Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unaona Uriti Wako wa Kiroho Kuwa wa Maana Sana?

Je, Unaona Uriti Wako wa Kiroho Kuwa wa Maana Sana?

‘Mungu kwa mara ya kwanza alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’—MDO. 15:14.

1, 2. (a) “Kibanda cha Daudi” kinamaanisha nini, na kilijengwa upya namna gani? (b) Ni nani wanaomutumikia Yehova kwa umoja leo?

 KATIKA mukutano mumoja wa lazima sana wa baraza linaloongoza uliofanywa huko Yerusalemu mwaka wa 49, mwanafunzi Yakobo alisema hivi: “Simioni [Petro] ameeleza kikamili jinsi Mungu kwa mara ya kwanza alivyoelekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake. Na maneno ya Manabii yanakubaliana na jambo hili, kama vile ambavyo imeandikwa, ‘Baada ya mambo hayo nitarudi na kukijenga upya kibanda cha Daudi ambacho kimeanguka chini; nami nitayajenga upya mabomoko yake na kukisimamisha tena, ili watu wanaobaki wamutafute Yehova kwa bidii, pamoja na watu wa mataifa yote, watu wanaoitwa kwa jina langu, asema Yehova, anayefanya mambo haya, yanayojulikana tangu zamani za kale.’”​—Mdo. 15:13-18.

2 “Kibanda cha Daudi” [ao nyumba ya kifalme] kilianguka wakati Mufalme  Sedekia aliondoshwa kwenye kiti cha ufalme. (Amo. 9:11) Hata hivyo, Yesu, muzao wa Daudi, ambaye ni Mufalme wa milele angejenga upya “kibanda” hicho. (Eze. 21:27; Mdo. 2:29-36) Kulingana na maneno ambayo Yakobo alisema kwenye mukutano huo wa lazima sana, unabii huo ulikuwa ukitimizwa: watu ambao wangetawala na Yesu kutoka taifa la Israeli na kutoka watu wa mataifa walikuwa wakikusanywa. Leo, mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta na mamilioni ya “kondoo wengine” wa Yesu wanafanya pamoja kazi ya kutangaza kweli ya Biblia.​—Yoh. 10:16.

WATU WA YEHOVA WANAPELEKWA UHAMISHONI

3, 4. Ni nini ilisaidia watumishi wa Yehova wasichafuliwe na mafundisho ya uongo ya Babiloni?

3 Wayahudi walipopelekwa uhamishoni Babiloni, ilionekana wazi kwamba “kibanda cha Daudi” kimeanguka. Watu hao wa Mungu wangepitisha miaka 70 katika Babiloni, ni kusema kuanzia mwaka wa 607 mupaka 537. Katika muji huo wenye kujaa ibada ya uongo, ni nini ingesaidia ibada yao isichafuliwe? Jambo linalosaidia ibada yetu isichafuliwe katika ulimwengu huu wa Shetani leo ndilo liliwasaidia wao pia. (1 Yoh. 5:19) Tuna uriti mukubwa ambao umesaidia ibada yetu isichafuliwe.

4 Neno la Mungu Biblia ni sehemu ya uriti wetu wa kiroho. Wayahudi waliopelekwa uhamishoni huko Babiloni hawakuwa na Biblia nzima, lakini walijua Sheria ya Musa, na Amri Kumi za sheria hiyo. Walijua “nyimbo za Sayuni,” walikumbuka mezali nyingi, na walijua mambo ya ajabu yaliyofanywa na watumishi wa zamani wa Yehova. Waisraeli hao walilia walipokumbuka Sayuni, na hawakumusahau Yehova. (Soma Zaburi 137:1-6.) Kufanya hivyo kulisaidia ibada yao isichafuliwe hata ikiwa mafundisho na desturi za kipagani zilienea katika Babiloni.

FUNDISHO LA UTATU HALIKUANZA LEO

5. Ni mambo gani yanayoonyesha kama Wababiloni na Wamisri waliamini utatu?

5 Wababiloni waliamini sana utatu, ao miungu mitatu-mitatu katika mungu mumoja. Kwa mufano, waliamini kama kuna Sin (mungu-mwezi), Shamash (mungu-jua), na Ishtar (mungu-muke wa uzazi na vita). Kitabu kimoja kinasema kwamba Wamisri waliamini kama mungu alioa mungu-muke ambaye alimuzalia mutoto, “wote walifanyiza utatu ambamo mungu-mume hakuwa mukubwa siku zote; ikiwa mungu-muke alikuwa mukubwa wa muji, mungu-mume alikuwa tu bwana ya mungu-muke.” Utatu fulani ambao Wamisri waliamini ulifanyizwa na mungu-mume Ozirisi, mungu-muke Izisi, na Horise mutoto wao.

