Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Wakaaji wa Muda” Wanamuabudu Mungu wa Kweli Katika Umoja

“Wakaaji wa Muda” Wanamuabudu Mungu wa Kweli Katika Umoja

“Wakaaji wa Muda” Wanamuabudu Mungu wa Kweli Katika Umoja

‘Watu wa inchi nyingine watakuwa wakulima wenu na watunza​-mizabibu wenu. Nanyi mutaitwa makuhani wa Yehova.’​—ISA. 61:5, 6.

UNGEJIBU NAMNA GANI?

Watu fulani wanawaona wageni namna gani, lakini namna gani mawazo ya Biblia yanaachana na mawazo yao?

Ni mwaliko gani ambao unatolewa watu wa mataifa yote?

Ni mambo gani yanayoonyesha kwamba tumeanza kuishi katika dunia isiyo na wageni?

1. Watu fulani wanawaona wageni namna gani, na sababu gani maoni yao si mazuri?

 KAMA tulivyozungumuzia katika habari iliyotangulia, watu fulani wanawazarau sana wageni, ao watu wanaotoka katika inchi nyingine. Kujiona kuwa bora kuliko watu wa inchi nyingine ni vibaya. Na ni kudanganyika kwa sababu hakuna taifa lililo bora kuliko lingine. Kitabu kimoja (The Races of Mankind) kinasema hivi: “Watu wa rangi zote ni ndugu kama vile Biblia inavyofundisha.” Kwa kawaida kuna mambo yanayowafanya watoto wa tumbu moja kuwa tofauti, hata hivyo, wao ni ndugu tu.

2, 3. Yehova anawaona wageni namna gani?

2 Wageni wanapatikana mahali pote. Hata Waisraeli waliokuwa na uhusiano wa pekee na Yehova Mungu kupitia agano la Sheria waliishi pamoja na wageni. Wageni hao hawakuwa na haki ya kufanya mambo mengi, lakini Yehova aliwaamuru Waisraeli wawaheshimie na kuwatendea kwa haki. Huo ni mufano muzuri kwetu. Wakristo wa kweli hawapaswe kuwa na ubaguzi wala kuwawazia wengine vibaya. Sababu gani? Mutume Petro aliandika hivi: ‘Kwa hakika ninaona kwamba Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.’​—Mdo. 10:34, 35.

3 Wageni walioishi pamoja na Waisraeli walibarikiwa. Namna gani? Yehova aliwakubali. Miaka mingi baadaye, mutume Paulo alisema hivi kumuhusu Yehova: “Je, yeye ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si wa watu wa mataifa pia? Ndiyo, wa watu wa mataifa pia.”​—Rom. 3:29; Yoe. 2:32.

4. Sababu gani tunaweza kusema kwamba hakuna wageni katika “Israeli wa Mungu”?

4 Kisha Mungu kufanya agano jipya na Wakristo watiwa-mafuta, Waisraeli wa kimwili hawakuwa tena na uhusiano wa pekee pamoja naye; Wakristo hao watiwa​-mafuta ndio walichukua nafasi yao. Ndio sababu wanaitwa “Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:16) Na mutume Paulo alionyesha kwamba katika taifa hilo jipya ‘hakuna Mugiriki wala Muyahudi, tohara wala kutotahiriwa, mugeni, Musikithe, mutumwa, mutu huru, bali Kristo ni kila kitu na katika vitu vyote.’ (Kol. 3:11) Kwa hiyo, tunaweza kusema kwamba hakukuwa na hakuna wageni katika kutaniko la Kikristo.

5, 6. (a) Tunaweza kujiuliza ulizo gani kuhusu andiko la Isaya 61:5, 6? (b) “Makuhani wa Yehova” ni nani na ‘watu kutoka inchi nyingine’ ambao Isaya anataja ni nani? (c) Vikundi hivyo viwili vinafanya kazi gani?

5 Lakini mutu anaweza kuonyesha unabii unaopatikana katika kitabu cha Isaya sura 61. Unabii huo unazungumuzia mambo yanayotimizwa leo katika kutaniko la Kikristo. Mustari wa 6 wa sura hiyo, unazungumuzia wale watakaokuwa “makuhani wa Yehova.” Lakini, mustari wa 5, unazungumuzia ‘watu wa inchi nyingine’ ao wageni ambao watashirikiana na kufanya kazi pamoja na hao “makuhani.” Wageni hao ni nani?

