Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Ndiye Rafiki Yetu Muzuri Zaidi

Yehova Ndiye Rafiki Yetu Muzuri Zaidi

“[Abrahamu] akaitwa rafiki ya Yehova.”​—YAK. 2:23.

1. Kwa kuwa tumeumbwa kwa mufano wa Mungu, tuna uwezo gani?

 “MUTOTO wa nyoka ni nyoka.” Watu wengi wanazoea kusema hivyo. Kwa kawaida, watoto wengi wanafanana sana wazazi wao. Inakuwa hivyo kwa sababu mutoto anariti tabia ao sifa za baba na mama yake. Baba yetu wa mbinguni, Yehova, ndiye aliyetupatia maisha. (Zab. 36:9) Ndio sababu, sisi watoto wake wa kibinadamu tunamufanana kwa njia fulani. Kwa kuwa tumeumbwa kwa mufano wake, tuna uwezo wa kufikiri na kuchukua maamuzi na kufanya urafiki.​—Mwa. 1:26.

2. Ni nini inayofanya urafiki kati yetu na Yehova uwezekane?

2 Yehova anaweza kuwa Rafiki yetu muzuri zaidi. Urafiki huo unawezekana kwa sababu Mungu anatupenda na sisi tunamuamini yeye na Mwana wake. Yesu alisema hivi: ‘Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba alimutoa Mwana wake muzaliwa​-pekee, ili kila mutu anayemuamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.’ (Yoh. 3:16) Kuna mifano mingi ya watu waliokuwa na urafiki wa karibu na Yehova. Tuzungumuzie wawili kati yao.

“ABRAHAMU RAFIKI YANGU”

3, 4. Kuna tofauti gani kati ya Abrahamu na wazao wake?

3 Yehova alimuita muzee wa zamani na babu ya Waisraeli “Abrahamu rafiki yangu.” (Isa. 41:8) Andiko la Mambo ya Nyakati 20:7 linamuita pia Abrahamu kuwa rafiki ya Mungu. Ni nini iliyomusaidia mwanaume huyo mwaminifu aendelee kuwa rafiki ya Muumbaji wake? Ni imani yake.​—Mwa. 15:6; soma Yakobo 2:21-23.

4 Mwanzoni, Yehova alikuwa Baba na Rafiki ya wazao wa Abrahamu ambao walifanyiza taifa la Israeli. Lakini, baadaye walipoteza urafiki wao na Mungu. Sababu gani? Kwa sababu hawakuendelea kuonyesha imani katika ahadi za Yehova.

5, 6. (a) Namna gani ulianza kufanya urafiki pamoja na Yehova? (b) Tunapaswa kujiuliza nini?

5 Unapoendelea kujifunza mengi juu ya Yehova, imani yako itakuwa nguvu zaidi, na utamupenda zaidi. Fikiria wakati ulivumbua kwamba Mungu ni mutu halisi ao si mutu wa kuwazia​-wazia tu, lakini yeye ni mutu anayeweza kuwa rafiki yako. Ulijifunza pia kwamba sisi wote tumezaliwa katika zambi kwa sababu ya kutokutii kwa Adamu. Ulifikia kuelewa kwamba wanadamu wote walikuwa wametenganishwa na Mungu. (Kol. 1:21) Kisha ulitambua kwamba Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo iko karibu na sisi na anatuhangaikia. Tulipojifunza kwamba Yehova alimutoa Mwana wake kuwa zabihu ya ukombozi na tulipoanza kuamini zabihu hiyo, tulianza kufanya urafiki na Mungu.

6 Tunapofikiria mambo tuliyojifunza, tunaweza kujiuliza: ‘Je, ninaendelea kufanya urafiki wangu na Mungu uwe muzuri zaidi? Je, upendo wangu kwa rafiki yangu mupendwa, Yehova unaendelea kukomaa kila siku, na je, nina imani yenye nguvu katika Yehova?’ Mutu mwengine wa zamani aliyekuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni Gideoni. Tuzungumuzie sasa mufano wake na tuone namna tunavyoweza kumuiga.

“YEHOVA NI AMANI”

7-9. (a) Gideoni alijionea jambo gani la kushangaza, na lilimusaidia namna gani? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.) (b) Ni nini inayoweza kutusaidia tuwe na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova?

