Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Tazama! Mimi Nipo Pamoja Nanyi Siku Zote”

“Tazama! Mimi Nipo Pamoja Nanyi Siku Zote”

‘Tazama! mimi nipo pamoja nanyi siku zote mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’​—MT. 28:20.

1. (a) Eleza kwa kifupi mufano wa ngano na magugu. (b) Namna gani Yesu alifasiria maana ya mufano huo?

 YESU alitoa mifano mingi iliyozungumuzia Ufalme, moja kati ya mifano hiyo ni ule mufano wa mulimaji aliyepanda mbegu nzuri za ngano na adui aliyepanda magugu katikati ya mbegu hizo nzuri. Magugu yalikomaa na kufunika ngano, lakini mulimaji aliwaamuru watumwa wake ‘waache zikue [zikomalie] pamoja mupaka wakati wa mavuno.’ Wakati wa mavuno, magugu yangeharibiwa na ngano zingekusanywa. Yesu mwenyewe alifasiria mufano huo. (Soma Mathayo 13:24-30, 37-43.) Mufano huo unafunua nini? (Ona kisanduku “Ngano na Magugu.”)

2. (a) Mambo yaliyotokea katika shamba la mulimaji yanaonyesha nini? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Mambo yaliyotokea katika shamba la mulimaji huyo yanaonyesha namna gani na wakati gani Yesu angekusanya kutoka katika mataifa kikundi cha watu wanaofananishwa na ngano, ni kusema, Wakristo watiwa-mafuta ambao watatawala pamoja naye katika Ufalme wake. Mbegu zilianza kupandwa kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33. Kukusanywa kutamalizika wakati watiwa-mafuta watakaokuwa wangali duniani mwishoni mwa ulimwengu huu watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho na kisha watainuliwa ili kuenda mbinguni. (Mt. 24:31; Ufu. 7:1-4) Kama vile kupanda juu ya mulima kunaweza kumufanya mutu aone vizuri maeneo fulani yaliyo kandokando, vilevile mufano huo unatusaidia kuona vizuri mambo ambayo yangetokea katika kipindi cha miaka 2 000 hivi. Tunapochunguza wakati wetu, ni mambo gani yanayohusiana na Ufalme tunayojionea? Mufano huo unazungumuzia wakati wa kupandwa kwa mbegu, wakati wa kukomaa kwazo, na wakati wa mavuno. Habari hii itazungumuzia zaidi sana wakati wa mavuno. *

YESU ANAENDELEA KULINDA WAKRISTO WATIWA-MAFUTA

3. (a) Ni hali gani iliyotokea kisha kifo cha mitume? (b) Kulingana na Mathayo 13:28, ni ulizo gani lililotokezwa, na liliulizwa na nani? (Ona maelezo ya kumalizia.)

3 Kisha mwaka wa 100, “magugu yalionekana” wakati wale wanaojidai kuwa Wakristo walianza kuonekana katika shamba, ni kusema, ulimwengu. (Mt. 13:26) Kisha tu mwaka wa 300, Wakristo wa uongo, ni kusema, magugu, waliongezeka zaidi kuliko Wakristo watiwa-mafuta. Kumbuka kwamba katika mufano wa Yesu, watumwa walimuomba bwana wao ruhusa ya kuondoa magugu. * (Mt. 13:28) Bwana wao aliwajibu namna gani?

4. (a) Jibu la Yesu, ambaye ni Bwana wa mavuno, linatuonyesha nini? (b) Ni wakati gani Wakristo wanaofananishwa na ngano walianza kutambuliwa?

4 Alipozungumuzia ngano na magugu, Yesu alisema hivi: ‘Acheni zikue [zikomalie] pamoja mupaka wakati wa mavuno.’ Amri hiyo inaonyesha kwamba tangu wakati wa mitume mupaka leo, duniani kumekuwa siku zote Wakristo watiwa​-mafuta, ni kusema, Wakristo walio mufano wa ngano. Jambo hilo linahakikishwa na yale ambayo Yesu aliwaambia baadaye wanafunzi wake aliposema hivi: ‘Mimi nipo pamoja nanyi siku zote mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mt. 28:20) Kwa hiyo, Yesu angewalinda Wakristo watiwa-mafuta siku zote mupaka wakati wa mwisho. Hata hivyo, kwa kuwa walifunikwa na Wakristo wanaofananishwa na magugu, hatujue kwa kweli ni nani waliokuwa sehemu ya kikundi cha Wakristo wanaofananishwa na ngano katika kipindi hicho kirefu cha wakati. Lakini, miaka fulani mbele ya wakati wa mavuno kuanza, kikundi cha watu wanaofananishwa na ngano kilianza kutambuliwa. Namna gani?

