Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Endelea Kuonyesha Roho ya Kujitoa

Endelea Kuonyesha Roho ya Kujitoa

‘Mutu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe.’​—MT. 16:24.

1. Namna gani Yesu alituachia mufano muzuri wa kuonyesha roho ya kujitoa?

 ALIPOKUWA duniani, Yesu alituachia mufano muzuri wa kuonyesha roho ya kujitoa. Kuliko kutafuta faida zake mwenyewe na kuwa na maisha mazuri, alifanya mapenzi ya Mungu. (Yoh. 5:30) Kwa kubaki mwaminifu mupaka kifo kwenye muti wa mateso, alionyesha kwamba hakuna jambo lolote ambalo lingemuzuia asionyeshe roho ya kujitoa.​—Flp. 2:8.

2. Namna gani tunaweza kuonyesha roho ya kujitoa, na sababu gani tunapaswa kufanya hivyo?

2 Sisi wafuasi wa Yesu, tunapaswa pia kuonyesha roho ya kujitoa. Inamaanisha nini kuwa na roho ya kujitoa? Kwa kifupi, inamaanisha kuwa tayari kutumia mali na uwezo wetu ili kuwasaidia wengine. Katika maana nyingine, ni kutokuwa na roho ya kujipenda wenyewe. (Soma Mathayo 16:24.) Roho ya kujitoa inatuchochea tutafute kwanza faida za wengine kuliko kufuatia faida zetu wenyewe. (Flp. 2:3, 4) Yesu alifundisha kwamba roho ya kujitoa ni ya maana sana katika ibada yetu. Sababu gani? Kwa sababu upendo wa Kikristo, unaomuchochea mutu kuonyesha roho ya kujitoa, ni alama inayotambulisha wanafunzi wa kweli wa Yesu. (Yoh. 13:34, 35) Zaidi ya hilo, tunafurahia baraka nyingi kwa sababu tuko katika familia ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada wanaoonyesha roho ya kujitoa.

3. Ni nini inayoweza kuharibu roho yetu ya kujitoa?

3 Lakini, kuna adui fulani anayeweza kuharibu roho yetu ya kujitoa bila sisi kujua. Adui huyo ni tamaa yetu ya kujipenda wenyewe. Fikiria namna Adamu na Eva walivyoonyesha roho ya kujipenda wenyewe. Roho hiyo ilimufanya Eva atamani kuwa kama Mungu. Bwana yake alionyesha pia roho ya kujipenda mwenyewe kwa kutaka kumufurahisha bibi yake. (Mwa. 3:5, 6) Kisha kuwachochea Adamu na Eva waache kumuabudu Mungu, Shetani aliendelea kuwachochea watu wawe na roho ya kujipenda wenyewe. Alijaribu hata kufanya hivyo alipomushawishi Yesu. (Mt. 4:1-9) Leo, Shetani amewapotosha watu wengi sana kwa kuwachochea waonyeshe roho ya kujipenda katika njia mbalimbali. Tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu jambo hilo kwa sababu sisi pia tunaweza kuambukizwa na roho ya kujipenda wenyewe yenye kuenea sana.​—Efe. 2:2.

4. (a) Je, tunaweza kuondoa kwa sasa tamaa ya kuwa na roho ya kujipenda wenyewe katika moyo wetu? Eleza. (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

4 Roho ya kujipenda mwenyewe inaweza kulinganishwa na kutu inayokua kwenye chuma. Kama chuma kinapatwa na maji ao baridi, kinaweza kuwa na kutu. Ikiwa hatufanye jambo lolote ili kuzuia kutu hiyo, inaweza kuendelea mupaka kuharibu chuma chote ao kukifanya kivunjike. Vivyo hivyo, hata ikiwa hatuwezi kuondoa kwa sasa uzaifu mbalimbali na tamaa ya kuwa na roho ya kujipenda wenyewe katika moyo wetu, tunapaswa kutambua hatari za kuwa na tamaa hiyo na kuendelea kuipiganisha. (1 Kor. 9:26, 27) Namna gani tunaweza kutambua kwamba tumeanza kuonyesha roho ya kujipenda wenyewe? Na namna gani tunaweza kuonyesha vizuri zaidi roho ya kujitoa?

