Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari zilizozungumuziwa hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Basi, jaribu kujibu maulizo yanayofuata:

Bibliomansia ni nini, na Wakristo wanapaswa kuiona namna gani?

Bibliomansia ni zoea la kufungua Biblia kwa gafula na kusoma andiko ambalo mutu anaona kwanza na kufikiri kwamba maneno ya andiko hilo yatatoa musaada ao uongozi unaohitajiwa. Wakristo wa kweli hawatafute ishara za bahati. Lakini, wanajifunza Biblia ili kupata ujuzi wa kweli na uongozi wa Mungu.​—15/12, ukurasa wa 3.

“Ulimwengu” ambao utapitilia mbali ni nini?

“Ulimwengu” ambao utapitilia mbali ni watu wote wa ulimwengu ambao hawaishi kupatana na mapenzi ya Mungu. (1 Yoh. 2:17) Dunia haitaharibiwa na wanadamu waaminifu wataokolewa.​—1/1, ukurasa wa 5-7.

Ijapokuwa alikufa, namna gani Abeli angali anasema na sisi? (Ebr. 11:4)

Abeli anasema na sisi kupitia imani yake. Tunaweza kujifunza kutokana na imani yake na kujikaza kuiga imani hiyo. Mufano wake ni wenye nguvu mupaka leo.​—1/1, ukurasa wa 12.

Ni mambo gani ambayo hatupaswe kuruhusu yatutenganishe na Mungu?

Mambo fulani kati ya hayo ni: kazi yetu, namna yetu ya kujifurahisha, uhusiano wetu na mutu wa familia aliyetengwa na kutaniko, namna tunavyotumia teknolojia ya sasa, mahangaiko kuhusu afya yetu, maoni yasiyofaa kuhusu feza, na kuwa na kiburi na kufikiri kwamba tunajua mambo mengi sana kupita wengine.​—15/1, ukurasa wa 12-21.

Unyenyekevu wa Musa unatufundisha nini?

Kuliko kuacha mamlaka yake yamuletee kiburi, Musa hakujitegemea, lakini aliendelea kumutegemea Yehova. Hatutaki hata kidogo kuruhusu uwezo, mamlaka, ao vipawa vyetu vitufanye kuwa wenye kiburi, lakini tunataka kumutegemea Yehova. (Met. 3:5, 6)​—1/2, ukurasa wa 5.

Wale watakaofufuliwa wataishi wapi?

Hesabu ndogo ya watu 144 000 wataishi mbinguni. Watu wengine wengi watafufuliwa wakiwa na tumaini la kuishi milele hapa duniani.​—1/3, ukurasa wa 6.

Ni katika maana gani Waisraeli “hawakutahiriwa moyoni”? (Yer. 9:26)

Moyo wao uliazimia kuasi na walipaswa kuachana na mambo yaliyofanya mioyo yao iwe migumu, kama vile mawazo yao, mambo waliyohangaikia ao kupenda sana, ao nia yao iliyopingana na mapenzi ya Mungu. (Yer. 5:23, 24)​—15/3, ukurasa wa 9-10.

Namna gani Yesu alikuwa mufano muzuri wa mutu aliyekuwa na maisha yenye maana?

Alikuwa na kusudi katika maisha, ni kusema, kufanya mapenzi ya Mungu. Alikuwa na upendo mwingi kwa baba yake, na alipenda watu. Kwa hiyo, Yesu alijua kwamba baba yake alimupenda na alimukubali. Hayo ndiyo mambo yanayoweza kufanya maisha yawe na maana.​—1/4, ukurasa wa 4-5.

Sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova hapa duniani inatia ndani nini?

Inatia ndani Baraza Linaloongoza, halmashauri za biro za tawi, waangalizi wanaosafiri, mabaraza ya wazee, makutaniko, na wahubiri.​—15/4, ukurasa wa 29.

Sababu gani hatuwezi kusema kwamba hukumu za Mungu zilikuwa bila huruma?

Yehova hapendezwe na kifo cha waovu. (Eze. 33:11) Mufano wa hukumu za Mungu za wakati wa zamani unaonyesha kama Mungu anawaonya watu kwa upendo mbele ya kuleta hukumu. Hilo linaweza kututolea tumaini la kuokoka hukumu inayokuja.​—1/5, ukurasa wa 5-6.

Je, Waisraeli waliwaua wahalifu kwa kuwatundika kwenye miti?

Hapana. Mataifa mengine ya zamani yaliwaua wahalifu kwa kuwatundika kwenye miti, lakini Waisraeli hawakufanya hivyo. Inawezekana, wakati Maandiko ya Kiebrania yalikuwa yakiandikwa, mutenda mabaya aliuawa kwanza, kama vile kwa kupigwa mawe. (Law. 20:2, 27) Kisha mwili wake ulitundikwa kwenye muti ili kuwatolea wengine onyo.​—15/5, ukurasa wa 13.

Sababu gani amani imekosekana kabisa duniani?

Hata ikiwa wanadamu wametimiza mambo ya ajabu, hawakuumbwa wakiwa na uwezo wa kuongoza hatua zao wenyewe. (Yer. 10:23) Kwa kuwa Shetani ndiye anayetawala ulimwengu, wanadamu hawataweza kuleta amani. (1 Yoh. 5:19)​—1/6, ukurasa wa 16.