Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kuwatendea Wengine Katika Mahubiri

Namna ya Kuwatendea Wengine Katika Mahubiri

‘Mambo yote munayotaka watu wawatendee ninyi, lazima muwatendee wao pia vivyo hivyo.’MT. 7:12.

1. Kuwatendea watu vizuri katika mahubiri kunaweza kuwa na matokeo gani? Toa mufano. (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

MIAKA fulani iliyopita ndugu mumoja na bibi yake wa huko Fiji, walikuwa katika kampanye ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Mvua ilianza kunyesha walipokuwa wakizungumuza na mama mumoja inje ya nyumba yake. Ndugu alimupatia mama huyo mwamvuli ili ajifunike. Yeye na bibi yake walijifunika mwamvuli mwingine. Ndugu huyo na bibi yake walifurahi sana walipomuona mama huyo usiku kwenye Ukumbusho. Mama huyo alisema kwamba hakumbuke tena mambo yote ambayo waliongea na Mashahidi hao wakati walimutembelea. Lakini alipendezwa sana na namna ndugu huyo na bibi yake walivyomutendea na hilo lilimuchochea afike kwenye Ukumbusho. Ni jambo gani ambalo lilimuchochea ndugu huyo na bibi yake watende hivyo? Walitumia ile ambayo watu wengi wanaita Kanuni Iliyo Nzuri Sana.

2. Kanuni Iliyo Nzuri Sana ni nini, na namna gani tunaweza kuitumia?

2 Kanuni Iliyo Nzuri Sana ni nini? Ni shauri ambalo Yesu alitoa aliposema hivi: ‘Mambo yote munayotaka watu wawatendee ninyi, lazima muwatendee wao pia vivyo hivyo.’ (Mt. 7:12) Tunaweza kutumia kanuni hiyo kwa kufanya mambo mawili. Kwanza, tunapashwa kujiuliza hivi: ‘Ikiwa ningekuwa katika hali hii ningependa wanitendee namna gani?’ Kisha, tunaweza sasa kumutendea mwengine hivyo na kumusaidia kulingana na uwezo wetu.—1 Kor. 10:24.

3, 4. (a) Eleza sababu gani hatupashwe kutumia Kanuni Iliyo Nzuri Sana pamoja na Mashahidi wenzetu tu. (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

 3 Kila mara tunatumia Kanuni Iliyo Nzuri Sana katika uhusiano wetu pamoja na ndugu na dada zetu. Lakini Yesu hakusema kwamba tunapashwa kutumia kanuni hiyo pamoja na Mashahidi wenzetu tu. Yesu alitaja Kanuni Iliyo Nzuri Sana alipokuwa akizungumuza kuhusu namna tunaweza kuwatendea watu wote kwa ujumla na hata wale ambao ni maadui wetu. (Soma Luka 6:27, 28, 31, 35.) Ikiwa tunapashwa kutumia Kanuni Iliyo Nzuri Sana kuwaelekea maadui wetu, tunaweza kuitumia hata zaidi tunapowahubiria watu wengine. Wengi wanaweza kuwa na ‘muelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele’!—Mdo. 13:48.

4 Tutazungumuzia sasa maulizo ine tunayopashwa kufikiria tunapokuwa katika mahubiri: Nitazungumuza na watu wa namna gani? Nitawapata wapi? Ni wakati gani ulio muzuri wa kuwapata watu? Nitazungumuza nao namna gani? Kama vile tutaona, maulizo hayo yanaweza kutusaidia kuelewa namna wale ambao tunahubiria wanajisikia na kupatanisha mazungumuzo yetu kulingana na hali yao.—1 Kor. 9:19-23.

NITAZUNGUMUZA NA WATU WA NAMNA GANI?

5. Ni maulizo gani ambayo tunaweza kujiuliza?

5 Katika kazi yetu ya kuhubiri, kila mara tunazungumuza na watu tofauti-tofauti. Kila mutu alikomaa tofauti na mwengine na ana magumu yake. (2 Nya. 6:29) Unapojaribu kumuhubiria mutu fulani, ujiulize hivi: ‘Ikiwa ni yeye angezungumuza na mimi ningependa anitendee namna gani? Ningefurahi ikiwa angeniwazia vibaya? Ao ningefurahi ikiwa angenitendea kwa heshima?’ Kufikiria maulizo hayo, kunaweza kutusaidia tumutendee kila musikilizaji wetu kwa heshima.

6, 7. Tunapashwa kufanya nini ikiwa mutu ambaye tunakutana katika mahubiri anaonekana kuwa mukali?