TUMIA BIBLIA ILI KUJICHUNGUZA

5. (a) Sababu gani Biblia inalinganishwa na kioo? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.) (b) Tunapochunguza ikiwa tuna roho ya kujipenda wenyewe, tunapaswa kuepuka nini?

5 Kama vile tunavyotumia kioo ili kuangalia sura yetu, tunaweza pia kutumia Biblia ili kuchunguza moyo wetu na kuondoa uzaifu fulani ambao tunaweza kutambua. (Soma Yakobo 1:22-25.) Hata hivyo, kioo kinaweza kutusaidia tuone vizuri sura yetu ikiwa tu tunakitumia vizuri. Kwa mufano, ikiwa tunatazama haraka-haraka katika kioo, tunaweza kushindwa kuona kasoro kidogo lakini ambayo hatupaswe kuzarau. Ao ikiwa mutu hakamate kioo vizuri, kuliko kuona sura yake mwenyewe, anaweza kuona sura ya mutu mwingine. Vivyo hivyo, tunapotumia Biblia ili kuchunguza ikiwa tuna roho ya kujipenda wenyewe, hatupaswe kuisoma kijuu-juu ao kuisoma ili kuona makosa ya wengine.

6. Namna gani ‘tunadumu’ katika sheria kamilifu?

6 Kwa mufano, tunaweza kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida, na hata kila siku, lakini bila kutambua kwamba tamaa ya kujipenda wenyewe imeanza kukomaa katika moyo wetu. Hilo linawezekana namna gani? Ona kwamba Yakobo alipozungumuzia mutu anayetumia kioo, hakusema kwamba mutu huyo hakujiangalia vizuri katika kioo. Yakobo aliandika kwamba mutu huyo ‘anajitazama.’ Katika andiko hilo, Yakobo alitumia neno la Kigiriki linalokazia uangalifu ao kuchunguza kwa uangalifu. Ikiwa ni hivyo, tatizo lilikuwa nini? Yakobo aliongezea hivi: ‘Anaenda zake na kusahau mara moja yeye ni mutu wa namna gani.’ Bila shaka, alienda zake bila kuondoa uchafu ambao aliona. Tofauti na mutu huyo, mutu anayepata matokeo mazuri ‘anachunguza ndani ya sheria kamilifu ya uhuru’ na ‘kudumu katika hiyo.’ Kuliko kuzarau sheria kamilifu ya Neno la Mungu, yeye anaendelea kufuata mafundisho ya sheria hiyo. Yesu alizungumuzia jambo kama hilo aliposema hivi: ‘Mukikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu.’​—Yoh. 8:31.

7. Namna gani tunaweza kutumia Biblia ili kuchunguza tamaa yetu ya kujipenda wenyewe?

7 Kwa hiyo, ili tupiganishe vizuri tamaa ya kujipenda mwenyewe, tunapaswa kwanza kusoma Neno la Mungu kwa uangalifu. Kufanya hivyo kunaweza kukusaidia ujue ni wapi unahitaji kufanya mabadiliko. Lakini hilo halitoshe. Tafuta kujua mengi zaidi kwa kufanya utafiti. Ukisha kuelewa vizuri habari fulani ya Biblia, ona namna habari hiyo inavyokuhusu kwa kujiuliza maulizo kama haya: ‘Ningetenda namna gani katika hali hii? Je, kwa kweli ningetenda kwa hekima?’ Lakini, kisha kutafakari kuhusu habari ambayo umesoma, jambo la maana sana ni kujikaza kutenda kulingana nayo. (Mt. 7:24, 25) Tuzungumuzie sasa namna gani tunaweza kutumia habari kuhusu Mufalme Sauli na mutume Petro ili kutusaidia tuendelee kuonyesha roho ya kujitoa.

MUFANO WA MUFALME SAULI UNATUTOLEA ONYO GANI?

