Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Mimi Niko Pamoja Nawe”

“Mimi Niko Pamoja Nawe”

“Mimi Niko Pamoja Nawe”

‘Wengi wataenda huku na huku, na ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.’​—DAN. 12:4.

UNGEJIBU NAMNA GANI?

Ule “ujuzi wa kweli” umekuwa mwingi namna gani katika wakati wetu?

Ni nini imefanya wale wanaokubali ile kweli waongezeke na kuwa wengi?

Ni njia gani ambazo zimesaidia ili ule ujuzi wa kweli uwe “mwingi”?

1, 2. (a) Tunajua namna gani kama Yesu iko pamoja na watu wake na kama ataendelea kuwa pamoja nao wakati ujao? (b) Kulingana na Danieli 12:4, wale wanaojifunza Maandiko kwa uangalifu watapata baraka gani?

 JIWAZIE uko katika paradiso. Kila asubuhi unaamuka ukiwa na furaha na tayari kuanza siku mupya. Hauna maumivu yoyote. Hauna tena uzaifu wowote wa kimwili uliokuwa nao. Uwezo wako wa kuona, kusikia, kunusa, kugusa, kuonja unatumika kwa ukamilifu. Una nguvu nyingi, kazi nzuri, marafiki wengi, na hauna tena wasiwasi. Hizo ndizo baraka unazoweza kufurahia katika Ufalme wa Mungu. Yesu Kristo, Mufalme aliyechaguliwa na Mungu, atawabariki watu wake wote na kuwasaidia wajifunze juu ya Yehova.

2 Wakati huo, Yehova atawasaidia watumishi wake waaminifu ili wawafundishe wengine katika dunia yote. Kwa miaka mingi, Mungu na Mwana wake wameendelea kuwasaidia watu waaminifu. Mbele ya kupanda mbinguni, Yesu aliwahakikishia wanafunzi wake waaminifu kama atakuwa pamoja nao. (Soma Mathayo 28:19, 20.) Ili tuamini kabisa maneno hayo ya Yesu, tutazungumuzia mustari mumoja tu wa unabii ulioongozwa na roho ya Mungu ulioandikwa katika muji wa zamani wa Babiloni miaka zaidi ya 2 500 iliyopita. Kuhusu “wakati wa mwisho” tunamoishi sasa, nabii Danieli aliandika hivi: ‘Wengi wataenda huku na huku, na ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.’ (Dan. 12:4) Maneno ya Kiebrania ‘kuenda huku na huku’ yanapotumiwa kwa njia ya mufano kuhusiana na siku zetu, yanamaanisha kujifunza kwa uangalifu. Wale wanaoenda huku na huku watabarikiwa sana! Wale wanaojifunza Maandiko kwa uangalifu watabarikiwa sababu watapata ujuzi wa kweli, ao ujuzi ulio sahihi wa Neno la Mungu. Unabii huo unaonyesha pia kama wengi wataukubali ule “ujuzi wa kweli.” Zaidi ya hayo, ujuzi huo utakuwa mwingi, utafundishwa mahali pote na kila mutu anaweza kuupata. Tutakapochunguza namna unabii huu umetimizwa, tutaona kama Yesu iko pamoja na wanafunzi wake leo na Yehova iko tayari kutimiza mambo yote ambayo ametuaga.

ULE “UJUZI WA KWELI” UNAPATIKANA

3. Kisha kufa kwa mitume, ni jambo gani lilitokea?

3 Kisha kufa kwa mitume, uasi-imani uliotabiriwa ulitokea kati ya Wakristo wa kweli na ulienea haraka kama moto. (Mdo. 20:28-30; 2 Tes. 2:1-3) Miaka mingi baadaye, wale wasioijua Biblia na wale waliojiita kuwa Wakristo hawakupata ule “ujuzi wa kweli” kwa wingi. Ijapokuwa walisema kama wanaamini Biblia, viongozi wa kidini walifundisha mafundisho ya uongo, “mafundisho ya mashetani” yaliyomufanya Mungu alaumiwe. (1 Tim. 4:1) Kwa hiyo, waliwatia watu wengi katika giza la kiroho. Waasi-imani hao walifundisha mafundisho ya uongo kama vile Utatu, nafsi isiyoweza kufa, na kwamba nafsi za watu wengine zinateswa milele katika moto.

