Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake

Namna Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake

Namna Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake

‘Hamuko gizani, hivi kwamba siku hiyo iwafikie ninyi kama vile ambavyo ingewafikia wezi.’​—1 THE. 5:4.

UNAWEZA KUFASIRIA?

Ni mambo gani yasiyoonekana bado ambayo yanazungumuziwa katika maandiko haya?

1 Wathesalonike 5:3

Ufunuo 17:16

Danieli 2:44

1. Ni nini itatusaidia tuendelee kukesha na kushinda majaribu?

 MAMBO yatakayotetemesha dunia yatatokea hivi karibuni. Unabii mbalimbali wa Biblia unaotimia unaonyesha jambo hilo, kwa hiyo tunapaswa kuendelea kukesha. Ni nini itatusaidia kufanya hivyo? Mutume Paulo anatushauri ‘tuendelee kukaza macho yetu juu ya vitu visivyoonekana.’ Kwa kweli, hatupaswe kusahau zawadi yetu ya uzima wa milele, iwe ni mbinguni ao duniani. Mistari inayozunguka andiko hilo, inaonyesha kama Paulo aliandika maneno hayo ili kuwatia moyo Wakristo waaminifu wafikirie wakati ujao wenye furaha ulio mbele yao. Kufanya hivyo kungewasaidia kushinda majaribu na upinzani.​—2 Kor. 4:8, 9, 16-18; 5:7.

2. (a) Tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa na imani yenye nguvu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii na ile inayofuata?

2 Shauri la Paulo linatufundisha kanuni moja ya lazima sana: Ili tuendelee kuwa na imani yenye nguvu, tunapaswa kukaza akili juu ya mambo yaliyo mbele, mambo makubwa ambayo yatatokea karibuni. (Ebr. 11:1; 12:1, 2) Acheni tuzungumuzie mambo kumi yatakayotokea wakati ujao na yanayohusiana sana na tumaini letu la uzima wa milele. *

MAMBO YATAKAYOTOKEA KARIBU TU NA MWISHO

3. (a) Ni jambo gani litakalotokea linalozungumuziwa katika 1 Wathesalonika 5:2, 3? (b) Viongozi wa dunia watafanya nini, na ni nani watakaowaunga mukono?

3 Paulo anataja jambo moja litakalotokea wakati ujao katika barua yake kwa Wathesalonika. (Soma 1 Wathesalonike 5:2, 3.) Yeye anazungumuzia “siku ya Yehova.” Katika andiko hili “siku ya Yehova” ni kipindi kinachoanza na uharibifu wa dini ya uongo na kufikia mwisho kwenye vita ya Har-Magedoni. Lakini, mbele siku hiyo ya Yehova ianze, viongozi wa ulimwengu watatangaza “Amani na usalama!” Labda tangazo hilo linaweza kutolewa kwa sababu ya tukio moja ao mufululizo wa matukio. Labda mataifa yatafikiri kama yako karibu kutatua matatizo yao makubwa. Viongozi wa dini watakuwa na musimamo gani? Kwa kuwa wao ni sehemu ya ulimwengu, inawezekana waunge mukono viongozi wa dunia. (Ufu. 17:1, 2) Kwa kufanya hivyo, viongozi hao wa dini watatenda kama manabii wa uongo wa wakati wa zamani wa Yuda. Yehova alisema hivi kuhusu manabii hao: “Wanasema, ‘Kuna amani! Kuna amani!’ wakati hakuna amani.”​—Yer. 6:14; 23:16, 17.

4. Tofauti na watu wengi, sisi tunajua nini?

4 Tangazo la “Amani na usalama!” litaonyesha kama siku ya Yehova inataka kuanza. Kwa hiyo, Paulo alisema hivi: ‘Akina ndugu, hamuko gizani, hivi kwamba siku hiyo iwafikie ninyi kama vile ambavyo ingewafikia wezi, kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru.’ (1 The. 5:4, 5) Tofauti na watu wengi, sisi tunajua maana ya mambo yanayotendeka leo. Unabii kuhusu tangazo la “Amani na usalama!” utatimia namna gani kabisa? Inatupasa tungojee na kuona vile mambo yatakuwa. Kwa hiyo, acheni tuazimie ‘kukaa macho na kutunza akili zetu.’​—1 The. 5:6; Sef. 3:8.

“MALKIA” ANAYEJIDANGANYA KABISA

5. (a) Ile ‘ziki kubwa’ itaanza namna gani? (b) Ni “malkia” gani anayejidanganya kwa kufikiri kama ataendelea milele?