6 Tunaelewa kwamba “makuhani [hao] wa Yehova” ni Wakristo watiwa​-mafuta wanaoshiriki katika “ufufuo wa kwanza.” “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.” (Ufu. 20:6) Lakini zaidi ya hao, kuna Wakristo wengi waaminifu walio na tumaini la kuishi duniani. Hata ikiwa wanashirikiana kabisa na kufanya kazi pamoja na Wakristo watiwa​-mafuta, wao ni wageni katika maana fulani. Kwa furaha, wanategemeza “makuhani wa Yehova,” na wanafanya kazi pamoja nao kama “wakulima” na “watunza​-mizabibu.” Wakristo hao wanasaidia kwa kuonyesha tunda la roho ili kumutukuza Mungu, wanalisha na kuvuna watu kwa njia ya mufano. Kwa kweli, Wakristo watiwa-mafuta na “kondoo wengine” wanatafuta watu wanaotamani kumutumikia Mungu milele na wanawatunza kwa upendo.​—Yoh. 10:16.

“WAKAAJI WA MUDA” KAMA ABRAHAMU

7. Hali ya Wakristo leo inafanana namna gani na ile ya Abrahamu na wanaume wengine waaminifu wa zamani?

7 Habari iliyotangulia ilionyesha kwamba Wakristo wa kweli wanaishi kama wageni, ao wakaaji wa muda katika ulimwengu huu muovu wa Shetani. Kwa hiyo, hali yao inafanana na ile ya wanaume waaminifu wa zamani kama vile Abrahamu. Biblia inasema kwamba ‘walikuwa wageni na wakaaji wa muda katika inchi.’ (Ebr. 11:13) Iwe sisi ni watiwa​-mafuta ao kondoo wengine, tuna pendeleo la kuwa marafiki wa Yehova kama Abrahamu. Yakobo, anasema kwamba “‘Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova, na ikahesabiwa kwake kuwa ni uadilifu,’ naye aliitwa ‘rafiki ya Yehova.’”​—Yak. 2:23

8. Abrahamu alipewa ahadi gani, naye alitumaini nini?

8 Mungu aliahidi kwamba kupitia Abrahamu na wazao wake, familia zote za dunia zingebarikiwa. Ahadi hiyo haihusu taifa moja tu. (Soma Mwanzo 22:15-18.) Hata ikiwa ahadi hiyo ingetimia wakati ujao, Abrahamu aliendelea kutumaini kwamba itatimia. Miaka mingi ya maisha yake, Abrahamu alikuwa akihama-hama pamoja na familia yake. Wakati wote huo Abrahamu alibaki rafiki ya Yehova.

9, 10. (a) Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Abrahamu? (b) Ni mwaliko gani ambao tunaweza kuwatolea wengine?

9 Hata ikiwa hakujua kama angengojea miaka ngapi ili kuona utimizo wa ahadi hiyo, Abrahamu aliendelea kumupenda Yehova na imani yake haikutikisika. Aliendelea kungojea, hakufikiria kuwa na maisha ya kawaida ao ya kudumu kama mukaaji yeyote katika taifa fulani. (Ebr. 11:14, 15) Ni jambo la hekima kwetu kumuiga Abrahamu kwa kuishi maisha mepesi na bila kuhangaikia sana vitu vya kimwili, vyeo katika ulimwengu ao miradi ya kuwa tu na kazi nzuri. Sababu gani tutafute maisha ambayo watu wanaona kuwa ya kawaida katika ulimwengu huu unaokaribia kuangamizwa? Sababu gani tuendelee kushikamana sana ao kukankamana na mambo ambayo ni ya muda tu? Tunangojea kitu kizuri sana, na tuko tayari kuvumilia mupaka wakati tumaini letu litatimia.​—Soma Waroma 8:25.

10 Yehova anaendelea kuwaalika watu wa mataifa yote ili waje kubarikiwa kupitia uzao wa Abrahamu. Na “makuhani wa Yehova,” ni kusema, watiwa​-mafuta na pia ‘watu kutoka inchi nyingine,’ ni kusema, kondoo wengine, wanaendelea kualika watu duniani pote katika luga zaidi ya 600 ili waje kujifunza baraka ambazo wanadamu watapata kupitia uzao wa Abrahamu.

