Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Furahia Amani Katika Utawala wa Miaka Elfu Moja na Milele

Furahia Amani Katika Utawala wa Miaka Elfu Moja na Milele

Furahia Amani Katika Utawala wa Miaka Elfu Moja na Milele

‘Ili Mungu awe vitu vyote kwa kila mutu.’—1 KOR. 15:28.

UNAWEZA KUFASIRIA?

Maandiko yafuatayo yanakutolea tumaini gani?

Mika 4:4

Isaya 11:6-9

Yohana 5:28, 29

1. ‘Mukutano mukubwa’ unangojea nini kwa furaha?

 FIKIRIA mambo mengi mazuri ambayo serikali ao guvernema yenye nguvu inayoongozwa na mufalme mwenye huruma inaweza kuwafanyia raia wake kwa muda wa miaka elfu moja! ‘Mukutano mukubwa’ ao wale watakaookoka ile ‘ziki kubwa,’ wanangojea matukio ya ajabu yatakayoongoza kwenye uharibu kabisa wa ulimwengu huu muovu.​—Ufu. 7:9, 14.

2. Ni mambo gani ambayo yamewapata wanadamu kwa muda wa miaka 6 000 iliyopita?

2 Kwa muda wa miaka 6 000 iliyopita, wanadamu wameteseka sana kwa sababu ya kujiamulia mambo na kujitawala wenyewe. Hapo zamani Biblia ilisema hivi: ‘Mwanadamu amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’ (Mhu. 8:9) Ni mambo gani tunayojionea leo? Vita, uasi, umaskini, magonjwa, uharibifu wa mambo kama vile hewa na maji, mabadiliko ya hali ya hewa na mambo mengine mengi yanaendelea kuwatesa wanadamu. Viongozi wa dunia wanaonya kwamba ikiwa hatufanye mabadiliko na kuacha kuharibu dunia, matokeo yatakuwa mabaya zaidi.

3. Utawala wa Miaka Elfu Moja utafanya nini?

3 Ufalme wa Mungu utakaoongozwa na Yesu Kristo pamoja na watawala wenzake 144 000, utaitengeneza dunia polepole na kuwarudisha wanadamu katika hali nzuri. Utawala wa Miaka Elfu Moja utatimiza ahadi hii ya Yehova Mungu yenye kuchangamusha moyo: ‘Mimi ninaumba mbingu mupya na dunia mupya; na mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.’ (Isa. 65:17) Basi, ni mambo gani mazuri yasiyoonekana bado tunayongojea? Ili tujue namna maisha yatakavyokuwa wakati ujao, unabii wa Biblia unazungumuzia vitu vizuri “visivyoonekana” tunavyongojea.​—2 Kor. 4:18.

‘WATAJENGA NYUMBA NA KUPANDA MASHAMBA YA MIZABIBU’

4. Leo watu wanaishi katika hali gani kwa sababu ya kukosa nyumba nzuri?

4 Ni nani kati yetu ambaye hangefurahi kuwa na nyumba yake, ambamo yeye na familia yake wanaweza kuishi kwa amani na usalama? Hata hivyo, leo ni vigumu kuwa na nyumba nzuri. Watu wanasongamana katika miji. Watu wengi wanalazimika kuishi katika nyumba ambazo haziweze kudumu na katika nyumba chafu na miji michafu. Watu wengi wanafikiri kama hakuna siku wanaweza kuwa na nyumba yao wenyewe.

5, 6. (a) Maandiko ya Isaya 65:21 na Mika 4:4, yatatimia namna gani? (b) Tufanye nini ili kupata baraka hizo?

5 Ufalme wa Mungu utakapotawala, kila mutu atakuwa na nyumba yake. Isaya alisema hivi: “Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.” (Isa. 65:21) Lakini, tunatazamia mambo mengi zaidi tu ya kuwa na nyumba. Watu fulani leo wanaishi katika nyumba zao wenyewe, wengine wanaishi katika nyumba kubwa kabisa. Lakini kila siku wanaogopa kufukuzwa kwa sababu ya kukosa feza za kulipia nyumba ao wanaogopa kwamba wezi ao watu wengine wabaya wanaweza kuvunja nyumba na kuingia ndani. Katika Ufalme wa Mungu mambo yote yatakuwa tofauti. Nabii Mika aliandika hivi: ‘Wataketi, kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya mutini wake, wala hakutakuwa na mutu yeyote atakayewatetemesha.’​—Mika. 4:4.