5 Ni jambo gani lingine lisiloonekana litakalotokea baadaye? Mutume Paulo anaeleza hivi: “Wakati watakapokuwa wakisema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa gafula utakapokuwa juu yao mara moja.” Sehemu ya kwanza ya ‘uharibifu huo wa gafula’ ni kushambuliwa kwa ‘Babiloni Mukubwa,’ dini zote za uongo, zinazoitwa pia “kahaba.” (Ufu. 17:5, 6, 15) Ile ‘ziki kubwa’ itaanza na kushambuliwa kwa dini za uongo, kutia ndani dini zinazojiita kuwa za Kikristo. (Mt. 24:21; 2 The. 2:8) Jambo hilo litawashitua watu wengi. Kwa nini? Kwa sababu mupaka wakati huo, kahaba huyo atakuwa bado anajiona kuwa yeye ni “malkia” ambaye ‘hataona maombolezo kamwe.’ Lakini kwa gafula atatambua kama alikuwa amejidanganya kwa kufikiri kama ataendelea milele. Kahaba huyo ataharibiwa kwa gafula, kama vile “katika siku moja.”​—Ufu. 18:7, 8.

6. Ni nani watakaoharibu dini ya uongo?

6 Neno la Mungu linaonyesha kama ‘munyama​-mwitu’ mwenye “pembe kumi” ndiye atakayeshambulia kahaba huyo. Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kama munyama huyo ni Umoja wa Mataifa. “Pembe kumi” zinamaanisha serikali zote za leo zinazosaidia ‘munyama-mwitu mwenye rangi nyekundu.’ * (Ufu. 17:3, 5, 11, 12) Shambulio hilo litakuwa namna gani? Mataifa yanayounda Umoja wa Mataifa yatamunyanganya huyo kahaba mali yake, yatafunua wazi hali yake, yatamurarua, na ‘kumuteketeza kabisa.’ Ataharibiwa kabisa na hataonekana tena.​—Soma Ufunuo 17:16.

7. Shambulio litakalofanywa na ‘munyama-mwitu’ litaanza namna gani?

7 Unabii wa Biblia unaonyesha pia jambo litakaloanzisha shambulio hilo. Kwa njia fulani Yehova atatia katika mioyo ya viongozi wa ulimwengu mawazo ya “kutekeleza wazo lake,” ni kusema, kumuharibu kahaba. (Ufu. 17:17) Kwa kuwa dini imeendelea kuchochea vita na kuvuruga amani katika dunia; mataifa yatafikiri kama kumuharibu kahaba kutaletea mataifa yao amani. Kwa kweli, wakati viongozi wa ulimwengu watashambulia kahaba, watafikiri kama wako wanatimiza “wazo lao.” Lakini, watakuwa tu chombo ambacho Mungu atatumia ili kuharibu dini ya uongo. Kwa hiyo, mambo yatabadilika kwa gafula, sehemu moja ya ulimwengu wa Shetani itashambulia sehemu ingine, na Shetani hataweza kuzuia mambo hayo.​—Mt. 12:25, 26.

WATUMISHI WA MUNGU WANASHAMBULIWA

8. Shambulio la ‘Gogu wa inchi ya Magogu’ ni nini?

8 Kisha dini ya uongo kuharibiwa, watumishi wa Mungu wataonekana bado ‘wanakaa kwa usalama’ na “bila ukuta.” (Eze. 38:11, 14) Wao wataendelea kumuabudu Yehova, lakini wataonekana kama hawana mutu wa kuwapigania. Ni jambo gani litakalowapata? Inaonekana kwamba watashambuliwa na “vikundi vingi vya watu.” Biblia inaita shambulio hilo shambulio la ‘Gogu wa inchi ya Magogu.’ (Soma Ezekieli 38:2, 15, 16.) Je, tunapaswa kuogopa shambulio hilo?

9. (a) Ni jambo gani hasa ambalo Mukristo anapaswa kuhangaikia? (b) Ni lazima tufanye nini ili kutia imani yetu nguvu?