7 Muamuzi Gideoni alimutumikia Yehova katika kipindi cha musukosuko kisha Waisraeli kuingia katika Inchi ya Ahadi. Sura ya sita ya kitabu cha Waamuzi inaeleza namna malaika wa Yehova alivyomutembelea Gideoni huko Ofra. Wakati huo, taifa jirani la Wamidiani lilikuwa adui wa Israeli na lilikuwa linashambulia inchi yao mara nyingi. Ndiyo sababu, Gideoni hakuwa akipura ao kupigapiga ngano inje katika shamba, lakini mahali pa kukamulia divai, ambako angeweza kuficha haraka ngano yake. Gideoni alishangaa wakati malaika alimutokea na kumuita ‘mwanaume mwenye nguvu,’ kwa hiyo alimuuliza malaika huyo ikiwa Yehova, aliyekuwa amewakomboa Waisraeli katika utumwa wa Misri, atawakomboa tena wakati huo. Akimuwakilisha Yehova, malaika huyo alimuhakikishia Gideoni kwamba Yehova angemusaidia.

8 Gideoni alijiuliza namna gani yeye angeweza ‘kuokoa Israeli kutoka katika mikono ya Midiani.’ Lakini Yehova alimuambia hivi: ‘Kwa sababu nitakuwa pamoja nawe, utapiga Midiani kama mutu mumoja.’ (Amu. 6:11-16) Lakini alikuwa tu angali na mashaka, kwa hiyo aliomba ishara. Ona kwamba katika mazungumuzo hayo, Gideoni alimuona Yehova kuwa mutu halisi.

9 Jambo lililotokea baadaye lilitia nguvu imani ya Gideoni na lilimufanya awe na uhusiano wa karibu zaidi pamoja na Mungu. Gideoni alitayarisha chakula na kumupatia malaika. Kisha malaika alichoma chakula hicho kwa njia ya muujiza kupitia fimbo yake. Gideoni alipoona kwamba malaika huyo alitumwa na Mungu, aliogopa. Kwa hiyo alisema hivi: ‘Ole wangu, Bwana Mwenye Enzi Kubwa Yehova, kwa sababu nimeona malaika wa Yehova uso kwa uso!’ (Amu. 6:17-22) Je, jambo hilo lilimufanya aogope kumukaribia Mungu? Hapana kabisa! Tofauti na hilo, Gideoni alijisikia kuwa na amani pamoja na Mungu. Tunajua hilo kutokana na jina ambalo Gideoni alipatia mazabahu aliyojenga mahali hapo. Aliita mazabahu hayo “Yehova-shalomu,” maana yake “Yehova ni Amani.” (Soma Waamuzi 6:23, 24.) Ikiwa tunafikiria yale ambayo Yehova anatutendea kila siku, tutatambua kwamba yeye ni Rafiki wa kweli kabisa. Kusali kwa ukawaida kunatusaidia tujisikie wenye amani zaidi na kunafanya urafiki wetu pamoja naye uwe nguvu zaidi.

NI NANI ATAKAYEKUWA ‘MUGENI KATIKA HEMA LA YEHOVA’?

10. Kulingana na Zaburi 15:3, 5, Yehova anatuomba nini ili tuwe marafiki wake?

10 Ili Yehova awe Rafiki yetu, tunapaswa kutimiza masharti fulani. Katika Zaburi ya 15, Daudi aliimba kuhusu yale ambayo mutu anapaswa kufanya ili awe ‘mugeni katika hema la Yehova,’ ao ili awe rafiki ya Mungu. (Zab. 15:1) Tuzungumuzie mambo mawili ambayo tunapaswa kufanya: Kuepuka kusingizia wengine na kuwa waaminifu katika mambo yetu yote. Kuhusiana na mambo hayo, Daudi alisema hivi kuhusu yule anayetaka kuwa mugeni katika hema la Yehova: ‘Yeye hakuchongea [ao kusingizia] kwa ulimi wake . . . Hakuchukua rushwa zidi ya mutu asiye na hatia.’​—Zab. 15:3, 5.

11. Sababu gani tunapaswa kuepuka kuwasingizia wengine?

11 Katika Zaburi nyingine, Daudi anatuonya hivi: “Linda ulimi wako na yaliyo mabaya.” (Zab. 34:13) Ikiwa hatutumie mashauri hayo yaliyoongozwa na roho ya Mungu, tunaweza kuharibu uhusiano wetu na Baba yetu wa mbinguni mwenye haki. Zaidi ya hilo, kusingizia wengine ni tabia ya Shetani, adui mukubwa wa Yehova. Neno “Ibilisi” linatoka katika neno la Kigiriki linalomaanisha “musingiziaji.” Ili tuendelee kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova, tunapaswa kuchunguza sana mambo tunayowaambia wengine na yale tunayoongea kuwahusu. Zaidi sana tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu yale tunayoongea kuhusu wazee wa kutaniko.​—Soma Waebrania 13:17; Yuda 8.

