VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU
Filme Yenye Kujenga Imani Imefanya Miaka 100
‘Huyu ni Ndugu Russell kabisa!’—Maneno ya mutu aliyetazama “Foto-Drama” katika mwaka wa 1914.
KUMEPITA sasa miaka 100 tangu “Foto-Drama ya Uumbaji” ilipoonyeshwa kwa mara ya kwanza. Filme hiyo yenye kupendeza ilitayarishwa ili kusaidia watu wawe na imani yenye nguvu katika Neno la Mungu Biblia. Katika wakati ambao watu waliamini sana mageuzi, walipenda kuchambua sana mambo, na mashaka yalikuwa yameharibu imani ya wengi, “Foto-Drama” ilionyesha waziwazi kwamba Yehova ndiye Muumbaji.
Charles T. Russell, aliyekuwa akisimamia Wanafunzi wa Biblia, aliendelea kutafuta njia zenye matokeo zaidi na ambazo zingesaidia kueneza haraka kweli za Biblia. Wanafunzi wa Biblia walikuwa tayari wametumia vichapo kwa zaidi ya miaka makumi tatu. Sasa walivumbua njia mupya ya kuhubiri, ni kusema, filme.
KUENEZA INJILI KUPITIA FILME
Filme zisizokuwa na sauti zilianza kuonyeshwa katika miaka ya 1890. Mwanzoni mwa 1903, filme moja ya mambo ya dini ilionyeshwa katika kanisa moja la New York City. Utayarishaji wa filme ulikuwa tu umeanza katika mwaka wa 1912. Wakati huo Russell naye alianza kutayarisha ile “Foto-Drama.” Alitambua kwamba njia hiyo ya kutolea watu kweli za Biblia itakuwa na matokeo zaidi kuliko kuwatolea vichapo tu.
“Foto-Drama” iliyokuwa na urefu wa saa nane, ilionyeshwa kwa kawaida katika sehemu ine, ilitia ndani hotuba fupi 96 zilizorekodiwa ambazo zilitolewa na mutu fulani aliyekuwa musemaji muzuri na aliyekuwa na sauti nzuri. Muziki wenye kupendeza uliambatana na sehemu nyingi. Mafundi walipiga sauti na rekodi za muziki kwenye fono, walifanya sauti zifuatane kwa wakati mumoja na picha zenye rangi za watu wenye kucheza hadisi za Biblia zenye kujulikana sana.
“Ilikuwa na picha zote kuanzia uumbaji wa nyota mupaka mwisho wa Utawala mutukufu wa Miaka Elfu wa Kristo.”—F. Stuart Barnes, aliyekuwa na miaka 14 katika mwaka wa 1914
Sehemu nyingi za filme na picha zenye rangi zilinunuliwa kwenye studio za kibiashara. Wachoraji wenye ufundi wa Philadelphia, New York, Paris, na London walichapa kwa mikono picha zenye rangi na filme, moja baada ya ingine. Vikundi vya wale waliofanya kazi katika Biro ya Mambo ya Picha ya Beteli Mwa. 22:9-12.
walichapa picha nyingi pia, kila mara walibadilisha picha zilizokuwa zimezeeka. Zaidi ya kununua filme, washiriki wa familia ya Beteli walipigwa picha za video katika Yonkers, New York, walipokuwa wanacheza sehemu za Abrahamu, Isaka, na malaika aliyemuzuia Abrahamu ili asimutoe mwana wake.—Rafiki mumoja wa Ndugu Russell aliwaambia wapasha-habari kwamba njia hiyo ‘ingewafanya wengi wapendezwe zaidi na Maandiko, kuliko jambo lingine lolote ambalo lilikuwa limefanywa ili kuchochea imani ya watu hapo mbele.’ Je, viongozi wa makanisa wangefurahia njia hiyo mupya ya kugusa mioyo ya vikundi vya watu waliokuwa na njaa ya kiroho? Hapana kabisa, viongozi wa makanisa kwa ujumla walichambua “Foto-Drama;” wengine hata walitumia njia za ujanja ili kutafuta kuwazuia watu wasiitazame. Ilipoonyeshwa mahali fulani, kikundi kimoja cha viongozi wa dini kilifanya mipango ili umeme ukatwe.
Hata hivyo, watu walijaa katika majumba ya sinema ili kutazama “Foto-Drama” bila kulipa. Watu walitazama “Foto-Drama” kila siku katika miji 80 huko Amerika. Kwa watazamaji wengi, hii ilikuwa mara yao ya kwanza kuona ‘filme yenye kuwa na sauti.’ Ufundi wa kupiga picha jambo fulani linalotokea hatua kwa hatua uliwawezesha kutazama namna kitoto cha ndege kilivyobomoa ganda la yayi na kutoka inje na namna maua yalivyokuwa yakifunguka pole kwa pole. Habari nyingi za kisayansi walizoona siku hiyo zilionyesha hekima kubwa ya Yehova. Kama ilivyoonyeshwa mwanzoni, alipoona Ndugu Russell kwenye skrini (écran) akisema maneno ya utangulizi ya “Foto-Drama,” mutu mumoja alisema hivi: ‘huyu ni Ndugu Russell kabisa!’
HATUA YA MAANA SANA KATIKA KUWAFUNDISHA WATU BIBLIA
Tim Dirks, ambaye ni muandikaji na mwanahistoria wa mambo ya filme alieleza “Foto-Drama” kuwa “filme ya kwanza kabisa iliyokuwa na sauti (maneno yenye kurekodiwa), picha zenye kutembea, na picha zinazoweza kuonyeshwa kwenye ubao.” Filme zilizotolewa mbele ya “Foto-Drama” zilikuwa na mambo fulani kati ya hayo yaliyotajwa lakini hakuna hata moja iliyokuwa na mambo yote hayo, zaidi sana yenye kuzungumuzia Biblia. Na hakuna hata moja iliyotazamwa na watu wengi hivyo. Kwa mufano, watu milioni kenda waliitazama huko Amerika ya Kaskazini, Ulaya, Australia, na Nyuzilandi katika mwaka wake wa kwanza pekee!
“Foto-Drama” ilionyeshwa kwa mara ya kwanza tarehe 11/01/1914, huko New York City. Kisha miezi saba, musiba mukubwa uliokuja kuitwa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, ulianza. Lakini, watu waliendelea kukusanyika ulimwenguni pote ili kutazama ile “Foto-Drama,” na walifarijiwa na sehemu zake zilizoonyesha baraka ambazo Ufalme utaleta wakati ujao. Katika mwaka wa 1914, hakuna filme iliyolingana na “Foto-Drama;” filme hiyo ilikuwa nzuri sana.