WEWE USIANGALIE MIPAKA YA INCHI

11. Sulemani aliwaomba watu wa mataifa wafanye nini?

11 Katika mwaka wa 1026, mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati Sulemani alimutolea Yehova hekalu alilojenga, alitambua kwamba watu wa mataifa yote wangejiunga na Waisraeli katika kumusifu Yehova. Jambo hilo lilipatana na ahadi ya Yehova kwa Abrahamu. Sulemani alisali hivi kutoka moyoni: ‘Pia kwa mugeni, ambaye si sehemu ya watu wako Israeli na ambaye anatoka katika inchi ya mbali kwa sababu ya jina lako (kwa maana watasikia habari za jina lako kubwa na za mukono wako wenye nguvu na za mukono wako ulionyooshwa), naye kwa kweli aje na kusali kuelekea nyumba hii, basi na usikilize ukiwa mbinguni, makao yako yaliyofanywa imara, nawe ufanye kulingana na yote ambayo mugeni huyo anakuomba; kusudi watu wote wa dunia wajue jina lako ili wakuogope kama vile watu wako Israeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba jina lako limeitwa juu ya nyumba hii ambayo nimeijenga.’​—1 Fal. 8:41-43.

12. Sababu gani watu fulani wanaweza kuona Mashahidi wa Yehova kama “wageni”?

12 Kwa kawaida mugeni ni mutu anayetembelea inchi nyingine ao anayeishi katika inchi isiyokuwa yake. Maelezo hayo yanaonyesha wazi hali ya Mashahidi wa Yehova. Hata ikiwa wanaishi katika inchi mbalimbali, uaminifu wao kwanza ni kuelekea serikali ya mbinguni, ni kusema, Ufalme wa Mungu unaoongozwa na Kristo. Ndiyo sababu wanakataa kabisa kujiingiza katika politike, hata ikiwa watu fulani hawawaelewe na kufikiri kwamba haifae Mashahidi wajiendeshe hivyo leo.

13. (a) Sababu gani tunaweza kusema kwamba wale wanaofikiriwa kuwa “wageni” si wageni kabisa? (b) Je, Yehova alikusudia mwanzoni kuwe wageni duniani? Eleza.

13 Ni rahisi kutambua kwamba watu fulani ni wageni ao wanatoka katika inchi nyingine kupitia usemi wao, desturi zao, sura zao, na hata mutindo na namna yao ya kuvalia. Hata hivyo, mambo wanayofanya kama watu wengine, hata wawe wa taifa gani, ndiyo ya maana kuliko mambo yanayowatofautisha na wengine. Kwa hiyo, watu wanasema kwamba mutu fulani ni mugeni kwa sababu tu wanaangalia mambo yanayomutofautisha na wengine. Ikiwa tunaacha kutazama mambo hayo yanayomutofautisha mutu ao tunayowazia kuwa yanamufanya awe tofauti, basi hatutamuona tena kuwa mugeni. Ikiwa wanadamu wote wangeishi katika serikali moja tu duniani, hakuna mutu ambaye angeitwa mugeni, sivyo? Na kusudi la Yehova hapo mwanzoni lilikuwa kwamba wanadamu wote wawe familia moja yenye umoja inayoongozwa na utawala mumoja, ni kusema, utawala wake. Je, leo kuna kitu fulani kinachoweza kuwaunganisha hivyo watu wa mataifa yote duniani?

14, 15. Mashahidi wa Yehova kwa ujumla wamejifunza kufurahia nini?

14 Katika ulimwengu huu unaojaa watu wanaojipenda na wanaopenda sana inchi zao, inafurahisha sana kujua kwamba kuna watu wasioona wengine kuwa wageni. Kwa kweli, si rahisi kuacha kuwabagua watu. Kisha kufanya kazi na watu fulani wenye uwezo mbalimbali kutoka mataifa mengi, Ted Turner aliyeanzisha kituo cha televizyo inayoitwa CNN alisema hivi: “Kukutana na watu wa inchi mbalimbali lilikuwa jambo la ajabu sana. Nilifikia kutambua kwamba watu wanaotoka katika inchi zingine si wageni lakini wao ni raia wenzangu katika duniani hii. Nilianza kuona kwamba neno ‘mugeni’ halifae hata kidogo na nilitia sheria ili wafanyakazi wangu wasilitumie neno hilo, iwe katika mazungumuzo yao katika biro ao kwenye televizyo. Badala ya kusema kwamba mutu fulani ni mugeni walipaswa kusema ‘ametoka inchi nyingine.’”

