Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani Munara wa Mulinzi Ulitolewa Katika Kiingereza Rahisi?

Sababu Gani Munara wa Mulinzi Ulitolewa Katika Kiingereza Rahisi?

Sababu Gani Munara wa Mulinzi Ulitolewa Katika Kiingereza Rahisi?

KWA miaka mingi wanaume na wanawake duniani pote wamefurahia na kufaidika na habari zinazotegemea Biblia zinazochapishwa katika Munara wa Mulinzi. Katika Mwezi wa 7, 2011, gazeti la kwanza la Munara wa Mulinzi lilichapishwa katika Kiingereza rahisi. Gazeti hilo lilieleza hivi: “Gazeti hili jipya litajaribiwa kwa mwaka mumoja, na ikiwa litasaidia, litaendelea kuchapishwa.”

Tunafurahi sasa kuwajulisha kwamba tumeamua kuendelea kuchapisha gazeti hilo. Zaidi ya hilo, katika siku zinazokuja Munara wa Mulinzi utapatikana pia katika Kifaransa rahisi, Kiportige rahisi, na Kiespanyole rahisi.

SABABU GANI WATU WANAFURAHIA GAZETI HILO?

Kisha kupata Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi, wengi katika Pacifique Sud walisema hivi: “Sasa ndugu na dada wanaweza kuelewa vizuri kabisa habari zilizo katika Munara wa Mulinzi.” Barua ingine ilisema hivi: “Sasa ndugu wanatumia wakati waliokuwa wanatumia kutafuta maana ya maneno na kufasiria usemi mbalimbali ili kuelewa maandiko yaliyotajwa na namna yanavyopatana na habari.”

Mwanafunzi aliyemaliza masomo ya juu huko États-Unis anasema hivi: “Kwa miaka 18 nilizungumuza na kuandika luga isiyo wazi inayotumiwa kwenye masomo ya juu. Nilianza kuwa na tabia ya kuzungumuza na kufikiri katika njia ngumu isivyolazima. Nilitambua kwamba nilipaswa kubadilisha sana namna yangu ya kufikiri na kusema.” Sasa yeye ni muhubiri mwenye matokeo, na anaandika hivi: “Gazeti Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi limenisaidia sana. Luga rahisi inayotumiwa katika gazeti hilo inanisaidia nitumie maneno yaliyo rahisi kuelewa.”

Kuhusiana na gazeti Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi, dada mumoja wa Angleterre aliyebatizwa katika mwaka wa 1972 aliandika hivi: “Niliposoma gazeti la kwanza, nilisikia kama Yehova amekaa pembeni yangu akiwa amezungusha mukono wake nyuma ya mabega yangu na kusoma pamoja nami. Ilikuwa kama vile baba anavyomusomea mutoto wake hadisi mbele ya kulala.”

Dada mumoja anayetumikia kwenye Beteli ya États-Unis aliyebatizwa miaka zaidi ya 40 iliyopita alisema kwamba gazeti hilo limemusaidia kuelewa mambo kwa njia mupya. Kwa mufano, kisanduku ‘Maana ya Maneno Fulani’ katika gazeti la tarehe 15 Mwezi wa 9, 2011, kilifasiria maneno “wingu la mashahidi” linalopatikana katika Waebrania 12:1 hivi: “Mashahidi hao walikuwa wengi sana na haingewezekana kuwahesabu.” Alisema: “Mafasiriyo hayo yalinisaidia kuelewa vizuri zaidi andiko hilo.” Kuhusu funzo la kila juma, dada huyo alisema: “Hata ikiwa mutoto anasoma moja kwa moja maneno ya Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi ili kujibu, maneno yake yanatofautiana na yale yaliyo katika gazeti la kawaida ambalo watoto wengi walitumia hapo mbele. Kwa hiyo wasikilizaji wanaelewa vizuri kabisa majibu yake.”

Dada mwengine anayetumika kwenye Beteli aliandika hivi: “Ninangojea kwa hamu kusikiliza majibu ya watoto katika kutaniko letu. Gazeti Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi limewasaidia kueleza waziwazi mambo wanayoamini. Maelezo yao yamenitia moyo.”

Ili kuonyesha namna alivyofurahia gazeti hilo dada mumoja aliyebatizwa katika mwaka wa 1984, alisema hivi: “Ninajisikia kama gazeti hilo liliandikwa zaidi sana kwa ajili yangu. Gazeti hilo linanisaidia kuelewa kwa urahisi mambo ninayosoma. Sasa siogope kutoa majibu wakati wa funzo la Munara wa Mulinzi.”

WAZAZI WANALIFURAHIA

Mama mumoja aliye na kijana wa miaka saba alisema hivi: “Kutayarisha funzo la Munara wa Mulinzi kulichukua muda murefu na kulichokesha sababu nililazimika kumufasiria kijana wangu maneno mengi.” Gazeti Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi limemusaidia namna gani? Yeye anaandika hivi: “Ninashangaa kuona kwamba kijana wangu anaweza kunisaidia kusoma mafungu na anaelewa kabisa habari anayosoma. Kwa kuwa maneno ni mepesi na misemwa ni mifupi, yeye haogope. Ameanza kutayarisha majibu yake yeye mwenyewe, na anafuatana kabisa na gazeti muda wote wa funzo.”

Mama mumoja aliye na binti wa miaka kenda aliandika hivi: “Mbele tulimusaidia binti yetu kutayarisha majibu. Sasa anatayarisha yeye mwenyewe. Tunatumia wakati muchache tu ili kumufasiria habari. Kwa sababu gazeti linaeleweka, sasa anaweza kuelewa sehemu kubwa ya funzo.”

WATOTO NAO WANAJISIKIA NAMNA GANI?

Watoto wengi wanasema kwamba Gazeti Munara wa Mulinzi katika Kiingereza rahisi lilifanywa kabisa kwa ajili yao. Rebbecca mwenye miaka kumi na mbili alisema hivi: “Tafazali musiache kuchapisha gazeti hili jipya!” Aliongeza hivi: “Ninapenda namna mumetia sehemu ‘Maana ya Maneno Fulani.’ Watoto wanaelewa kwa urahisi sana gazeti hilo.”

Nicolette mwenye miaka saba anafikiri hivyo pia: Zamani ilikuwa vigumu kwangu kuelewa gazeti Munara wa Mulinzi. Sasa ninaweza kutoa maelezo mengi mimi mwenyewe.” Emma mwenye miaka kenda aliandika hivi: “Gazeti hilo limenisaidia sana mimi na ndugu yangu, aliye na miaka sita. Tunaweza kuelewa mambo mengi vizuri zaidi ! Asante!”

Bila shaka, wengi wanafaidika na gazeti Munara wa Mulinzi linalotumia maneno rahisi. Linasaidia na litaendelea kuchapishwa pamoja na gazeti la kawaida ambalo lilianza kuchapishwa tangu mwaka wa 1879.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 30]

“Sasa ndugu wanatumia wakati waliokuwa wanatumia kutafuta maana ya maneno na kufasiria usemi mbalimbali ili kuelewa maandiko yaliyotajwa na namna yanavyopatana na habari”

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 31]

“Ninashangaa kuona kwamba kijana wangu anaweza kunisaidia kusoma mafungu na anaelewa kabisa habari anayosoma”