Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Gani Unaweza Kufaidika na Musamaha wa Yehova?

Namna Gani Unaweza Kufaidika na Musamaha wa Yehova?

Namna Gani Unaweza Kufaidika na Musamaha wa Yehova?

‘Yehova [ni] Mungu mwenye rehema na neema, si mwepesi wa hasira, anasamehe kosa na ubaya na zambi.’​—KUT. 34:6, 7.

TAFUTA MAJIBU YA MAULIZO HAYA

Namna gani Yehova aliwatendea Daudi na Manase walipofanya zambi, na kwa nini alitenda hivyo?

Sababu gani Yehova hakusamehe taifa la Israeli?

Tunapaswa kufanya nini ili kufaidika na musamaha wa Yehova?

1, 2. (a) Yehova alikuwa Mungu wa namna gani kwa Waisraeli? (b) Habari hii inatokeza ulizo gani?

 KATIKA siku za Nehemia, Walawi fulani walimuambia Yehova katika sala kwamba mababu wao ‘walikataa kusikiliza’ amri za Yehova. Lakini, mara kwa mara Yehova alikuwa ‘Mungu wa matendo ya kusamehe, mwenye neema na rehema, si mwepesi wa hasira na mwingi wa fazili zenye upendo.’ Yehova aliendelea kuwaonyesha fazili zisizostahiliwa wayahudi hao waliokuwa wakiishi uhamishoni katika siku za Nehemia.​—Neh. 9:16, 17.

2 Kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Namna gani ninaweza kufaidika na musamaha wa Yehova?’ Ili kupata jibu la ulizo hilo la maana, acheni tuzungumuzie namna Yehova alivyowasamehe wafalme wawili: Daudi na Manase.

ZAMBI NZITO ZA DAUDI

3-5. Namna gani Daudi alifikia kufanya zambi nzito?

3 Daudi alikuwa mutu aliyemuogopa Mungu, hata hivyo alifanya zambi nzito. Kati ya zambi hizo, kuna mbili zinazohusiana na Uriya na Bath-sheba. Zambi hizo zilikuwa na matokeo mabaya juu ya Daudi, Uriya na Bath-sheba. Lakini namna Mungu alivyomukaripia Daudi inatufundisha mengi kuhusu musamaha wa Yehova. Acheni tuone namna mambo yalivyotendeka.

4 Daudi alituma jeshi la Israeli kuenda kushambulia Raba, muji mukubwa wa Waamoni. Muji huo ulipatikana umbali wa kilometre 80 mashariki mwa Yerusalemu, mbali na Muto Yordani. Wakati huo, Daudi akiwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba yake huko Yerusalemu, aliomuona Bath-sheba akioga. Bwana yake hakukuwa nyumbani. Kwa sababu ya kumutazama sana Bath-sheba, Daudi alishikwa na tamaa na hivyo akafanya mipango ili mwanamuke huyo aletwe katika nyumba yake ya kifalme, na humo alizini pamoja naye.​—2 Sam. 11:1-4.

5 Alipoambiwa kama Bath-sheba amekua na mimba, Daudi alifanya mipango ili Uriya arudi Yerusalemu akitumaini kama atalala na bibi yake. Daudi alifanya yake yote ili Uriya alale nyumbani kwake, lakini haikuwezekana. Kwa hiyo, mufalme alimuandikia kwa siri mukubwa wa jeshi lake ili amutie Uriya mahali ambapo mashambulio yalikuwa “makali zaidi” na awaambie maaskari wengine warudi nyuma na kumuacha peke yake. Mutego huo ulishika, kwani Uriya alikufa katika mapambano kama vile Daudi alivyokuwa amepanga. (2 Sam. 11:12-17) Kwa hiyo, zaidi ya kufanya uzinifu, Daudi alimuuisha mutu ambaye hakufanya jambo lolote la kustahili kufa.

