Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anakusanya Tena Familia Yake

Yehova Anakusanya Tena Familia Yake

Yehova Anakusanya Tena Familia Yake

‘Nawasihi kuushika umoja wa roho.’​—EFE. 4:1, 3.

UNGEJIBU NINI?

Usimamizi wa Mungu una kusudi gani?

Namna gani tunaweza ‘kuushika umoja wa roho’?

Ni nini kitatusaidia ‘kuwa wenye fazili’?

1, 2. Yehova ana kusudi gani juu ya dunia na wanadamu?

 FAMILIA! Unaposikia neno hilo unafikiria nini? Je, unafikiria mahali penye upendo na furaha? Unafikiria watu wa familia wanaotumika pamoja ili kufikia muradi fulani? Ao unafikiria mahali fulani penye amani ambapo mutu anaweza kufurahia kukomalia, kujifunza, na kuelezea wengine mawazo yake? Unaweza kuwaza hivyo ikiwa unaishi katika familia inayokujali. Yehova yeye mwenyewe ndiye aliyeanzisha familia. (Efe. 3:14, 15) Kusudi lake lilikuwa: viumbe vyake vyote mbinguni na duniani viwe familia moja yenye usalama, yenye kutumainiana, na yenye umoja wa kweli.

2 Adamu na Eva walipofanya zambi, wao na wanadamu wengine wote ambao wangezaliwa baadaye hawakuwa tena sehemu ya familia ya Mungu. Lakini, hilo halikuzuia kusudi la Mungu la kuona siku fulani dunia inajaa na watoto wa Adamu na Eva. (Mwa. 1:28; Isa. 45:18) Amefanya matayarisho yote yanayohitajiwa ili kutimiza kusudi hilo. Kitabu cha Waefeso kinazungumuzia mipango fulani ambayo Mungu amechukua na zaidi sana kinazungumuzia umoja. Sasa, tuzungumuzie maandiko fulani kutoka katika kitabu hicho cha Waefeso, na kisha tuone namna tunavyoweza kuunga mukono kusudi la Yehova la kuunganisha familia yake.

USIMAMIZI NA NAMNA UNAVYOFANYA KAZI

3. Usimamizi wa Mungu unaozungumuziwa kwenye Waefeso 1:10 unamaanisha nini, na kazi ya kwanza iliyofanywa na usimamizi huo ilianza wakati gani?

3 Musa aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja.’ (Kum. 6:4) Yehova anatenda siku zote kulingana na kusudi lake. Kwa hiyo, “kwenye kikomo kamili cha nyakati zilizowekwa rasmi,” Mungu ameweka “usimamizi,” ni kusema, mupango wa kuunganisha viumbe vyake vyote vyenye akili. (Soma Waefeso 1:8-10.) Usimamizi huo utatimiza kusudi lake katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza: kuwatayarisha Wakristo watiwa-mafuta watakaoishi mbinguni chini ya uongozi wa Yesu Kristo, aliye Kichwa chao. Jambo hilo lilianza siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33, wakati Yehova alianza kukusanya wale ambao watatawala pamoja na Kristo mbinguni. (Mdo. 2:1-4) Kwa kuwa Wakristo watiwa-mafuta wameonyesha imani katika zabihu ya ukombozi ya Kristo, Yehova anawatangaza ao anawaona kuwa wenye haki wanaostahili kupata uzima. Kwa hiyo, wanatambua kama wamefanywa kuwa “watoto wa Mungu.”​—Rom. 3:23, 24; 5:1; 8:15-17.

4, 5. Usimamizi wa Mungu unatimiza kazi gani katika sehemu yake ya pili?

4 Sehemu ya pili: kutayarisha wale watakaoishi katika Paradiso duniani wakiongozwa na Ufalme wa Kristo. Ule ‘Umati mukubwa’ ndio sehemu ya kwanza ya wale watakaoishi duniani. (Ufu. 7:9, 13-17; 21:1-5) Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja, wale watakaofufuliwa watakuja kujiunga nao. (Ufu. 20:12, 13) Wazia namna ufufuo utakavyoonyesha kama tuko katika umoja ao tumeunganishwa! Mwishoni mwa ile miaka elfu moja, “vitu vilivyo duniani,” maana yake, watumishi wa Yehova walio duniani, watapata jaribu la mwisho. Wale watakaobaki waaminifu watafanywa kuwa “watoto wa Mungu” wa duniani.​—Rom. 8:21; Ufu. 20:7, 8.

5 Leo kazi hiyo ya usimamizi wa Mungu ya kutayarisha wale watakaoishi mbinguni na wale watakaoishi duniani inaendelea vizuri. Kwa hiyo, namna gani kila mumoja wetu anaweza kuunga mukono usimamizi huo wa Mungu?