4. Namna gani kikundi fulani cha Wakristo kilianza kutafuta ule “ujuzi wa kweli” katika miaka ya 1870?

4 Hata hivyo, katika miaka ya 1870, maana yake, miaka 40 hivi mbele ya kuanza kwa “siku za mwisho,” kikundi kidogo cha Wakristo wanaopenda kujua kweli kilianza kukusanyika huko Pennsylvania, Amerika, ili kujifunza Biblia kwa uangalifu na kutafuta ule “ujuzi wa kweli.” (2 Tim. 3:1) Walijiita Wanafunzi wa Biblia. Hawakuwa wale watu “wenye hekima na wenye akili” ambao Yesu alisema kama wangefichwa ujuzi wa kweli. (Mt. 11:25) Walikuwa watu wanyenyekevu waliotamani kwa moyo wote kujua mapenzi ya Mungu. Walisoma Maandiko, waliyachunguza, na kutafakari sana na kusali ili kupata muongozo. Walilinganisha Maandiko ya Biblia na pia walichunguza vitabu vya watu wengine ambao pia walikuwa wamekwisha kufanya uchunguzi kama wao hapo mbele. Polepole, Wanafunzi hao wa Biblia walianza kutambua kweli zilizofichwa kwa miaka mingi.

5. Sababu gani wanafunzi wa Biblia walichapisha kwa mufululizo trakti inayoitwa Teolojia ya Zamani?

5 Wanafunzi wa Biblia walifurahia sana mambo waliyokuwa wakijifunza, hata hivyo hawakujivuna juu ya ujuzi waliokuwa wamepata wala hawakusema kama wao ndio watu wa kwanza kutangaza mafundisho hayo. (1 Kor. 8:1) Kwa hiyo, walichapisha mufululizo wa trakti zilizoitwa Teolojia ya Zamani katika Kiingereza. Kusudi lao lilikuwa kuwasaidia wasomaji waelewe kweli ya Biblia. Trakti hizo za kwanza​-kwanza zilitolea wasomaji “musaada wa kujifunza Biblia, na kuwaonyesha namna ya kuachana na mafundisho yote ya uongo ya wanadamu na namna ya kurudisha ile teolojia ya Bwana wetu na ya mitume wake.”​—The Old Theology, Na. 1, mwezi wa 4, 1889, uku. 32.

6, 7. (a) Mungu ametusaidia kuelewa kweli gani kuanzia miaka ya 1870? (b) Ni mafundisho gani ya kweli ambayo wewe umefurahia kujifunza?

6 Kumepita zaidi ya miaka 100 tangu kikundi hicho kidogo kianze, na tangu wakati huo mafundisho mengi ya kweli yamevumbuliwa! * Tofauti na mafundisho yasiyo wazi ya wanateolojia, mafundisho hayo ya kweli ni mepesi na wazi. Mafundisho hayo yanachangamusha moyo, yanatuweka huru na kutuwezesha kuwa na maisha yenye kusudi na yanajaza moyo wetu na furaha na tumaini. Kweli hizo zinatusaidia kumujua Yehova, ni kusema, kujua sifa zake na makusudi yake. Kweli hizo zinaonyesha waziwazi daraka la Yesu katika mupango wa Mungu, kwa nini alikufa, na mambo anayofanya sasa. Kweli hizo nzuri zinatuonyesha sababu gani Mungu anawaacha watu wateseke, sababu gani tunakufa, namna ya kusali, na namna ya kupata furaha ya kweli.

