Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Aliwalinda Katika Vivuli vya Milima

Yehova Aliwalinda Katika Vivuli vya Milima

MWANAMUKE mumoja anapotoka katika nyumba yake asubuhi, anaona furushi moja kwenye mwingilio wa mulango wa mbele wa nyumba yake. Anaokota furushi hilo na kuangalia pande zote, lakini haone mutu yeyote katika barabara. Mutu fulani asiyejulikana ndiye aliacha furushi hilo usiku. Mwanamuke huyo anafungua furushi hilo kidogo na anarudi katika nyumba yake haraka na kufunga mulango. Katika furushi hilo muna vichapo vya Biblia vilivyokatazwa na serikali! Anakumbatia furushi hilo na kutoa sala ya kimyakimya. Katika sala hiyo, anamushukuru Yehova kwa sababu ya chakula hicho kizuri cha kiroho.

Mambo kama hayo yalitokea huko Ujerumani katika miaka ya 1930. Wanazi walipoanza kutawala katika mwaka wa 1933, kazi ya Mashahidi wa Yehova ilipigwa marufuku ao kukatazwa katika Ujerumani. Ndugu Richard Rudolph, * aliye sasa na miaka zaidi ya 100 anasema hivi: “Tulikuwa hakika kama sheria ya mwanadamu haiwezi kuzuia kazi ya kutangaza habari za Yehova na jina lake. Vichapo vya Biblia ndivyo tulikuwa tunatumia ili kujifunza na kuhubiri. Lakini, haikuwa rahisi kuvipata kwa sababu ya marufuku. Tulijiuliza namna gani kazi ingeendelea.” Baadaye ndugu Richard alivumbua kwamba angeweza kusaidia kwa njia isiyokuwa ya kawaida kabisa ili vichapo vipatikane. Mambo yalipaswa kufanywa katika vivuli vya milima.​—Amu. 9:36.

KUPITISHA VICHAPO KISIRISIRI

Ukipanda katika muto Elbe (ao Labe), utafika kwenye Milima ya Krkonoše, inayofanyiza mupaka kati ya Jamuhuri ya Cheki na Polandi. Milima hiyo inafikia tu urefu wa metre 1 600 hivi, hata hivyo watu wanaoishi sehemu ya katikati ya Ulaya wameita milima hiyo kisiwa cha aktiki. Teluji yenye urefu wa metre tatu inafunika milima hiyo kwa nusu ya mwaka. Wale wanaopuuza hali ya majira yenye kubadilika​-badilika wanaweza kufunikwa haraka na ukungu ao mawingu mazito yanayofunika sehemu za juu za milima hiyo.

Kwa miaka mingi, milima hiyo imefanyiza mupaka wa kiasili kati ya majimbo, falme na inchi. Zamani ilikuwa vigumu kwa askari kufanya ulinzi katika sehemu hiyo, kwa hiyo watu walikuwa wanapitisha vitu vyao hapo kwa njia ya magendo ao kisirisiri. Katika miaka ya 1930, wakati ambapo Milima ya Krkonoše ilifanyiza mipaka kati ya Chekoslovakia na Ujerumani, Mashahidi wa Yehova wenye ujasiri walianza kutumia njia zilizokuwa zikitumiwa zamani na watu waliokuwa wakipitisha hapo vitu kwa njia ya magendo. Sababu gani? Ili kusafirisha vichapo vya Biblia kutoka mahali ambapo vilipatikana kwa urahisi. Ndugu Young Richard alikuwa mumoja wa Mashahidi hao.

Ndugu na dada waliovaa kama watu wanaoenda kujitembeza milimani walibeba vichapo katika Milima ya Krkonoše na kuviingiza Ujerumani

HATARI TULIZOPAMBANA NAZO

Ndugu Richard anakumbuka: “Siku ya Posho na Siku ya Yenga, tulienda kwenye milima tukiwa vikundi-vikundi. Kila kikundi kilikuwa na ndugu vijana saba waliokuwa wamevaa kama watu walioenda kujitembeza milimani. Kuanzia upande wa Ujerumani, tulifanya saa tatu hivi ili kuvuka milima na kufika Špindlerův Mlýn”​—upande wa Jamuhuri ya Cheki. Watu walienda mahali hapo, panapopatikana umbali wa kilometre 16 na nusu, ili kufanya mapumuziko. Wakati huo, Wajerumani wengi waliishi katika eneo hilo. Mujerumani mumoja aliyekuwa mukulima alikubali kusaidia ndugu hao. Kwa kutumia motokari yake yenye kukokotwa na farasi ambayo ilikuwa ikitumiwa ili kubeba wale waliokwenda kupumuzikia mahali hapo, alichukua katoni za vichapo kwenye muji uliokuwa karibu. Katoni hizo zilikuwa zimetumwa hapo kwa treni kutoka Prague. Alipeleka katoni hizo kwenye shamba lake na kuzificha mahali pa kuweka nyasi yenye kukauka ili kungoja wale ambao wangepeleka vichapo hivyo kwenye upande wa Ujerumani.

