Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mbele ya kujifunza kweli, kwa sababu tulipenda kupata mutoto, waganga walichukua mbegu yangu ya uzazi na wakaiunganisha na yai ao mbegu ya uzazi ya bibi yangu. Lakini walitumia tu chembe moja kati ya zile zilizounganishwa na zile zilizobaki walizigandisha na kuzichunga katika mashini. Je, ninapaswa kuomba mbegu ao chembe hizo za uzazi zilizounganishwa na zilizobaki ili ziharibiwe ao ziendelee kuchungwa?

▪ Hilo ni moja ya maulizo mengi ya lazima ambayo bwana na bibi wanaochagua kupata mutoto kwa ufundi wa kutungisha mimba inje ya tumbo la uzazi wanapaswa kufikiria kwa uzito. Ni bibi na bwana ndio watatoa hesabu mbele ya Yehova kuhusu uamuzi wao. Hata hivyo, kujua ufundi huo kunaweza kuwasaidia wajue uamuzi ambao watachukua.

Katika mwaka wa 1978 mwanamuke mumoja huko Angleterre alikuwa wa kwanza kuzaa mutoto kupitia mimba iliyotungwa inje ya tumbo la uzazi. Mwanamuke huyo alikuwa na tatizo kwa sababu njia zake mbili zinazopeleka mbegu za uzazi za mwanaume kwenye tumbo lake la uzazi zilikuwa zimefungana, kwa hiyo, mbegu za uzazi za mwanaume hazingeweza kupita ili kukutana na mbegu ao yai lake. Kwa njia ya upasuaji, waganga walichukua yai ao mbegu ya uzazi ya mwanamuke huyo, walilitia katika chombo fulani kilicho kama chupa, na wakaiunganisha na mbegu ya uzazi ya bwana yake katika chombo hicho. Kisha chembe hiyo iliingizwa katika tumbo la uzazi la mama ili iendelee kukomaa kwa njia ya kawaida. Kisha muda fulani, mwanamuke huyo alizaa mutoto mwanamuke. Ufundi huo na njia zake mbalimbali unaitwa katika Kifaransa fécondation in vitro (FIV).

Ufundi huo unaweza kuachana kulingana na kila inchi, lakini kwa kawaida unafanywa hivi: Kwa muda wa majuma fulani mwanamuke anapewa dawa za kusaidia kifumba mbegu chake cha uzazi kizae mayai ao mbegu nyingi. Bwana anaweza kuombwa aguse-guse kiungo chake cha uzazi ili atoe mbegu ya uzazi na kisha inasafishwa. Sasa mbegu hiyo ya uzazi na ile ya mwanamuke inaunganishwa ao kutungishwa mimba katika mashini. Mbegu hiyo ya mwanamuke inaweza kutungwa na kuanza kujigawanya​-gawanya ili kuwa viini (embryons). Kisha siku moja ao zaidi, waganga wanachunguza viini hivyo kwa uangalifu ili kuangalia viini ambavyo vimeharibika na vile vilivyo katika hali nzuri ambavyo wanaweza kuingiza katika tumbo la uzazi la mwanamuke ili sasa viweze kuendelea kukomalia humo. Kisha siku tatu hivi, kwa kawaida wanaingiza katika tumbo la uzazi la mwanamuke viini viwili ao vitatu kati ya hivyo ambavyo vimeonekana kuwa na hali nzuri zaidi ili kuwe na uwezekano zaidi wa mwanamuke kubeba mimba. Ikiwa kiini kimoja ao viwili vinaingizwa katika tumbo la uzazi na mwanamuke anabeba mimba, na basi kuna matumaini kwamba atazaa mutoto.