6. Dini zinazojiita kuwa za Kikristo zinafundisha nini kuhusu Utatu, na sababu gani sisi tumelindwa ili tusichafuliwe na fundisho hilo la uongo?

6 Dini zinazojiita kuwa za Kikristo zina fundisho la Utatu. Viongozi wa dini wanafundisha kama Baba, Mwana na roho takatifu ni Mungu mumoja. Lakini fundisho hilo linamuzaraulisha Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote, Yehova, kwa kumufanya kuwa sehemu ya mungu mwenye vichwa vitatu. Watu wa Yehova wamelindwa ili wasidanganywe na fundisho hilo la uongo kwa sababu wanakubali maneno haya yaliyoongozwa na roho ya Mungu: ‘Sikiliza, Ee Israeli: Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja.’ (Kum. 6:4) Kwa kuwa Yesu alirudilia maneno hayo, kila Mukristo wa kweli anapaswa kuyaamini, sivyo?​—Mk. 12:29.

7. Sababu gani mutu anayeamini fundisho la Utatu hastahili kubatizwa?

7 Fundisho la Utatu linapingana na amri ya Yesu ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu.’ (Mt. 28:19) Ili kubatizwa na kuwa Mukristo wa kweli, Shahidi wa Yehova, mutu anapaswa kutambua mamlaka ya Baba, Yehova, vilevile cheo na mamlaka ya Mwana wa Mungu, Yesu. Anapaswa pia kuamini kwamba roho takatifu ni nguvu ambayo Mungu anatumia ili kutenda, na roho hiyo si sehemu ya Utatu. (Mwa. 1:2) Mutu anayeendelea kuamini fundisho la Utatu hastahili kubatizwa, kwa kuwa ubatizo ni alama inayoonyesha kwamba mutu amejitoa katika sala kwa Yehova. Tunafurahi sana kwa kuwa uriti wetu wa kiroho umetulinda ili tusichafuliwe na fundisho hilo linalomuzaraulisha Mungu.

KUZUNGUMUZA NA MASHETANI

8. Wababiloni waliamini nini kuhusu miungu na mashetani?

8 Katika Babiloni watu walikuwa na mawazo mengi ya kidini ambayo yaliwafanya waamini sana mafundisho mengi ya uongo, miungu, mashetani, na hata mambo ya kuzungumuza na mashetani. Kitabu kimoja kinasema kwamba “katika dini ya Wababiloni, kisha miungu watu waliamini mashetani; ambao walikuwa na uwezo wa kuwatesa watu kwa magonjwa ya kila namna, ya kimwili na ya kiakili. Inaonekana kwamba mambo mengi katika dini hiyo yalifanywa ili kupiganisha vikali mashetani hao, na mahali pote watu walikuwa wanaomba miungu iwasaidie ili wapambane na mashetani hao.”

9. (a) Namna gani Wayahudi wengi waliangukia katika mutego wa mafundisho ya uongo walipokuwa Babiloni? (b) Ni nini imetusaidia ili tusinaswe na mutego wa kuzungumuza na mashetani?

9 Walipokuwa Babiloni, Wayahudi wengi walianza kuamini mafundisho ya uongo. Kwa kuwa mawazo ya Wagiriki yalienea, Wayahudi wengi walinaswa katika mutego wa mashetani, kwa sababu walianza kuamini kwamba kuna mashetani wazuri na mashetani wabaya. Uriti wetu wa kiroho unatulinda ili tusinaswe na mutego wa kuzungumuza na mashetani, kwa sababu tunajua kwamba Mungu alikataa desturi kama hizo za Wababiloni. (Isa. 47:1, 12-15) Zaidi ya hayo, sisi tunafuata mawazo ya Mungu kuhusu kuzungumuza na mashetani.—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Ufunuo 21:8.

10. Tunaweza kusema nini kuhusu mazoea na mafundisho ya Babiloni Mukubwa?

10 Leo, waamini wa Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo, wana mazoea ya kuzungumuza na mashetani kama vile Wababiloni wa zamani walivyofanya. (Ufu. 18:21-24) Kitabu kimoja kinasema kwamba “ndani ya Babiloni [Mukubwa] muna mazoea yote ao desturi zote mbaya. Inatambuliwa kwa ibada ya sanamu mahali popote duniani.” Mazoea ya kuzungumuza na mashetani, ibada ya sanamu na zambi zingine, mambo hayo yanajaa katika Babiloni mukubwa, lakini tengenezo hilo litaharibiwa hivi karibuni.​—Soma Ufunuo 18:1-5.