MUJUMBE ‘ANAFUNGUA NJIA’

5. Unabii wa Malaki ulitimia namna gani wakati wa Yesu?

5 Miaka mingi mbele ya Yesu kuzungumuzia mufano wa ngano na magugu, Yehova alimuongoza nabii wake Malaki atabiri mambo fulani yanayozungumuziwa katika mufano wa Yesu. (Soma Malaki 3:1-4.) Yohana Mubatizaji alikuwa ndiye ‘mujumbe aliyefungua njia.’ (Mt. 11:10, 11) Alipofika katika mwaka wa 29, wakati wa kuhukumu taifa la Israeli ulikuwa umekaribia. Yesu alikuwa mujumbe wa pili. Alisafisha hekalu la Yerusalemu mara mbili. Mara ya kwanza, wakati alianza kazi yake ya kuhubiri; na mara ya pili alipokaribia mwisho wa kazi yake. (Mt. 21:12, 13; Yoh. 2:14-17) Kwa hiyo, kazi ya Yesu ya kusafisha hekalu ilichukuwa kipindi fulani cha wakati.

6. (a) Unabii wa Malaki ulitimia kwa njia kubwa zaidi namna gani? (b) Ni wakati gani Yesu alifanya uchunguzi wa hekalu la kiroho? (Ona maelezo ya kumalizia.)

6 Unabii wa Malaki ulitimia kwa njia kubwa zaidi namna gani? Miaka fulani mbele ya 1914, Charles Taze Russell na wenzake walifanya kazi inayofanana na ile ya Yohana Mubatizaji. Kazi hiyo ya lazima ilitia ndani kurudisha tena mafundisho ya kweli ya Biblia. Wanafunzi wa Biblia walifundisha kweli kuhusu zabihu ya ukombozi ya Kristo, walionyesha wazi uongo wa fundisho la moto wa mateso, na walitangaza mwisho wa Nyakati za Mataifa. Hata hivyo, kulikuwa vikundi vingi vya kidini vilivyodai kuwa vinamufuata Kristo. Kwa hiyo ulizo la maana lilihitaji kujibiwa: Ni nani kati ya vikundi hivyo ambao walikuwa ngano? Ili kujua jambo hilo, Yesu alianza kuchunguza hekalu la kiroho katika mwaka wa 1914. Uchunguzi na kazi ya kusafisha hekalu la kiroho ilichukua kipindi fulani cha wakati, ni kusema, kuanzia 1914 mupaka mwanzoni mwa 1919. *

MIAKA YA UCHUNGUZI NA USAFISHAJI

7. Yesu alipoanza kufanya uchunguzi wake katika 1914, alikuta hali gani?

7 Yesu alipoanza kufanya uchunguzi, alikuta hali gani? Alikuta kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia wenye bidii ambao kwa miaka zaidi ya 30 walikuwa wametumia nguvu zao na mali yao katika kampanye kubwa ya Mahubiri. * Yesu na malaika walifurahi sana kuona kwamba kulikuwa hesabu ndogo ya shina za ngano ambazo hazikusongwa na magugu ya Shetani! Hata hivyo, ilionekana kwamba ilifaa ‘kutakasa wana wa Lawi,’ ni kusema, watiwa​-mafuta hao. (Mal. 3:2, 3; 1 Pet. 4:17) Sababu gani?

8. Ni mambo gani yaliyotokea kisha 1914?

8 Mwishoni mwa 1914, Wanafunzi fulani wa Biblia walivunjika moyo kwa sababu hawakuenda mbinguni. Katika 1915 na 1916, walipunguza bidii yao katika kazi ya kuhubiri kwa sababu ya upinzani uliotoka inje ya tengenezo. Jambo la kuhuzunisha zaidi ni kwamba kisha kifo cha Ndugu Russell katika Mwezi wa 10, 1916, upinzani ulitokea pia katika tengenezo. Ndugu wane kati ya wale saba waliosimamia Watch Tower Bible and Tract Society walipinga uamuzi wa kumufanya Ndugu Rutherford kuwa musimamizi wa sosaiti. Walijaribu kutia migawanyiko kati ya ndugu, lakini katika Mwezi wa 8, 1917, waliacha Beteli. Hiyo ilikuwa kabisa kazi ya kusafisha! Pia, Wanafunzi fulani wa Biblia waliogopa mwanadamu. Lakini, wengi walikubali kusafishwa na Yesu na walifanya mabadiliko yaliyohitajiwa. Kwa hiyo, Yesu aliona kwamba wao ndio Wakristo wa kweli waliofananishwa na ngano, lakini alikataa wote waliokuwa wanajifanya kuwa Wakristo, kutia ndani wote kati ya wale waliopatikana katika dini zinazojidai kuwa za Kikristo. (Mal. 3:5; 2 Tim. 2:19) Ni jambo gani lililotokea baadaye? Ili kupata jibu, acheni tuzungumuzie tena mufano wa ngano na magugu.