6 Hakuna mutu anayependa aonwe kuwa mutu asiyefaa kitu. Kwa mufano: Sisi Wakristo tunajikaza kutumia shauri la Biblia linalosema kwamba ‘maneno yetu yawe yenye neema siku zote.’ (Kol. 4:6) Lakini, kwa kuwa hatukamilike, nyakati fulani tunasema mambo ambayo tunahuzunikia baadaye. (Yak. 3:2) Pengine kwa sababu haukupitisha muchana vizuri, unaweza kumujibia vibaya mutu fulani, lakini haungependa mutu huyo akuone kuwa “mukosa-adabu” ao mutu “anayesema bila kufikiri.” Kwa kawaida tunapenda wengine watuelewe. Kwa hiyo, sisi pia tunapashwa kuwaelewa.

7 Ikiwa mutu fulani ambaye tunahubiria anaonekana kuwa mukali, je, haingekuwa vizuri kuelewa kwamba ana sababu fulani zinazomufanya awe hivyo? Pengine ana magumu kwenye masomo ao kwenye kazi. Ao pengine anapambana na ugonjwa mubaya sana. Katika hali nyingi, wasikilizaji ambao hapo mbele walitujibia kwa ukali, wamekubali habari njema watumishi wa Yehova walipowatendea kwa upole na heshima.—Met. 15:1; 1 Pet. 3:15.

8. Sababu gani tunapashwa kuwahubiria “watu wa namna zote” habari njema ya Ufalme?

8 Katika mahubiri, tunazungumuza na watu wa aina zote. Kwa mufano, miaka michache iliyopita, habari zaidi ya 60 zenye kichwa: “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” zimezungumuziwa katika gazeti la watu wote la Munara wa Mulinzi. Watu wanaozungumuziwa katika habari hizo, walikuwa zamani wa mwizi, walevi, wanyanganyi, watu wenye kutumia sana dawa za kulewesha. Wengine walikuwa katika politike, wakubwa wa dini, ao waliopenda sana kazi yao. Wengine walikuwa na mwenendo muchafu. Lakini, walisikiliza habari njema, walikubali kujifunza Biblia, walifanya mabadiliko katika maisha yao, na wakaanza kumuabudu Yehova. Kwa hiyo,  hatupashwe kufikiri kwamba watu fulani hawastahili kuhubiriwa habari njema ya Ufalme. (Soma 1 Wakorintho 6:9-11.) Lakini, tunajua kwamba “watu wa namna zote” wanaweza kukubali habari njema.—1 Kor. 9:22.

NITAPATA WATU WAPI?

9. Sababu gani tunapashwa kuheshimia nyumba za wengine?

9 Mara nyingi tunawakuta watu wapi tunapokuwa katika mahubiri? Tunawakuta nyumbani kwao. (Mt. 10:11-13) Kwa kawaida, tunafurahi wengine wanapoheshimia nyumba yetu na vitu vyetu. Zaidi ya hilo, nyumba yetu ni ya lazima kwetu. Tunataka iwe mahali penye kuheshimiwa na penye usalama. Tunapashwa kufanya hivyohivyo kuelekea majirani wetu. Kwa hiyo katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, ni vizuri tufikirie namna ya kujiendesha tunapokuwa katika nyumba za wasikilizaji wetu.—Mdo 5:42.

10. Namna gani tunaweza kuepuka kuwauzi wengine tunapohubiri?

10 Kwa kuwa leo dunia imejaa watu wabaya sana, wasikilizaji wengi wanashakia ao kuwazia vibaya watu ambao hawawajue. (2 Tim. 3:1-5) Tunapashwa kuepuka jambo lolote ambalo litawafanya watu watuwazie vibaya. Kwa mufano, tuseme tunakaribia nyumba fulani na tunapiga hodi kwenye mulango. Ikiwa hakuna mutu ambaye anatujibia, tunaweza kuangukia katika mutego wa kuchungulia ndani ya dirisha ao kutembea-tembea katika kiwanja ili kumutafuta mwenye nyumba. Katika eneo lenu, je, kufanya hivyo kunaweza kumuuzi mwenye nyumba? Majirani wake watawaza nini? Bila shaka, tunapashwa kuwa waangalifu tunapokuwa katika kazi ya kuhubiri. (Mdo 10:42) Tunatamani kabisa kuwaelezea wengine habari njema, na tunachochewa na nia nzuri. (Rom. 1:14, 15) Hata hivyo, tunajikaza kuwa waangalifu ili tusifanye jambo lolote ambalo linaweza kuwauzi watu tunaohubiria katika eneo letu. Mutume Paulo aliandika hivi: “Sisi hatutoi sababu yoyote ya kukwaza kwa njia yoyote, ili huduma yetu isilaumiwe.” (2 Kor. 6:3) Tunapoheshimia nyumba na vitu vya wale tunaohubiria katika eneo letu, mwenendo wetu unaweza kuwachochea watu waikubali kweli.—Soma 1 Petro 2:12.