8. Sauli alikuwa na sifa gani alipoanza kutawala, na namna gani alionyesha sifa hizo?

8 Mufano wa mufalme Sauli wa Israeli unatuonyesha namna roho ya kujipenda wenyewe inavyoweza kuharibu roho yetu ya kujitoa. Sauli alipoanza kutawala, alikuwa mwenye kiasi na munyenyekevu. (1 Sam. 9:21) Alijizuia kuwaazibu wale waliosema vibaya kuhusu utawala wake, hata ikiwa angefikiri kwamba alikuwa na haki ya kutetea mamlaka ambayo Mungu alimupatia. (1 Sam. 10:27) Mufalme Sauli alikubali uongozi wa roho ya Mungu kwa kuwasaidia Waisraeli washinde vita juu ya Waamoni. Na kuliko kujitafutia sifa, alionyesha kwa unyenyekevu kwamba Yehova ndiye aliyewatolea Waisraeli ushindi.​—1 Sam. 11:6, 11-13.

9. Namna gani Sauli alianza kuonyesha roho ya kujipenda mwenyewe?

9 Kisha, Sauli aliacha roho ya kujipenda mwenyewe na kiburi vikomae katika moyo wake, kama vile kutu yenye kuharibu. Alipowashinda Waamaleki katika vita, alitia faida yake mwenyewe pa nafasi ya kwanza kuliko kumutii Yehova. Kwa sababu ya tamaa, Sauli alihurumia mufalme, wanyama wanono na vitu vizuri kuliko kuharibu kila kitu kama vile Mungu alivyomuagiza. Na alijijengea kwa kiburi munara wa ukumbusho. (1 Sam. 15:3, 9, 12) Nabii Samweli alipomuambia kwamba Yehova hakufurahia jambo hilo, Sauli alianza kujitetea kwa kuonyesha kwamba alikuwa ametii maagizo ya Mungu kwa kiasi fulani na alianza kuwatupia wengine kosa lake. (1 Sam. 15:16-21) Zaidi ya hilo, kwa sababu ya kiburi, alitaka kulinda heshima yake mbele ya watu kuliko kumupendeza Mungu. (1 Sam. 15:30) Namna gani tunaweza kutumia mufano wa Sauli kama kioo ili kuona namna tunaweza kuendelea kuonyesha roho ya kujitoa?

10, 11. (a) Mambo yaliyomupata Sauli yanatufundisha nini kuhusu kuendelea kuonyesha roho ya kujitoa? (b) Namna gani tunaweza kuepuka mwenendo mubaya wa Sauli?

10 Kwanza, mambo yaliyomupata Sauli yanaonyesha kwamba hatupaswe kujiaminia sana kwa kufikiri kwamba ikiwa tulikuwa na roho ya kujitoa hapo zamani, tutaendelea tu kuionyesha. (1 Tim. 4:10) Tusisahau kwamba Sauli alitenda kwa hekima na alikubaliwa na Mungu kwa kipindi fulani, lakini baadaye alishindwa kuondoa tamaa ya kujipenda mwenyewe ambayo ilianza kukomaa katika moyo wake. Mwishowe, Yehova alimukataa kwa sababu hakuendelea kuwa mutiifu.

11 Pili, tunapaswa kuepuka kuona tu mambo mazuri ambayo tunafanya, na kusahau uzaifu fulani tulio nao. Kuona tu mambo mazuri tunayofanya ni kama vile kutumia kioo ili kuona tu mavazi yetu mapya na kusahau kwamba kuna uchafu fulani kwenye sura yetu. Hata ikiwa hatutafikia kuwa na kiburi kama Sauli, tunapaswa kabisa kujikaza ili kuepuka muelekeo wowote unaoweza kutufanya tuige mwenendo huo mubaya. Ikiwa tunashauriwa, tuepuke kujitetea​-tetea, kupunguza uzito wa makosa yetu, ao kuwatupia wengine makosa yetu. Kuliko kutenda kama Sauli, ni vizuri zaidi tuwe tayari kukubali mashauri.​—Soma Zaburi 141:5.