MAMBO YALIYOTOKEA KISHA WAKATI WA MAVUNO KUANZA

9, 10. (a) Tutazungumuzia nini sasa kuhusiana na wakati wa mavuno? (b) Ni jambo gani lililotokea kwanza wakati wa mavuno?

9 Yesu alisema hivi: ‘Yale mavuno ni umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mt. 13:39) Wakati huo wa mavuno ulianza katika 1914. Tutazungumuzia mambo matano yaliyotabiriwa na Yesu, ambayo yangetokea wakati huo.

10 Jambo la kwanza ni kukusanywa kwa magugu. Yesu alisema hivi: “Katika majira ya mavuno nitawaambia wavunaji, Kwanza kusanyeni magugu na kuyafunga matita-matita [mafungu-mafungu].” Kisha 1914, malaika walianza ‘kukusanya’ Wakristo wanaofananishwa na magugu kwa kuwatenganisha na “wana wa Ufalme,” ni kusema, watiwa​-mafuta.​—Mt. 13:30, 38, 41.

11. Ni kazi gani ambayo mupaka leo inaendelea kutofautisha Wakristo wa kweli na wale wanaojidai kuwa Wakristo?

11 Kazi ya kukusanya ilipokuwa ikisonga mbele, tofauti kati ya vikundi hivyo viwili ilianza kuonekana waziwazi zaidi. (Ufu. 18:1, 4) Mwanzoni mwa 1919, ilionekana wazi kwamba Babiloni Mukubwa alikuwa ameanguka. Ni jambo gani lililowatofautisha kabisa Wakristo wa kweli na wale waliojidai kuwa Wakristo? Ni kazi ya kuhubiri. Wale waliosimamia kazi ya kuhubiri ya Wanafunzi wa Biblia walianza kukazia kwamba kila mwanafunzi wa Biblia anapaswa kufanya kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Kwa mufano, kijitabu chenye kichwa Ni Nani Waliopewa Kazi Hii? kilichotolewa katika mwaka wa 1919 [katika Kiingereza] kiliwatia moyo Wakristo wote watiwa-mafuta kuhubiri nyumba kwa nyumba. Kijitabu hicho kilisema hivi: “Kazi hii inaonekana kuwa kubwa sana, lakini ni kazi ya Bwana, na kwa nguvu zake, tutaitimiza. Muna pendeleo la kufanya kazi hiyo.” Je, Wanafunzi wa Biblia walikubali pendeleo hilo? Katika 1922, gazeti Munara wa Mulinzi lilionyesha kwamba kuanzia wakati huo na kuendelea, Wanafunzi wa Biblia waliongeza bidii yao katika kazi ya kuhubiri. Tangu wakati huo mupaka leo, kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba imekuwa alama inayotambulisha Wakristo hao waaminifu.

12. Wakristo wanaofananishwa na ngano wameendelea kukusanywa tangu wakati gani?

12 Jambo la pili ni kukusanywa kwa ngano. Yesu aliamuru malaika wake hivi: ‘Nendeni mukusanye ngano galani mwangu.’ (Mt. 13:30) Kuanzia 1919, Wakristo watiwa-mafuta wameendelea kukusanywa na kuingizwa katika kutaniko la Kikristo lililoanzishwa upya. Watiwa-mafuta watakaokuwa wangali wanaishi wakati mwisho utafika, watakusanywa kwa mara ya mwisho wakati watapokea zawadi yao ya kuenda mbinguni.​—Dan. 7:18, 22, 27.

13. Andiko la Ufunuo 18:7 linaonyesha kwamba kahaba, ao Babiloni Mukubwa, kutia ndani dini zinazojidai kuwa za Kikristo, iko katika hali gani leo?