Tuheshimie musikilizaji wetu na vitu vyake(Ona fungu la10)

NITAWAPATA WAKATI GANI?

11. Sababu gani tunafurahi wengine wanapoheshimia wakati yetu?

11 Wakristo wengi kati yetu wana kazi nyingi za kufanya. Ili kutimiza madaraka yetu, tunapanga mambo ya kutia pa nafasi ya kwanza na kufanya programu nzuri. (Efe. 5:16; Flp. 1:10) Ikiwa jambo ao mutu fulani anavuruga programu yetu, tunaweza kukasirika. Lakini, tunafurahi wengine wanapoheshimia wakati yetu na wanapofikiria ikiwa mazungumuzo yatachukua muda gani. Tukiwa na Kanuni Iliyo Nzuri Sana katika akili zetu, namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunawaheshimia wale tunaohubiria?

12. Namna gani tunaweza kujua wakati unaofaa wa kuwapata watu katika eneo letu?

12 Tunapashwa kujikaza kujua wakati unaofaa wa kuzungumuza na wasikilizaji. Katika eneo letu, watu wanazoea kupatikana wakati gani? Ni wakati gani wanaweza kutusikiliza vizuri? Tunafanya vizuri ikiwa tunabadilisha programu yetu kulingana na eneo letu. Katika sehemu fulani za dunia, tunapata matokeo mazuri katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba tunapowatembelea watu mangaribi. Ikiwa ni hivyo katika eneo lako, je, unaweza kupanga kuhubiri nyumba kwa nyumba mangaribi? (Soma 1 Wakorintho 10:24.) Tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atabariki roho yetu ya kujitoa ili kuhubiri wakati unaowafaa wakaaji wa eneo letu.

13. Namna gani tunaweza kumuonyesha musikilizaji heshima?

13 Ni katika njia gani nyingine tunaweza kuonyesha heshima ? Tunapokutana mutu mwenye kupendezwa, tunapashwa kumuhubiria, lakini tusizungumuze naye kwa muda murefu sana. Pengine musikilizaji alipanga kutumia wakati huo ili kufanya mambo mengine ambayo anaona kuwa ya lazima. Musikilizaji akisema kwamba hana wakati, tunaweza kumuambia kwamba tutasema kwa kifupi na tunapashwa kutimiza maneno yetu. (Mt. 5:37) Tunapomaliza mazungumuzo, tunaweza kumuuliza musikilizaji ni wakati gani anapenda tumutembelee tena. Wahubiri fulani wameona kwamba ni vizuri kusema hivi: “Nitafurahi kukutembelea tena. Je, ninaweza kukuita kwanza kwenye telefone ao kukutumia ujumbe mbele nifike?” Tunapopatanisha programu yetu na ya watu wa eneo letu, tunafuata mufano wa mutume Paulo, ambaye ‘hakutafuta faida yake mwenyewe bali ile ya wengi ili wapate kuokolewa.’—1 Kor. 10:33.

NITAZUNGUMUZA NA WATU NAMNA GANI?

14-16. (a) Kwa nini ni vizuri kumuelezea waziwazi musikilizaji sababu gani tunamutembelea? Toa mufano. (b) Ni ufundi gani ambao mwangalizi mumoja ameona kuwa wenye matokeo?

14 Tuseme kwamba mutu fulani ambaye hautambue sauti yake anakuita kwenye telefone. Haumujue, lakini anakuuliza ni chakula gani ambacho unafurahia. Utajiuliza mutu huyo ni nani na anataka kabisa nini. Pengine kwa sababu ya adabu, unaweza kuongea naye kidogo, kisha unakata mazungumuzo. Kwa upande mwingine, wazia kwamba mutu anayetuita anajieleza kwanza, kisha anasema kwamba yeye ana elimu ya mambo ya chakula, na anatuambia kwa upole  kwamba ana habari fulani ambayo inaweza kutusaidia. Pengine tunaweza kuwa tayari kumusikiliza. Zaidi ya hilo, tunafurahi watu wanapozungumuza na sisi waziwazi na kwa heshima. Namna gani tunaweza kuonyesha heshima kama hiyo kwa wale tunaohubiria?

