Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Nitamuogopa Nani?’

‘Nitamuogopa Nani?’

‘Nitamuogopa Nani?’

‘Vita vijapozuka juu yangu, bado nitakuwa na tegemeo wakati huo.’​—ZAB. 27:3.

KULINGANA NA MAANDIKO HAYA, NI JAMBO GANI LINALOWEZA KUKUSAIDIA USIOGOPE?

Zaburi 27:1

Zaburi 27:4

Zaburi 27:11

1. Zaburi ya 27 itatusaidia tuelewe nini?

 SABABU gani kazi ya kuhubiri inaendelea kuwa na matokeo mazuri ijapokuwa hali za ulimwengu zinaendelea kuharibika sana? Kwa nini tunafurahi kutumia wakati wetu na nguvu zetu ili kuhubiri ijapokuwa watu wengi wana matatizo ya kifeza? Kwa kuwa watu wengi wanaogopa wakati ujao, nini itatusaidia tusiwe na woga kama wao? Wimbo wa Mufalme Daudi, ulioongozwa na roho ya Mungu, unaopatikana katika Zaburi ya 27, unajibu maulizo hayo.

2. Hofu ao kuogopa sana kunaweza kumufanya mutu ajisikie namna gani, lakini sisi tuna tumaini gani?

2 Wimbo huo wa Daudi unaanza hivi: ‘Yehova ni nuru yangu na wokovu wangu. Nitamuogopa nani? Yehova ni ngome ya uhai wangu. Nitamuhofu nani?’ (Zab. 27:1) Ni kweli hofu ao kuogopa sana kunaweza kumufanya mutu akose nguvu ya kufanya jambo fulani. Lakini, mutu anayemuogopa ao kumutumainia Yehova hapaswe kuwa na hofu. (1 Pet. 3:14) Wakati tunamufanya Yehova kuwa ngome yetu, ‘tutakaa salama wala hatutasumbuliwa na hofu ya musiba.’ (Met. 1:33; 3:25) Sababu gani?

“YEHOVA NI NURU YANGU NA WOKOVU WANGU”

3. Yehova ni nuru yetu katika maana gani, lakini sisi wenyewe tunapaswa kufanya nini?

3 Biblia inasema hivi: “Yehova ni nuru yangu.” Andiko hilo linamulinganisha Yehova na nuru ili kuonyesha kama yeye anatukomboa kutoka katika ujinga na giza la kiroho. (Zab. 27:1) Mwangaza unaweza kutusaidia kuona hatari ao kizuizi fulani, lakini hauwezi kuondoa hatari hiyo. Ni sisi wenyewe tunaopaswa kutenda kwa hekima tunapoona hatari. Vivyo hivyo, Yehova anatusaidia kuelewa maana ya hali za ulimwengu. Anatuonyesha hatari zilizo katika ulimwengu huu. Anatupatia kanuni za Biblia zilizo za hekima kila siku, lakini ni sisi tunaopaswa kutumikisha mambo tunayojifunza. Tukifuata mashauri hayo, tutakuwa na hekima, kama mutunga​-zaburi aliyekuwa na hekima kuliko maadui wake na walimu wake.​—Zab. 119:98, 99, 130.

4. (a) Kwa nini Daudi angeweza kusema hivi bila kusita: ‘Yehova ni wokovu wangu’? (b) Yehova atakuwa wokovu wetu wakati gani hasa?

4 Maneno ya Daudi kwenye Zaburi 27:1 yanaonyesha kama alikumbuka namna Yehova alivyomukomboa ao kumuokoa katika hatari nyingi. Kwa mufano, Yehova alimuokoa “kutoka katika makucha ya simba na kutoka katika makucha ya dubu.” Yehova pia alimusaidia ashinde Goliathi. Baadaye, Mufalme Sauli alijaribu kumuua kwa mukuki, lakini kila mara Yehova alimuokoa. (1 Sam. 17:37, 49, 50; 18:11, 12; 19:10) Kwa kweli Daudi angeweza kusema hivi bila kusita: ‘Yehova ni wokovu wangu’! Yehova atawaokoa watumishi wake kama alivyomuokoa Daudi. Wakati gani? Yehova atafanya hivyo hasa wakati wa ile ‘ziki kubwa.’​—Ufu. 7:14; 2 Pet. 2:9.

KUMBUKA KILA WAKATI YEHOVA ALIPOKUSAIDIA

5, 6. (a) Kukumbuka namna Yehova ametusaidia kunatusaidia namna gani kutokuwa na woga? (b) Tutapata faida gani ikiwa tunakumbuka namna Yehova alivyowasaidia watumishi wake?