7 Leo, tunaweza kuelewa maana ya unabii mwingi uliokuwa umewekwa kuwa “siri” kwa maelfu ya miaka na unaotimia sasa katika siku hizi za mwisho. (Dan. 12:9) Unabii huo unapatikana mahali mbalimbali katika Biblia, zaidi sana katika Injili na kitabu cha Ufunuo. Yehova ametusaidia pia kuelewa maana ya matukio ambayo hatungeweza kuona kwa macho yetu, ni kusema, kutiwa kwa Yesu kwenye kiti cha Ufalme, kutokea kwa vita huko mbinguni, na kutupwa kwa Shetani hapa duniani. (Ufu. 12:7-12) Mungu ametusaidia pia kuelewa maana ya mambo tunayoweza kuona; kama vile vita, matetemeko ya dunia, magonjwa ya kuambukiza, ukosefu wa chakula, na watu wasiomuogopa Mungu wanaofanya hali ziwe mbaya zaidi katika ‘nyakati hizi za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’​—2 Tim. 3:1-5; Lu. 21:10, 11.

8. Ni nani anayestahili kupewa sifa kwa ajili ya mambo yote ambayo tumeona na kusikia?

8 Hali yetu inatukumbusha maneno ambayo Yesu aliwaambia wanafunzi wake: ‘Yenye furaha ni macho yanayoona mambo ambayo ninyi munayaona. Kwa maana ninawaambia ninyi, Manabii na wafalme wengi walitamani kuyaona mambo ambayo ninyi munayaona lakini hawakuyaona, na kuyasikia mambo ambayo ninyi munayasikia lakini hawakuyasikia.’ (Lu. 10:23, 24) Tunamushukuru na kumusifu Yehova Mungu kwa kutusaidia kuona na kusikia mambo hayo. Tunafurahi pia kwa sababu alitumia ‘musaidizi,’ ni kusema, roho yake takatifu, ili kutuongoza sisi wanafunzi wa Yesu “ndani ya kweli yote”! (Soma Yohana 16:7, 13.) Kwa hiyo, siku zote tusisahau kama “ujuzi wa kweli” ni wenye samani sana na tusiwe na uchoyo wa kuwatolea wengine ujuzi huo bila malipo!

“WENGI” WANAKUBALI ULE “UJUZI WA KWELI”

9. Gazeti la Munara wa Mulinzi la mwezi wa 4, mwaka wa 1881 lilitoa mualiko gani?

9 Katika mwezi wa 4, mwaka wa 1881, zaidi ya mwaka moja kisha kuchapishwa kwa gazeti la kwanza la Munara wa Mulinzi, habari moja ya gazeti hilo ilionyesha kama wahubiri 1 000 walihitajiwa. Habari hiyo ilisema hivi: ‘Kwa wale wanaoweza kutoa nusu ya wakati wao ao wakati mwingi katika kazi ya Bwana, tunapenda wafikirie mupango huu, ni kusema, muende katika miji mikubwa na midogo, kulingana na uwezo wenu kama Wakolportere ao Waevanjeliste, mutafute kila mahali Wakristo wenye mioyo mizuri, mutakuta wengi wao ni wenye bidii kwa ajili ya Mungu, lakini si kulingana na ujuzi. Mujikaze kuwajulisha neema nyingi za Baba Yetu na mambo mazuri ya neno Lake.’

10. Watu waliitikia namna gani wakati mualiko ulitolewa wa kupata wahubiri wa wakati wote?

10 Mualiko huo ulionyesha kama Wanafunzi wa Biblia walitambua kama kazi ya lazima sana ya Wakristo ni kuhubiri habari njema. Lakini mualiko wa wahubiri wa wakati wote 1 000 ulionyesha kama walitazamia mengi zaidi kwa sababu wakati huo ni watu wachache tu ndio waliokuwa wakihuzuria mikutano ya Wanafunzi wa Biblia. Hata hivyo, kisha kusoma trakti ao gazeti, watu wengi walitambua kama walikuwa wameipata kweli na walikubali bila kukawia mualiko huo. Kwa mufano, katika mwaka wa 1882, musomaji mumoja kutoka Londres alipokwisha kusoma Munara wa Mulinzi na broshua iliyochapishwa na Wanafunzi wa Biblia, aliandika hivi: “Tafazali munifundishe namna ya kuhubiri na mambo ninayopaswa kuhubiri ili niweze kutimiza kazi iliyobarikiwa ambayo Mungu anataka ifanyike.”