 13 Jambo la tatu ni kulia na kusaga meno. Malaika watakapokwisha kukusanya magugu, ni jambo gani litakalotokea? Alipozungumuzia hali ya kikundi kinachofananishwa na magugu, Yesu alisema hivi: “Humo ndimo watalia na kusaga meno yao.” (Mt. 13:42) Je, jambo hilo linafanyika leo? Hapana. Leo, dini zinazojidai kuwa za Kikristo ni sehemu ya yule kahaba. Kahaba huyo angali anasema hivi: ‘Ninaketi nikiwa malkia, nami si mujane, nami sitaona maombolezo kamwe.’ (Ufu. 18:7) Bila shaka, dini zinazojidai kuwa za Kikristo, zinajiaminia sana, na hata kudai kwamba ‘zinaketi zikiwa malkia’ juu ya viongozi wa ulimwengu. Kwa sasa, wale wanaofananishwa na magugu hawalie lakini wanaendelea kujisifu. Lakini hivi karibuni watalia na kusaga meno.

Urafiki wa karibu kati ya dini zinazojiita kuwa za Kikristo na viongozi wa ulimwengu utaisha karibuni

14. (a) Wale wanaojidai kuwa Wakristo ‘watasaga meno yao’ wakati gani na sababu gani? (b) Namna gani mafasirio hayo mapya kuhusu andiko la Mathayo 13:42 yanapatana na mawazo yaliyo katika Zaburi 112:10? (Ona maelezo ya kumalizia.)

14 Wakati wa ziki kubwa, kisha kuharibiwa kwa dini zote za uongo, waamini wa dini hizo watakimbia ili kujificha, lakini hawatapata mahali popote salama pa kujificha. (Lu. 23:30; Ufu. 6:15-17) Kisha, watakapotambua kwamba hakuna mahali popote pa kujificha, watalia kwa uchungu na ‘kusaga meno yao’ kwa hasira. Kama Yesu alivyotabiri katika unabii wake kuhusu ziki kubwa, katika kipindi hicho kibaya sana, ‘watajipiga-piga wenyewe kwa kuomboleza.’ *​—Mt. 24:30; Ufu. 1:7.

15. Magugu yatafanyiwa nini, na jambo hilo litatokea wakati gani?

 15 Jambo la ine ni kutupwa katika tanuru ya moto. Magugu yenye kufungwa matita-matita yatafanyiwa nini? Malaika ‘watayatupa katika tanuru ya moto.’ (Mt. 13:42) Hilo linamaanisha kuharibiwa milele. Kwa hiyo, waamini hao wa dini za uongo wataharibiwa katika sehemu ya mwisho ya ziki kubwa, ni kusema, Har-magedoni.​—Mal. 4:1.

16, 17. (a) Ni jambo gani la mwisho ambalo Yesu alionyesha katika mufano wake? (b) Sababu gani tunasema kama jambo hilo litatimia wakati ujao?

 16 Jambo la tano ni kungaa sana. Yesu alimalizia unabii wake kwa kusema hivi: ‘Wakati huo waadilifu watangaa kwa uangavu kama jua katika ufalme wa Baba yao.’ (Mt. 13:43) Jambo hilo litatendeka wakati gani na wapi? Maneno hayo yatatimia wakati ujao. Yesu hakuwa anatabiri jambo fulani linalotendeka sasa duniani, lakini jambo litakalotokea wakati ujao huko mbinguni. * Kwa nini tunasema hivyo? Tuzungumuzie sababu mbili.

17 Sababu ya kwanza ni maneno ambayo Yesu alitumia yanayoonyesha wakati. Yesu alisema hivi: ‘Wakati huo waadilifu watangaa.’ Maneno “wakati huo” yanahusiana kabisa na jambo ambalo Yesu alikuwa ameonyesha, ni kusema, ‘kutupwa kwa magugu katika tanuru la moto.’ Hilo litatokea wakati wa sehemu ya mwisho ya ziki kubwa. Kwa hiyo, Wakristo watiwa​-mafuta ‘watangaa kwa uangavu’ kabisa wakati huo ujao. Sababu ya pili ni neno ambalo Yesu alitumia linaloonyesha mahali. Yesu alisema kwamba wenye haki ‘watangaa katika ufalme.’ Hilo linamaanisha nini? Wakristo wote watiwa-mafuta waaminifu ambao watakuwa wangali duniani kisha sehemu ya kwanza ya ziki kubwa watakuwa tayari wametiwa muhuri kwa mara ya mwisho. Kisha, kama vile Yesu alivyoonyesha katika unabii wake kuhusu ziki kubwa, wataenda kujiunga na wenzao huko mbinguni. (Mt. 24:31) Huko watangaa “katika ufalme wa Baba yao,” na muda kidogo kisha Har-magedoni, kama bibi-arusi mwenye furaha, watafanya ‘ndoa’ pamoja na Mwana Kondoo.​—Ufu. 19:6-9.