Lakini sasa wanafanya nini na viini hivyo vingine vyenye kuwa katika hali nzuri vinavyobaki, hata na vile vilivyo haribika? Viini hivyo vikiachwa vyenyewe hakuna kile kinaweza kuishi. Ndiyo sababu, mbele ya wakati viini hivyo vinagandishwa katika maji yenye gaze isiyo na rangi ao harufu inayoitwa nitrojene. Sababu gani? Kwa sababu ikiwa viini vilivyoingizwa katika tumbo la uzazi havifanikiwe, wanaweza kutumia tena bila kazi nyingi vile vilivyochungwa. Lakini, jambo hilo linatokeza maulizo fulani. Wenzi wengi, kama bwana na bibi waliouliza ulizo lililo hapo mwanzoni, hawajue uamuzi wa kuchukua kuhusu viini hivyo vilivyobaki na kugandishwa. Pengine hawatake tena kuwa na watoto wengine. Labda wanaona kwamba wamezeeka ao hawana tena feza za kulipia jambo hilo ao kumukomalisha mutoto huyo. Labda wanaweza kuogopa hatari zinazotokana na mwanamuke kutungwa​-tungwa mimba. * Kifo ao kuvunjika kwa ndoa kati ya bibi na bwana vinaweza pia kufanya mambo yawe magumu. Kwa kweli, kuna mambo mengi ya kufikiria, kwa hiyo, wenzi fulani wanaendelea kulipa feza ili viini hivyo viendelee kulindwa kwa miaka fulani.

Katika mwaka wa 2008, muganga fulani anayejua vizuri ufundi huo alieleza katika gazeti The New York Times kwamba wenzi wengi wanashindwa kufanya uamuzi kuhusu viini hivyo vilivyobakia. Gazeti hilo liliendelea kusema hivi: “Kwa vyovyote, viini karibu 400 000 vimegandishwa na kulindwa katika mashini katika hospitali mbalimbali za inchi yake, na hesabu yavyo inaongezeka kila siku . . . Ikiwa viini vimegandishwa vizuri vinaweza kuendelea kuishi kwa kipindi cha miaka kumi ao zaidi, lakini vinapoyeyushwa si vyote vinavyoendelea kuishi.” Jambo hilo linafanya Wakristo wengine wafikiri sana mbele ya kuchukua uamuzi. Sababu gani?

Bwana na bibi Wakristo wanaofikiria ufundi huo wa kutunga mimba inje ya tumbo la uzazi wanaweza kufikiria hali zote zinazohusika. Kwa mufano, labda Mukristo anaweza kufikiri kama hali hiyo inafanana na hali ya mutu fulani wa familia yake ambaye ni mugonjwa na aliye karibu kufa, lakini anasaidiwa na mashini, kama vile mashini ya kumusaidia kupumua. Kulingana na Kutoka 20:13 na Zaburi 36:9, Wakristo wa kweli wanakataa kufupisha maisha ya mugonjwa kama huyo; kwa sababu wanaona uzima kuwa kitu kitakatifu. Amkeni! ya Mwezi wa 8, 1974, ilisema hivi: ‘Kwa sababu wanaheshimu maoni ya Mungu anayeona uzima kuwa mutakatifu, Wakristo wanaheshimu zamiri zao na sheria za serikali, wale wanaotaka kuishi kulingana na kanuni za Biblia hawaweze hata kidogo kuruhusu waganga wamuue mushiriki wa familia sababu ameteseka sana,’ kufanya hivyo ni kumuua mutu kimakusudi. Lakini, katika hali fulani, ikiwa mutu huyo anaishi kwa ufundi wa mashini tu, ni kusema mashini ndio inamuzuia asikufe, basi watu wa familia wanapaswa kuamua ikiwa njia hiyo ya mashini itaendelea kutumiwa ao kuondoa mashini hiyo inayomutegemeza.

Kwa kweli, hali hii ni tofauti na ile ya bibi na bwana waliokubali ufundi wa kutunga mimba inje ya tumbo la uzazi, na ambao kwa sasa wamekubali viini vilindwe. Lakini uamuzi moja ambao wanaweza kufanya ni ule wa kuomba viini vilivyowekwa katika mashini fulani ili kugandishwa, viondolewe humo na kuacha viyeyuke. Kwa sababu vikiondolewa katika mashini hiyo haviweze kuishi tena. Bibi na bwana wanapaswa kuamua wenyewe ikiwa wataruhusu jambo hilo.​—Gal. 6:7.

