Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Ni ‘Mufunuaji wa Siri’

Yehova Ni ‘Mufunuaji wa Siri’

Yehova Ni ‘Mufunuaji wa Siri’

‘Kwa kweli Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme na Mufunuaji wa siri.’​—DAN. 2:47.

UNAWEZA KUJIBU NAMNA GANI?

Yehova ametufunulia mambo gani ya wakati ujao?

Vichwa sita vya kwanza vya munyama-mwitu vinafananisha nini?

Ni sehemu gani za munyama​-mwitu na za sanamu ya Nebukadneza ambazo zinalingana?

1, 2. Yehova ametufunulia mambo gani, na sababu gani alitufunulia mambo hayo?

 WAKATI Ufalme wa Mungu utakuja kuvunja serikali za dunia, ni serikali gani zitakazokuwa zikitawala? Tunajua jibu. Yehova Mungu, ‘Mufunuaji wa siri,’ ametufunulia hilo. Ametusaidia kuelewa serikali hizo kupitia unabii wa Danieli na wa Yohana.

2 Katika maono, Yehova aliwaonyesha wanyama mbalimbali waliotokea moja baada ya nyingine. Tena, Danieli aliona sanamu kubwa na Yehova alimufunulia maana ya maono ya sanamu hiyo. Yehova aliandikisha mambo hayo katika Biblia kwa faida yetu. (Rom. 15:4) Alifunua mambo hayo ili imani yetu iwe nguvu na ili tujue kama karibuni Ufalme wake utaharibu serikali zote za wanadamu.​—Dan. 2:44.

3. Ili kuelewa vizuri unabii wa Danieli na wa Yohana, tunapaswa kujua nini kwanza, na sababu gani?

3 Unabii wa Danieli na wa Yohana unataja wafalme wanane, ao utawala wa wanadamu, na pia unaonyesha namna wafalme hao wangefuatana. Hata hivyo, ili kuelewa vizuri unabii huo ni lazima tujue vizuri maana ya unabii wa kwanza wa Biblia. Sababu gani? Kwa sababu unabii wote ulio katika Biblia unapatana na unabii huo. Tunaweza kulinganisha unabii wa kwanza wa Biblia na kamba inayounganisha kila unabii wa Biblia.

UZAO WA NYOKA NA MUNYAMA-MWITU

4. Ni nani wanaounda uzao wa mwanamuke, nao uzao huo utafanya nini?

4 Kisha tu uasi uliotokea katika Edeni, Yehova aliahidi kama ‘mwanamuke’ angetokeza “uzao.” * (Soma Mwanzo 3:15.) Mwishowe, uzao huo ungeponda kichwa cha Shetani. Kisha, Yehova alifunua kama uzao huo ungetokea kupitia familia ya Abrahamu, katika taifa la Israeli, katika kabila la Yuda, na katika kizazi cha Daudi. (Mwa. 22:15-18; 49:10; Zab. 89:3, 4; Lu. 1:30-33) Yesu Kristo ndiye sehemu ya kwanza ya uzao huo. (Gal. 3:16) Sehemu ya pili ya uzao huo inaundwa na Wakristo watiwa-mafuta wa kutaniko la Kikristo. (Gal. 3:26-29) Yesu na Wakristo hao watiwa-mafuta ndio wanaounda Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali ambayo Mungu atatumia ili kumuharibu Shetani.​—Lu. 12:32; Rom. 16:20.

5, 6. (a) Danieli na Yohana walizungumuzia serikali ngapi kubwa? (b) Vichwa vya munyama-mwitu vinavyozungumuziwa katika Ufunuo, vinafananisha nini?

5 Unabii huo wa kwanza uliotolewa katika Edeni ulionyesha pia kama Shetani angetokeza “uzao.” Na kungekuwa uadui, ao chuki kati ya uzao wa Shetani na uzao wa mwanamuke. Ni nani wanaofanyiza uzao wa nyoka? Ni wale wote wanaomuiga Shetani kwa kumuchukia Mungu ao watu wake. Katika historia ya wanadamu, Shetani amefanya uzao wake utokeze serikali za kila namna, ao falme nyingi. (Lu. 4:5, 6) Lakini, ni serikali fulani tu kati ya serikali hizo ambazo zimewatesa watu wa Mungu: taifa la Israeli ao Wakristo watiwa​-mafuta. Jambo hilo linatusaidia kuelewa nini? Jambo hilo linatusaidia kuelewa kwa nini maono ya Danieli na Yohana yanataja serikali kubwa munane tu hata ikiwa kulikuwako na serikali zingine zilizotawala ulimwenguni.