TUNAPASWA ‘KUSHIKA UMOJA WA ROHO’

6. Ni Maandiko gani yanayoonyesha kama Wakristo wanapaswa kukusanyika pamoja?

6 Maandiko yanaonyesha kama Wakristo wanapaswa kukusanyika pamoja. (1 Kor. 14:23; Ebr. 10:24, 25). Umoja wa kweli unatia ndani mambo mengi kuliko tu kukusanyika pamoja kama watu wanaokusanyika katika soko ao kwenye uwanja wa michezo. Ili tuwe na umoja wa kweli, tunapaswa kutumia maagizo ya Yehova na kuacha roho yake itubadilishe kabisa.

7. Namna gani tunaonyesha kama ‘tunaushika umoja wa roho’?

7 Kwa musingi wa zabihu ya ukombozi wa Kristo, Yehova amewatangaza ao anawaona Wakristo watiwa-mafuta kuwa wanye haki na kuwafanya kuwa wana wake, na wale wa kondoo wengine anawatangaza ao kuwaona kuwa wenye haki na kuwafanya kuwa rafiki zake. Hata hivyo, kutoelewana kunaweza kutokea kati yetu kwa sababu tunaishi katika ulimwengu huu muovu. (Rom. 5:9; Yak. 2:23) Ikiwa sivyo, haingekuwa lazima Neno la Mungu liendelee kutushauria kama tuendelee ‘kuvumiliana.’ Tunapaswa kufanya nini ili kuishi kwa umoja na ndugu na dada zetu? Ni lazima tuonyeshe “unyenyekevu kamili wa akili na upole.” Zaidi ya hayo, Paulo anatutia moyo tujikaze sana “kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Soma Waefeso 4:1-3.) Tunaonyesha kama tunatumikisha shauri hilo kwa kujiacha tuongozwe na roho ya Mungu na kuiacha izae tunda lake ndani yetu. Tunda hilo la roho linatufanya tumalize kutokuelewana kunakoweza kutokea na kuishi kwa umoja, lakini matendo ya mwili yanawatenganisha siku zote watu.

8. Matendo ya mwili yanaongoza watu kwenye migawanyiko namna gani?

8 “Matendo ya mwili” yanaongoza kwenye migawanyiko. Namna gani? (Soma Wagalatia 5:19-21.) Uasherati unamutenganisha mutu na Yehova na kutaniko, na uzini unaweza kuwatenganisha watoto na wazazi wao, pia unaweza kumutenganisha mutu aliyefanya uzinzi huo na mwenzi wake wa ndoa asiye na kosa. Uchafu unaharibu urafiki wa mutu pamoja na Mungu na watumishi wake wanaomupenda. Mutu ambaye amejaribu kuunganisha vitu viwili pamoja kwa kutumia gundi (colle) anajua kama sehemu zote mbili zinapaswa kuwa safi ili zikamatane vizuri. Mutu anapojiingiza katika mwenendo mupotovu anaonyesha kama anazarau kabisa sheria za Mungu. Matendo mengine ya mwili ambayo hatuzungumuzie hapa yanamutenganisha mutu na Wakristo wengine na yanamutenganisha pia na Mungu. Matendo hayo hayapatane hata kidogo na sifa za Yehova.

9. Namna gani tunaweza kujichunguza sisi wenyewe ili kuona ikiwa tunajikaza “kuushika umoja wa roho”?

9 Kwa hiyo, kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Ninajikaza kabisa “kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani”? Ninatenda namna gani matatizo yanapotokea kati yangu na ndugu ao dada fulani? Je, ninaelezea​-elezea marafiki wangu matatizo hayo ili waniunge mukono? Je, ninatazamia wazee watatue matatizo yangu pahali pangu ao mimi mwenyewe najikaza ili kurudisha amani kati yangu na ndugu yangu ao dada yangu? Je, ninawaepuka wengine ao kujitenga nao ili tusiweze kuzungumuzia matatizo yetu?’ Ikiwa tunafanya hivyo, je, tunaweza kusema kama tunaunga mukono kusudi la Yehova la kukusanya tena pamoja vitu vyote katika Kristo?

10, 11. (a) Kwa nini ni jambo la lazima sana kuishi kwa amani pamoja na ndugu na dada zetu? (b) Tunapaswa kufanya nini ili kuwe na amani kati yetu na wengine na kupata baraka za Yehova?