Ikiwa bibi na bwana waliamua kutungisha mimba inje ya tumbo la uzazi ili wapate mutoto, labda wanaweza kuchagua kukubali matokeo yoyote kuhusu jambo hilo la kufanya viini viendelee kugandishwa katika kusudi la kuvitumia wakati ujao ili kujaribu kupata mutoto. Lakini, wengine wanaweza kuamua kwamba jambo hilo halipaswe kuendelea hivyo kwa sababu ni mashini ndiyo inayofanya viini hivyo viendelee kuishi. Wakristo wanaofanya uamuzi juu ya jambo hilo wanapaswa kutumia zamiri yao iliyozoezwa na Biblia na kujua kwamba watatoa hesabu ya uamuzi wao kwa Mungu. Nia yao inapaswa kuwa kulinda zamiri yao ikiwa safi, na pia hawapaswe kuwakwaza wengine.​—1 Tim. 1:19.

Muganga mumoja aliyejifunza sana namna kemikali inavyofanya kazi ndani ya mwili, alitambua kwamba wenzi wengi wa ndoa “walikuwa bado wenye kuvurugika na kuhangaishwa sana kwa sababu ya uamuzi ambao wanapaswa kufanya kuhusu kuharibu ao kutoharibu viini vyao vilivyokuwa katika mashini katika hali ya kugandishwa.” Alimalizia kwa kusema hivi: “Wenzi wengi waliona kama hawana uamuzi wowote muzuri wanaoweza kuchukua.”

Kwa kweli, Wakristo wa kweli wanaofikiria ufundi wa kutunga mimba inje ya tumbo la uzazi wanapaswa kufikiria kwa uzito kila jambo linalohusu ufundi huo. Biblia inashauri hivi: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha, lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.’​—Met. 22:3.

Mwanaume na mwanamuke wanaoishi pamoja bila kuoana mbele ya serikali, wanajifunza Biblia na wanataka kubatizwa, lakini haiwezekane kuandikisha ndoa yao kwenye serikali sababu mwanaume hajulikane kisheria kuwa raia wa inchi hiyo. Serikali haimuruhusu mugeni asiyejulikana kisheria kufunga ndoa. Je, wanaweza tu kutia sinyatire zao kwenye Kiapo cha Uaminifu na kisha wabatizwe?

▪ Labda kufanya hivyo kunaweza kuonekana kuwa njia ya kumaliza matatizo hayo, lakini hakupatane na Maandiko. Acheni tuzungumuzie mambo matatu kuhusu kutia sinyatire kwenye Kiapo cha Uaminifu. Sababu gani jambo hilo linafanywa, namna gani linafanywa na ni wapi jambo hilo linaweza kufanywa.

Kiapo cha Uaminifu ni maandishi ambayo mwanaume na mwanamuke, ambao sheria hairuhusu kufunga ndoa, wanaweza kutia sinyatire zao juu yayo mbele ya mashahidi. Kupitia maandishi hayo, wanaapa kwamba kila mumoja wao atabaki mwaminifu kwa mwenzake, na kwamba itakapowezekana wataandikisha ndoa yao kwenye serikali. Kutaniko linaweza kuona kama mwanaume na mwanamuke huyo wameapa mbele ya Mungu na wanadamu kwamba watakuwa waaminifu mumoja kwa mwenzake. Kwa hiyo ndoa yao inaweza kuonwa kama ndoa ambayo imekubaliwa na serikali.

Sababu gani na wakati gani mwanaume na mwanamuke wanaweza kutia sinyatire zao kwenye Kiapo cha Uaminifu? Yehova ndiye aliyeanzisha mupango wa ndoa ya wanadamu na anaiheshimu sana. Mwana wake alisema hivi: ‘Kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.’ (Mt. 19:5, 6; Mwa. 2:22-24) Yesu aliongeza tena hivi: ‘Mutu yeyote anayemutaliki [anayeachana na] muke wake na kumuoa mwengine, ila kwa sababu ya uasherati, anafanya uzinzi.’ (Mt. 19:9) Kwa hiyo, “uasherati,” ndio musingi pekee wa Kimaandiko unaoweza kufanya ndoa ivunjike. Kwa mufano, ikiwa mwanaume anafanya kitendo cha ndoa na mutu mwengine, bibi yake iko huru kuamua kama atavunja ndoa yao ao hapana. Bibi yake akiamua kuvunja ndoa yao, yeye iko huru kabisa kuolewa na mwanaume mwengine.

