Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Je, hekalu la Yerusalemu lilijengwa tena kisha mwaka wa 70?

YESU alitabiri kwamba hakuna jiwe la hekalu la Yehova ambalo lingebaki juu ya lingine bila kubomolewa. Unabii huo ulitimia wakati jeshi la Roma lililoongozwa na Titus liliharibu muji wa Yerusalemu katika mwaka wa 70. (Mt. 24:2) Miaka fulani baadaye, Mufalme Julien alifanya mipango ya kujenga tena hekalu hilo.

Julien ameitwa mufalme mupagani wa mwisho wa Roma. Yeye alikuwa mupwa wa Constantin Le Grand na alipewa mafundisho fulani ya Kikristo. Hata hivyo, kisha kusimamishwa kuwa mutawala katika mwaka wa 361, alikataa mafundisho hayo na Ukristo wa uongo wa siku hizo na akapendelea kuwa mupagani. Vitabu vya historia vinamuita “Muasi-imani.”

Julien alichukia sana Ukristo. Labda alifanya hivyo kwa sababu alipokuwa na miaka sita, aliona jinsi watu fulani waliojiita Wakristo walivyomuua baba yake na ndugu zake. Wanahistoria wa mambo ya dini wanaonyesha kwamba ili kuonyesha kwamba Yesu alikuwa nabii wa uongo, Julien aliwatia moyo Wayahudi wajenge tena hekalu lao. *

Bila shaka, Julien alifanya mipango ya kujenga tena hekalu hilo. Wanahistoria wanabishana ili kutafuta kujua ikiwa kweli Julien alianza kazi hiyo na ikiwa aliianza, sababu gani hakuendelea na kazi hiyo. Lakini, jambo tunalojua kabisa ni kwamba Julien aliuawa kisha kutawala karibu miaka miwili tu, na mipango yake iliishia hapo.

Labda hekalu lilifanana hivi wakati wa Yesu, hapa limewekwa juu ya mahali ambapo lilijengwa

^ Yesu hakusema kwamba hekalu hilo halitajengwa tena, lakini alitabiri tu kwamba litaharibiwa, na hilo lilitokea katika mwaka wa 70.