Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Una “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”?

Je, Una “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”?

‘Kristo Yesu, alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili kujisafishia mwenyewe watu walio wake kwa njia ya pekee, walio na bidii kwa ajili ya kazi njema.’​—TITO 2:13, 14.

1, 2. Sisi Mashahidi wa Yehova tuna pendeleo gani la pekee, na tunaliona namna gani?

 WATU wengi wanaona kuwa ni pendeleo kupewa zawadi fulani kwa sababu ya kazi nzuri waliyofanya. Kwa mufano, watu fulani wamepewa Zawadi ya Nobeli kwa sababu walijikaza kurudisha amani kati ya inchi zilizokuwa hazisikilizane. Lakini, ni pendeleo kubwa zaidi kuwa waambasadere wa Mungu ao watu waliotumwa ili kuwasaidia watu wawe na uhusiano muzuri pamoja na Muumba wao!

2 Sisi Mashahidi wa Yehova, tuna pendeleo hilo la pekee. Chini ya uongozi wa Mungu na Yesu, tunawaomba watu ‘wapatanishwe pamoja na Mungu.’ (2 Kor. 5:20) Yehova anatutumia ili kuwasaidia watu wamukaribie. Kupitia sisi, mamilioni ya watu katika inchi zaidi ya 235 wamekuwa na uhusiano muzuri pamoja na Mungu na wana tumaini la kupata uzima wa milele. (Tito 2:11) Kwa bidii, tunamualika ‘yeyote anayetaka kuchukua maji ya uzima bure.’ (Ufu. 22:17) Kwa kuwa tunapenda mugao wetu na tunautimiza kwa bidii, tunastahili kuitwa watu “walio na bidii kwa ajili ya kazi njema.” (Tito 2:14) Acheni tuzungumuzie sasa namna bidii yetu kwa ajili ya kazi njema inavyowasaidia watu wamukaribie Yehova. Njia moja inayowasaidia watu wamukaribie Yehova ni kazi yetu ya kuhubiri.

TUIGE BIDII YA YEHOVA NA YESU

3. “Bidii ya Yehova” inatutolea uhakika gani?

3 Linapozungumuzia mambo ambayo utawala wa Mwana wa Mungu utafanya, andiko la Isaya 9:7 linasema hivi: “Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.” Maneno hayo yanatuhakikishia kama Baba yetu wa mbinguni anapenda kabisa wanadamu waokolewe. Kwa kuwa Yehova ni mwenye bidii, hilo linatuonyesha waziwazi kwamba sisi wahubiri wa Ufalme, tunapaswa kutegemeza kazi ambayo Mungu ametutolea kwa moyo wetu wote, kwa furaha, na kwa bidii. Tamaa yetu kubwa ya kuwasaidia watu wamujue Mungu inaonyesha kwamba tunamuiga Yehova. Kwa hiyo, kwa kuwa tunafanya kazi pamoja na Mungu, je, tumeazimia sisi wenyewe kufanya mengi katika kazi ya kuhubiri kadiri hali zetu zinavyoruhusu?​—1 Kor. 3:9.

4. Namna gani Yesu alituachia mufano wa kuendelea kuhubiri kwa bidii?

4 Tufikirie pia bidii ya Yesu. Alituachia mufano mukamilifu wa kuendelea kuhubiri kwa biii. Ijapokuwa alipambana na upinzani mukali, Yesu aliendelea kuhubiri kwa bidii mupaka kifo chake chenye maumivu mengi. (Yoh. 18:36, 37) Alipokaribia kufa kifo cha kujizabihu, Yesu aliongeza bidii yake ili kuwasaidia wengine wamujue Yehova.