12. Namna gani roho ya kujitoa inaweza kutusaidia ikiwa tunatenda zambi nzito?

12 Hata hivyo, namna gani ikiwa tunatenda zambi nzito? Sauli alitaka kulinda heshima yake, na hilo lilimufanya asifaidike na mashauri aliyotolewa. Lakini, roho ya kujitoa inaweza kutusaidia tusisikie haya ya kutafuta musaada. (Met. 28:13; Yak. 5:14-16) Kwa mufano, ndugu mumoja alianza kutazama ponografia alipokuwa na miaka 12, na aliendelea kufanya hivyo kwa siri kwa zaidi ya miaka kumi. Anaeleza hivi: “Nilishindwa kumuambia bibi yangu na kuwaambia wazee kwamba nilikuwa na tabia hiyo. Sasa nimewaambia, na kwa hiyo ninasikia kuwa muzigo muzito umeondolewa kwenye mabega yangu. Marafiki wangu walihuzunika sana wakati nilipoteza pendeleo langu la kuwa mutumishi wa huduma, ni kama vile nilikuwa nimewavunja moyo. Hata hivyo, ninajua kwamba Yehova anapendezwa sana na utumishi wangu sasa kuliko wakati nilikuwa nikitazama ponografia, na namna anavyoniona ndilo jambo la maana sana.”

PETRO ALISHINDA ROHO YA KUJIPENDA MWENYEWE

13, 14. Namna gani Petro alionyesha tamaa ya kujipenda mwenyewe?

13 Mutume Petro alionyesha roho ya kujitoa alipokuwa akizoezwa na Yesu. (Lu. 5:3-11) Hata hivyo, alipaswa kupiganisha tamaa ya kujipenda mwenyewe. Kwa mufano, alikasirika wakati mutume Yakobo na Yohana waliomba kukaa karibu na Yesu katika Ufalme wa Mungu. Pengine Petro alifikiri kwamba yeye ndiye alistahili kukaa karibu naye kwa sababu Yesu alikuwa amekwisha kusema kwamba Petro angetimiza daraka fulani la pekee. (Mt. 16:18, 19) Kwa vyovyote, Yesu alionya Yakobo na Yohana, vilevile Petro na mitume wengine wasitafute faida yao wenyewe kwa “kupiga ubwana” juu ya ndugu zao.​—Mk. 10:35-45.

14 Hata kisha Yesu kujaribu kurekebisha maoni ya Petro, mutume huyo aliendelea kuonyesha muelekeo wa kujipenda mwenyewe. Yesu alipowaambia mitume kwamba wangemuacha kwa muda fulani, Petro alijiinua mbele ya wengine kwa kudai kwamba yeye pekee ndiye angebaki mwaminifu. (Mt. 26:31-33) Hata hivyo, hakutenda kulingana na maneno yake ya kujitumainia, kwa sababu usiku huohuo alishindwa kuonyesha roho ya kujitoa. Ili kutafuta kujilinda, Petro alimukana Yesu mara tatu.​—Mt. 26:69-75.

15. Ijapokuwa uzaifu na makosa yake, sababu gani Petro ni mufano muzuri kwetu?

15 Ijapokuwa uzaifu na makosa yake, Petro ni mufano muzuri kwetu. Kwa kuwa alijikaza na kutegemea musaada wa roho takatifu ya Mungu, Petro alishinda tamaa yake mbaya ya kujipenda mwenyewe na alionyesha roho ya kujizuia na upendo wa kujitoa. (Gal. 5:22, 23) Alivumilia majaribu yanayoweza kuonwa kuwa makali yanapolinganishwa na yale aliyoshindwa kupambana nayo hapo mbele. Alionyesha unyenyekevu wakati mutume Paulo alimukaripia mbele ya watu. (Gal. 2:11-14) Kisha kukaripiwa, Petro hakuweka kinyongo na hakufikiri kwamba karipio la Paulo lilimupunguzia heshima. Petro aliendelea kumupenda Paulo. (2 Pet. 3:15) Mufano wa Petro unaweza kutusaidia tuonyeshe roho ya kujitoa.