9 Kujua mbele ya wakati namna watu wa Mungu watakavyoshambuliwa, hilo halituogopeshe sana. Hata hivyo, jambo tunalohangaikia sana si wokovu wetu, lakini ni kuona jina la Yehova linatakaswa na pia watu wajue kama yeye ndiye anayestahili kutawala ulimwengu wote muzima. Kwa kweli, Yehova anasema zaidi ya mara 60: ‘Nanyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ (Eze. 6:7) Kwa hiyo, tunangojea kwa hamu sana kuona wakati unabii huo wa Ezekieli utatimia, na tunaamini kama “Yehova anajua jinsi ya kuwakomboa watu wenye ujitoaji​-kimungu kutoka katika jaribu.” (2 Pet. 2:9) Tunapongojea utimizo wa unabii huo, tunatumia kila nafasi kuitia imani yetu nguvu ili tuweze kubaki waaminifu kwa Yehova hata kutokee jaribu la namna gani. Tufanye nini basi? Tunapaswa kusali, kujifunza na kutafakari Neno la Mungu, na kuwaelezea wengine ujumbe wa Ufalme. Kwa kufanya hivyo, tumaini letu la uzima wa milele halitatikisika na litakuwa kama “nanga.”​—Ebr. 6:19; Zab. 25:21.

MATAIFA YATALAZIMIKA KUMUJUA YEHOVA

10, 11. Ni nini itaonyesha kama vita ya Har-Magedoni imeanza, na ni mambo gani yatakayotokea wakati huo?

10 Watumishi wa Yehova watakaposhambuliwa, hilo litatokeza jambo gani lenye kutetemesha? Yehova atamutuma Yesu atakayeongoza majeshi ya mbinguni ili kuwaokoa watu Wake. (Ufu. 19:11-16) Hapo sasa ndipo kutatokea Har-Magedoni, ni kusema, ‘vita ya ile siku kuu ya Mungu Mweza​-Yote.’​—Ufu. 16:14, 16.

11 Kupitia nabii Ezekieli, Yehova alitangaza hivi kuhusu vita hiyo: “‘Nami nitaita upanga juu yake [Gogu] kotekote katika eneo langu lote lenye milima,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Upanga wa kila mumoja utakuwa juu ya ndugu yake.’” Kwa sababu ya kuogopa sana, wale walio upande wa Shetani wataingia katika muvurugo mukubwa sana, watachukua silaha zao na kuanza kuuana wao kwa wao. Lakini, Shetani naye hataponyoka. Yehova anasema: “Nami nitanyesha moto na kiberiti juu yake [Gogu] na juu ya vikosi vyake na juu ya vikundi vingi vya watu vitakavyokuwa pamoja naye.” (Eze. 38:21, 22) Matokeo yatakuwa nini?

12. Mataifa yatalazimika kufanya nini?

12 Mataifa yatalazimika kutambua kama ni Yehova ndiye anayefanya wapondwe-pondwe hivyo. Kisha, kama walivyofanya Wamisri waliofuatilia Waisraeli kwenye Bahari Nyekundu, labda mataifa yanayoongozwa na Shetani yatalalamika hivi kwa uchungu: “Hakika Yehova anawapigania”! (Kut. 14:25) Kwa kweli, mataifa yatalazimika kumujua Yehova. (Soma Ezekieli 38:23.) Tunakaribia sana kuona mambo hayo.

SERIKALI KUBWA YA MWISHO YA ULIMWENGU

13. Tunajua mambo gani kuhusu sehemu ya tano ya sanamu ambayo Danieli anazungumuzia?

13 Unabii wa Danieli unatusaidia kujua mahali tulipo katika kipindi cha wakati. Danieli anazungumuzia sanamu inayofanana na mutu na ambayo imefanywa na sehemu mbalimbali. (Dan. 2:28, 31-33) Sanamu hiyo inafananisha serikali kubwa ambazo zimewatesa watu wa Mungu zamani na leo. Serikali hizo ni Babiloni, Utawala wa Wamede na Waperse, Ugiriki (Grèce), Roma na mwishowe serikali kubwa ya ulimwengu inayotawala leo. Katika unabii wa Danieli serikali hiyo ya mwisho inafananishwa na miguu na vidole vya miguu ya sanamu. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali za Uingereza na Amerika zilianzisha uhusiano wa pekee ili kutumika pamoja. Hakika, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ndiyo sehemu ya tano ya sanamu ya Danieli. Kwa kuwa miguu ndiyo sehemu ya mwisho ya sanamu hiyo, hilo linaonyesha kama hakuna serikali ingine kubwa ya ulimwengu itakayotokea duniani. Miguu na vidole vya sanamu vimetengenezwa na chuma na udongo, hilo linaonyesha uzaifu ulio katika Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika.

14. Ni serikali gani kubwa ya ulimwengu itakayotawala mupaka Har-Magedoni?

14 Unabii huohuo unaonyesha kama jiwe kubwa linalofananisha Ufalme wa Mungu, lilikatwa katika mulima mwaka wa 1914. Mulima huo unafananisha mamlaka ya Yehova. Jiwe hilo linashuka haraka kuelekea sanamu hiyo ili kuponda miguu yake. Kwenye Har-Magedoni, miguu na sehemu zingine za sanamu zitapondwa-pondwa. (Soma Danieli 2:44, 45.) Kwa hiyo, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika itaendelea kutawala mupaka Har-Magedoni. Itafurahisha sana kuona utimizo kamili wa unabii huo! * Lakini, ni mambo gani yanayomungojea Shetani?