Richard anaendelea kusema hivi: “Tulipofika kwenye shamba hilo, tulipakiza vichapo katika sakoshe zetu za kubeba mugongoni, zaidi sana sakoshe ambazo zilitengenezwa ili kubeba mizigo mizito. Kila mumoja wetu alibeba kilo 50 hivi.” Ili wasikamatwe, walitembea katika giza, walianza safari wakati jua lilikuwa limeshuka na walifika nyumbani asubuhi sana. Ndugu Ernst Wiesner, aliyekuwa mwangalizi wa muzunguko huko Ujerumani wakati huo, alieleza namna walivyofanya ili wasikamatwe: “Ndugu wawili walikuwa mbele na kila mara walipokutana na mutu fulani, waliwasha mara moja torshe zao. Ishara hiyo iliwaonyesha ndugu waliokuwa wanabeba sakoshe za mizigo na ambao walikuwa nyuma umbali wa metre 100 hivi kwamba walipaswa kujificha katika pori mupaka wakati ndugu waliokuwa mbele wangerudi nyuma na kuwatolea neno fulani la siri. Neno hilo lilikuwa linabadilishwa kila juma.” Lakini, hatari waliyopaswa kupambana nayo haikuwa tu polisi wa Ujerumani waliokuwa wanavaa nguo za rangi ya bluu.

Richard anakumbuka: “Mangaribi moja, nilikuwa na kazi nyingi, kwa hiyo niliwatangulia ndugu zangu ili kwenda upande wa Jamuhuri ya Cheki. Kulikuwa giza na kunguku, na nilikuwa nikitetemeka nilipokuwa nikitembea katika mvua ya barafu. Nilipotea katika miti midogo-midogo, na nilikosa njia kwa saa nyingi. Watu wengi waliokuwa wakijitembeza katika eneo hilo walikufa kwa njia hiyo. Niliona njia wakati tu nilikutana na ndugu waliokuwa wakirudia asubuhi.”

Kwa miaka mitatu hivi, kikundi kidogo cha ndugu wenye ujasiri kilikuwa kinapita katika milima hiyo kila juma. Wakati wa majira ya baridi, walitumia chombo kinachotumiwa ili kutembea juu ya barafu wakiwa na mizigo yao migongoni. Wakati fulani, vikundi-vikundi vya ndugu 20 hivi vilivuka mipaka muchana kwa kupita katika njia zilizokuwa zikitumiwa na watu waliokuwa wanaenda kujitembeza milimani. Kulikuwa dada fulani katika vikundi hivyo ili ionekane kwamba walikuwa tu wakienda kujitembeza milimani. Dada fulani walikuwa mbele na walipoona hatari, walitupa juu kofia zao.

Ilikuwa hatari kupita katika Milima ya Krkonoše kwa sababu sehemu zake za juu zinafunikwa na teluji

Ni mambo gani yalifanywa kisha safari hizo za usiku? Mipango ilichukuliwa mara moja ili vichapo hivyo vigawanywe. Namna gani? Vichapo vilifungwa katika vifurushi kama sabuni na kupelekwa mahali pa kungojea treni huko Hirschberg. Kisha, vifurushi hivyo vilitumwa katika sehemu mbalimbali za Ujerumani, ambako ndugu na dada walivigawia waamini wenzao kwa siri kama ilivyoonyeshwa mwanzoni mwa habari hii. Mambo yalipaswa kufanywa kwa siri kabisa kwa sababu ikiwa jambo lolote lingevumbuliwa, matokeo yangekuwa mabaya. Lakini, siku moja mambo yalivumbuliwa bila kutazamia.

Katika 1936, depo moja ya vichapo ilivumbuliwa karibu na Berlin. Kati ya vitu vilivyovumbuliwa kulikuwa vifurushi viwili vilivyotumwa na mutu fulani wa Hirschberg. Polisi walichunguza mwandiko ili kuvumbua mutu aliyevituma kisirisiri na kisha mutu huyo alikamatwa. Muda mufupi baadaye, wengine wawili, kutia ndani Richard Rudolph, walikamatwa. Kwa kuwa ndugu walikubali makosa yao, wengine waliendelea kufanya safari hizo hatari kwa muda fulani.

HABARI HII INATUFUNDISHA NINI?

Mashahidi wa Ujerumani walipokea vichapo vingi vilivyokuwa vikibebwa mugongoni katika Milima hiyo ya Krkonoše. Lakini, kulikuwa njia zingine zilizokuwa zikitumiwa. Majeshi ya Ujerumani yalipokamata Chekoslovakia mwishoni mwa 1939, kulikuwa njia kama hizo kwenye mupaka wa inchi hiyo. Katika inchi nyingine zinazopatikana kwenye ujirani wa Ujerumani, kama vile Ufaransa, Uholanzi, na Uswisi, Mashahidi wa pande zote mbili walihatarisha maisha yao ili kupeleka chakula cha kiroho kwa waamini wenzao waliokuwa wakiteswa.

Leo, wengi kati yetu wanaweza kupata vichapo vingi vya Biblia na vya aina mbalimbali. Unapochukua kichapo kipya kwenye Jumba la Ufalme ao unapokichukua kwenye adresi yetu ya Internete jw.org, kwa nini usifikirie kazi mbalimbali zilizofanywa ili uweze kupata kichapo hicho? Pengine haikuwa kama vile kutembea katika milima yenye teluji usiku, lakini waamini wenzako wengi wanaokutumikia kwa kujipendea walifanya kazi nyingi kabisa ili uweze kupata kichapo hicho.

^ Richard Rudolph alitumikia katika Kutaniko la Hirschberg huko Silesia. Muji wa Hirschberg, unaopatikana kusini​-mangaribi mwa Polandi, unaitwa sasa Jelenia Góra.