6 Kisha miaka elfu mbili hivi, Yesu aliyefufuliwa alimuonyesha mutume Yohana maono mengi yenye kushangaza sana. (Ufu. 1:1) Katika moja ya maono hayo, Yohana aliona joka mukubwa akisimama juu ya muchanga wa bahari kubwa. Joka huyo ni Shetani. (Soma Ufunuo 13:1, 2.) Tena, Yohana aliona munyama wa kuogopesha akitoka katika bahari hiyo; Shetani alimupatia munyama huyo mamlaka makubwa. Baadaye, malaika alimuambia Yohana kama vichwa saba vya yule munyama mwenye rangi nyekendu, ambaye ni sanamu ya yule munyama anayezungumuziwa katika Ufunuo 13:1, vinafananisha “wafalme saba” ao serikali saba. (Ufu. 13:14, 15; 17:3, 9, 10) Yohana alipokuwa akiandika maono hayo, wafalme watano walikuwa wameanguka, mumoja alikuwa angali anatawala na mwingine alikuwa “hajafika bado.” Hizo ni serikali gani ao mamlaka gani makubwa ya ulimwengu? Acheni tujifunze maana ya kila kichwa cha munyama anayetajwa katika Ufunuo. Tutajifunza pia namna maelezo ya nabii Danieli yalivyotoa habari zaidi juu ya serikali hizo miaka mingi mbele zianze kutawala.

VICHWA VIWILI VYA KWANZA —MISRI NA ASIRIA

7. Kichwa cha kwanza kinafananisha nini, na sababu gani hicho ndicho kichwa cha kwanza?

7 Kichwa cha kwanza cha munyama kinafananisha Ufalme wa Misri. Ufalme wa Misri ulikuwa serikali kubwa ya kwanza ulimwenguni kuwachukia watu wa Mungu. Wazao wa Abrahamu ambao wangetokeza uzao ulioahidiwa walizidi kuongezeka katika inchi ya Misri. Kisha, Ufalme huo wa Misri ukaanza kuwatesa Waisraeli. Shetani alitaka kuwaangamiza watu wa Mungu mbele ili uzao huo usitokee. Namna gani? Kwa kumuchochea Farao awaue watoto wote wanaume wa Waisraeli. Yehova hakuruhusu jambo hilo litokee na aliwakomboa Waisraeli katika utumwa wa Misri. (Kut. 1:15-20; 14:13) Kisha akawapeleka Waisraeli katika Inchi ya Ahadi.

8. Kichwa cha pili kinafananisha nini, na kilijaribu kufanya nini?

8 Kichwa cha pili cha munyama kinafananisha serikali ya Asiria. Ufalme huo wenye nguvu ulijaribu pia kuwaangamiza watu wa Mungu. Kwa kweli, Yehova alitumia Asiria ili kuazibu ufalme wa makabila kumi ya Israeli kwa sababu ya uasi wao na ibada ya sanamu. Lakini, baadaye Asiria ilishambulia Yerusalemu. Inaonekana kama Shetani alitafuta kuangamiza kizazi ambacho kingetokeza Mufalme, Yesu Kristo. Yehova hakutaka majeshi ya Asiria yaharibu Yerusalemu, kwa hiyo aliharibu majeshi ya Asiria na kuwakomboa watu wake.​—2 Fal. 19:32-35; Isa. 10:5, 6, 12-15.

KICHWA CHA TATU—BABILONI

9, 10. (a) Yehova aliwaruhusu Wababiloni wafanye nini? (b) Ni mambo gani ambayo yalipaswa kutokea ili unabii utimie?