Petro aliitikia namna gani alipokaripiwa? Je, sisi pia tunaitikia hivyo? (Ona fungu la 15)

16. Namna gani tunaweza kuonyesha roho ya kujitoa tunapopambana na matatizo?

16 Fikiria namna unavyotenda unapopambana na matatizo. Petro na mitume wengine walipofungwa na kisha kupigwa fimbo kwa sababu ya kuhubiri, walifurahi sana “kwa sababu walikuwa wamehesabiwa kuwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake [Yesu].” (Mdo. 5:41) Wewe pia unapopatwa na upinzani, hilo linaweza kukutolea nafasi ya kumuiga Petro na kufuata hatua za Yesu kwa kuonyesha roho ya kujitoa. (Soma 1 Petro 2:20, 21.) Kuwa na maoni hayo kunaweza kukusaidia ikiwa wazee wanakutolea mashauri ao karipio. Kuliko kukasirika, iga mufano wa Petro.​—Mhu. 7:9.

17, 18. (a) Tunaweza kujiuliza nini kuhusu miradi yetu ya kiroho? (b) Tunaweza kufanya nini ikiwa muelekeo wa kujipenda wenyewe umeanza kukomaa katika moyo wetu?

17 Mufano wa Petro unaweza pia kukusaidia kuhusiana na miradi ya kiroho. Fuatia miradi hiyo katika njia inayoonyesha kwamba una roho ya kujitoa. Kwa kweli, unapaswa kuwa mwangalifu ili usifanye hivyo ili kuwinda madaraka ao kujitafutia sifa. Jiulize hivi: ‘Je, ninaongeza utumishi wangu kwa Yehova ao ninatafuta kuufanya uwe muzuri zaidi ili nijulikane ao ninatafuta tu kuwa na madaraka, kama vile ilivyokuwa kuhusu Yakobo na Yohana walipomutolea Yesu ombi lao?’

18 Ikiwa unatambua kwamba umeanza kukomalisha muelekeo wa kujipenda mwenyewe katika moyo wako, umuombe Yehova arekebishe akili na mawazo yako; kisha ujikaze sana kutafuta utukufu wa Mungu wala si utukufu wako mwenyewe. (Zab. 86:11) Unaweza kufuatia miradi ambayo haitakufanya usifiwe​-sifiwe sana. Kwa mufano, unaweza kujikaza kukomalisha sifa fulani za tunda la roho ambazo unashindwa kuonyesha. Ao ikiwa unatayarisha vizuri migawo unayopewa kwenye mikutano lakini haushiriki kwa bidii katika usafi wa Jumba la Ufalme, unaweza kujiwekea muradi wa kutenda kulingana na shauri linalopatikana kwenye Waroma 12:16.​—Soma.

19. Tunaweza kufanya nini ili tusivunjwe moyo na yale tunayoona katika kioo cha Neno la Mungu?

19 Tunapojiangalia katika kioo cha Neno la Mungu na kutambua kwamba tuna uzaifu fulani, ao hata tamaa ya kujipenda wenyewe, hilo linaweza kutuvunja moyo. Ikiwa unavunjika moyo, fikiria mutu anayepata matokeo mazuri ambaye Yakobo alizungumuzia. Yakobo hakuonyesha kwamba mutu huyo alifanya mabadiliko mara moja ao ikiwa aliondoa kila uchafu ambao aliona; lakini, Yakobo alisema kwamba ‘alidumu katika sheria kamilifu.’ (Yak. 1:25) Mutu huyo hakusahau yale aliyoona katika kioo na aliendelea kufanya mabadiliko. Kwa hiyo, usivunjike moyo kuhusu hali yako na uwe na maoni yenye usawaziko kuhusu uzaifu wako. (Soma Mhubiri 7:20.) Endelea kuchunguza sheria kamilifu, na uendelee kuonyesha roho ya kujitoa. Yehova iko tayari kukusaidia, kama vile amewasaidia ndugu na dada zako wengi wakubaliwe na kubarikiwa naye hata ikiwa wao ni watu wasio wa kamilifu.