Lakini, zamani katika inchi fulani, dini kubwa hazikukubaliana na jambo hilo lililo wazi ambalo Biblia inafundisha. Dini hizo zilifundisha kama hakuna sababu yoyote inayoweza kumufanya mutu avunje ndoa. Kwa hiyo, mahali fulani ambako dini ilikuwa na uwezo mukubwa, sheria ya serikali hairuhusu kuvunja ndoa, hata kwa musingi ule ambao Yesu alizungumuzia. Katika inchi nyingine, inawezekana kuvunja ndoa, lakini si rahisi na inachukua muda murefu na pesa nyingi. Inaweza kuchukua miaka mingi sana mbele ya serikali kukubali ndoa ivunjike. Katika inchi hizo, ni kama vile dini ao serikali ‘inazuia’ jambo ambalo Mungu anakubali.​—Mdo. 11:17.

Kwa mufano, labda bwana na bibi wanaishi katika inchi ambako haiwezekane ao ni vigumu kabisa kuvunja ndoa, ao labda inaweza kuchukua miaka mingi sana kufanya hivyo. Ikiwa wamefanya yote wanayoweza ili kuvunja ndoa ya zamani inayojulikana kisheria na ikiwa wanastahili machoni pa Mungu kuoana, wanaweza kutia sinyatire zao kwenye Kiapo cha Uaminifu. Huo ni mupango wa rehema wa kutaniko la Kikristo kwa ajili ya wale wanaoishi katika inchi kama hizo. Hata hivyo, mupango huo haupaswe kutumiwa katika inchi ambamo serikali inaruhusu kuvunja ndoa, hata ikiwa kufanya hivyo kutachukua feza nyingi na kunaomba mambo mengi.

Kwa sababu ya kutokuelewa mupango huo, ndugu na dada wengine ambao wanaishi katika inchi ambako serikali inaruhusu kuvunja ndoa wameuliza ikiwa wao pia wanaweza kutia sinyatire kwenye Kiapo cha Uaminifu sababu kuvunja ndoa kunachukua muda murefu na feza nyingi.

Mwanaume na mwanamuke tuliozungumuzia mwanzoni wanaishi pamoja bila kuoana kisheria na sasa wanataka kuoana kisheria. Kulingana na Maandiko, kila mumoja wao iko huru; hakuna aliyekuwa na mwenzi mwengine wa ndoa hapo zamani. Lakini, mwanaume hana vikaratasi vya serikali vinavyomuruhusu kuwa katika inchi hiyo na kwa hiyo serikali haikubali kuhalalisha ao kuandikisha ndoa ya mugeni. (Katika inchi nyingi, serikali inaruhusu watu wafunge ndoa hata ikiwa mumoja ao wote wawili hawajulikane kuwa raia wa inchi hiyo.) Kiapo cha Uaminifu hakipaswe kufanywa katika inchi ambamo serikali inawaruhusu watu kuvunja ndoa. Lakini, kumbuka kwamba mwanaume na mwanamuke tunaozungumuzia hawatafute kuvunja ndoa lakini serikali haikubali kuandika ao kuhalalisha ndoa yao. Wote wawili wako huru kuoana. Lakini, wataoana namna gani kwa sababu mwanaume hajulikane kisheria kuwa raia wa inchi hiyo? Basi wanaweza kuenda katika inchi nyingine ambako serikali itakubali kuandika ao kuhalalisha ndoa yao. Ao wanaweza kuoana katika inchi wanamoishi ikiwa bwana anajikaza kuchukua hatua zinazohitajiwa ili kupata vikaratasi vya serikali vitakavyomuruhusu kubaki katika inchi hiyo.