9 Kichwa cha tatu kinafananisha ufalme ambao muji wake mukubwa ulikuwa Babiloni. Yehova aliruhusu Wababiloni waharibu Yerusalemu na kuwapeleka watu wake wafungwa huko Babiloni. Mbele ya kutokea kwa uharibifu huo, Yehova aliwaonya Waisraeli waasi kama musiba huo ungewapata. (2 Fal. 20:16-18) Yehova aliwaambia Waisraeli kama hataruhusu tena kizazi cha wafalme wao walioketi juu ya ‘kiti chake cha ufalme’ huko Yerusalemu waendelee kufanya hivyo. (1 Nya. 29:23) Lakini, Yehova aliahidi pia kama kungekuwa muzao wa Mufalme Daudi aliye na “haki ya kisheria,” ambaye angekuja na kuketi juu ya kiti cha ufalme cha Yehova.​—Eze. 21:25-27.

10 Unabii mwengine ulionyesha kama wakati Masiya, ao Mutiwa​-mafuta atafika, Wayahudi watakuwa wangali wanaabudu katika hekalu la Yerusalemu. (Dan. 9:24-27) Unabii mwengine ulioandikwa mbele Waisraeli wapelekwe Babiloni, ulionyesha kama Masiya angezaliwa Bethlehemu. (Mika 5:2) Ili unabii huo mbalimbali utimie, iliomba Wayahudi watoke Babiloni, warudi katika inchi yao na wajenge tena hekalu. Lakini, Wababiloni walijulikana kuwa watu wasioachilia wafungwa. Kwa hiyo, namna gani watu wa Mungu wangerudi kwao? Yehova alifunulia manabii wake jambo ambalo angefanya.​—Amo. 3:7.

11. Utawala wa Babiloni ulifananishwa na nini? (Soma maelezo yaliyo chini kwenye ukurasa wa 10.)

11 Nabii Danieli alikuwa kati ya wafungwa waliopelekwa Babiloni. (Dan. 1:1-6) Yehova alimuonyesha serikali kubwa za ulimwengu ambazo zingetokea kisha serikali ya Babiloni kuanguka. Yehova alitumia mifano mbalimbali ili kufunua siri hizo. Kwa mufano, alimufanya Mufalme Nebukadneza wa Babiloni aote ndoto na katika ndoto hiyo Yehova alimuonyesha sanamu kubwa yenye sehemu mbalimbali. (Soma Danieli 2:1, 19, 31-38.) Kupitia nabii wake Danieli, Yehova alifunua kama kichwa cha zahabu cha sanamu hiyo kilifananisha Utawala wa Babiloni. * Kifua na mikono ya feza vilifananisha serikali kubwa ya ulimwengu ambayo ingetokea kisha ile ya Babiloni. Hiyo ingekuwa serikali gani, na ingewatendea namna gani watu wa Mungu?

KICHWA CHA INE​—UTAWALA WA WAMEDE NA WAPERSE

12, 13. (a) Yehova alifunua mambo gani juu ya kuanguka kwa Utawala wa Babiloni? (b) Sababu gani tunaweza kusema kama utawala wa Wamede na Waperse unafananishwa kabisa na kichwa cha ine cha munyama-mwitu?

12 Zaidi ya miaka mia moja mbele ya siku za Danieli, Yehova alimutolea nabii Isaya maelezo juu ya utawala wa ulimwengu ambao ungeangusha utawala wa Babiloni. Yehova alionyesha namna muji wa Babiloni ungeharibiwa na pia jina la kiongozi ambaye angeshinda Babiloni. Kiongozi huyo aliitwa Sirisi ao Koreshi, Muperse. (Isa. 44:28–45:2) Danieli aliona maono mengine mawili kuhusu Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Wamede na Waperse. Katika maono ya kwanza, ufalme huo ulifananishwa na dubu aliyeinuliwa upande mumoja. Munyama huyo aliruhusiwa ‘kula nyama nyingi.’ (Dan. 7:5) Katika maono mengine, Danieli aliona utawala huo wenye sehemu mbili ukifananishwa na kondoo-dume mwenye pembe mbili.​—Dan. 8:3, 20.