11, 12. (a) Ni muradi gani tulio nao kama ule wa wakolportere? (b) Namna gani wakolportere walianzisha makutaniko mapya ao madarasa?

11 Kufikia mwaka wa 1885, Wanafunzi wa Biblia karibu 300 walikuwa wakifanya kazi ya ukolportere. Wahubiri hao wa wakati wote walikuwa na muradi kama sisi, ni kusema, kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo. Lakini, njia zao za kuhubiri zilitofautiana na zetu. Kwa kawaida leo, sisi tunajifunza Biblia na mutu mumoja-mumoja, na hivyo tunamufundisha kupatana na mahitaji yake. Kisha tunamualika mwanafunzi huyo wa Biblia aanze kuhuzuria mikutano ya kutaniko. Lakini hapo zamani, wakolportere waliwaachia watu vitabu na kisha walikusanya watu waliopendezwa ili kujifunza pamoja nao Biblia. Kuliko kujifunza na mutu mumoja -mumoja, walianzisha makutaniko mapya ambayo walikuwa wakiita kuwa madarasa.

12 Kwa mufano, katika mwaka wa 1907, kikundi kimoja cha wakolportere kilizunguka katika muji fulani ili kutafuta wale waliokuwa tayari wamepata vitabu L’Aurore du Millénium (vilivyoitwa pia Études des Écritures). Munara wa Mulinzi ulieleza hivi: “Wale waliopendezwa walikusanyika katika nyumba moja. Siku ya Yenga nzima kolportere alizungumuza nao juu ya Mupango wa Mungu wa Zile Enzi (Le Divin Plan des Âges), na Siku ya Yenga iliyofuata aliwatia moyo waendelee kukusanyika pamoja kwa ukawaida.” Katika mwaka wa 1911, mambo yalibadilika. Wahubiri wenye kusafiri wa pekee 58 walisafiri katika Amerika yote na Canada ili kutoa hotuba za watu wote. Ndugu hao walichukua majina na adresi za watu waliopendezwa waliohuzuria hotuba na waliwaambia kama wanapaswa kukusanyika pamoja katika nyumba za watu na kuunda “madarasa” mapya. Kufikia mwaka wa 1914, kulikuwa makutaniko 1 200 ya Wanafunzi wa Biblia duniani pote.

13. Kwa nini kuenea kwa ule “ujuzi wa kweli” kunashangaza sana leo?

13 Leo, duniani pote kuna makutaniko karibu 109 400, na ndugu na dada 895 800 hivi ni mapainia. Karibu watu milioni munane wanaukubali sasa ule “ujuzi wa kweli,” na kuutumia katika maisha yao. (Soma Isaya 60:22.) * Hilo linashangaza sana kwa sababu Yesu alitabiri kama wanafunzi wake ‘watachukiwa na watu wote’ kwa sababu ya jina lake. Tena alisema kama wanafunzi wake watateswa, watafungwa, na hata kuuawa. (Lu. 21:12-17) Tunaendelea kupata matokeo mazuri katika kazi yetu ya kufanya wanafunzi ijapokuwa upinzani wa Shetani, mashetani wake, na watu wanaotutesa. Leo tunahubiri katika “dunia yote inayokaliwa;” tunahubiri katika misitu mikubwa, katika maeneo yenye baridi yanayopatikana kaskazini mwa Ulaya, Asia na Amerika, katika maeneo ya milima, katika miji, na katika maeneo ya mbali. (Mt. 24:14) Mambo yote hayo yamefanyika kwa musaada wa Mungu.