DAUDI ANAKUBALI MAKOSA YAKE

6. Mungu alifanya nini Daudi alipofanya zambi, na hilo linatufundisha nini kumuhusu Yehova?

6 Bila shaka, Yehova aliona mambo yote yaliyotendeka. Hakuna jambo hata moja lililofichwa machoni pake. (Met. 15:3) Mufalme Daudi alilazimika kumuoa Bath-sheba, ‘lakini jambo ambalo alikuwa amefanya lilikuwa baya machoni pa Yehova.’ (2 Sam. 11:27) Kwa hiyo basi, Mungu alifanya nini Daudi alipofanya zambi hizo nzito? Mungu alimutumia nabii Nathani. Yehova ni Mungu anayesamehe, kwa hiyo alitaka kujua ikiwa Daudi atatubu kabisa. Je, hautiwe moyo na namna Mungu alivyoshugulikia mambo? Mungu hakumulazimisha Daudi atubu lakini alimutuma Nathani amuelezee mufalme hadisi iliyoonyesha uzito wa zambi zake. (Soma 2 Samweli 12:1-4.) Njia hiyo ya kushugulikia hali hiyo ngumu ilikuwa na matokeo mazuri!

7. Daudi aliitikia namna gani kisha kusikia hadisi ya Nathani?

7 Mufalme Daudi alikubali kama mwanaume tajiri wa mufano wa Nathani alifanya makosa sana, na alimukasirikia mwanaume tajiri huyo. Kwa hiyo alimuambia Nathani hivi: ‘Kama Yehova anavyoishi, mutu huyo aliyefanya hivyo anastahili kufa!’ Zaidi ya hayo, Daudi alisema kama maskini huyo anapaswa kurudishiwa yale aliyonyanganywa. Kisha Nathani akamuambia maneno haya yenye kushtua. ‘Wewe mwenyewe ndiye yule mwanaume!’ Baadaye Nathani alimuambia kwamba “upanga” hautaondoka katika nyumba yake na musiba utaipiga familia yake. Alimuambia pia kwamba atafezeheshwa mbele ya watu kwa sababu ya makosa yake. Daudi alitambua uzito wa yale aliyofanya na alihuzunika sana na kukubali hivi: ‘Nimemutendea Yehova zambi.’—2 Sam. 12:5-14.

DAUDI ANAOMBA MUSAMAHA WA MUNGU

8, 9. (a) Namna gani Zaburi ya 51 inaonyesha namna Daudi alivyojisikia? (b) Na Zaburi hiyo inatufundisha nini kumuhusu Yehova?

8 Maneno ya wimbo ambao Daudi alitunga baadaye yanaonyesha namna alivyosikitika sana kwa sababu ya zambi alizofanya. Katika Zaburi 51 Daudi anamulilia Yehova na kuonyesha kama anakubali kabisa makosa yake. Daudi pia alitubu zambi zake. Daudi alihangaikia kwanza uhusiano wake na Yehova. Kwa hiyo alitubu zambi zake na kumuambia Yehova hivi: ‘Zidi yako wewe, wewe peke yako, nimetenda zambi. Uumbe moyo safi ndani yangu, Ee Mungu, Na kuweka ndani yangu roho mupya, iliyo imara. Unirudishie shangwe ya wokovu wako, Nawe unitegemeze kwa roho ya kupenda.’ (Zab. 51:1-4, 7-12) Unapomuambia Yehova kuhusu makosa yako, je, unamuambia mambo waziwazi na bila kuficha kitu?

9 Yehova hakumuepusha Daudi na matokeo mabaya ya makosa yake. Matokeo mengine yaliendelea kumutesa maisha yake yote. Hata hivyo, Yehova alimusamehe kwa sababu alionyesha roho ya kutubu ao “moyo uliovunjika na kupondwa.” (Soma Zaburi 32:5; Zab. 51:17) Mungu mweza​-yote anaelewa namna mutu aliyefanya zambi anavyojisikia na sababu zilizomuongoza kufanya zambi. Kwa hiyo, Mungu hakuomba waamuzi wanadamu wakatie Daudi na Bath-Sheba hukumu ya kifo kama vile Sheria ya Musa ilivyoonyesha. Lakini, yeye mwenyewe alihukumu Daudi na Bath-sheba na aliwaonyesha rehema. (Law. 20:10) Na hata alimuchagua mwana wao Sulemani ili awe mufalme juu ya taifa la Israeli.​—1 Nya. 22: 9, 10.

10. (a) Ni sababu gani nyingine ambayo labda ilimufanya Yehova amusamehe Daudi? (b) Tunapaswa kufanya nini ili Yehova atusamehe?

