Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Gani Tunapashwa ‘Kumujibia Kila Mutu’?

Namna Gani Tunapashwa ‘Kumujibia Kila Mutu’?

‘Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote, . . . ili mujue jinsi munavyopashwa kumujibia kila mutu.’KOL. 4:6.

1, 2. (a) Toa mufano unaoonyesha faida ya kuuliza maulizo kwa ufundi. (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.) (b) Sababu gani hatupashwe kuogopa kuzungumuzia maulizo magumu?

MIAKA fulani iliyopita, dada mumoja alikuwa akizungumuza na bwana yake ambaye si Shahidi. Zamani, bwana yake alikuwa katika dini moja inayojiita kuwa ya Kikristo. Wakati wa mazungumuzo yao, bwana yake alisema kwamba aliamini fundisho la Utatu. Alipotambua kwamba pengine bwana yake hakujua kabisa maana ya fundisho la Utatu, alimuuliza hivi kwa ufundi: “Unaamini kwamba Mungu ni Mungu, kwamba Yesu ni Mungu, na kwamba roho takatifu ni Mungu; na hakuna wa Mungu watatu lakini wote ni Mungu mumoja?” Kwa kushangaa, bwana yake alisema hivi: “Hapana, siamini hivyo!” Kwa njia hiyo, walianza mazungumuzo yenye kupendeza kuhusu ukweli juu ya Mungu.

2 Mufano huo unaonyesha faida ya kuchagua maulizo vizuri na kuyatumia kwa ufundi. Unaonyesha pia kwamba hatupashwe kuogopa kuzungumuzia maulizo magumu kama vile yale yanayohusu Utatu, moto wa mateso ao kuwapo kwa Muumbaji. Ikiwa tunategemea Yehova na kutumia mazoezi ambayo anatutolea, tunaweza kutoa kila mara majibu yenye kusadikisha, na ambayo yanaweza kugusa mioyo ya wasikilizaji wetu. (Kol. 4:6) Acheni tuzungumuzie sasa yale ambayo wahubiri  wenye ufundi wanafanya wanapozungumuzia maulizo kama hayo. Tutachunguza (1) namna ya kuuliza maulizo yanayomuchochea mutu atoe mawazo yake, (2) namna ya kufikiri na watu juu ya yale ambayo Maandiko yanasema, na (3) namna ya kutumia mifano ili kuwasaidia watu waelewe vizuri habari fulani.

MAULIZO YANAYOWACHOCHEA WASIKILIZAJI WATOE MAWAZO YAO

3, 4. Sababu gani ni jambo la lazima kutumia maulizo ili kujua yale ambayo mutu anaamini? Toa mufano.

3 Maulizo yanaweza kutusaidia tujue mambo ambayo mutu anaamini. Sababu gani hilo ni jambo la lazima? Methali 18:13 inasema hivi: “Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia, huo ni upumbavu na aibu [ao haya] kwake.” Bila shaka, mbele ya kuanza kuzungumuzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu habari fulani, ni vizuri kujua kwanza yale ambayo musikilizaji anaamini. Ikiwa hatufanye hivyo, tunaweza kutumia wakati mwingi ili kupinga ao kukataa fundisho ambalo mutu hakuwa anaamini hata kidogo hapo mbele!—1 Kor. 9:26.

4 Fikiria kwamba unazungumuza na mutu fulani kuhusu moto wa mateso. Watu wote hawaamini kwamba moto wa mateso ni mahali fulani ambapo watu wanateswa katika moto. Wengi wanaamini kwamba moto wa mateso ni hali ya kutengwa na Mungu. Kwa hiyo, tunaweza kusema hivi: “Kwa kuwa watu wana maoni mbalimbali kuhusu moto wa mateso, wewe unawaza moto wa mateso ni nini?” Kisha kusikiliza jibu lake, ndipo tunaweza kujua namna ya kumusaidia aelewe maoni ya Biblia kuhusu fundisho hilo.

5. Namna gani maulizo yanaweza kutusaidia tujue sababu inayomufanya mutu aamini fundisho fulani?

5 Kuuliza maulizo kwa ufundi kunaweza kutusaidia tuelewe sababu inayomufanya mutu aamini fundisho fulani. Kwa mufano, tutafanya nini ikiwa mutu fulani anatuambia kwamba hamuamini Mungu? Inaweza kuwa rahisi kufikiri kwamba mutu huyo amechochewa na mafundisho yanayoenea sana leo kama vile fundisho la mageuzi. (Zab. 10:4) Hata hivyo, watu fulani hawamuamini tena Mungu kwa sababu ya mateso mengi ambayo wamejionea ao wamepata. Wanaweza kuona kwamba haiwezekane Muumbaji mwenye upendo aachilie mateso hayo. Kwa hiyo, ikiwa musikilizaji ana mashaka kwamba kuna Mungu, unaweza kumuuliza hivi: “Umekuwa na mawazo hayo tangu zamani?” Ikiwa anajibu hapana, unaweza kumuuliza ikiwa kuna jambo fulani ambalo limefanya aanze kuwa na mashaka kwamba kuna Mungu. Jibu lake linaweza kutusaidia tujue njia nzuri ya kumusaidia.—Soma Methali 20:5.