5. Namna gani Yesu alitenda kulingana na mufano aliotoa kuhusu muti wa tini?

5 Kwa mufano, mwishoni mwa mwaka wa 32, Yesu alizungumuzia mufano wa mutu aliyekuwa na muti wa tini katika shamba lake la mizabibu ambao haukuzaa hata tunda moja kwa miaka mitatu. Mutunza​-mizabibu alipoambiwa kwamba akate muti huo, aliomba apewe wakati ili kuutilia mbolea. (Soma Luka 13:6-9.) Wakati Yesu alizungumuzia mufano huo, ni hesabu ndogo tu ya wanafunzi ndio ilikuwa imekubali mahubiri yake. Lakini kama mufano huo wa mutunza-mizabibu ulivyoonyesha, Yesu alitumia wakati mufupi uliobaki, ao miezi sita hivi, ili kuhubiri sana katika Yudea na Perea. Siku chache mbele ya kifo chake, Yesu aliwalilia Wayahudi wenzake ambao ‘walisikia kwa masikio yao bila kuitikia.’​—Mt. 13:15; Lu. 19:41.

6. Sababu gani tunapaswa kuongeza bidii katika kazi yetu ya kuhubiri?

6 Kwa kuwa tunakaribia sana mwisho, hauone kwamba ni jambo la maana tuongeze bidii yetu katika kazi ya kuhubiri? (Soma Danieli 2:41-45.) Tuna pendeleo nzuri la kuwa Mashahidi wa Yehova! Ni sisi tu ndio tunaowatolea watu tumaini la kweli kuhusu matatizo yanayowapata wanadamu. Mwandishi wa gazeti moja aliandika karibuni kwamba watu wengi hawana jibu la ulizo hili: “Sababu gani watu wazuri wanapatwa pia na mambo mabaya?” Sisi Wakristo tuna daraka na pendeleo la kuwatolea watu wanaopendezwa jibu la Biblia kwa ulizo hilo na kwa maulizo mengine. Tuna kila sababu ya ‘kuwaka roho’ tunapofanya kazi ambayo Mungu ametutolea. (Rom. 12:11) Kwa baraka ya Mungu, bidii yetu katika kazi ya kuhubiri inaweza kuwasaidia wengine wamujue na kumupenda Yehova.

KUONYESHA ROHO YA KUJITOA KUNAMULETEA YEHOVA UTUKUFU

7, 8. Namna gani roho ya kujitoa inamuletea Yehova utukufu?

7 Mambo ambayo mutume Paulo alijionea yanaonyesha kwamba wakati fulani sisi wahubiri tunaweza “kukosa usingizi usiku” na tunaweza kuwa na “nyakati za kuwa bila chakula.” (2 Kor. 6:5) Maneno hayo yanaonyesha waziwazi roho ya kujitoa na yanaweza kutukumbusha mapainia wanaotia mahubiri pa nafasi ya kwanza na wakati huo huo wakijitafutia mahitaji yao ya kimwili. Fikiria pia wamisionere wetu wenye bidii ‘wanaojimimina [wanaojimwanga] kama toleo la kinywaji’ ili kuhubiria watu wa inchi za mbali. (Flp. 2:17) Tuseme nini kuhusu wazee wenye bidii wanaokosa wakati wa kula chakula ao wanaokosa usingizi ili kutunza kondoo za Yehova? Kuna pia wazee​-wazee na wagonjwa wanaojikaza sana ili kuhuzuria mikutano ya Kikristo na kushiriki katika mahubiri. Mioyo yetu inajaa shukrani tunapofikiria roho ya kujitoa ya watumishi hao wa Mungu. Jitihada zao zinawafanya wengine wawe na maoni mazuri kuhusu kazi yetu ya kuhubiri.

8 Katika barua aliyoandikia waandishi wa gazeti la Boston Target la Lincolnshire, Grande-Bretagne, musomaji mumoja asiyekuwa Shahidi alisema hivi: “Watu hawaaminie tena dini . . . Viongozi wa dini wanafanya nini kila siku? Kwa kweli, hawawatembelee watu kama Kristo alivyofanya . . . Mashahidi wa Yehova ndio dini pekee inayoonyesha kwamba inawahangaikia watu kwa kuwatembelea na kuwahubiria ukweli.” Katika ulimwengu huu ambamo kila mutu anatafuta faida yake, roho ya kujitoa inamuletea Yehova Mungu utukufu.​—Rom. 12:1.

