Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ndoto Yangu Imetimia” _

“Ndoto Yangu Imetimia” _

“Ndoto Yangu Imetimia” _

Miaka 15 iliyopita, dada Emilia alikuwa painia wa kawaida. Lakini, alilazimika kusimamisha utumishi huo. Katika miaka ya hivi karibuni, alikuwa akikumbuka namna alivyokuwa mwenye furaha sana alipokuwa painia, na alipenda kupitisha tena wakati mwingi katika utumishi. _

Kazi ya kimwili ya dada Emilia ilimuchukua wakati mwingi, na hivyo hakuwa na furaha. Wakati fulani, mbele ya wafanyakazi wenzake, alisema hivi kwa uchungu: “Sipendi tena kutumika kwa saa nyingi!” Mukubwa wa kazi alisikia yale aliyosema, basi akamuuliza ikiwa mambo ambayo amesema ni kweli. Emilia akamuhakikishia kama ni kweli. Lakini, ili jambo hilo liwezekane iliomba musimamizi wa kazi akubali, kwa kuwa, kulingana na kanuni za kompanyi hiyo, wafanyakazi wote waliombwa kutumika sana. Dada yetu alijitayarisha ili kukutana na musimamizi na akasali ili azungumuze naye bila woga na akiwa mwenye kutulia.

Walipokutana na musimamizi, dada Emilia, kwa hekima lakini pia bila woga, aliomba wamupunguzie saa za kutumika. Alimuelezea kama anapenda kutumia wakati huo ili kuwasaidia wengine: “Mimi ni Shahidi wa Yehova, na ninasaidia watu wajue Neno la Mungu. Siku hizi, watu wengi wanakuwa na mwenendo mubaya sana. Watu wana lazima ya kujua mwenendo unaomufurahisha Mungu, kwa hiyo mashauri ya hekima ya Biblia ninayowatolea ni ya lazima sana kwao. Sipendi kazi hiyo inichokeshe sana hivi kwamba ninapokuja kufanya kazi nisifanye kazi vizuri, lakini pia ninapenda kuwa na wakati wa kusaidia watu. Ndiyo maana ninapenda munipunguzie saa zangu za kazi.”

Musimamizi alimusikiliza kwa uangalifu na akasema kama wakati fulani yeye pia alifikiria kazi ya kuwasaidia watu wanaoteseka. Kisha akasema: “Sababu unazotoa zinafanya nikubali ombi lako. Lakini, je, unajua kama utapata sasa feza kidogo?” Dada Emilia akamujibu kama anajua hilo na kama atalazimika kurahisisha maisha yake. Dada Emilia akaongeza: “Muradi wangu wa kwanza ni kufanya jambo fulani litakalosaidia watu.” Musimamizi akamuambia: “Ninapendezwa sana na watu wanaotoa wakati wao juu ya wengine.”

Ilikuwa ni mara ya kwanza mufanyakazi kupokea pendeleo kama hilo katika kompanyi hiyo. Dada Emilia sasa anaruhusiwa kutumika siku ine tu katika juma. Alishangaa kuona kama hakupunguziwa mushahara! Basi akasema: “Ndoto yangu imetimia, na ninaweza kurudilia kazi yangu ya upainia wa kawaida!”

Je, umekwisha kufikiria kutengeneza programu yako ili kuanza ao kurudilia kazi ya upainia?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 32]

Musimamizi akamuambia: “Ninapendezwa sana na watu wanaotoa wakati wao juu ya wengine”