6. Tunapashwa kufanya nini kisha kumuuliza mutu ulizo fulani?

6 Kisha kumuuliza mutu ulizo fulani, tunahitaji kabisa kusikiliza jibu lake na kuelewa vizuri mawazo yake. Kwa mufano, mutu anaweza kukuambia kwamba musiba fulani umemufanya awe na mashaka kwamba kuna Muumbaji mwenye upendo. Mbele ya kumuonyesha mambo yanayoshuhudia kwamba kuna Mungu, tunapashwa kwanza kujitia pa nafasi yake na kumuambia kwamba si vibaya kujiuliza sababu gani watu wanateseka. (Hab. 1:2, 3) Uvumilivu na upendo wetu unaweza kumuchochea mutu huyo awe na hamu ya kujua mengi. *

KUFIKIRI NA WATU JUU YA YALE AMBAYO MAANDIKO YANASEMA

Matokeo mazuri katika mahubiri yanategemea nini? (Ona fungu la  7)

7. Matokeo mazuri katika mahubiri yanategemea nini?

7 Acheni tuone sasa namna ya kutumia Maandiko ili kufikiri na watu. Bila shaka, Biblia ndio chombo tunachotumia sana katika mahubiri. Na inaweza kutusaidia tuwe na ‘uwezo kamili, tukiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’ (2 Tim. 3:16, 17) Ili kupata matokeo mazuri katika mahubiri hatuhitaji kusoma Maandiko mengi. Lakini tunaweza kupata matokeo mazuri ikiwa tunafikiri vizuri na watu juu ya Maandiko  tunayosoma na kuyafasiria vizuri. (Soma Matendo 17:2, 3.) Tuzungumuzie hali tatu zinazofuata.

8, 9. (a) Namna gani tunaweza kufikiri na mutu anayeamini kwamba Yesu iko sawa na Mungu? (b) Ni namna gani ingine ya kufikiri na watu ambayo umeona kuwa ina matokeo?

8 Hali ya 1: Katika mahubiri, tunakutana na mutu fulani anayeamini kwamba Yesu iko sawa na Mungu. Ni maandiko gani tunayoweza kutumia ili kufikiri na mutu huyo? Tunaweza kumuambia asome andiko la Yohana 6:38. Katika andiko hilo, Yesu alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni kufanya, si mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.” Kisha kusoma andiko hilo, tunaweza kumuuliza hivi: “Ikiwa Yesu ni Mungu ni nani aliyemutuma kutoka mbinguni ili aje duniani? Yule aliyemutuma hapashwe kuwa mukubwa zaidi kuliko Yesu? Ni kweli kwamba, yule anayemutuma mutu mwengine ni mukubwa kumushinda.”

9 Tunapoendelea na mazungumuzo, tunaweza pia kusoma Wafilipi 2:9; katika andiko hilo, mutume Paulo anaeleza jambo ambalo Mungu alimufanyia Yesu kisha kufa na kufufuliwa. Andiko hilo linasema hivi: ‘Mungu alimupandisha [Yesu] kwenye cheo cha juu zaidi na kumupa kwa fazili jina lililo juu ya kila jina lingine.’ Ili kumusaidia mutu huyo afikiri juu ya andiko hilo, tunaweza kumuuliza hivi: “Ikiwa Yesu alikuwa sawa na Mungu mbele ya kufa, na kisha ufufuo wake Mungu alimupandisha kwenye cheo cha juu zaidi, hauone kwamba hilo lingemufanya Yesu awe mukubwa kuliko Mungu? Unafikiri kuna mutu aliye mukubwa kuliko Mungu?” Ikiwa mutu huyo anaheshimu Neno la Mungu na anapenda kabisa kujua mengi, kufikiri naye kwa njia hiyo kunaweza kumuchochea awe na hamu ya kuchunguza mambo vizuri zaidi.—Mdo. 17:11.

10. (a) Namna gani tunaweza kufikiri na mutu anayeamini fundisho la moto wa mateso? (b) Ni namna gani ingine ya kufikiri na watu ambayo umeona kuwa ina matokeo?