12, 13. (a) Sababu gani tunapaswa kuwa waaminifu katika mambo yote? (b) Uaminifu wetu unaweza kuwa na matokeo gani juu ya wengine?

12 Watumishi wa Yehova wanajulikana kuwa watu walio waaminifu katika mambo yote. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Endeleeni kusali kwa ajili yetu, kwa maana sisi tuna uhakika kwamba tuna zamiri nyoofu [nzuri], kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.’ (Ebr. 13:18) Tunataka “kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote,” kwa hiyo tunaepuka kuwaiba ndugu zetu. Kwa mufano, ikiwa wanatufanyia kazi fulani, tunahakikisha kwamba tunawatendea kwa haki na tunawalipa kulingana na mapatano tuliyofanya pamoja nao. Sisi Wakristo, tunawatendea kwa haki wafanyakazi wetu na wengine wote. Na ikiwa bose wetu ni ndugu, tunakuwa waangalifu ili tusijitafutie faida zetu wenyewe kwa kumuomba atutendee kwa njia ya pekee kwa sababu tu sisi wote ni ndugu.

13 Tunasikia mara nyingi namna watu wanavyowasifu Mashahidi wa Yehova! Kwa mufano, musimamizi wa shirika moja kubwa la ujenzi aliona kwamba Mashahidi wa Yehova wanatimiza mambo wanayosema. Alisema hivi: “Kila mara ninyi munaheshimu mapatano.” (Zab. 15:4) Mwenendo kama huo unatusaidia tuendelee kuwa marafiki wa Yehova. Zaidi ya hilo, unamutukuza Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.

SAIDIA WENGINE ILI WAWE MARAFIKI WA YEHOVA

Tuwasaidie wengine ili wawe marafiki wa Yehova (Ona mafungu ya 14, 15)

14, 15. Namna gani tunaweza kuwasaidia wengine ili wawe marafiki wa Yehova tunapohubiri?

14 Watu wengi tunaokutana nao katika mahubiri wanaamini kwamba Mungu iko, lakini hawamuone kuwa Rafiki yao muzuri zaidi. Tunaweza kuwasaidia namna gani? Fikiria maagizo ambayo Yesu aliwatolea wanafunzi wake 70 alipowatuma wawili​-wawili katika mahubiri. Aliwaambia hivi: “Popote pale mutakapoingia katika nyumba kwanza semeni, ‘Nyumba hii na iwe na amani.’ Na ikiwa rafiki wa amani yumo, amani yenu itakaa juu yake. Lakini ikiwa hayumo, itawarudia ninyi.” (Lu. 10:5, 6) Tunaweza kuwasaidia watu wapendezwe na kweli tunapoongea nao kwa njia ya urafiki. Ikiwa tunawatendea kwa upole wale wanaopinga ujumbe wetu, hilo linaweza kupunguza upinzani wao na linaweza kuwafanya watukaribishe vizuri wakati mwingine.

15 Tunapokutana na watu wanaoamini sana mafundisho ya dini za uongo ao wanaofuata desturi zinazopingana na Biblia, tunaendelea kuongea nao kwa upole na kwa njia ya amani. Tunawaalika kwa furaha kwenye mikutano yetu wale ambao hali zenye kuvunja moyo za ulimwengu wa leo zinawafanya wawe na hamu ya kujifunza mengi kuhusu Mungu ambaye tunaabudu. Habari zenye kichwa “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu,” katika gazeti la watu wote la Munara wa Mulinzi, zinazungumuzia mifano mingi ya watu kama hao.

TUTUMIKE PAMOJA NA RAFIKI YETU MUZURI ZAIDI

16. Namna gani tunaweza kuwa marafiki na “wafanyakazi” pamoja na Yehova?

16 Kwa kawaida, watu wanaotumika pamoja wanakuwa marafiki wa karibu zaidi. Wote ambao wamejitoa kwa Yehova wana pendeleo la kuwa marafiki na “wafanyakazi” pamoja naye. (Soma 1 Wakorintho 3:9.) Bila shaka, tunapoendelea kuhubiri, tunajifunza mengi kuhusu sifa nzuri za Baba yetu wa mbinguni. Tunaona namna roho yake inavyotusaidia ili tutimize vizuri kazi yetu ya kuhubiri habari njema.