6 Kwa kuwa tunatazamia mambo hayo mazuri, tunapaswa kufanya nini? Kwa kweli, kila mutu kati yetu anahitaji nyumba nzuri. Hata hivyo, kuliko kujihangaisha sana, labda hata kujiingiza katika madeni ili tu kuwa na nyumba nzuri leo, je, hauone kama jambo la hekima ni kufikiria ahadi ya Yehova? Kumbuka maneno haya ya Yesu: “Mbweha wana mapango na ndege wa mbinguni wana viota, lakini Mwana wa binadamu hana mahali popote pa kulaza kichwa chake.” (Lu. 9:58) Yesu alikuwa na uwezo na nguvu ya kujenga ao kununua nyumba nzuri kupita nyumba zote. Lakini hakuhangaishwa na jambo hilo. Sababu gani? Kwa kweli, Yesu aliepuka jambo lolote ao mutego wowote ambao ungemuzuia kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yake. Je, tunaweza kufuata mufano wake na kuwa na jicho rahisi lisilokengeushwa na vitu vya kimwili na mahangaiko ya dunia?​—Mt. 6:33, 34.

‘MBWA​-MWITU NA MWANA-KONDOO WATAKULA PAMOJA’

7. Hapo mwanzo Yehova aliwapa wanadamu daraka gani?

7 Yehova aliwaumba wanadamu kisha kuumba viumbe vingine vyote duniani. Yehova alimuambia Fundi wake wa Kazi, Mwana wake muzaliwa wa kwanza, kusudi lake la kuumba mwanadamu. Alimuambia hivi: ‘Na tufanye mutu kwa mufano wetu, kwa sura yetu, nao watawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na wanyama wa kufugwa na dunia yote na kila munyama anayetembea juu ya dunia.’ (Mwa. 1:26) Kwa hiyo, Adamu na Eva, na wanadamu wengine wote, walipewa daraka la kuwatala wanyama.

8. Wanyama wanatenda namna gani?

8 Je, kweli wanadamu wanaweza kuwatawala wanyama wote na kuishi nao kwa amani? Watu wengi wanafurahia sana kuishi pamoja na wanyama kama vile imbwa na pusi. Lakini, tuseme nini juu ya wanyama wa pori? Ripoti moja inasema hivi: “Watu ambao wameishi na wanyama na kujifunza tabia zao wamevumbua kama wanyama wote wanaonyonyesha wanaweza kufurahi ao kukasirika.” Bila shaka, wanapoona kama maisha yao yamo katika hatari wanaogopa ao wanakuwa wakali, lakini, je, wanyama wanaweza kuonyesha upendo na huruma? Ripoti hiyo inaongeza hivi: “Wanyama wanaonyonyesha wanaonyesha sifa yao kubwa ya upendo wenye shauku wanapotunza watoto wao.”

9. Tunangojea mabadiliko gani kuhusu wanyama?

9 Kwa hiyo si jambo la kushangaza tunaposoma katika Biblia kama amani itakuwa kati ya wanadamu na wanyama. (Soma Isaya 11:6-9; 65:25.) Sababu gani? Kumbuka wakati Noa na jamaa yake walitoka katika safina kisha Garika, Yehova aliwaambia hivi: “Kila kiumbe hai cha dunia kitawahofu na kuwaogopa ninyi.” Woga huo unawasaidia wanyama kujilinda. (Mwa. 9:2, 3) Je, Yehova hatawaondolea wanyama kiasi fulani cha woga na hofu hiyo ili wanadamu wawatawale kama vile alivyokusudia mwanzoni? (Hos. 2:18) Kipindi cha furaha kinawangojea wale watakaookoka ili kuishi duniani!

‘ATAFUTA KILA CHOZI KATIKA MACHO YAO’

10. Sababu gani kwa kawaida wanadamu wanatoa machozi?

10 Mufalme Sulemani alipoona ‘matendo yote ya uonevu yanayofanywa chini ya jua,’ alisema hivi kwa uchungu: ‘Tazama! machozi ya wale wanaokandamizwa, lakini hawakuwa na mutu wa kuwafariji.’ (Mhu. 4:1) Mambo yako hivyo leo, na hata zaidi. Ni nani kati yetu ambaye hajafikia siku moja kutoa machozi kwa sababu fulani? Ni kweli kwamba wakati fulani tunaweza kutoa machozi ya furaha. Lakini, kwa kawaida tunatoa machozi kwa sababu ya huzuni ya moyo, sivyo?

