MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 2, 2014

Gazeti hili linaeleza matukio yenye kufurahisha yaliyo katika Zaburi 45. Inatuonyesha namna gani Yehova anatutimizia mahitaji yetu na kutulinda, na yeye ndiye Rafiki yetu muzuri zaidi.

Tumutukuze Kristo—Mufalme Mwenye Utukufu

Zaburi ya 45 inazungumuzia matukio gani ya maana yanayotuhusu leo?

Furahia Ndoa ya Mwana​-Kondoo!

Bibi-arusi ni nani, na namna gani Kristo amekuwa akimutayarisha kwa ajili ya ndoa? Ni wa nani watakaofurahia ndoa ya Mwana-Kondoo?

Mujane wa Sarefathi Alibarikiwa kwa Sababu ya Imani Yake

Ufufuo wa mwana wa mujane ulikuwa moja kati ya mambo yenye kutia nguvu ambayo alijionea katika maisha yake. Habari hiyo inaweza kutufundisha nini?

Yehova Anatutimizia Mahitaji Yetu na Kutulinda

Yehova ndiye Baba yetu wa mbinguni. Jifunze namna tunavyoweza kutia nguvu uhusiano wetu pamoja na Mungu, Mutimizaji Mukubwa wa Mahitaji yetu na Mulinzi wetu.

Yehova Ndiye Rafiki Yetu Muzuri Zaidi

Fikiria mifano ya Abrahamu na Gideoni, ambao walikuwa na urafiki wa karibu na Yehova Mungu. Tunapaswa kufanya nini ili tuwe marafiki wa Yehova?

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wayahudi wa wakati wa mitume walikuwa na sababu gani za kungojea Masiya wakati huo?

‘Ona Uzuri wa Yehova’

Mufalme Daudi wa Israeli alifurahia mupango ambao Mungu amefanya kwa ajili ya ibada ya kweli. Namna gani sisi pia tunaweza kufurahia ibada ya kweli leo?

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Filme Yenye Kujenga Imani Imefanya Miaka 100

Kumepita sasa miaka 100 tangu “Foto-Drama ya Uumbaji” ilionyeshwa kwa mara ya kwanza. Filme hiyo ilitayarishwa ili kusaidia watu wawe na imani iliyo nguvu katika Neno la Mungu Biblia.