Unapoonekana kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri, hilo linawatolea wanaokutazama ushahidi mukubwa

9. Nini kinachoweza kutuchochea tuendelee kuwa na bidii kwa ajili ya kazi njema ya kuhubiri?

9 Hata hivyo, tunaweza kufanya nini ikiwa tumeanza kupoteza bidii yetu katika kazi ya kuhubiri? Jambo ambalo linaweza kutusaidia ni kufikiria mambo ambayo Yehova anaendelea kutimiza kupitia kazi ya kuhubiri. (Soma Waroma 10:13-15.) Watu wanapaswa kuliitia jina la Yehova kwa imani ili waokolewe, lakini hawawezi kufanya hivyo kama hatuwahubirie. Kujua hivyo kutatuchochea tuendelee kuwa na bidii kwa ajili ya kazi njema na kuendelea kufanya yote tunayoweza ili kuhubiri habari njema ya ufalme.

MWENENDO WETU MUZURI UNAWACHOCHEA WATU WAMUKARIBIE MUNGU

Watu wanaona namna unavyofanya kazi yako vizuri na kwa bidii

10. Sababu gani tunaweza kusema kwamba mwenendo wetu muzuri unawachochea watu wamukaribie Yehova?

10 Katika kazi yetu ya kuhubiri, bidii pekee yake haitoshe ilikuwachochea watu wamukaribie Mungu. Njia nyingine inayowasaidia watu wamukaribie Mungu ni mwenendo wetu muzuri. Paulo alikazia umaana wa mwenendo wetu alipoandika hivi: ‘Sisi hatutoe sababu yoyote ya kukwaza kwa njia yoyote, ili huduma yetu isilaumiwe.’ (2 Kor. 6:3) Maneno yetu mazuri na mwenendo wetu unaofaa vinapamba mafundisho ya Mungu, vinafanya ibada ya Yehova iwe yenye kuvutia. (Tito 2:10) Tena, tunasikia mara nyingi habari za watu waliokubali ibada ya kweli kisha kutazama mwenendo wetu.

11. Sababu gani tunapaswa kufikiri sana na kusali juu ya matendo yetu?

11 Tunajua kwamba mwenendo wetu unaweza kuwachochea watu wamukaribie Yehova, lakini mwenendo wetu unaweza pia kuwafanya watu wasiwe na hamu ya kumukaribia Mungu. Kwa hiyo, tunapokuwa kwenye kazi, nyumbani, ao kwenye masomo, tujikaze kuepuka jambo lolote linaloweza kuwafanya watu walaumu kazi yetu ya kuhubiri na mwenendo wetu. Ikiwa tunafanya zambi kimakusudi, matokeo yanaweza kuwa mabaya zaidi. (Ebr. 10:26, 27) Jambo hili linapaswa kutufanya tufikiri sana na kusali juu ya mambo tunayofanya na namna watu wanavyoona matendo yetu. Kadiri tabia za watu zinavyoendelea kuharibika, watu wenye akili nzuri wanaendelea kuona waziwazi ‘tofauti kati ya muadilifu na muovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na mutu ambaye hajamutumikia.’ (Mal. 3:18) Bila shaka, mwenendo wetu muzuri unawasaidia sana watu wamurudilie Mungu.

12-14. Namna gani uvumilivu wetu unaweza kuwasaidia wale wanaotutazama wakubali kweli? Toa mufano.