10 Labda sababu nyingine iliyomufanya Yehova amusamehe Daudi ni kwamba Daudi mwenyewe alimuonyesha Sauli rehema. (1 Sam. 24:4-7) Kama vile Yesu alivyosema, Yehova anatutendea namna tunavyowatendea wengine. Yesu alisema hivi: ‘Acheni kuhukumu ili musihukumiwe; kwa maana kwa hukumu munayohukumu, mutahukumiwa; na kwa kipimo munachopimia, watawapimia ninyi.’ (Mt. 7:1, 2) Inafariji kujua kama Yehova atatusamehe zambi zetu, hata ziwe nzito kama vile uzinifu na kuua! Mungu atatusamehe ikiwa tunawasamehe wengine, ikiwa tunatubu zambi zetu kwake, na ikiwa tunasikitika kabisa kwa sababu ya makosa hayo. Yehova anawatolea watenda-zambi wanaotubu kikweli “majira ya kuburudisha.”​—Soma Matendo 3:19.

MANASE ANAFANYA ZAMBI NZITO NA KUTUBU

11. Mufalme Manase alifanya mambo gani mabaya?

11 Acheni tuzungumuzie mufano mwingine unaopatikana katika Biblia unaoonyesha ni kwa kadiri gani Yehova yuko tayari kusamehe. Karibu miaka 360 kisha Daudi kuanza kutawala, Manase akawa mufalme wa Yuda. Kwa miaka 55 ya utawala wake, Manase alifanya mambo mengi mabaya, na Yehova alimuhukumu kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza aliyofanya. Manase alijenga mazabahu kwa ajili ya Baali, aliabudu “jeshi lote la mbinguni,” aliwapitisha watoto wake katika moto, alifanya matendo mengi ya uchawi, na mambo mengine. Kwa kweli, “alifanya kwa kiasi kikubwa yale yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.”​—2 Nya. 33:1-6.

12. Manase alifanya nini ili kumurudilia Yehova?

12 Mwishowe, Manase alihamishwa kutoka katika inchi yake na kufungwa katika gereza huko Babiloni. Labda huko alikumbuka maneno haya ambayo Musa aliwaambia Waisraeli: ‘Utakapokuwa katika ziki kali na maneno yote haya yawe yamekupata mwishoni mwa siku hizo, basi utarudi kwa Yehova Mungu wako na kuisikiliza sauti yake.’ (Kum. 4:30) Manase alimurudilia Yehova. Namna gani? ‘Aliendelea kujinyenyekeza sana’ na ‘aliendelea kusali’ kwa Mungu (kama inavyoonyeshwa katika picha iliyo kwenye ukurasa wa 21). (2 Nya. 33:12, 13) Hatujue kwa kweli maneno ambayo Manase alitumia katika sala zake, lakini tunafikiri kwamba yalifanana kidogo na maneno ya Mufalme Daudi katika Zaburi 51. Tunajua tu kwamba Manase alisikitika kabisa kwa sababu ya makosa yake.

13. Sababu gani Yehova alimusamehe Manase?

13 Yehova alijibu namna gani sala ya Manase? “Yeye akakubali kusihiwa naye [Manase] kisha Yeye akasikia ombi lake la kutaka kibali.” Kama vile Daudi alivyofanya, Manase alitambua uzito wa zambi zake na kutubu kikweli. Hiyo ndiyo sababu Mungu alimusamehe na kumurudisha Yerusalemu ili awe tena mufalme. Kwa hiyo, “Manase akapata kujua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.” (2 Nya. 33:13) Huu ni mufano mwingine unaofariji na kuonyesha kwamba Mungu wetu mwenye rehema anasamehe wale wanaotubu kikweli!

JE, YEHOVA ANASAMEHE MAKOSA YOTE?

14. Yehova anamusamehe mutu wa namna gani?

14 Wengi kati yetu hawajawahi kufanya zambi kama zile za Daudi na Manase. Hata hivyo, kujua kwamba Yehova aliwasamehe wafalme hao wawili kunatusaidia kuelewa kwamba Mungu yuko tayari kusamehe hata zambi nzito ikiwa mutu aliyezifanya anatubu kikweli.