Kwa kweli, mwanaume na mwanamuke huyo wanaweza kupatanisha maisha yao na sheria za Mungu na za serikali. (Mk. 12:17; Rom. 13:1) Tunatumaini kama watafanya hivyo. Kisha, wanaweza kustahili kubatizwa.​—Ebr. 13:4.

[Maelezo ya chini]

^ Lakini itakuwa namna gani ikiwa kitoto kinachoanza kukomaa katika tumbo la uzazi ao ikiwa vile viini vinakuwa na kosoro? Kuharibu viini kimakusudi ni kuondoa mimba. Kwa kawaida viini vinapoingizwa katika tumbo la uzazi, mwanamuke anaweza kubeba mimba ya watoto wengi (mapasa, watoto watatu ao zaidi) na jambo hilo linaleta matatizo zaidi, kama vile kuzaa watoto wasiofikia bado wakati wao na kupoteza damu wakati wa kuzaa. Waganga wanaweza kumushauri mwanamuke aliyetungwa mimba ya watoto wengi kwa ufundi huo aue kitoto kimoja ao zaidi. Kufanya hivyo ni kuondoa mimba kimakusudi, na jambo hilo ni kuua mutu.​—Kut. 21:22, 23; Zab. 139:16.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 14]

Wakristo wanaofanya uamuzi juu ya jambo hilo wanapaswa kutumia zamiri yao iliyozoezwa na Biblia na kujua kwamba watatoa hesabu ya uamuzi wao kwa Mungu

[Sanduku katika ukurasa wa 15]

NJIA ZINGINE ZA KUTUNGA MIMBA INJE YA TUMBO LA UZAZI

Ufundi wa kutunga mimba inje ya tumbo la uzazi la mwanamuke, ni kusema fécondation in vitro (FIV) umeendelea sana, na jambo hilo limetokeza njia zingine zisizopatana na mawazo ya Mungu kama yanavyoonyeshwa katika Biblia. Kwa mufano, yai ao mbegu ya uzazi ya mwanamuke inaweza kutungwa mimba na mbegu ya uzazi ya mwanaume asiye bwana yake. Labda atafikia kukubali viini hivyo viingizwe katika tumbo lake la uzazi. (Wakati fulani wanawake ambao wameolewa na wanawake wenzao wanatumia njia hii.) Ao wakati mwengine mbegu ya uzazi ya mwanaume inaweza kuunganishwa na mbegu ya mwanamuke asiyekuwa bibi yake. Kisha bibi ya mwanaume huyo anaweza kukubali viini vilivyotokana na muungano huo viingizwe katika tumbo lake la uzazi.

Njia nyingine ni kuchukua viini vilivyosalia wakati wengine walitunga mimba. Viini hivyo vinavyotiwa katika tumbo la mwanamuke havitokane na mayai ya mwanamuke huyo ao shahawa za bwana yake. Lakini katika njia nyingine, mbegu ya uzazi ya bwana inaweza kuunganishwa na mbegu ya uzazi ya bibi yake inje ya tumbo la uzazi. Kisha viini hivyo vinaingizwa katika tumbo la uzazi la mwanamuke mwengine atakayewazalia mutoto. *

Watumishi wa Yehova hawapaswi kutumia njia hizo sababu wanatii uongozi huu wa Mungu: ‘Nawe usimupe muke wa mwenzako shahawa inayokutoka awe asiye safi kutokana nayo.’ (Law. 18:20, 29; Met. 6:29) Kuingiza shahawa za bwana ndani ya mayai ya mwanamuke asiyekuwa bibi yake ni kufanya jambo ambalo Biblia inaita, por·neiʹa, ao uasherati. Kufanya hivyo ni kutumia vibaya viungo vya uzazi.​—Mt. 5:32; 1 Kor. 5:11; 6:9, 18; Ebr. 13:4.

[Maelezo ya chini]

^ Gazeti Amkeni! la tarehe 08/03/1993, ukurasa wa 26-27, linazungumuzia kirefu maoni ya Wakristo kuhusu mama kumuomba mwanamuke mwengine amuzalie mutoto.