17. Namna gani chakula cha kiroho tunachopokea kwenye mikusanyiko yetu kinaonyesha kwamba Yehova ni Rafiki yetu?

17 Tunapoendelea kufanya mengi katika kazi ya kuhubiri, tunajisikia kuwa karibu zaidi na Yehova. Kwa mufano, tunaona namna Yehova anavyowanyamazisha wale wanaotafuta kuzuia kazi yetu. Tufikirie yale yaliyotokea miaka michache iliyopita. Je, hatuone waziwazi kwamba Mungu amekuwa akituongoza? Tunashangaa kuona namna tunavyopokea chakula kizuri cha kiroho na kwa ukawaida. Mafundisho tunayopokea kwenye mikusanyiko yetu yanaonyesha kwamba Baba yetu mwenye upendo anaelewa kabisa magumu na mahitaji yetu. Ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya mukusanyiko, familia moja iliandika hivi: “Programu iligusa kabisa mioyo yetu. Tuliona namna Yehova anavyomupenda kila mumoja wetu na anatutakia mema.” Kisha kuhuzuria mukusanyiko mumoja wa pekee huko Irelandi, bibi mumoja na bwana yake wa huko Ujerumani walishukuru namna walivyokaribishwa kwa furaha na namna ndugu walivyowatunza. Walisema tena hivi: “Zaidi ya yote, tunamushukuru Yehova na Mufalme wake Yesu Kristo. Wametualika ili tuwe katika taifa hili lenye umoja wa kweli. Hatuseme tu kwamba tuna umoja lakini tunajionea umoja huo kila siku. Mambo ambayo tumejionea kwenye mukusanyiko wa pekee huko Dublin yataendelea kutukumbusha kwamba tuna pendeleo kubwa la kumutumikia Mungu wetu mukubwa pamoja na ninyi wote.”

MARAFIKI WANAZUNGUMUZA KWA UKAWAIDA

18. Tunaweza kujiuliza nini kuhusu namna tunavyozungumuza na Yehova?

18 Kuzungumuza kwa ukawaida kunasaidia urafiki uwe nguvu. Leo, watu wengi wanazungumuza na marafiki wao kupitia Internete na wanatumiana ujumbe kwa njia ya telefone. Lakini, je sisi pia tunazungumuza na Rafiki yetu muzuri zaidi, Yehova? Kwa kweli, yeye ni ‘musikiaji wa sala.’ (Zab. 65:2) Lakini, je, tunaongea naye kwa ukawaida?

19. Ni nini inayoweza kutusaidia ikiwa tunashindwa kumuelezea Yehova mambo yaliyo katika moyo wetu?

19 Watumishi fulani wa Mungu wanaona kuwa ni vigumu kumuelezea Yehova namna wanavyojisikia kabisa katika moyo wao. Lakini, Yehova anapenda tufanye hivyo tunaposali. (Zab. 119:145; Omb. 3:41) Wakati fulani, tunaweza kushindwa kumuelezea Yehova namna tunavyojisikia kabisa, lakini tusivunjike moyo. Mutume Paulo aliwaandikia hivi Wakristo huko Roma: ‘Kwa maana hatujue yale ambayo tunapaswa kuomba katika sala zetu kulingana na mahitaji yetu. Lakini, roho yenyewe inatuombea kwa maombi yasiyoweza kusemeka; na yeye anayechunguza mioyo anajua ni nini tamaa ya roho; anajua kwamba inaomba kupatana na Mungu kwa ajili ya watakatifu.’ (Rom. 8:26, 27, Bible de Crampon, 1905) Ikiwa tunatafakari kuhusu maneno yaliyoandikwa katika vitabu vya Biblia kama vile Ayubu, Zaburi na Methali, hilo litatusaidia tupate maneno tunayoweza kutumia ili kumuelezea Yehova namna tunavyojisikia.

20, 21. Maneno ya mutume Paulo kwenye Wafilipi 4:6, 7 yanatufariji namna gani?

20 Tunapopambana na matatizo, acheni tutumie shauri hili ambalo mutume Paulo aliwatolea Wafilipi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.’ Kumuelezea waziwazi Rafiki yetu muzuri zaidi namna tunavyojisikia kutatufariji na kutatuliza mioyo yetu, kwa sababu mutume Paulo aliongezea hivi: “Amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.” (Flp. 4:6, 7) Acheni tuendelee kuwa wenye shukrani kwa “amani ya Mungu” inayolinda kabisa mioyo na akili zetu.

Namna gani sala inatusaidia tuendelee kuwa marafiki wa Mungu? (Ona fungu la 21)

21 Kwa kuwa sala inatusaidia tuendelee kuwa marafiki wa Yehova, acheni ‘tusali bila kuacha.’ (1 Thes. 5:17) Acheni habari hii itie nguvu uhusiano wetu na Mungu na azimio letu la kutimiza mambo anayotuomba tufanye. Acheni tuendelee kutafuta wakati ili kutafakari kuhusu baraka ambazo tunafurahia sasa kwa sababu Yehova ni Baba yetu, Mungu wetu, na Rafiki yetu.