13 Yehova alitumia utawala wa Wamede na Waperse kushinda Babiloni na kuwarudisha Waisraeli katika inchi yao kama alivyoahidi. (2 Nya. 36:22, 23) Lakini, baadaye utawala huohuo ulijaribu kuwaangamiza watu wa Mungu. Kitabu cha Esta kinaeleza makusudi mabaya ya waziri mukubwa wa Waperse aliyeitwa Hamani. Alifanya mupango wa kuwaangamiza Wayahudi wote walioishi katika utawala huo wa Waperse na aliweka tarehe ya maangamizi hayo makubwa. Yehova aliwakomboa tena watu Wake na chuki ya Shetani juu ya uzao. (Esta 1:1-3; 3:8, 9; 8:3, 9-14) Kwa hiyo, tunaweza kusema kama Utawala wa Waperse unafananishwa kabisa na kichwa cha ine cha munyama-mwitu anayetajwa katika kitabu cha Ufunuo.

KICHWA CHA TANO—UGIRIKI

14, 15. Ni mambo gani ambayo Yehova alifunua juu ya Utawala wa Ugiriki?

14 Katika kitabu cha Ufunuo kichwa cha tano cha munyama-mwitu kinafananisha Ugiriki (Grèce). Alipofasiria ndoto ya Nebukadneza, Danieli alionyesha kama utawala huohuo unafananishwa na tumbo na kiuno cha sanamu. Danieli alipokea tena maono mawili yaliyokuwa na maelezo zaidi juu ya ufalme wa Ugiriki na mutawala wake mwenye nguvu zaidi.

15 Katika moja ya maono hayo, Danieli aliona ufalme wa Ugiriki ukifananishwa na chui aliyekuwa na mabawa mane, hilo lilionyesha kama utawala huo ungeshinda kwa uharaka falme zingine. (Dan. 7:6) Katika maono mengine, Danieli alieleza namna mbuzi​-dume mwenye pembe kubwa alivyovunja​-vunja kondoo​-dume mwenye pembe mbili, maana yake, Utawala wa Wamede na Waperse. Yehova alimuambia Danieli kama mbuzi​-dume huyo alifananisha Utawala wa Ugiriki na pembe kubwa ilifananisha mumoja wa wafalme wa utawala huo. Danieli alionyeshwa pia kama pembe hiyo kubwa ingevunjika, na pembe ine ndogo zingesimama mahali pa pembe hiyo kubwa. Hata ikiwa unabii huo uliandikwa mamia ya miaka mbele ya kutokea kwa Utawala wa Ugiriki, maelezo yote ya unabii huo yalitimia kabisa. Mufalme mwenye nguvu zaidi wa Ugiriki, Alexandre le Grand, alishambulia Utawala wa Wamede na Waperse. Pembe hiyo kubwa ilivunjika wakati mufalme huyo mwenye nguvu zaidi alikufa kwa gafula akiwa tu na umri wa miaka 32. Kisha, majenerali wake wane wakagawanyana utawala huo.​—Soma Danieli 8:20-22.

16. Mufalme Antiokisi wa 4 alifanya nini?

16 Kisha kushinda Waperse, Ugiriki ilianza kutawala watu wa Mungu. Wakati huo Wayahudi walikuwa wamekwisha rudi katika inchi yao na kujenga tena hekalu la Yerusalemu. Waisraeli walikuwa bado wachaguliwa wa Mungu na walikuwa wangali wakimuabudu Yehova katika hekalu ambalo walijenga upya, mahali ambapo Yehova alikubali aabudiwe. Hata hivyo, katika kipindi cha kuanzia mwaka wa 101 mupaka mwaka wa 200 mbele ya Kristo, Ugiriki, ni kusema, kichwa cha tano cha munyama​-mwitu, iliwashambulia watu wa Mungu. Mufalme Antiokisi wa 4, aliyekuwa mumoja wa wale walioriti utawala uliogawanyika wa Alexandre, alijenga mazabahu ya kipagani katika uwanja wa hekalu la Yerusalemu na akasema kama mutu yeyote atakayefuata dini ya Wayahudi anapaswa kufa. Uzao wa Shetani ulichukia kabisa watu wa Mungu. Lakini, baadaye utawala mwingine ulichukua nafasi ya Utawala wa Ugiriki. Ni utawala gani ambao ungefananishwa na kichwa cha sita cha munyama-mwitu?