15 Katika maeneo mengi, tunahitaji kumuelezea musikilizaji wetu sababu gani tunamutembelea. Ni kweli kwamba tunajua mambo mengi kuliko musikilizaji. Lakini, wazia kwamba tunafika kwa mutu na mbele hata ya kumuambia sisi ni nani na tunakuja kufanya nini, mara moja tunamuuliza hivi: “Ikiwa ungekuwa na uwezo wa kumaliza matatizo yote katika dunia, ungemaliza tatizo gani kwanza?” Tunajua kwamba kusudi la ulizo hilo ni kutaka kujua mawazo ya mutu na kisha kumuonyesha yale ambayo Biblia inasema. Lakini musikilizaji wetu, anaweza kujiuliza katika moyo wake hivi: ‘Mutu huyu anatoka wapi, na sababu gani ananiuliza ulizo hili? Sababu gani ananisumbua hivi?’ Kwa hiyo, tunapashwa kujaribu kumufanya musikilizaji wetu asiwe na mashaka juu yetu. (Flp. 2:3, 4) Namna gani tunaweza kufanya hivyo?

16 Mwangalizi mumoja mwenye kusafiri ameona ufundi unaofuata kuwa wenye matokeo mazuri. Kisha kumusalimia musikilizaji, anamutolea trakte yenye kichwa; Je, Ungependa Kujua Kweli? na anasema hivi: “Leo, tunawatolea watu trakte hii katika eneo hili. Inazungumuzia maulizo sita ambayo watu wengi wanajiuliza. Yako hii.” Ndugu huyo anasema kwamba watu wengi wanaonekana kuwa wenye kutulia wakati tunawaelezea sababu ya kuwatembelea. Mara nyingi, kisha kufanya hivyo inakuwa rahisi kuanzisha mazungumuzo. Kisha mwangalizi anamuuliza hivi mutu huyo: “Umekwisha kujiuliza ulizo gani kati ya maulizo haya?” Ikiwa musikilizaji anachagua ulizo moja, ndugu anafungua trakte hiyo na anaanza kumuonyesha mawazo ya Biblia kuhusu ulizo hilo. Ao, ndugu anachagua ulizo moja na kuanza kuzungumuza na musikilizaji wake bila kumuuliza-uliza maulizo. Njia hizo mbili ni kati ya njia nyingi tunazotumia ili kuanzisha mazungumuzo. Katika maeneo fulani, tunapashwa kufuata desturi fulani tunaposalimu watu mbele ya kuwaambia sababu gani tunawatembelea. Jambo la maana ni kuanzisha mazungumuzo kulingana na namna watu wa eneo letu wanavyotaka.

ENDELEA KUFUATA KANUNI ILIYO NZURI SANA UNAPOHUBIRI

17. Kama vile tumeona katika habari hii, ni katika njia gani mbalimbali tunaweza kutumia Kanuni Iliyo Nzuri Sana?

17 Kwa hiyo, ni katika njia gani mbalimbali tunaweza kutumia Kanuni Iliyo Nzuri Sana tunapokuwa katika mahubiri? Tunamutendea kila musikilizaji wetu kwa heshima. Tunaheshimia nyumba ya musikilizaji na vitu vyake. Tunajikaza kuenda katika mahubiri wakati wasikilizaji wanapatikana nyumbani na wako tayari kutusikiliza. Na tunaanzisha mazungumuzo kwa njia itakayowafanya wasikilizaji wafurahie kutusikiliza.

18. Tunapata faida gani tunapowatendea watu wa eneo letu namna tungependa watutendee?

18 Tunapata faida nyingi kwa kuwatendea watu wa eneo letu kama vile tungependa watutendee. Kwa kutenda kwa upole na heshima, tunaendelea kuacha nuru yetu iangaze, tunawasaidia watu waone faida ya kutumia kanuni za Maandiko katika maisha, na tunamuletea Baba yetu wa mbinguni utukufu. (Mt. 5:16) Namna yetu ya kuzungumuza inaweza kuwachochea watu wengi wamuabudu Yehova. (1 Tim. 4:16) Hata ikiwa wale tunaohubiria wanakataa ujumbe wa Ufalme, tunafurahi kwa sababu tunafanya yote tunayoweza ili kutimiza kazi yetu ya kuhubiri. (2 Tim. 4:5) Acheni kila mumoja wetu amuige mutume Paulo aliyeandika hivi: “Ninafanya mambo yote kwa ajili ya habari njema, ili niishiriki hiyo pamoja na wengine.” (1 Kor. 9:23) Acheni basi, siku zote tutumie Kanuni Iliyo Nzuri Sana tunapohubiri.