11. Ni masimulizi gani ya Biblia yanayogusa moyo wako?

11 Fikiria masimulizi mengi yenye kugusa moyo tunayosoma katika Biblia. Sara alipokufa akiwa na miaka 127; ‘Abrahamu aliingia ndani kumuombolezea Sara na kumulilia.’ (Mwa. 23:1, 2) Naomi alipowaaga binti wakwe zake ‘walipaaza sauti zao na kulia’ na kisha ‘walipaaza sauti zao na kulia tena.’ (Rut. 1:9, 14) Mufalme Hezekia alipoteswa na ugonjwa karibu kufa, alisali kwa Mungu na “akaanza kulia sana,” jambo ambalo lilimugusa sana Yehova. (2 Fal. 20:1-5) Unaposoma namna Petro alivyomukana Yesu, je, hauguswe moyoni na jambo alilofanya? Jogoo ilipowika, Petro ‘alienda inje akalia kwa uchungu.’​—Mt. 26:75.

12. Ufalme wa Mungu utawaletea wanadamu kitulizo gani?

12 Kwa sababu ya mambo mengi yenye kuhuzunisha, iwe mambo makubwa ao madogo, wanadamu wanahitaji faraja na kitulizo. Hayo ndiyo mambo ambayo ule Utawala wa Miaka Elfu Moja utawaletea wanadamu. Biblia inasema hivi: ‘[Mungu] atafuta kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.’ (Ufu. 21:4) Inafurahisha sana kujua kama kilio, na maumivu havitakuwapo tena, Mungu anaahidi pia kuondoa adui wetu wa mwisho, ni kusema, kifo. Ataondoa kifo namna gani?

‘WALE WOTE WALIO NDANI YA MAKABURI YA UKUMBUSHO WATATOKA’

13. Namna gani kifo kimewatesa wanadamu tangu Adamu alipofanya zambi?

13 Adamu alipofanya zambi, kifo kilianza kuwatawala wanadamu kama mufalme. Wanadamu wenye zambi hawaweze kushinda na kuepuka kifo, na kimewaletea huzuni na maumivu mengi sana. (Rom. 5:12, 14) Zaidi ya hayo, “kwa kuogopa kifo,” mamilioni ya watu wamekuwa “maisha yao yote katika hali ya utumwa.”​—Ebr. 2:15, La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo.

14. Kuangamizwa kwa kifo kutaleta matokeo gani?

14 Biblia inazungumuzia wakati ambapo kifo ‘adui wa mwisho atakapoangamizwa.’ (1 Kor. 15:26) Kuna vikundi viwili vya watu watakaofaidika na ahadi hiyo. Kwanza, ‘mukutano mukubwa,’ wa watu wanaoishi sasa, wataokoka na kuingia katika dunia mupya wakiwa na tumaini la kuishi milele. Kisha, mamilioni ya watu ambao wamekufa watafufuliwa. Je, unaweza kuwazia namna mukutano mukubwa utakavyofurahia kuwakaribisha wale watakaofufuliwa? Kuchunguza vizuri masimulizi fulani ya ufufuo katika Biblia kunaweza kutusaidia tuone namna mambo yatakavyokuwa.​—Soma Marko 5:38-42; Luka 7:11-17.

15. Utajisikia namna gani utakapoona mutu uliyemupenda anafufuliwa?

15 Fikiria maneno “wakawa na shangwe kubwa” na ‘wakaanza kumutukuza Mungu’ ambayo tumesoma katika maandiko hayo. Kama ungejionea mambo hayo, labda wewe pia ungejisikia hivyo. Kwa kweli, kuwaona tena wapendwa wetu waliokufa kutatuletea furaha kubwa na shangwe. Yesu alisema hivi: ‘Saa inakuja ambayo wale wote walio ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka.’ (Yoh. 5:28, 29) Hakuna mutu hata mumoja kati yetu ambaye amekwisha kuona mambo hayo, lakini yatakuwa kati ya “vitu visivyoonekana” vya ajabu.

MUNGU ATAKUWA ‘VITU VYOTE KWA KILA MUTU’

16. (a) Sababu gani inafaa kuzungumuzia kwa furaha baraka za wakati ujao? (b) Paulo alisema nini ili kuwatia moyo Wakristo wa kutaniko la Korintho?