KICHWA CHA SITA​—ROMA, ‘YENYE KUOGOPESHA NA YENYE KUTISHA’

17. Kichwa cha sita kilitimiza sehemu gani ya maana ya unabii wa Mwanzo 3:15?

17 Roma ilikuwa serikali kubwa ya ulimwengu wakati Yohana alipokea maono ya munyama​-mwitu. (Ufu. 17:10) Roma ilikuwa kichwa cha sita cha munyama​-mwitu na ilitimiza sehemu ya maana ya unabii wa Mwanzo 3:15. Shetani alitumia watawala wa Roma ili kuumiza kwa muda uzao “kwenye kisigino.” Namna gani? Walimushitaki Yesu kwa uongo kwa kusema kama aliwachochea watu waasi utawala wao na wakamutundika juu ya muti. (Mt. 27:26) Lakini, kidonda hicho kilipona bila kukawia kwa sababu Yehova alimufufua Yesu.

18. (a) Yehova alichagua taifa gani jipya, na sababu gani? (b) Namna gani uzao wa nyoka uliendelea kuchukia uzao wa mwanamuke?

18 Viongozi wa dini ya Wayahudi walisikilizana na watawala wa Roma ili kumuua Yesu, na Waisraeli wengi walimukataa. Kwa hiyo, Yehova alikataa taifa hilo la Israeli. (Mt. 23:38; Mdo. 2:22, 23) Kisha, akajichagulia taifa jipya, “Israeli wa Mungu.” (Gal. 3:26-29; 6:16) Taifa hilo lilikuwa kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, na liliundwa na Wayahudi na Watu wa Mataifa. (Efe. 2:11-18) Kisha kifo na ufufuo wa Yesu, uzao wa nyoka uliendelea kuchukia sana uzao wa mwanamuke. Mara nyingi, Roma ilijaribu kuangamiza sehemu ya pili ya uzao wa mwanamuke, yaani, kutaniko la Kikristo. *

19. (a) Danieli anafasiria namna gani utawala wa sita wa ulimwengu? (b) Habari nyingine itajibu maulizo gani?

19 Katika ndoto ambayo Danieli alimufasiriya Nebukadneza, Roma ilifananishwa na miguu ya chuma. (Dan. 2:33) Danieli aliona tena utawala mwengine ambao ungetokana na utawala wa Roma. (Soma Danieli 7:7, 8.) Kwa miaka mingi, Roma ilikuwa ‘yenye kuogopesha na yenye kutisha na yenye nguvu isiyo ya kawaida’ kuliko maadui wake. Hata hivyo, unabii ulionyesha kama “pembe kumi” zingetokea katika utawala huo na pembe nyingine, iliyokuwa ndogo, ingekuwa na nguvu kuliko zingine zote. Pembe hizo kumi zinafananisha nini, na pembe ndogo inafananisha nini? Ni sehemu gani ya sanamu kubwa ya Nebukadneza ambayo inalingana na pembe hiyo ndogo? Habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 14 itajibu maulizo hayo.

[Maelezo ya chini]

^ Mwanamuke huyo anafananisha tengenezo la Yehova la malaika waaminifu. Biblia inalinganisha tengenezo hilo na muke wa Yehova.​—Isa. 54:1; Gal. 4:26; Ufu. 12:1, 2.

^ Katika kitabu cha Danieli, Utawala wa Babiloni unafananishwa na kichwa cha sanamu na pia katika kitabu cha Ufunuo utawala huo unafananishwa na kichwa cha tatu cha munyama​-mwitu. Ona kisanduku kwenye ukurasa wa 12-13.

^ Hata ikiwa Roma iliharibu Yerusalemu katika mwaka wa 70, huo haukuwa utimizo wa Mwanzo 3:15. Kwa sababu wakati huo, Israeli haikuwa tena taifa chaguliwa la Mungu.

[Maulizo ya Funzo]