Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Faidika na Usemi wa Biblia Wenye Kutofautisha Mawazo

Faidika na Usemi wa Biblia Wenye Kutofautisha Mawazo

Bila shaka unakubali kwamba Yesu alikuwa Mwalimu mukubwa sana kuliko wote ambao wamekwisha kuishi duniani. Pengine umejaribu kuiga njia fulani alizotumia ili kufundisha, kama vile namna alivyotumia maulizo na mifano. Lakini, je, umejaribu kufikiria namna alivyotumia mara nyingi usemi wenye kutofautisha mawazo alipokuwa akifundisha?

Watu wengi wanazoea kutumia usemi wenye kutofautisha mawazo wanapozungumuza. Wewe pia unaweza kutumia usemi huo mara nyingi pasipo hata kujua. Kwa mufano, unaweza kusema hivi: “Walisema kwamba matunda yote yameivya, lakini, matunda haya yangali mabichi.” Ao, “Zamani mutoto huyu alikuwa mwenye haya, lakini sasa haogope tena watu.”

Katika mifano kama hiyo, kwanza unazungumuzia hali ao wazo fulani; kisha unatumia maneno kama vile lakini, hata hivyo, kuliko, ao kwa upande mwingine ili kuonyesha tofauti kati ya mawazo mawili. Ao unaweza kuongeza jambo fulani linalokazia wazo ulilozungumuzia mwanzoni. Kuzungumuza hivyo kutafanya maneno yako yawe wazi na kunaweza kuwasaidia wengine waelewe yale unayosema.

Hata ikiwa usemi wenye kutofautisha mawazo hautumiwe sana katika luga fulani, tunapaswa kujua kwamba usemi huo ni wa maana sana. Sababu gani? Kwa sababu mifano mbalimbali ya usemi huo inapatikana katika Neno la Mungu lililoongozwa na roho yake. Yesu alitumia mara nyingi usemi wenye kutofautisha mawazo. Fikiria mifano hii: ‘Watu wanawasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa.’ “Sikuja kuharibu [Sheria], bali kutimiza.” “Ninyi mulisikia kwamba ilisemwa, ‘Usifanye uzinzi.’ Lakini mimi ninawaambia ninyi kwamba kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke . . . ” “Ilisemwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’ Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Musimupinge yeye aliye mwovu; bali yeyote anayekupiga kofi kwenye shavu lako la kuume, mugeuzie lile lingine pia.”​—Mt. 5:15, 17, 27, 28, 38, 39.

Usemi wenye kutofautisha mawazo unapatikana katika vitabu vingine vya Biblia. Usemi huo unaweza kukusaidia kuelewa jambo fulani ao kuonyesha njia nzuri zaidi ya kufanya jambo fulani. Ikiwa wewe ni muzazi, fikiria usemi huu: ‘Nanyi, akina baba, musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nizamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.’ (Efe. 6:4) Ikiwa mutume Paulo alimaanisha tu kwamba baba (ao mama) anapaswa kumufundisha mutoto kanuni za Yehova, hilo lingekuwa jambo la hekima na la kweli. Lakini wazo lake linaeleweka waziwazi zaidi anaposema ‘musiwe mukiwakasirisha bali endeleeni kuwalea katika nizamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.’

Katika sura hiyo ya kitabu cha Waefeso, Paulo aliandika hivi: “Tuna kushindana mweleka, si juu ya damu na mwili, bali juu ya . . . majeshi ya roho waovu katika mahali pa kimbingu.” (Efe. 6:12) Usemi huo wenye kutofautisha mawazo unakusaidia kuelewa kwamba unapaswa kupigana vita kali sana. Haupigane na wanadamu wa hali ya chini, lakini, unapigana na majeshi ya roho waovu.

NAMNA YA KUFAIDIKA NA USEMI WA BIBLIA WENYE KUTOFAUTISHA MAWAZO

Katika kitabu hichohicho cha Waefeso, utaona maandiko mengi ambamo mutume Paulo alitumia usemi wenye kutofautisha mawazo. Kufikiri kuhusu usemi huo kunaweza kutusaidia kuelewa mambo aliyokuwa akizungumuzia na kunaweza kutusaidia kuelewa waziwazi zaidi jambo tunalopaswa kufanya.

Unaweza kufurahia na kuona kuwa jambo la maana kufikiria kisanduku kinachopatikana katika habari hii kinachoonyesha usemi mbalimbali wenye kutofautisha mawazo unaopatikana katika sura ya 4 na 5 ya kitabu cha Waefeso. Unaposoma kila usemi wenye kutofautisha mawazo, fikiri kuhusu maisha yako. Jiulize hivi: ‘Kwa kweli mimi ni mutu wa namna gani? Ninatenda namna gani katika hali hii ao katika hali inayofanana na hii? Wengine wanaweza kusema kwamba ni sehemu gani ya usemi huu inayofunua hali yangu?’ Ikiwa usemi huo unaonyesha waziwazi mambo unayopaswa kubadili, jikaze kufanya mabadiliko yanayohitajiwa. Faidika na usemi huo wenye kutofautisha mawazo.

Labda unaweza kutumia kisanduku kinachopatikana katika habari hii wakati wa ibada ya familia. Kwanza, kila mushiriki wa familia yako anaweza kusoma kila usemi wenye kutofautisha mawazo. Kisha mumoja kati yenu anaweza kutaja sehemu ya kwanza ya usemi huo na kuwaachia wengine wajaribu kukumbuka jambo linalokaziwa katika sehemu ya pili. Hilo linaweza kuwasaidia muwe na mazungumuzo yenye kufurahisha katika familia kuhusu namna munavyoweza kutumikisha vizuri zaidi sehemu hiyo ya pili katika maisha yenu. Bila shaka, kuchunguza usemi mbalimbali wenye kutofautisha mawazo kwa njia hiyo kunaweza kuwasaidia watoto na watu wazima kuwa na mwenendo muzuri katika familia na mahali pengine.

Je, unaweza kukumbuka sehemu ya pili ya usemi huu wenye kutofautisha mawazo?

Utakapoelewa vizuri zaidi faida ya usemi huo, unaweza kuanza kuuvumbua kwa urahisi, na utaona kwamba unaweza kukusaidia sana katika kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, unaweza kumwambia musikilizaji wako hivi: “Watu wengi wanasema kwamba kila mutu ana nafsi isiyokufa, lakini tuone yale ambayo Neno la Mungu linasema kuhusu jambo hilo.” Ao unapoongoza funzo la Biblia, unaweza kuuliza hivi: “Watu wengi hapa kwetu wanaamini kwamba Mungu na Yesu ni mutu mumoja; lakini, tumeona Biblia inafundisha nini? Na wewe unaamini nini?”

Kwa kweli, Biblia inatumia usemi mbalimbali wenye kutofautisha mawazo unaoweza kutusaidia tutembee katika njia ya Mungu. Na tunaweza kutumia usemi huo ili kusaidia watu wajue kweli ya Biblia.