10 Yesu alisema hivi: ‘Basi, ikiwa unaleta zawadi yako kwenye mazabahu na hapo unakumbuka kwamba ndugu yako ana jambo fulani juu yako, acha zawadi yako hapo mbele ya mazabahu, na uende zako; kwanza fanya amani yako pamoja na ndugu yako, na ndipo, ukiisha kurudi, itoe zawadi yako. Uwe tayari kusuluhisha mambo upesi.’ (Mt. 5:23-25) Yakobo aliandika kwamba “mbegu ya tunda la uadilifu hupandwa chini ya hali zenye amani kwa wale wanaofanya amani.” (Yak. 3:17, 18) Kwa hiyo, ikiwa hatuishi kwa amani na wengine mambo tunayofanya hayawezi kuwa ya haki.

11 Tuchukue mufano. Katika maeneo ya vita, wakaaji wengi ambao wangelima sehemu kubwa ya udongo wanaogopa kulima kwa sababu ya bombe zinazotegwa katika udongo. Bombe inapolipuka walimaji wanakimbia na kuacha mashamba yao, wezi wanakuja kuiba chakula katika vijiji, na hivyo watu wanakosa chakula. Vivyo hivyo, hatuwezi kufanya maendeleo ya kiroho ikiwa tuna tabia fulani zinazovuruga amani kati yetu na ndugu ao dada zetu. Lakini, tukiwa wenye kusamehe wengine haraka na ikiwa tunatafuta faida ya wengine, tutakuwa na amani na tutapata baraka za Yehova.

12. Wazee wanaweza kutusaidia namna gani ili tuishi kwa umoja?

12 Pia, wazee ambao ni “zawadi katika wanadamu” wanaweza kutusaidia kuishi kwa umoja. Mungu aliwaweka katika kutaniko ili watusaidie kufikia “umoja katika imani.” (Efe. 4:8, 13) Wazee wanapotumika pamoja nasi katika utumishi mutakatifu na wanapotupatia mashauri yanayotegemea Neno la Mungu; wanatusaidia kusonga mbele katika kuvaa utu mupya. (Efe. 4:22-24) Unaposhauriwa na wazee, je, unajua kama ni njia ambayo Yehova anatumia ili kukutayarisha kwa ajili ya uzima katika dunia mupya itakayoongozwa na Mwana wake? Ninyi wazee, je, munajaribu kuwasaidia wengine mukijua kama Yehova anawatumia kwa kusudi hilo?—Gal. 6:1.

‘MUWE WENYE FAZILI’

13. Ikiwa ndugu ao dada alikataa kutii shauri lililo katika andiko la Waefeso 4:25-32, hilo linaweza kuwa na matokeo gani?

13 Andiko la Waefeso 4:25-29 linaonyesha mambo tunayopaswa kuepuka. Mambo hayo ni: kusema uongo, kuwa na gazabu ao kuwa wavivu, na kusema maneno yaliyooza. Kuliko kujiendesha hivyo ni vizuri kusema mambo mazuri na yenye kutia moyo. Ikiwa mutu anakataa kutumikisha shauri hilo, basi anaweza kukasirisha roho ya Mungu kwa sababu roho hiyo ni nguvu inayochochea watu wawe na umoja. (Efe. 4:30) Ili kuwe amani na umoja, ni jambo pia la lazima kufuata shauri hili lingine la Mutume Paulo: ‘Uchungu wote wenye uovu na hasira na gazabu na kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu pamoja na ubaya wote. Bali iweni wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mukisameheana kwa hiari kama vile Mungu pia kupitia Kristo alivyowasamehe ninyi kwa hiari.’​—Efe. 4:31, 32.

14. (a) Maneno “iweni wenye fazili” yanaonyesha nini? (b) Ni nini kitatusaidia kuwa wenye fazili?

14 Maneno “iweni wenye fazili” yanaonyesha kama wakati fulani labda hatukuwatendea wengine kwa fazili na kwa hiyo inaomba kuwatendea kwa fazili ao wema. Inafaa tujifunze kusikiliza mawazo ya wengine ao kuona namna wanavyojisikia kuliko kujifikiria tu. (Flp. 2:4) Labda jambo fulani tunalotaka kusema litawachekesha watu na kuonyesha kama sisi tuna akili. Lakini je, jambo hilo litaonyesha kama sisi ni wenye fazili? Ikiwa tunafikiri mbele ya kusema, jambo hilo litatusaidia kuwa ‘wenye fazili.’

