Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari zilizozungumuziwa hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Basi, jaribu kujibu maulizo yanayofuata:

Ni wakati gani Yesu ‘aliwahubiria roho walio katika gereza’? (1 Pet. 3:19)

Inaonekana kwamba Yesu aliwatangazia roho hao waovu hukumu ya haki ambayo wanastahili kupewa wakati fulani kisha kufufuliwa.​—15/6, ukurasa wa 23.

Ni matatizo gani matatu yanayoweza kufanya ndoa ya pili isiwe na matokeo mazuri?

Matatizo hayo ni: kulinganisha ndoa ya pili na ile ya kwanza; kuona kuwa ni vigumu kushirikiana na marafiki waliomujua bibi ao bwana yako wa kwanza; kushindwa kutumainia bibi ao bwana yako mupya kwa sababu yule wa kwanza hakuwa mwaminifu.​—1/7, ukurasa wa 9-10.

Yesu atahukumu kondoo na mbuzi wakati gani? (Mt. 25:32)

Yesu atahukumu watu walio mufano wa kondoo ao mbuzi atakapokuja wakati wa ziki kubwa, itakuwa kisha kuharibiwa kwa dini zote za uongo.​—15/7, ukurasa wa 6.

Watu wanaoasi sheria wanaozungumuziwa katika mufano wa Yesu watalia na kusaga meno wakati gani? (Mt. 13:36, 41, 42)

Watafanya hivyo wakati wa ziki kubwa watakapotambua kwamba hakuna mahali popote ambapo wanaweza kujificha ili kuponyoka uharibifu.​—15/7, ukurasa wa 13.

Maneno ya Yesu kuhusu mutumwa mwaminifu na mwenye busara yalitimia wakati gani? (Mt. 24:45-47)

Maneno hayo hayakuanza kutimia kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 , lakini yalianza kutimia kisha 1914. Katika 1919, mutumwa mwaminifu aliwekwa juu ya watumishi wa nyumbani, ambao ni Wakristo wote wanaolishwa chakula cha kiroho na mutumwa huyo.​—15/7, ukurasa wa 21-23.

Ni wakati gani Yesu atamuweka mutumwa mwaminifu juu ya mali yake yote?

Atafanya hivyo wakati ujao, katika kipindi cha ziki kubwa wakati wale wanaofanyiza mutumwa mwaminifu wataanza kutawala pamoja na Kristo mbinguni.​—15/7, ukurasa wa 25.

Je, Biblia haitaje majina ya watu fulani kwa sababu watu hao walikuwa wabaya ao hawakuwa wa maana?

Hapana. Biblia haitaje majina ya watu fulani waliokuwa wazuri na ya wengine waliokuwa wabaya. (Rut. 4:1-3; Mt. 26:18) Ni majina ya malaika wawili tu waaminifu ndio yanatajwa katika Biblia.​—1/8, ukurasa wa 10.

Zaidi ya kutegemezwa na nguvu ya Mungu, ni jambo gani lingine lililosaidia Mashahidi 230 wavumilie matatizo waliyopata muda wa safari ya kifo kutoka kambi ya mateso ya Sachsenhausen?

Hata ikiwa walikuwa wameregea kwa sababu ya njaa na magonjwa, waliendelea kutiana moyo ili kuendelea na safari.​—15/8, ukurasa wa 18.

Sababu masimulizi kuhusu namna Waisraeli walivyovuka Muto Yordani ili kuingia katika Inchi ya Ahadi ni yenye kutia moyo?

Hata ikiwa muto ulikuwa umejaa sana, Yehova alisimamisha maji ili watu wake wavuke. Jambo hilo lilitia nguvu imani yao na liliwafanya wamutumainie Mungu zaidi. Sisi pia tunaweza kutiwa moyo na masimulizi hayo.​—15/9, ukurasa wa 16.

Biblia inataja mara nyingi rangi, hilo linaonyesha nini?

Biblia inapotaja rangi, hilo linaonyesha kwamba Mungu anaelewa kuwa rangi inaweza kumugusa mutu moyo na kumuchochea kufanya jambo fulani na inaweza kutusaidia tukumbuke mambo fulani.​—1/10, ukurasa wa 14-15.

Unabii wa Mika 5:5 kuhusu watawala wadogo na wachungaji unatimia namna gani leo?

Tunaelewa kwamba ‘wachungaji saba na watawala wadogo wanane’ wanaozungumuziwa kwenye Mika 5:5 ni wazee wa makutaniko, wanaotia nguvu watu wa Mungu ili wawe tayari kwa ajili ya shambulio ambalo limetabiriwa kuja juu yao wakati ujao.​—15/11, ukurasa wa 20.

Toa sababu fulani zinazofanya tuwe na lazima ya Mungu

Tuna lazima ya muongozo muzuri na majibu ya maulizo ambayo tunajiuliza kuhusu matatizo ya maisha, na Mungu ndiye anayetoa mambo yote hayo. Mungu anataka wanadamu waishi vizuri na wawe na furaha, na atatimiza ahadi zake zinazopatikana katika Neno lake ili tuweze kuishi vizuri na kwa furaha.​—1/12, ukurasa wa 4-6.