15 Duniani pote ni Mashahidi wa Yehova tu ndio wanaoona watu wa mataifa yote kama vile Mungu anavyowaona. Kujifunza kuwaona watu kama vile Mungu anavyowaona kumewasaidia waondoe ubaguzi katika akili na mioyo yao. Kuliko kuwazarau watu wa taifa lingine, kukosa kuwatumainia, kuwachukia ao hata kuwawazia vibaya, wamejifunza kufurahia sifa na uwezo mbalimbali wa watu wa mataifa mengine. Je, umewahi kufikiria jambo hilo la ajabu na umeona faida ya kuishi na wengine bila kuwabagua?

DUNIA ISIYO NA WAGENI

16, 17. Maisha yako yatakuwa namna gani wakati unabii wa Ufunuo 16:16 na Danieli 2:44 utatimia?

16 Karibuni Yesu na majeshi yake ya mbinguni watapigana vita ya mwisho na mataifa yote yanayopinga utawala wa Mungu, vita hiyo ‘inaitwa katika Kiebrania Har–Magedoni.’ (Ufu. 16:14, 16; 19:11-16) Zaidi ya miaka 2 500 iliyopita, nabii Danieli alitabiri mambo yatakayopata serikali za wanadamu zinazopinga kusudi la Mungu. Yeye aliandika hivi: ‘Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama kwa wakati usio na kipimo.’​—Dan. 2:44.

17 Unafikiri maisha yako yatakuwa namna gani wakati unabii huo utatimia? Mipaka ya inchi iliyotiwa na wanadamu, ambayo leo tunaweza kusema inamufanya kila mutu kuwa mugeni haitakuwa tena. Tofauti yoyote ya sura ao hali yoyote ya mwili inayotofautiana itaonyesha tu maajabu ya uumbaji wa Mungu. Tumaini hilo nzuri linapaswa kuchochea sisi wote kufanya yote tunayoweza ili kumutukuza Muumbaji wetu, Yehova Mungu.

18. Ni mambo gani ya hivi karibuni yanayoonyesha kwamba inawezekana kuondoa wazo la kuwaona wengine kama “wageni”?

18 Je, ni vigumu kwako kuamini kwamba mabadiliko hayo yanaweza kutokea katika dunia yote? Tuna sababu nyingi za kuamini kwamba mambo yatakuwa hivyo. Tufikirie Mashahidi wa Yehova: Kwao mutu kuwa “mugeni” hakuwaambie kabisa kitu; kati yao hawafikirie sana jambo la mutu kuwa wa taifa hili ao lile. Kwa mufano, hivi karibuni ili kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme ifanywe vizuri zaidi na isimamiwe vizuri, Beteli nyingi ndogondogo za inchi fulani zilifungwa na kazi ya inchi hizo inasimamiwa na Beteli fulani kubwa. (Mt. 24:14) Ikiwa tu sheria ya serikali iliruhusu kufanya hivyo, mipaka ya inchi haikuzuia kuchukua mipango kama hiyo. Hilo ni jambo lingine lililo wazi linaloonyesha kwamba Mutawala wa haki aliyesimamishwa na Mungu, Yesu Kristo, ameanza kuondoa mipaka iliyowekwa na wanadamu, na karibuni ‘atakamilisha ushindi wake.’​—Ufu. 6:2.

19. Luga safi ya ukweli imefanya nini?

19 Mashahidi wa Yehova wanatoka katika mataifa mengi na wanazungumuza luga mbalimbali, hata hivyo wana luga safi ya ukweli ambayo imewaunganisha na kifungo hicho cha umoja hakiweze kuvunjwa. (Soma Sefania 3:9.) Wao wanafanyiza familia moja kutoka katika mataifa yote na ambayo inajitenga kabisa na ulimwengu huu muovu. Familia hiyo yenye umoja inaonyesha kwamba dunia mupya itakuwa dunia isiyo na wageni. Wakati huo, kila mutu atatambua ukweli wa maneno ya kitabu tulichozungumuzia mwanzoni: “Watu wa rangi zote ni ndugu kama vile Biblia inavyofundisha.”​—The Races of Mankind.

[Maulizo ya Funzo]

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 28]

Je, unangojea kwa hamu kuona wakati ambapo hakutakuwa mipaka iliyotiwa na wanadamu inayogawanya inchi, na wakati neno “mugeni” halitatumiwa tena?

[Picha katika ukurasa wa 25]

Je, utaendelea kungojea kuona utimizo wa ahadi za Mungu kama Abrahamu?

[Picha katika ukurasa wa 27]

Machoni pa Yehova hakuna mutu aliye mugeni