12 Alipowaandikia Wakorintho, Paulo alionyesha kwamba alipata ziki, magumu, mapigo, na alifungwa katika gereza. (Soma 2 Wakorintho 6:4, 5.) Tunapopatwa na majaribu, uvumilivu wetu unaweza kuwasaidia wale wanaotutazama wakubali kweli. Kwa mufano, miaka fulani iliyopita, wakubwa wa serikali walitaka kuangamiza Mashahidi wa Yehova katika eneo moja la Angola. Mashahidi wawili, bwana na bibi yake, na watu 30 waliokuwa wanahuzuria mikutano walikamatwa. Kisha watu wa eneo hilo walikusanyika ili kuona namna wapinzani wanavyowapiga fimbo watu hao wasio na kosa mupaka damu ilipoanza kuwatoka. Wanawake na watoto, wote walitendewa kinyama. Kusudi la wapinzani lilikuwa kuwaogopesha watu ili mutu yeyote asiwasikilize tena Mashahidi wa Yehova. Lakini kisha kupigwa mbele ya watu, watu wengi wa eneo hilo walitafuta Mashahidi na kuwaomba wajifunze nao Biblia! Baadaye, kazi ya kuhubiri Ufalme ilisonga mbele, na kulikuwa ongezeko na baraka nyingi.

13 Mufano huo unaonyesha matokeo mazuri tunayoweza kupata kwa sababu ya kuwa waaminifu kwa kanuni za Biblia. Tunafikiri kwamba ujasiri wa mutume Petro na mitume wengine uliwasaidia wengi wamukaribie Mungu. (Mdo. 5:17-29) Wanafunzi wenzetu, wafanyakazi, ao watu wa jamaa zetu wanaweza kukubali habari njema wanapoona namna tunavyovumilia majaribu.

14 Kila wakati, ndugu na dada zetu wanapambana na upinzani. Kwa mufano, katika inchi ya Arménie, ndugu zetu 40 hivi wako katika gereza kwa sababu wanakataa kujiingiza katika vita, na inawezekana ndugu na dada wengine wengi watafungwa katika siku zinazokuja. Katika Érythrée, ndugu na dada 55 wako katika gereza, wengine kati yao wana miaka zaidi ya 60. Katika Corée du Sud, Mashahidi 700 hivi wako katika gereza kwa sababu ya imani yao. Hali hiyo imeendelea huko kwa miaka 60. Acheni tusali ili uaminifu wa ndugu na dada zetu katika inchi mbalimbali umuletee Yehova utukufu na uwasaidie wanaopenda haki wakubali ibada ya kweli.​—Zab. 76:8-10.

15. Toa mufano unaoonyesha namna mwenendo wetu muzuri unavyoweza kufanya watu wakubali kweli.

15 Mwenendo wetu muzuri unaweza pia kuwasaidia watu wakubali kweli. (Soma 2 Wakorintho 6:4, 7.) Kwa mufano, fikiria jambo hili: “Dada mumoja alipotaka kulipa feza za bisi, rafiki yake alimuambia kwamba haikuwa lazima alipe kwa sababu hatafika mbali. Dada huyo alimujibu kwamba ilikuwa vizuri alipe feza za bisi. Kisha, rafiki yake huyo akashuka. Shofere aligeuka na kumuuliza dada yetu: “Je, wewe ni Shahidi wa Yehova?” Dada yetu alijibu “ndiyo,” na kumuuliza hivi: “Sababu gani unaniuliza hivyo?” Shofere huyo akajibu hivi: “Nilisikia namna ulivyokuwa ukizungumuza na rafiki yako kuhusu kulipa feza za bisi, na ninajua kwamba Mashahidi wa Yehova ni kati ya watu wachache sana wanaofanya hivyo na wanaosema kweli katika mambo yote.” Miezi michache baadaye, dada alipokuwa kwenye mikutano, mwanaume mumoja alikuja mbele yake na kumuuliza hivi: “Je, unanijua? Mimi ndiye yule shofere aliyezungumuza na wewe kuhusu kulipa feza za bisi. Kisha kutazama mwenendo wako, niliamua kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova.” Bila shaka, mwenendo wetu muzuri unatufanya tuwe watumishi wa Mungu wenye kuaminika.