5 Jambo la maana linaloweza kutufanya tusiwe na woga linaonyeshwa katika Zaburi 27:2, 3. (Soma.) Daudi alikumbuka kila jambo ambalo Yehova alimufanyia ili kumuokoa. (1 Sam. 17:34-37) Mambo hayo ambayo hakusahau yalimupa nguvu ya kushindana na majaribu makubwa zaidi. Je, wewe pia unajisikia mwenye nguvu unapokumbuka mambo ambayo Yehova alikufanyia? Kwa mufano, je, kuna siku ulimuomba Yehova sana ili akusaidie ushindane na tatizo fulani lililokusumbua sana na kisha ukaona namna alivyokupatia hekima na nguvu ya kupambana nalo? Ao je, unaweza kukumbuka namna Yehova alivyokusaidia kuondoa jambo lililokukosesha furaha ya kuhubiri ao namna alivyokufungulia mulango mukubwa unaoongoza kwenye utendaji zaidi? (1 Kor. 16:9) Kukumbuka mambo hayo kunaweza kukusaidia namna gani? Kukumbuka hilo kunapaswa kukusadikisha kama Yehova anaweza kukusaidia kushinda ao kuvumilia matatizo makubwa zaidi, sivyo?​—Rom. 5:3-5.

6 Tunaweza kuogopa ikiwa guvernema fulani yenye nguvu inafanya mupango wa kuwaangamiza Mashahidi wote wa Yehova? Viongozi wengi walijaribu kufanya hivyo katika siku zilizopita, lakini hawakuweza. Tukikumbuka namna Yehova amewasaidia watu wake katika siku zilizopita, hatutaogopa matatizo yanayoweza kutokea wakati ujao​—Dan. 3:28.

FURAHIA IBADA SAFI

7, 8. (a) Kulingana na Zaburi 27:4, Daudi alimuomba Yehova nini? (b) Hekalu kubwa la kiroho la Yehova ni nini, na namna gani tunaabudu katika hekalu hilo?

7 Kupenda sana ibada safi ni jambo lingine la lazima sana linaloweza kutufanya tusiogope. (Soma Zaburi 27:4.) Katika siku za Daudi, hema ya ibada ilikuwa ndio “nyumba ya Yehova.” Daudi ndiye aliyetayarisha kila kitu ili mwana wake Sulemani amujengee Yehova hekalu kubwa. Miaka mingi baadaye, Yesu alionyesha kama hekalu hiyo iliyobarikiwa na Mungu haikuwa tena ya lazima ili mutu amuabudu Yehova katika njia anayoikubali. (Yoh. 4:21-23) Katika kitabu cha Waebrania sura ya 8 mupaka ya 10, mutume Paulo alionyesha ya kama hekalu kubwa la kiroho lilitokezwa wakati wa ubatizo wa Yesu katika mwaka wa 29. Wakati huo, Yesu alijitoa kwa Yehova ili kufanya mapenzi yake. (Ebr. 10:10) Hekalu hilo kubwa la kiroho ni mupango ambao Yehova amefanya ili tuweze kumuabudu kwa njia anayokubali, maana yake, kuwa na imani katika zabihu ya ukombozi ya Yesu. Namna gani tunaabudu katika hekalu hilo? Tunafanya hivyo kwa kusali “tukiwa na mioyo ya kweli katika uhakikisho kamili wa imani;” kwa kutangaza waziwazi tumaini letu bila kuyumba​-yumba; na kwa kufikiria, kuchochea na kutia moyo waabudu wenzetu tunapokusanyika pamoja na pia wakati wa ibada ya familia. (Ebr. 10:22-25) Kufurahia mipango ambayo Yehova amefanya kuhusiana na ibada safi kunatupatia nguvu ya kumutumikia katika siku hizi za mwisho zenye hatari.

8 Katika dunia yote, watumishi waaminifu wa Yehova wanaendelea kuhubiri zaidi na zaidi, wanajifunza luga zingine na wanahamia mahali ambako kuna uhitaji mukubwa wa wahubiri. Kama mutunga-zaburi, wanaonyeha kupitia matendo yao kama wanataka kumuomba Yehova jambo moja tu. Wanataka kufurahia uzuri wa Yehova na kumutolea utumishi mutakatifu hata hali iwe namna gani.​—Soma Zaburi 27:6.

TEGEMEA MUSAADA WA MUNGU

9, 10. Maneno ya Zaburi 27:10 yanatupatia uhakika gani?

9 Tena Daudi anaonyesha kama alikuwa anategemea sana musaada wa Yehova. Alisema hivi: “Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha,Yehova mwenyewe angenichukua.” (Zab. 27:10) Tunaposoma 1 Samweli sura ya 22 tunaona kama wazazi wa Daudi hawakumuacha. Hata hivyo, ndugu na dada wengi leo wamekataliwa kabisa na familia zao. Lakini, kutaniko la Kikristo limewasaidia na kuwatunza kwa upendo.