MAMBO YATAKAYOMUPATA ADUI MUKUBWA WA MUNGU

15. Kisha Har-Magedoni, Shetani na mashetani wake watapatwa na nini?

15 Kwanza, Shetani atajionea kuanzia mwanzo mupaka mwisho namna tengenezo lake la duniani litakavyoharibiwa. Kisha, Shetani mwenyewe atakamatwa. Mutume Yohana anaeleza mambo yatakayotokea. (Soma Ufunuo 20:1-3.) Yesu Kristo ambaye ni “malaika mwenye ufunguo wa abiso,” atamukamata Shetani na mashetani wake na kuwatupa katika abiso na kuwaacha humo kwa miaka elfu. (Lu. 8:30, 31; 1 Yoh. 3:8) Hiyo ni hatua ya kwanza ya kupondwa kwa kichwa cha nyoka. *​—Mwa. 3:15.

16. Shetani atakuwa katika hali gani katika “abiso”?

16 “Abiso” ambamo Shetani na mashetani wake watatupwa ni nini? Neno la Kigiriki aʹbys·sos linalotumiwa na Yohana linamaanisha “ndefu kupita kiasi.” Linatafsiriwa pia “ndefu, bila mwisho,” na “shimo lisilo na mwisho.” Kwa hiyo, abiso ni mahali ambapo mutu haweze kufika isipokuwa tu Yehova na malaika “mwenye ufunguo wa abiso.” Katika abiso, Shetani atakuwa katika hali ya kutofanya jambo lolote kama katika kifo ili “asipotoshe mataifa tena.” Kwa kweli, huyo “simba anayenguruma” atanyamazishwa.​—1 Pet. 5:8.

MAMBO YATAKAYOONGOZA KWENYE KIPINDI CHA AMANI

17, 18. (a) Ni mambo gani yasiyoonekana ambayo tumejifunza? (b) Kisha mambo hayo kutokea, tutafurahia nini?

17 Huko mbele yetu kuna mambo makubwa na yatakayotetemesha dunia. Tunangojea kwa hamu kuona namna watawala watakavyotangaza “Amani na usalama!” Kisha tutajionea uharibifu wa Babiloni Mukubwa, shambulio la Gogu wa Magogu, vita ya Har-Magedoni, na kutupwa kwa Shetani katika abiso. Kisha mambo hayo, mambo mabaya yote yatakuwa yamepita, kwa hiyo tutaanza maisha mapya katika Utawala wa ile Miaka Elfu wa Kristo, ambamo tutafurahia “wingi wa amani.”​—Zab. 37:10, 11.

18 Zaidi ya mambo matano hayo ambayo tumejifunza, kuna ‘vitu vingine visivyoonekana’ tunavyopaswa “kukazia macho yetu.” Habari inayofuata itazungumuzia mambo hayo.

[Maelezo ya chini]

^ Mambo hayo kumi yanazungumuziwa katika habari hii na ile inayofuata.

^ Soma kitabu Ufunuo​—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! ukurasa wa 251-258.

^ Maneno “kuzikomesha falme hizi zote” kwenye Danieli 2:44 yanahusu falme, ao serikali kubwa za ulimwengu, zinazofananishwa na sehemu za sanamu. Hata hivyo, unabii mwengine wa Biblia unaonyesha kama “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” watajipanga ili kupigana na Yehova katika ‘vita ya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.’ (Ufu. 16:14; 19:19-21) Kwa hiyo, falme zinazofananishwa na sanamu hiyo na falme zingine zote zitaharibiwa kwenye Har-Magedoni.

^ Hatua ya mwisho ya kupondwa kwa kichwa cha nyoka itatokea mwishoni mwa miaka elfu wakati Shetani na mashetani wake watatupwa katika “ziwa la moto na kiberiti.”​—Ufu. 20:7-10; Mt. 25:41.

[Maulizo ya Funzo]

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 4, 5]

MAMBO MATANO TUNAYONGOJEA:

1 Tangazo la “Amani na usalama!”

2 Kushambuliwa na kuharibiwa kwa ‘Babiloni Mukubwa’

3 Kushambuliwa kwa watumishi wa Yehova

4 Vita ya Har-Magedoni

5 Kutupwa kwa Shetani na mashetani wake katika abiso