, 1918, ndugu wanane walioishi kwenye makao makuu ya Mashahidi wa Yehova walifungwa