10 Kwa kuwa Yehova iko tayari kutegemeza watumishi wake wanaokataliwa na familia zao, hilo linaonyesha kama atawategemeza pia wanapopambana na matatizo mengine, sivyo? Kwa mufano, ikiwa tuna wasiwasi kuhusu namna ya kutosheleza mahitaji ya familia yetu, tunapaswa kukumbuka kama Yehova atatusaidia (Ebr. 13:5, 6) Yehova anaelewa hali na anajua mahitaji ya watumishi wake wote waaminifu.

11. Ikiwa tunamutumaini kabisa Yehova, hilo linaweza kuwafanya watu waseme nini juu yetu? Toa mufano.

11 Fikiria mufano wa Victoria, huko Liberia. Alipokaribia kubatizwa, mwanaume aliyekuwa akiishi naye alimuacha yeye na watoto watatu. Hakuwa na nyumba wala kazi, lakini aliendelea kufanya maendeleo ya kiroho. Kisha Victoria kubatizwa, binti yake wa miaka 13 aliokota mufuko uliojaa pesa. Victoria na binti yake waliamua kutohesabu pesa hizo ili wasishawishiwe. Basi, walifanya haraka ili kuzungumuza na mutu aliyepoteza pesa hizo, alikuwa askari. Askari huyo aliwaambia kama ikiwa watu wote wangekuwa waaminifu kama Mashahidi wa Yehova, dunia ingekuwa mahali bora pa kuishi na penye amani. Victoria alitumia Biblia ili kumuonyesha askari huyo kama Yehova ametuahidi dunia mupya. Askari huyo alishangaa kuona uaminifu wa Victoria na akamupatia zawadi kutokana na pesa hizo. Bila shaka, Mashahidi wa Yehova wanaamini kabisa kama Yehova anaweza kuwatimizia mahitaji yao na wanajulikana mahali pote kuwa ni watu wenye kuaminika kabisa.

12. Tunapoendelea kumutumikia Yehova hata tuwe katika ukosefu, hilo litaonyesha nini? Toa mufano.

12 Tuzungumuzie mufano wa Thomas, muhubiri asiyebatizwa huko Sierra Leone. Alianza kufundisha katika masomo moja ya segondari, lakini aliimwa mushahara wake kwa kipindi cha karibu mwaka moja mupaka wakati angemaliza kazi zote alizopaswa kufanya. Na aliombwa afanye nini tena ili alipwe mushahara wake? Alipaswa kwanza kuwa na mazungumuzo pamoja na mukubwa wa masomo ambaye ni padiri. Padiri huyo alimuambia Thomas kama mafundisho ya Mashahidi wa Yehova hayakubaliwe kwenye masomo hayo. Akamuambia achague kati ya kazi na imani yake. Thomas alikubali kuacha kazi hiyo na mushahara wake, na akapata kazi nyingine ya kutengeneza radio na telefone zenye kuharibika. Mufano huu na mifano mingine kama hiyo inaoonyesha kama tukimutumaini Yehova, hatuwezi kuogopa hata kidogo kama tukipoteza kazi tutakuwa wakosefu. Lakini, sisi tunajua kama Yehova atatimiza mahitaji yetu kwa sababu yeye ndiye Muumbaji wa vitu vyote na ni yeye anayewalinda watumishi wake.

13. Kazi ya kuhubiri inaendelea namna gani katika inchi masikini?

13 Wahubiri wa Ufalme wanaendelea kuhubiri kwa bidii katika inchi nyingi ambako hali ya maisha ni ngumu. Sababu gani? Biro moja ya tawi iliandika hivi: “Watu wengi wanaokubali kujifunza Biblia hawana kazi na kwa hiyo, wana wakati mwingi wa kujifunza. Pia, ndugu wana wakati mwingi wa kuhubiri. Watu wanaoishi katika inchi zenye umasikini sana, wanakubali mara moja kama tunaishi katika siku za mwisho; si lazima uwaambie jambo hilo.” Misionere moja ambaye ametumikia kwa miaka 12 katika inchi ambako kila muhubiri anaongoza mafunzo zaidi ya tatu aliandika hivi: “Wahubiri wengi wana maisha ya chini sana, hawana vitu vingi vinavyoweza kuwakengeusha akili. Kwa hiyo, wana wakati mwingi wa kuhubiri na kuongoza mafunzo ya Biblia.”

14. Namna gani Mungu anaweza kulinda umati mukubwa wa watumishi wake?

14 Yehova ameahidi kama atasaidia, atalinda, na ataokoa watumishi wake wote ao tengenezo lake kutokana na hatari za kimwili na za kiroho, na tunatumaini kama atafanya hivyo. (Zab. 37:28; 91:1-3) Watu watakaookoka ile ‘ziki kubwa’ watakuwa kweli umati mukubwa. (Ufu. 7:9, 14) Yehova ataulinda umati huo; hakuna mutu atakayeangamiza watumishi wake wote kwa ujumla katika siku hizi za mwisho zinazobaki. Yehova atawapa kila kitu wanachohitaji ili kuvumilia majaribu na kulinda urafiki wao pamoja naye. Pia, kuanzia mwanzo mupaka mwisho kabisa wa ziki kubwa, Yehova atawalinda watu wake.