TUNAFAIDIKA NAMNA GANI?

18, 19. Kuelewa mufano wa Yesu wa ngano na magugu kunatuletea faida gani?

18 Tunapata faida gani kwa kuelewa mufano huo vizuri? Tuzungumuzie faida tatu. Faida ya kwanza: Ujuzi wetu unaongezeka. Mufano huo unaonyesha sababu moja ya maana inayomufanya Yehova aruhusu mambo mabaya. ‘Anavumilia . . . vyombo vya gazabu’ ili kutayarisha “vyombo vya rehema,” ni kusema, watu wanaofananishwa na ngano. * (Rom. 9:22-24) Faida ya pili: Kuelewa mufano huo vizuri kunatia nguvu tumaini letu. Kwa kuwa mwisho unakaribia, adui zetu watafanya yote wanayoweza ili kupigana nasi ‘lakini hawatatushinda.’ (Soma Yeremia 1:19.) Kama vile Yehova alivyoendelea kulinda watu wanaofananishwa na ngano kwa miaka mingi, vivyo hivyo Baba yetu wa mbinguni, kupitia Yesu na malaika, atakuwa pamoja na sisi “siku zote” zinazokuja.​—Mt. 28:20.

19 Faida ya tatu: Kuelewa vizuri mufano huo kunatusaidia kutambua kikundi cha watu wanaofananishwa na ngano. Kwa nini jambo hilo ni la maana kwetu? Kujua Wakristo hao wanaofananishwa na ngano kunatusaidia kupata jibu la ulizo ambalo Yesu aliuliza katika unabii wake unaotimia kwa njia kubwa kuhusu siku za mwisho. Aliuliza hivi: ‘Ni nani kwa kweli mutumwa mwaminifu na mwenye busara?’ (Mt. 24:45) Habari mbili zinazofuata zitajibia vizuri ulizo hilo.

 

^ Fungu la 2: Ikiwa unapenda kujikumbusha maana ya sehemu zingine za mufano huo, tunakutia moyo usome habari yenye kichwa ‘Waadilifu Watangaa kwa Uangavu Kama Jua’ katika Munara wa Mulinzi wa Tarehe 15/03/2010.

^ Fungu la 3: Watumwa hao wanafananisha kabisa malaika kwa sababu mitume wa Yesu walikuwa wamekufa na mabaki ya watiwa-mafuta ndio waliofananishwa na ngano. Baadaye, katika mufano huo Yesu alionyesha kwamba wanaokusanya magugu ni malaika.​—Mt. 13:39.

^ Fungu la 6: Hayo ni mafasirio mapya. Zamani, tulielewa kwamba Yesu alichunguza hekalu katika 1918.

^ Fungu la 7: Kuanzia 1910 mupaka 1914, Wanafunzi wa Biblia walitolea watu vitabu 4 000 000 hivi, na trakti na vijitabu zaidi ya 200 000 000.

^ Fungu la 14: Hayo ni mafasirio mapya ya Mathayo 13:42. Zamani, vichapo vyetu vilionyesha kwamba watu wanaojidai kuwa Wakristo wamekuwa ‘wakilia na kusaga meno’ kwa miaka mingi, wakinungunika kwa sababu “wana wa ufalme” wanawafunua wazi kuwa “wana wa yule mwovu.” (Mt. 13:38) Lakini, inaonekana wazi kwamba, watasaga meno wakati wa uharibifu.​—Zab. 112:10.

^ Fungu la 16: Andiko la Danieli 12:3 linasema kwamba ‘wale walio na ufahamu [Wakristo watiwa-mafuta] watangaa kama mwangaza wa anga.’ Wanafanya hivyo wakiwa wangali duniani kwa kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Lakini, andiko la Mathayo 13:43 linazungumuzia wakati ambapo watangaa sana katika Ufalme wa mbinguni. Zamani, tulielewa kwamba maandiko hayo mawili yalizungumuzia jambo lilelile, ni kusema, kazi ya kuhubiri.

^ Fungu la 18: Soma kitabu Mkaribie Yehova, ukurasa wa 288-289.

(Ona  fungu la 13)