JIFUNZE KUWA NA UPENDO NA HESHIMA KATIKA FAMILIA

15. Kulingana na andiko la Waefeso 5:28, waume wanapaswa kumuiga Kristo kuhusu jambo gani?

15 Biblia inalinganisha uhusiano wa Kristo na kutaniko na uhusiano ulio kati ya bwana na bibi. Hilo linatukumbusha namna bwana anapaswa kuongoza, kupenda na kuhangaikia bibi yake, pia namna bibi anapaswa kujitiisha kwa bwana yake. (Efe. 5:22-33) Mutume Paulo aliandika: “Vivyo hivyo waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.” Alimaanisha nini kwa kusema “vivyo hivyo”? (Efe. 5:28) Maneno ambayo Paulo alitangulia kusema yanaonyesha namna “Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake, ili alitakase, akilisafisha na kuliosha kwa maji kwa njia ya neno.” Kwa kweli, ili kuunga mukono kusudi la Yehova la kuvikusanya vitu vyote katika Kristo, mume anapaswa kuwa mwangalifu ili atimize mahitaji ya kiroho ya familia yake.

16. Matokeo yanaweza kuwa nini wazazi wanapotimiza vizuri madaraka yao katika familia?

16 Wazazi wanapaswa kukumbuka kama daraka wanalotimiza ni daraka walilopewa na Yehova. Inasikitisha kuona kwamba leo, wazazi wengi katika dunia, hawana “upendo wa asili.” (2 Tim. 3:1, 3) Baba wengi wamekimbia madaraka yao na hilo linakuwa na matokeo mabaya juu ya watoto wao. Lakini, mutume Paulo aliwashauri baba Wakristo hivi: ‘Musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’ (Efe. 6:4) Ni katika familia ndiyo kwa mara ya kwanza watoto wanajifunza juu ya upendo na kuheshimu mamlaka. Wazazi wanaofundisha watoto wao mambo haya, wanaunga mukono kusudi la Yehova la kuwaunganisha watu wote. Tunapojikaza ili nyumba yetu iwe mahali palipo na upendo, mahali ambapo hakuna hasira wala matusi; watoto wetu wanajifunza mambo ya lazima sana katika maisha, wanajua namna ya kuonyesha upendo na kuheshimu mamlaka. Jambo hilo linawatayarisha watoto wetu kuishi katika dunia mupya ya Mungu.

17. Ili kumupinga Ibilisi, tunapaswa kufanya nini?

17 Ni lazima tukumbuke kama ni Ibilisi aliyekuwa wa kwanza kuvuruga amani ya ulimwengu wote, kwa hiyo, ataendelea kutupinga ili tusifanye mapenzi ya Mungu. Kwa kweli, makusudi ya Shetani yanatimia; leo, watu wengi wanavunja ndoa, watu wanaishi pamoja bila kufunga ndoa, na ndoa kati ya wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake inakubaliwa. Sisi hatupaswe kuiga tabia na mielekeo ya watu wa dunia hii. Kristo ndiye mufano wetu. (Efe. 4:17-21) Kwa hiyo, tunatiwa moyo ‘tuvae mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu’ ili kumupinga Shetani na mashetani wake.​—Soma Waefeso 6:10-13.

“ENDELEENI KUTEMBEA KATIKA UPENDO”

18. Ni nini siri ya umoja wetu wa Kikristo?

18 Sisi tuna umoja wa Kikristo, na siri yetu ni upendo. Tukiwa na mioyo inayojaa upendo kwa ‘Bwana wetu mumoja,’ ‘Mungu wetu mumoja,’ na kwa ndugu na dada zetu, tunaazimia “kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Efe. 4:3-6) Yesu alisali kwa ajili ya upendo kama huo. Alisali hivi: ‘Ninawaombea, si hawa tu, bali pia wale wanaoniamini kupitia neno lao; ili wote wapate kuwa kitu kimoja, kama vile ambavyo wewe, Baba, umo katika muungano pamoja na mimi na mimi nimo katika muungano pamoja na wewe, ili wao pia wapate kuwa katika muungano pamoja na sisi. Nami nimewajulisha jina lako nami nitalijulisha, ili upendo ulionipenda nao upate kuwa ndani yao nami katika muungano pamoja nao.’​—Yoh. 17:20, 21, 26.

19. Umeazimia kufanya nini?

19 Ikiwa tuna tabia fulani mbaya ambayo ni vigumu kuachana nayo kwa sababu ya kutokamilika kwetu, basi upendo na utuchochee kusali kama mutunga​-zaburi, aliyesali hivi: “Unganisha moyo wangu ili kuliogopa jina lako.” (Zab. 86:11) Acheni tuazimie kumupinga Ibilisi ili asitutenganishe na Baba yetu mwenye upendo na ndugu na dada zetu. Tujikaze sana ili ‘tuwe waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa, na tuendelee kutembea katika upendo,’ katika familia, katika utumishi na katika kutaniko.​—Efe. 5:1, 2.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 29]

Anaacha zawadi yake kwenye mazabahu, anaenda kufanya amani na ndugu yake

[Picha katika ukurasa wa 31]

Wazazi, muwafundishe watoto wenu kuonyesha heshima