“UNIFUNDISHE NJIA YAKO, EE YEHOVA”

15, 16. Tunapata faida gani tunapotii uongozi wa Mungu? Toa mufano.

15 Ili tuendelee kuwa na ujasiri, ni lazima tuendelee kufundishwa njia za Mungu. Daudi alisali hivi: “Unifundishe njia yako, Ee Yehova, Na uniongoze katika njia ya unyoofu kwa sababu ya adui zangu.” (Zab. 27:11) Tunaweza kuishi kulingana na sala hiyo ikiwa tunakuwa waangalifu ili kuona na kutii mara moja uongozi wowote unaotegemea Biblia ambao Yehova anatutolea kupitia tengenezo lake. Ndugu wengi ambao walifuata shauri lenye hekima la kuwa na maisha rahisi wamelipa madeni yao na kuuzisha vitu vyao ambavyo hawakuhitaji. Jambo hilo liliwasaidia sana wasiwe na mahangaiko mengi ya feza wakati huu ulimwengu unaendelea kupigwa na matatizo ya kifeza. Kuliko kujisumbua na kutafuta vitu ambavyo hawana uwezo wa kupata, wanakuwa na wakati mwingi wa kuhubiri zaidi. Kila mumoja wetu anahitaji kujiuliza hivi: “Je, ninatumia bila kusita mashauri ninayosoma katika Biblia na katika vitabu vya mutumwa mwaminifu na mwenye busara, hata ikiwa wakati mwengine jambo hilo linaweza kuomba kujinyima?”​—Mt. 24:45.

16 Tukikubali Yehova atufundishe na atuongoze katika njia ya uadilifu, hatutakuwa na sababu ya kuogopa. Painia moja wa kawaida huko États-Unis alipoomba apewe kazi ambayo ingemusaidia yeye na familia yake nzima kufanya kazi ya upainia, mukubwa wake wa kazi alimuambia kama hawezi kupewa kazi hiyo kwa sababu hana diplome ya masomo ya juu. Ukijikuta katika hali hiyo, je, utaanza kujuta kwa nini ulifuatia utumishi wa wakati wote kuliko kusoma masomo ya juu? Kisha majuma mawili, mukubwa huyo aliondoshwa na yule aliyechukua nafasi yake akamuuliza ndugu yetu juu ya miradi yake. Ndugu akamuambia kama yeye na bibi yake ni mapainia ao wahubiri wa wakati wote, na wangependa kuendelea kufanya hivyo. Mbele ya ndugu huyo kuongeza jambo lolote, mukubwa huyo wa kazi akamuambia: “Ninaajua kama Mashahidi wa Yehova ni watu tofauti. Baba yangu alipokaribia kufa, Mashahidi wawili walimutembelea kila siku na kumusomea Biblia. Nilipoona hilo niliahidi kama ikiwa siku moja nitakuwa na nafasi ya kumusaidia mumoja wa Mashahidi wa Yehova, basi nitafanya hivyo.” Siku iliyofuata, ndugu yetu alipewa kazi ambayo mukubwa wake wa kazi wa zamani alimukatalia. Kwa kweli, ikiwa tunaweka faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu, Yehova atatutimizia ahadi yake; ameahidi kama hatakosa kututimizia mahitaji yetu ya kimwili.​—Mt. 6:33.

NI LAZIMA TUWE NA IMANI NA TUMAINI

17. Ni nini itakayotusaidia tuendelee kupambana na matukio yoyote bila hofu?

17 Daudi anakazia pia ulazima wa kuwa na imani na tumaini. Alisema hivi: ‘Kama nisingalikuwa na imani katika kuuona wema wa Yehova katika inchi ya walio hai!’ (Zab. 27:13) Unafikiri maisha yetu yangekuwa namna gani ikiwa hatungekuwa na tumaini ambalo Mungu ametutolea na ikiwa hatungejua mambo yanayozungumuziwa katika Zaburi 27? Kwa hiyo, acheni tuendelee kumuomba Yehova atupatie nguvu na kutuokoa ili tuendelee kupambana na matukio yoyote mupaka kwenye Har-magedoni.​—Soma Zaburi 27:14.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 23]

Daudi alipata nguvu kwa kukumbuka namna Yehova alivyomuokoa zamani

[Picha katika ukurasa wa 25]

Matatizo ya kifeza yanayoupiga ulimwengu yanaweza kututolea nafasi ya kuhubiri zaidi, sivyo?