Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari zilizozungumuziwa hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Basi, jaribu kujibu maulizo yanayofuata:

Namna gani tunaweza kuzuia ulimi wetu usiwashe moto?

Tunapaswa kuchunguza moyo wetu. Kuliko kutilia shaka nia ya ndugu ao dada yetu, ni vizuri tujiulize kwa nini tunamuwazia vibaya. Labda tunafanya hivyo kwa sababu tunapenda kuonyesha mambo tuliyotimiza katika maisha ao kujionyesha tu ili kuwashusha wengine. Lakini, tujue kama kufanya hivyo kunaleta matokeo mabaya sana.​—15/08, ukurasa wa 21.

Namna gani Sheria ya Musa ilionyesha kama Mungu anawahangaikia wanawake?

Wanawake Waisraeli walikuwa na uhuru mwingi, na waliruhusiwa kusoma. Waliheshimiwa na walionwa kuwa wa lazima, na haki zao zililindwa.​—01/09, ukurasa wa 5-7.

Ni mambo gani yatatokea mbele tu ya mwisho kufika?

Tangazo la “Amani na usalama!” litatolewa. Mataifa yatashambulia na kuharibu Babiloni Mukubwa. Watumishi wa Mungu watashambuliwa pia. Vita ya Har-Magedoni itaanza na kisha Shetani na mashetani wake watatupwa katika abiso.​—15/09, ukurasa wa 4.

Kutokujua wakati mwisho utakuja kunatuletea faida gani?

Kutokujua siku ule mwisho utakapokuja kunafunua kabisa mambo yaliyo katika moyo wetu. Kunatutolea nafasi ya kufurahisha moyo wa Yehova. Kunatusaidia tuendelee kuishi maisha yasiyo ya uchoyo na kunatusaidia tumutegemee Yehova na Neno lake. Pia, kunafanya mateso yatusafishe na kutia nguvu imani yetu.​—15/09, ukurasa wa 24-25.

Namna gani tunaweza kutumia andiko la Mwanzo 3:19 ili kuzungumuza na mutu anayeamini moto wa mateso?

Andiko hilo linaonyesha kama wakati Adamu angekufa, hangeenda katika moto wa mateso, lakini alipaswa kurudi katika mavumbi ya udongo.​—01/10, ukurasa wa 13.

Ni nani wanaofananishwa na zile “nyota saba” zilizo katika mukono wa kuume wa Yesu zinazozungumuziwa katika andiko la Ufunuo 1:16, 20?

“Nyota” hizo zinafananisha wazee watiwa​-mafuta kutia ndani wazee wengine wote katika makutaniko.​—15/10, ukurasa wa 14.

Bibi na bwana wanaweza kufanya nini ili kushugulikia madeni waliyonayo?

Bibi na bwana wanapaswa kuzungumuzia madeni yao waziwazi na kwa utulivu. Ni vizuri pia wachunguze namna wanavyotumia feza zao. Je, wanaweza kuongeza mapato yao na kupunguza garama zao? Bibi na bwana wanapaswa kuamua namna watakavyoshugulikia madeni yao, labda kwa kuzungumuza na wale waliowakopesha. Lakini wanapaswa kuwa tayari kukubali hali yoyote inayoweza kutokea na wanapaswa kutia feza pa nafasi inayofaa. (1 Tim. 6:8)​—01/11, ukurasa wa 19-21.

Kulingana na andiko la Isaya 50:4, 5, namna gani Mwana muzaliwa-pekee wa Mungu alionyesha unyenyekevu?

Andiko hilo linaonyesha kama mutu aliye na ‘ulimi wa waliofundishwa hatageuka upande ulio kinyume.’ Yesu alionyesha unyenyekevu kwa kusikiliza kwa uangalifu sana mambo ambayo Baba yake alimufundisha. Yesu alikuwa tayari na alifurahia kufundishwa na Mungu, na alitazama kwa uangalifu kabisa namna Mungu alivyowatendea wanadamu wenye zambi kwa unyenyekevu na huruma.​—15/11, ukurasa wa 11.

Tembre iliyochapishwa na poste ya Estonie ilishuhudia namna gani uaminifu ambao Mashahidi wa Yehova walionyesha?

Katika mwaka wa 2007, Biro ya Poste ya Estonie ilitoa tembre ya posta iliyokumbusha mupango wa Staline wa kuwaangamiza Waestonia. Namba 382 iliyokuwa juu ya tembre hiyo ilionyesha hesabu ya Mashahidi na watoto wao ambao walichukuliwa mbali na inchi yao mupaka kwenye kambi za mateso za Russie katika 1951.​—01/12, ukurasa wa 27-28.