11. Ni maonyo gani ambayo yametolewa katika vichapo vyetu kuhusu kuzungumuza na mashetani?

11 Yehova alisema hivi: ‘Siweze kuvumilia matumizi ya nguvu za uchawi.’ (Isa. 1:13) Katika miaka ya 1800, watu wengi walipendezwa na mazoea ya kuzungumuza na mashetani. Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 5, 1885 ulisema hivi: “Fundisho la kwamba wafu wanapatikana katika ulimwengu mwengine halikuanza leo. Dini za zamani zilifundisha hivyo, na fundisho hilo lilitokana na hadisi za kutunga za zamani.” Gazeti hilo lilionyesha tena kwamba fundisho la uongo la kwamba wafu wanaweza kuzungumuza na watu wanaoishi “limefanya watu wengi wasadiki kama wafu wanageuka kuwa roho wanaoweza kuzungumuza nao. Roho hao wanaficha utambulisho wao, na katika njia hiyo wamewasadikisha watu wengi.” Broshua iliyotolewa zamani iliyokuwa na kichwa Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuzungumuza na Mashetani? (Kiingereza) ilitoa maonyo kuhusu zoea hilo kama yale yanayopatikana katika vichapo vilivyotolewa hivi karibuni.

JE, NAFSI ZA WATU WALIOKUFA ZINATESEKA KATIKA ULIMWENGU MWENGINE?

12. Akiongozwa na roho na ya Mungu, Sulemani alisema nini kuhusu hali ya watu waliokufa?

12 “Wale wote ambao wameijua kweli” wanaweza kujibu ulizo hilo. (2 Yoh. 1) Tunaamini kabisa maneno haya ya Mufalme Sulemani: ‘Mbwa aliye hai ni afazali kuliko simba aliyekufa. Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe. Yote ambayo mukono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.’​—Mhu. 9:4, 5, 10.

13. Namna gani Wayahudi walifikia kukubali mafundisho na desturi za Wagiriki?

13 Wayahudi walijua kweli kuhusu watu waliokufa. Hata hivyo, inchi ya Ugiriki ilipogawanywa kati ya majenerali wa Alexandre Mukubwa, Wagiriki walianza kutawala inchi ya Yuda na Siria na walifanya mipango ili kufundisha Wayahudi dini na desturi zao. Kwa hiyo, Wayahudi walianza kuamini kama mutu ana nafsi isiyokufa na kwamba kuna mahali fulani ambapo ni ulimwengu wa mateso. Wagiriki hawakuwa wa kwanza kuamini kwamba kuna ulimwengu wa mateso na kuna nafsi nyingi zenye kuteswa humo. Kitabu kimoja kinasema Wababiloni pia waliamini kwamba “ulimwengu wa mateso ni mahali penye kuogopesha sana, na ambapo palisimamiwa na miungu na roho wenye nguvu na wakali sana.” Bila shaka, Wababiloni waliamini kwamba mutu ana nafsi isiyoweza kufa.

14. Ayubu na Abrahamu walijua nini kuhusu kifo na ufufuo?

14 Hata ikiwa mwanaume mwaminifu Ayubu hakuwa na Biblia, yeye alijua kweli kuhusu kifo. Alitambua pia kwamba ikiwa atakufa, Yehova, Mungu mwenye upendo, atatamani sana kumufufua. (Ayu. 14:13-15) Abrahamu pia aliamini ufufuo. (Soma Waebrania 11:17-19.) Watumishi hao wenye kumuogopa Mungu hawakuamini kwamba mutu ana nafsi isiyoweza kufa kwa kuwa haiwezekane kumufufua mutu ambaye haweze kufa. Bila shaka, roho ya Mungu iliwasaidia Ayubu na Abrahamu ili wajue hali ya watu waliokufa na kuamini ufufuo. Mafundisho hayo ya kweli ni sehemu pia ya uriti wetu wa kiroho.

TUNA LAZIMA YA ‘KUKOMBOLEWA KUPITIA ZABIHU YA UKOMBOZI’

15, 16. Namna gani tumekombolewa kutoka katika zambi na kifo?

15 Sisi ni wenye furaha kwa sababu Yehova ametufunulia pia kweli kuhusu mipango ambayo amechukua ili kutukomboa kutoka katika zambi na kifo tulivyoriti kwa Adamu. (Rom. 5:12) Tunajua kwamba Yesu “alikuja, si kuhudumiwa, bali kuhudumu na kutoa nafsi yake iwe fidia [ao zabihu ya ukombozi] badala ya wengi.” (Mk. 10:45) Ni furaha kubwa kujua namna ‘tulivyokombolewa kwa njia ya zabihu ya ukombozi ambayo Kristo Yesu alilipa.’​—Rom. 3:22-24.