16 Bila shaka, wale wote wanaomutumikia Yehova kwa uaminifu katika siku hizi zenye taabu watapata baraka nyingi wakati ujao. Ijapokuwa hatujapokea baraka hizo, kuendelea kuzifikiria kutatusaidia tuendelee kutia mambo ya maana kabisa pa nafasi ya kwanza na kuepuka mambo ya ulimwengu yanayopita na yanayokengeusha akili. (Lu. 21:34; 1 Tim. 6:17-19) Tunapofanya funzo na ibada ya familia, tunapoongea na ndugu na dada zetu, na tunapozungumuza na watu tunaojifunza nao Biblia na wale wanaopendezwa na kweli, acheni tuzungumuzie kwa furaha tumaini letu nzuri na baraka tunazongojea. Kufanya hivyo kutatusaidia tuchunge baraka hizo katika akili na mioyo yetu. Mutume Paulo alifanya hivyo ili kuwatia moyo Wakristo wenzake. Maneno yake yaliwasaidia wafikirie mambo yatakayotokea mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo. Jaribu kufikiria maana kamili ya maneno ya Paulo yaliyo katika 1 Wakorintho 15:24, 25, 28.​—Soma.

17, 18. (a) Namna gani Yehova alikuwa ‘vitu vyote kwa kila mutu’ mwanzoni mwa historia ya wanadamu? (b) Yesu atafanya nini ili kurudisha umoja na upatano kati ya wanadamu?

17 Maneno ‘ili Mungu awe vitu vyote kwa kila mutu’ yanafaa kabisa ili kuzungumuzia wakati muzuri tunaongojea. Maneno hayo yanamaanisha nini? Fikiria wakati wanadamu wa kwanza wakamilifu, Adamu na Eva, walikuwa katika familia ya Yehova yenye amani na umoja, ni kusema, viumbe wake wa mbinguni na duniani. Yehova Mungu, Mutawala wa Ulimwengu Wote Muzima, alikuwa anaongoza moja kwa moja viumbe wake, malaika na wanadamu. Viumbe wake walizungumuza naye moja kwa moja, walimuabudu, na walibarikiwa naye. Mungu alikuwa ‘vitu vyote kwa kila mutu.’

18 Uhusiano huo muzuri ulikatizwa wakati Shetani aliwachochea wanadamu kuasi mamlaka ya Mungu. Hata hivyo, kuanzia mwaka wa 1914, Ufalme wa Kimasiya umeanza kurudisha polepole umoja na uhusiano huo. (Efe. 1:9, 10) Katika Utawala wa Miaka Elfu Moja, vitu vizuri vya ajabu “visivyoonekana” sasa vitaonekana waziwazi. Kisha “mwisho,” utafika, ni kusema, mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu Moja. Kutatokea nini baadaye? Kwa unyenyekevu Yesu ‘atamukabizi ufalme Mungu wake ambaye pia ni Baba yake.’ Atatumia cheo na mamlaka yake “kwa utukufu wa Mungu.” Hata kama amepewa “mamlaka yote . . . mbinguni na duniani,” Yesu hajitafutie mambo makubwa. Yeye hatafute kunyanganya cheo cha Yehova.​—Mt. 28:18; Flp. 2:9-11.

19, 20. (a) Namna gani watu wote watakaotawaliwa na Ufalme duniani wataonyesha kama wanakubali mamlaka ya Yehova ao hapana? (b) Ni pendeleo gani nzuri lililo mbele yetu?

19 Mwishoni mwa ile miaka elfu moja, watumishi wa Mungu hapa duniani watakuwa wamefikia ukamilifu. Kama Yesu, watakubali mamlaka ya Yehova kwa unyenyekevu na bila kulazimishwa. Wataonyesha hilo kwa kushinda jaribu la mwisho. (Ufu. 20:7-10) Kisha, wanadamu na malaika wote waasi wataharibiwa milele. Kwa kweli huo utakuwa wakati wa furaha! Kila mutu aliye katika familia ya Yehova, iwe mbinguni ao duniani atamusifu Yehova kwa furaha. Wakati huo Yehova atakuwa ‘vitu vyote kwa kila mutu.’​—Soma Zaburi 99:1-3.

20 Je, baraka zote ambazo Ufalme utaleta zinakuchochea utumie nguvu zako zote ili kufanya mapenzi ya Mungu bila kukengeushwa akili? Je, unaepuka kukengeushwa akili na tumaini la uongo na yale yanayoonekana kuwa maisha mazuri ambayo ulimwengu wa Shetani unawatolea watu? Je, utaendelea kuazimia kutetea na kuunga mukono utawala wa Yehova? Basi, matendo yako na yaonyeshe kama unatamani kufanya hivyo milele. Ukifanya hivyo utakuwa na pendeleo la kufurahia amani na usalama katika Utawala wa Miaka Elfu Moja na milele!

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 11]

Kisha kumaliza kazi ambayo Mungu alimupatia, kwa unyenyekevu Yesu atamurudishia Baba yake Ufalme