10 Hali ya 2: Musikilizaji anayeshikilia sana mafundisho ya dini na anayeona kuwa ni vigumu kuamini kwamba watu wabaya hawatateswa milele katika moto. Pengine anashikilia imani hiyo kwa sababu anapenda watu wabaya wapate malipizi kwa sababu ya matendo yao mabaya. Namna gani tunaweza kufikiri na mutu aliye na mawazo kama hayo? Kwanza, tunapashwa kumuhakikishia kwamba watu wabaya watapata malipizi. (2 Thes. 1:9) Kisha, tunaweza kumuambia asome andiko la Mwanzo 2:16, 17, linaloonyesha kwamba malipizi ya zambi ni kifo. Tunaweza kumuelezea kwamba kwa sababu ya zambi ya Adamu, wanadamu wote wanazaliwa wakiwa watenda zambi. (Rom. 5:12) Lakini tunaweza kumuambia kwamba Mungu hakusema jambo lolote kuhusu kuwapa watu malipizi katika moto wa mateso. Kisha tunaweza kumuuliza hivi: “Ikiwa Adamu na Eva wangeenda kuteseka katika moto wa mateso kwa sababu ya kosa fulani, je, Mungu hangewaambia jambo hilo mbele ya wakati?” Tunaweza sasa kusoma andiko la Mwanzo 3:19, linaloonyesha hukumu ambayo Mungu alitangaza kisha Adamu na Eva kufanya zambi . Mungu hakusema jambo lolote kuhusu moto wa mateso. Lakini, Mungu alimwambia Adamu kwamba angerudi katika mavumbi. Tunaweza kumuuliza hivi: “Lingekuwa jambo la haki Mungu amuambie Adamu kwamba angerudi katika udongo akijua kwamba Adamu ataenda kabisa katika moto wa mateso?” Ikiwa mutu huyo anapenda kuelewa vizuri, ulizo hilo linaweza kumufanya afikiri sana kuhusu fundisho hilo.

11. (a) Namna gani tunaweza kufikiri na mutu anayeamini kwamba watu wazuri wataenda mbinguni? (b) Ni namna gani ingine ya kufikiri na watu ambayo umeona kuwa ina matokeo?

11 Hali ya 3: Katika mahubiri, tunakutana na mutu anayeamini kwamba watu wote wazuri wataenda mbinguni. Imani hiyo inaweza kumufanya mutu aelewe vibaya mafundisho ya Biblia. Kwa mufano, tuseme kwamba tunazungumuzia andiko la Ufunuo 21:4. (Soma.) Pengine mutu huyo anawaza kwamba baraka zinazozungumuziwa katika andiko hilo zinahusu maisha ya mbinguni. Namna gani tunaweza kufikiri na mutu huyo? Kuliko kumusomea maandiko mengine, tunaweza kukazia wazo moja katika andiko hilo. Andiko hilo linasema kwamba “kifo hakitakuwapo tena.” Tunaweza kufikiri na mutu huyo hivi: ukisema kwamba kitu fulani hakitakuwa tena mahali fulani, ni kusema kilikuwa mahali hapo zamani, sivyo? Pengine, atasema ndiyo. Kisha tunaweza kumuelezea kwamba kifo kinapatikana tu hapa duniani, hapana mbinguni. Ndiyo sababu, andiko la Ufunuo 21:4 linazungumuzia baraka za wakati ujao hapa duniani.—Zab. 37:29.

TUMIA MIFANO ILI KUSAIDIA WATU WAELEWE

12. Sababu gani Yesu alitumia mifano?

12 Zaidi ya kutumia maulizo, Yesu alitumia mifano alipokuwa akihubiri. (Soma Mathayo 13:34, 35.) Mifano hiyo ilifunua yale yaliyokuwa katika mioyo ya wasikilizaji wake. (Mt. 13:10-15) Mifano ya Yesu ilifanya watu wafurahie mafundisho yake na kuyakumbuka. Namna gani tunaweza kutumia mifano tunapofundisha?

13. Tunaweza kutumia mufano gani ili kuonyesha kwamba Mungu ni mukubwa kuliko Yesu?

13 Ni vizuri kutumia mifano iliyo rahisi. Kwa mufano, tunapofasiria mutu kwamba Mungu ni mukubwa kuliko Yesu, pengine tunaweza kujaribu njia hii. Tunaweza kumuambia kwamba Mungu na Yesu walitumia maneno fulani ili kuzungumuzia uhusiano ulio kati yao. Mungu alimuita Yesu kuwa Mwana wake, na Yesu alimuita Mungu kuwa Baba yake. (Lu. 3:21, 22; Yoh. 14:28) Kisha tunaweza kumuuliza musikilizaji hivi: “Ikiwa unapenda nielewe kwamba watu wawili wako sawa, unaweza kutumia uhusiano gani wa familia ili kuonyesha jambo hilo?” Mutu huyo anaweza kusema hivi: Ninaweza kusema kwamba wao ni ndugu, dada, ao hata mapasa. Akijibu hivyo, tunaweza kumuambia kwamba ni hivyo mambo yanapashwa kuwa. Kisha tunaweza kumuuliza hivi: “Ikiwa wewe na mimi tunaelewa kwa urahisi mufano huo, je, Yesu ambaye alikuwa Mwalimu Mukubwa hangetumia mufano kama huo ili kuonyesha uhusiano ulio kati yake na Mungu? Lakini, Yesu alimuita Mungu kuwa Baba yake. Kwa kumuita hivyo, Yesu alionyesha kwamba Mungu ni mukubwa na ana mamlaka zaidi kuliko yeye.”