16 Wayahudi na Watu wa Mataifa wa wakati wa Yesu walipaswa kutubu zambi zao na kuonyesha imani katika zabihu hiyo ya ukombozi ambayo Yesu alitoa. Ikiwa hawangefanya hivyo, hawangesamehewa zambi zao. Ni hivyo pia leo. (Yoh. 3:16, 36) Mutu ambaye hatake kuachana na mafundisho ya uongo, kama vile Utatu na kutokufa kwa nafsi, haweze kufaidika na zabihu ya ukombozi. Lakini sisi tunaweza kufaidika nayo, kwa sababu tunajua kweli kuhusu ‘Mwana wa upendo [wa Mungu], ambaye kwa njia yake tunaachiliwa huru kupitia fidia, na kusamehewa zambi zetu.’—Kol. 1:13, 14.

TUENDELEE KUMUTUMIKIA YEHOVA

17, 18. Tunaweza kupata wapi habari kuhusu historia yetu, na namna gani tunaweza kufaidika kwa kuichunguza?

17 Zaidi ya mafundisho ya kweli na mambo ambayo tumejionea na baraka za kiroho na kimwili ambazo tunafurahia, kuna mambo mengine mengi yaliyo sehemu ya uriti wetu wa kiroho. Kwa miaka mingi, Kitabu cha Mwaka kimeeleza habari nyingi zenye kufurahisha juu ya kazi yetu katika inchi mbalimbali. Historia yetu imeelezwa tena katika video Watu Wanaotenda kwa Imani, sehemu ya 1 na ya 2, na katika vitabu kama vile Mashahidi wa Yehova​—Wapiga-mbiu wa Ufalme wa Mungu. Na habari zenye kutia moyo za ndugu na dada zetu wanaoeleza maisha yao zinapatikana kila mara katika magazeti yetu.

18 Tunapata faida nyingi tunapofikiria historia ya tengenezo la Yehova, kama vile Waisraeli walivyopata faida kwa kufikiria namna ambavyo Mungu aliwakomboa kutoka katika utumwa wa Misri. (Kut. 12:26, 27) Musa, mwanaume aliyezeeka, alijionea kazi za ajabu za Mungu, kwa hiyo aliwatia moyo Waisraeli hivi: ‘Fikirieni miaka iliyopita kutoka kizazi mupaka kizazi; muulize baba yako, naye anaweza kukuambia; wanaume wenu wazee, nao wanaweza kukuambia.’ (Kum. 32:7) ‘Sisi watu wa Yehova na wa kundi la malisho yake’ tunamusifu na kuwaelezea wengine kwa furaha matendo yake ya ajabu. (Zab. 79:13) Zaidi ya hayo, ni vizuri kuchunguza historia yetu kwa kuwa mambo tunayojifunza kutokana na historia hiyo yanatusaidia tuendelee kumutumikia Mungu.

19. Kwa kuwa tunafurahia nuru ya kiroho, tunapaswa kufanya nini?

19 Tunafurahi kwa kuwa sisi hatutange-tange katika giza, lakini tunaongozwa na nuru ya Mungu. (Met. 4:18, 19) Kwa hiyo, acheni tujifunze Neno la Mungu kwa bidii na tuwaelezee wengine kweli. Sisi tunajisikia kama mutunga​-zaburi aliyesali hivi: ‘Nitautangaza uadilifu wako pekee yako. Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, na mupaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu. Na mupaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache, mupaka nikitangazie kizazi habari za mukono wako, habari za nguvu zako, kwa wale watakaokuja.’​—Zab. 71:16-18.

20. Shetani amepinga na kutilia shaka nini, na umeazimia kufanya nini?

20 Sisi watumishi wa Yehova waliojitoa kwake, tunajua kwamba Shetani amepinga haki ya Mungu ya kutawala na kutilia shaka uaminifu wetu kwa Mungu. Kwa hiyo, tunatangaza ukweli huu ulio wazi: Yehova, Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote Muzima, ndiye anayestahili kuabudiwa. (Ufu. 4:11) Kwa kuwa roho ya Mungu ni juu yetu, tunawaelezea pia wapole habari njema, tunafunga vidonda vya waliovunjika moyo, na kuwafariji wale wanaoomboleza. (Isa. 61:1, 2) Hata ikiwa Shetani anajikaza kuwatawala watu wa Mungu na wanadamu wote, sisi tunaona kabisa uriti wetu wa kiroho kuwa wa maana sana na tumeazimia kuendelea kuwa waaminifu na kumusifu Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote, Yehova, sasa na milele.—Soma Zaburi 26:11; 86:12.