ENDELEA KUONYESHA SIFA ZINAZOMULETEA MUNGU UTUKUFU

16. Sababu gani watu wanaweza kuguswa moyo tunapoonyesha sifa kama vile uvumilivu, upendo, na wema? Toa mufano wa mambo ambayo viongozi wa dini wanafanya.

16 Tunawasaidia watu pia wamukaribie Yehova tunapoonyesha sifa kama vile uvumilivu, upendo na wema. Watu fulani wanaotutazama wanaweza kutamani kujifunza kumuhusu Yehova, makusudi yake, na watu wake. Mutazamo na mwenendo wa Wakristo wa kweli unatofautiana sana na hali ya watu wa dini nyingine ya kujionyesha-onyesha tu kama wanamupenda Mungu, ijapokuwa matendo yao ni ya unafiki tu. Viongozi fulani wa dini wamekuwa matajiri kwa kuwaiba waamini wao, wakitumia feza wanazoiba ili kuwa na nyumba na gari za bei kali, na imeripotiwa kwamba kiongozi mumoja alijengea imbwa yake nyumba iliyo na mashine inayoleta baridi ao joto. Kwa kweli, wengi wanaodai kwamba wanamufuata Kristo hawana nia ya ‘kutoa bure.’ (Mt. 10:8) Lakini kama vile makuhani waasi katika Israeli ya zamani, ‘wanafundisha ili tu wapate malipo’ na mafundisho yao mengi hayapatane na Biblia. (Mk. 3:11) Mwenendo kama huo wa unafiki haumusaidie mutu yeyote ajipatanishe na Mungu.

17, 18. (a) Namna gani tunamuletea Yehova utukufu tunapoonyesha sifa zake katika maisha yetu? Toa mufano. (b) Ni sababu gani zinazokuchochea uendelee kufanya kazi njema?

17 Kwa upande mwengine, watu wanaguswa moyo tunapowafundisha mafundisho ya Kikristo ya kweli na tunapowatendea matendo mazuri. Kwa mufano, alipokuwa katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, mujane mumoja mwanamuke mwenye kuzeeka alimufukuza haraka painia mumoja. Mujane huyo alisema kwamba wakati ndugu alipiga kengele ya mulango, yeye alikuwa kwenye ngazi katika chumba cha kupikia chakula akijaribu kubadili taa ya umeme (ampoule). Painia huyo alimuambia hivi: “Ni hatari kufanya hivyo wewe pekee yako.” Painia huyo alimusaidia kubadili taa hiyo na kuendelea na safari yake. Mwana wa mujane huyo aliposikia mambo yaliyotukia, alifurahi sana na alijaribu kumutafuta ndugu yetu ili amutolee shukrani yake. Baadaye, mwana wa mujane huyo alikubali funzo la Biblia.

18 Sababu gani umeazimia kuendelea kufanya kazi njema? Labda kwa sababu unajua kwamba tunapoonyesha bidii katika kazi yetu ya kuhubiri na tunapofanya mambo kulingana na mapenzi ya Mungu, tunamuletea Yehova utukufu na tunaweza kuwasaidia wengine waokolewe. (Soma 1 Wakorintho 10:31-33.) Tunahubiri kwa bidii na tunakuwa na mwenendo muzuri kwa sababu tunamupenda sana Yehova na wanadamu wenzetu. (Mt. 22:37-39) Ikiwa tunaonyesha bidii kwa ajili ya kazi njema, tutapata furaha nyingi na kutosheka sasa. Zaidi ya hayo, tunaweza kungojea kwa hamu wakati ambapo wanadamu wote watamuabudu Muumba wetu, Yehova, kwa bidii na kumuletea utukufu.