14. Ni mufano gani unaoonyesha kwamba ni jambo lisiloeleweka Mungu amupatie Ibilisi kazi ya kuwatesa watu katika moto?

14 Fikiria mufano mwengine. Watu fulani wanaamini kwamba Shetani ndiye anasimamia moto wa mateso. Mufano unaofuata unaweza kumusaidia muzazi aone kwamba ni jambo lisiloeleweka Mungu kumupatia Ibilisi kazi ya kuwatesa watu katika moto. Tunaweza kusema hivi: “Wazia kwamba mutoto wako amekuwa muasi sana na anafanya mambo mabaya sana. Unaweza kufanya nini?” Pengine, muzazi huyo anaweza kusema kwamba anapashwa kumupatia mutoto wake malipizi. Anaweza kujaribu tena na  tena kumusaidia mutoto wake aache kufanya mambo mabaya. (Met. 22:15) Kisha tunaweza kumuuliza kama anaweza kufanya nini ikiwa mutoto wake anakataa kubadilika hata kama anafanya yote anayoweza ili kumusaidia. Wazazi wengi wanaweza kusema kwamba ikiwa mutoto hapendi kubadilika, watalazimika kumupatia malipizi. Tunaweza tena kumuuliza hivi: “Utafanya nini ikiwa unavumbua kwamba kuna mutu fulani aliyemuchochea mutoto wako awe muasi sana?” Bila shaka, muzazi huyo atamukasirikia sana mutu huyo. Ili mufano huo umusaidie kuelewa, tunaweza kumuuliza muzazi huyo hivi: “Kwa kuwa unajua mutu aliyemuchochea mutoto wako awe muasi, unaweza kuambia mutu huyo amupatie mutoto wako malipizi?” Bila shaka, hapana. Kwa hiyo ni wazi kwamba, Mungu hangetumia Shetani ili awaazibu watu ambao yeye mwenyewe amechochea wafanye mambo mabaya!

USITAZAMIE KWAMBA KILA MUTU ATAKUSIKILIZA

15, 16. (a) Sababu gani hatuwezi kutazamia kwamba kila mutu ambaye tunahubiria atakubali habari njema ya Ufalme? (b) Tunahitaji kuwa na uwezo wa pekee ili tupate matokeo mazuri katika mahubiri? Eleza. (Ona pia kisanduku “ Habari Zinazotusaidia Kuwajibia Watu.”)

15 Tunatambua kwamba si kila mutu tunayehubiria ndiye atakubali habari njema ya Ufalme. (Mt. 10:11-14) Hata tutumie maulizo kwa ufundi namna gani, hata tufikiri vizuri na watu juu ya maandiko, na kutumia mifano vizuri ili kuwasaidia wasikilizaji waelewe, si wote watakaokubali habari njema ya Ufalme. Na tusisahau kwamba Yesu alikuwa mwalimu Mukubwa kuliko wote duniani, lakini ni wachache tu ndiyo walikubali mafundisho yake!—Yoh. 6:66; 7:45-48.

16 Kwa upande mwengine, hata ikiwa tunajisikia kuwa hatuko wafundishaji wazuri, tunaweza kupata matokeo mazuri katika mahubiri. (Soma Matendo 4:13.) Neno la Mungu linatuhakikishia kwamba ‘wale wote walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele’ watakubali habari njema. (Mdo. 13:48) Acheni basi tuendelee kuwa na maoni yanayofaa kuhusu sisi wenyewe na kuhusu wale ambao tunahubiria habari njema ya Ufalme. Na tuazimie kutumia mazoezi ambayo Yehova anatutolea, tukiwa hakika kwamba yatatuletea faida sisi, na wale wanaotusikiliza. (1 Tim. 4:16) Yehova anaweza kutusaidia tujue namna tunapashwa ‘kumujibia kila mutu.’ Katika habari inayofuata, tutazungumuzia kanuni moja nzuri ya kutumia katika mahubiri ili kupata matokeo mazuri.

^ fu. 6 Ona habari “Je, Inawezekana Kuamini Kuna Muumba?” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 01/10/2009.