ULE “UJUZI WA KWELI” UMEKUWA “MWINGI”

14. Namna gani kazi ya uchapishaji imesaidia kueneza ule “ujuzi wa kweli”?

14 Ule “ujuzi wa kweli” umekuwa mwingi kwa sababu wahubiri wengi wanaihubiri ile habari njema. Ujuzi huo umeongezeka pia kupitia kazi ya uchapishaji. Katika mwezi wa 7, 1879, Wanafunzi wa Biblia walichapisha kwa mara ya kwanza gazeti Le Phare de la Tour de Sion — Messager de la Présence de Christ. Gazeti hilo lilichapishwa na kompanyi moja ya ulimwengu, na ni magazeti 6 000 ndiyo yalichapishwa katika luga ya Kiingereza tu. Charles Taze Russell, akiwa na miaka 27, alichaguliwa ili asimamie uandikaji wa gazeti hilo, na ndugu wengine watano wenye kukomaa kiroho walikuwa wakiandika kwa ukawaida habari fulani katika gazeti hilo. Leo Munara wa Mulinzi unachapishwa katika luga 195. Munara wa Mulinzi ndilo gazeti lenye kuchapishwa sana duniani, hesabu ya magazeti ni 42182000. Amkeni! inachukua nafasi ya pili, magazeti 41 042 000 yanachapishwa katika luga 84. Zaidi ya hayo, vitabu na Biblia karibu milioni 100 vinachapishwa kila mwaka.

15. Feza zinazotumiwa ili kuchapa vitabu vyetu zinatoka wapi?

15 Kazi hiyo kubwa inawezekana kupitia michango ya kujipendea. (Soma Mathayo 10:8.) Hilo linashangaza sana wale wanaofanya kazi ya uchapishaji katika ulimwengu kwa sababu wao wanajua kama kazi hiyo inaomba feza nyingi ili kununua mashine za kuchapisha, karatasi, wino, na vitu vingine. Ndugu mumoja wa Beteli anayenunua vitu kwa ajili ya kazi ya kuchapisha alisema hivi: “Wafanya​-biashara wanaokuja kutazama mashine za kuchapisha vitabu tunazotumia hawaelewe namna gani mashine hizo, na kazi ya uchapishaji ya hali ya juu sana vinaweza kugaramiwa tu kupitia michango ya kujipendea. Wanashangaa pia kuona kwamba wale wanaofanya kazi kwenye Beteli wangali vijana na ni wenye furaha.”

UJUZI WA MUNGU UTAIJAZA DUNIA

16. Sababu gani Mungu anafanya ule “ujuzi wa kweli” ujulikane?

16 Ule “ujuzi wa kweli “ umekuwa mwingi kwa sababu Mungu anataka “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:3, 4) Yehova anataka watu wajue ile kweli ili waweze kumuabudu vile anavyopenda na kupata baraka zake. Kwa kufanya ule “ujuzi wa kweli” ujulikane, Yehova amewakusanya mabaki ya Wakristo watiwa​-mafuta. Anaendelea pia kukusanya ‘umati mukubwa;’ watu walio na tumaini la kuishi milele duniani, kutoka katika ‘mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.’​—Ufu. 7:9.

17. Kuenea kwa ibada ya kweli kunaonyesha nini?

17 Sasa miaka zaidi ya 130 imepita tangu ibada ya kweli ilianza kuenea mahali pote duniani, hilo linaonyesha waziwazi kama Mungu na Mufalme ambaye alichagua Yesu Kristo, wamekuwa pamoja na watumishi wa Yehova duniani ili kuwaongoza, kuwalinda, kuwapanga kwa utaratibu katika tengenezo, na kuwafundisha. Ongezeko lao pia linaonyesha kama ahadi za Yehova za wakati ujao zitatimia. ‘Dunia hakika itajawa na kumujua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.’ (Isa. 11:9) Wakati huo wanadamu watafurahia tena baraka za ajabu!

[Maelezo ya chini]

^ Utafaidika sana kwa kutazama DVD Mashahidi wa Yehova​—Watu Wanaotenda kwa Imani, Sehemu ya 1: Kutoka Katika Giza na DVD Mashahidi wa Yehova​—Watu Wanaotenda kwa Imani, Sehemu ya 2: Kuangaza Nuru.

^ Soma Unabii wa Isaya​—Nuru kwa Wanadamu Wote Buku la II, ukurasa wa 320.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 6]

Wanafunzi wa kwanza wa Biblia walikuwa watu wanyenyekevu waliotamani kabisa kujua mapenzi ya Mungu

[Picha katika ukurasa wa 7]

Yehova anapendezwa sana na jitihada unazofanya ili kueneza ule “ujuzi wa kweli”