15. Tunajua namna gani kwamba Yehova hasamehe makosa yote?

15 Je, tunapaswa kuwaza kwamba Yehova anasamehe zambi zote? Hapana kabisa! Ili kuelewa jambo hilo, acheni tulinganishe namna Daudi na Manase walivyoitikia walipofanya zambi na namna Waisraeli waasi wa Yuda walivyoitikia. Mungu alimutuma Nathani ili aende kumuona Daudi na kumupatia nafasi ya kutubu. Daudi alikubali kwa shukrani musaada huo. Wakati Manase alijikuta katika matatizo, alitambua kama alipaswa kutubu kikweli. Lakini, mara nyingi wakaaji wa Israeli na Yuda hawakutubu. Kwa hiyo, Yehova hakuwasamehe. Badala yake, aliwatumia mara kwa mara manabii wake ili wawaonye kuhusu mwenendo wao mubaya. (Soma Nehemia 9:30.) Hata kisha Waisraeli kutoka Babiloni na kurudi katika inchi yao, Yehova aliendelea kuwatumia wajumbe waaminifu, kama vile kuhani Ezra na nabii Malaki. Wakati Waisraeli walifanya mapenzi ya Yehova, walipata furaha nyingi.​—Neh. 12:43-47.

16. (a) Taifa la Israeli lilipata matokeo gani kwa sababu halikutubu? (b) Yehova anamupa mutu mumoja​-mumoja wa taifa hilo nafasi gani?

16 Kisha Yesu kutumwa duniani na kutoa zabihu kamilifu ya ukombozi, Yehova hakukubali tena zabihu za wanyama za Waisraeli. (1 Yoh. 4:9, 10) Alipokuwa mwanadamu, Yesu alionyesha maoni ya Baba yake aliposema maneno haya: ‘Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na ambaye huwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwake, ni mara ngapi nilitaka kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake! Lakini hamukutaka.’ Kwa hiyo aliongezea hivi: ‘Tazama! Nyumba yenu mumeachiwa hali ya ukiwa.’ (Mt. 23:37, 38) Kwa hiyo, Israeli la kiroho lilichukua nafasi ya taifa hilo lenye kutenda zambi na lisilotubu. (Mt. 21:43; Gal. 6:16) Lakini, namna gani mutu mumoja​-mumoja aliyezaliwa katika taifa hilo la Israeli la kimwili? Kila mutu katika taifa hilo anaweza kusamehewa na Yehova ikiwa anamuamini Mungu na kutia imani katika zabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo. Nafasi hiyo itatolewa pia kwa wale waliokufa bila kutubu zambi zao lakini ambao watafufuliwa ili kuishi katika dunia mupya.​—Yoh. 5:28, 29; Mdo. 24:15.

FAIDIKA NA MUSAMAHA WA YEHOVA

17, 18. Namna gani tunaweza kufaidika na musamaha wa Yehova?

17 Tunapaswa kufanya nini ili kufaidika na musamaha wa Yehova? Bila shaka tunapaswa kutenda kama Daudi na Manase. Tunapaswa kujua hali yetu ya zambi, kutubu makosa yetu, kutafuta kwa moyo wote musamaha wa Yehova, na kumuomba atupatie moyo safi. (Zab. 51:10) Ikiwa tumefanya zambi nzito, tunapaswa kutafuta musaada wa kiroho wa wazee. (Yak. 5:14, 15) Hata kama tumefanya zambi gani, inafariji kujua kwamba, Yehova iko kama alivyomuambia Musa kuhusu sifa zake, yeye ni ‘Mungu mwenye rehema na neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fazili zenye upendo na kweli, anayehifazi fazili zenye upendo kwa ajili ya maelfu, anayesamehe kosa na ubaya na zambi.’ Yehova hajabadilika.​—Kut. 34:6, 7.

18 Yehova alitumia ulinganisho wenye nguvu ili kuahidia Waisraeli wanaotubu kwamba atasamehe makosa yao kabisa, zambi zao zilizo “nyekundu” zitakuwa nyeupe kama ‘teluji.’ (Soma Isaya 1:18.) Namna gani basi tunaweza kufaidika na musamaha wa Yehova? Tunaweza kusamehewa kabisa zambi zetu ikiwa tunafurahia musamaha wa Yehova na kutubu kikweli.

19. Tutazungumuzia nini katika habari inayofuata?

19 Kwa kuwa Yehova anatusamehe, namna gani tunaweza kumuiga wakati wengine wanapotukosea? Namna gani tunaweza kuwasamehe wanaofanya zambi nzito lakini ambao wanatubu kikweli baadaye? Habari inayofuata itatusaidia kuchunguza moyo wetu ili tuwe kama Baba yetu, Yehova, ambaye ni “mwema na tayari kusamehe.”​—Zab. 86:5.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 24]

Yehova alimusamehe Manase na kumurudisha Yerusalemu ili awe tena mufalme