Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kusaidia Ndugu na Dada Ambao Ndoa Zao Zimevunjika

Namna ya Kusaidia Ndugu na Dada Ambao Ndoa Zao Zimevunjika

Pengine unajua mutu fulani ao watu wengi ambao ndoa zao zimevunjika. Ni hivyo kwa sababu limekuwa jambo la kawaida kuvunja ndoa. Kwa mufano, utafiti uliofanywa katika inchi ya Polandi unaonyesha kwamba watu walio na miaka 30 ambao wameoana kumepita tatu mupaka sita wanaelekea kuvunja ndoa; si hao tu ndio walio katika hali hiyo.

Shirika la Mambo ya Familia la Hispania, linasema hivi: “Hesabu zinaonyesha kwamba katika Ulaya nusu ya watu ambao wameoana watavunja ndoa zao.” Katika inchi nyingine tajiri, mambo yako hivyohivyo.

KUJISIKIA MWENYE KUVURUGIKA

Ni jambo gani linalohusika katika hali hiyo inayotokea kwa ukawaida? Mushauri mumoja mwenye uzoefu wa mambo ya familia katika Ulaya Mashariki alisema hivi: “Kuvunja ndoa kunaonyesha waziwazi jambo ambalo lilikuwa tayari limetokea—kuvunjika kwa uhusiano na kutengana, jambo lenye kumuumiza sana moyoni.” Aliongezea hivi: “Kisha ndoa kuvunjika, kuna hali ya huzuni nyingi inayoumiza sana moyoni, hasira, kujuta, kuvunjika moyo, kukosa tumaini na kusikia haya.” Wakati fulani, hali hiyo inaweza kuleta mawazo ya kutaka kujiua. “Wakati tribinale inakubali kuvunjika kwa ndoa, hatua ingine inaanza. Kila wakati mutu anajisikia kuwa amebakia peke yake na kutengwa na wengine. Yeye anaweza kujiuliza hivi: ‘Sasa ndoa yangu imevunjika, ninakuwa nani sasa? Maisha yangu yana kusudi gani?’”

Wakati anakumbuka namna alivyojisikia katika miaka iliyopita, Ewa anasema hivi: “Nilisikia haya sana wakati ndoa yetu ilivunjika, majirani wangu na wafanya kazi wenzangu waliniita ‘mutu ambaye ndoa yake imevunjika.’ Nilisikia hasira sana. Nilibaki na watoto wangu wawili na kulazimishwa kuwa baba na mama yao.” * Adam, aliyekuwa muzee wa kutaniko mwenye kuheshimiwa kwa muda wa miaka 12, anasema hivi: “Nilipoteza sana heshima yangu mwenyewe na wakati fulani nilisikia hasira sana, na nilipenda kujitenga na kila mutu.”

KUJIKAZA ILI KUPATA NGUVU TENA

Wanapoendelea kusumbuka kwa sababu ya huzuni, watu fulani ambao ndoa zao zimevunjika, wamejikaza kupata tena nguvu hata kisha miaka mingi kupita. Wanaweza kuona kwamba wengine hawawahangaikie. Zaidi ya hilo, mwandishi mumoja wa habari alisema kwamba wanapaswa sasa “kubadili tabia zao na kujifunza wenyewe namna ya kupambana na matatizo yao.”

Stanisław anasema hivi: “Ndoa yetu ilipovunjika, bibi yangu wa zamani alinizuia ao alikataa niwaone binti zangu wawili wadogo. Hilo lilifanya nijisikie kuwa hakuna hata mutu mumoja aliyenihangaikia na kuwaza kwamba pengine Yehova pia alikuwa ameniacha. Sikuwa tena na hamu ya kuishi. Kisha muda fulani, nilitambua kwamba nilikuwa nimeingiwa na mawazo mabaya sana.” Pia, Wanda ambaye ndoa yake ilikuwa imevunjika alikuwa na wasiwasi alipofikiria maisha yake ya wakati ujao. Alisema hivi: “Nilifikiri kabisa kwamba muda mufupi kisha ndoa yangu kuvunjika, watu kutia ndani Mashahidi wenzangu,  hawangenihangaikia hata kidogo mimi na watoto wangu. Hata hivyo, sasa ninaweza kuona kwamba ndugu walitutegemeza sana na kunisaidia nilipoendelea kujaribu kuwalea watoto wangu ili wamutumikie Yehova.”

Maneno hayo yanaweza kukusaidia uelewe kwamba kisha ndoa kuvunjika watu fulani wanasumbuliwa na maoni yasiyofaa. Wanaweza kujiona kuwa wana sifa mbaya, kwamba hawafae kitu hata kidogo na hawastahili kuhangaikiwa. Tena, wanaweza kuanza kusema vibaya juu ya ndugu na dada walio karibu yao. Kwa hiyo, wanaweza kuanza kufikiri kwamba ndugu na dada katika kutaniko hawana upendo na hawawahangaikie. Lakini, mufano wa Stanisław na Wanda unaonyesha kwamba ndugu na dada fulani ambao ndoa zao zimevunjika wanaweza kufikia kutambua kwamba ndugu na dada zao wanawahangaikia kabisa. Bila shaka, Wakristo wenzao wamewahangaikia kwa njia ya pekee, hata kama musaada ambao walitoa haukupokewa vizuri hapo mbele.

KUJISIKIA KUWA PEKEE NA MWENYE KUKATALIWA

Kumbuka kwamba hata kama tunajikaza kusaidia ndugu na dada ambao ndoa zao zimevunjika, wanaweza kujisikia mara kwa mara kuwa peke yao. Zaidi sana dada ambao ndoa zao zimevunjika wanaweza kufikiri kwamba ni watu wachache tu ndio wanawahangaikia. Alicja anasema hivi: “Kumepita miaka munane kisha ndoa yangu kuvunjika. Lakini, ningali ninajisikia kuwa mutu wa bure wakati fulani. Ninapojisikia hivyo, nina amua kujitenga na wengine na kuanza kulia na kuhuzunika.”

Hata kama ndugu na dada fulani ambao ndoa zao zimevunjika hawajisikie hivyo, Biblia inawashauria waepuke kujitenga na wengine. Ikiwa hawafuate shauri hilo, wanaweza kukataa “hekima inayotumika.” (Met. 18:1) Hata hivyo, yule anayejisikia kuwa peke yake, anapaswa kutenda kwa hekima kwa kuepuka kutafuta kila mara shauri ao faraja kwa mutu fulani wa jinsia tofauti. Kufanya hivyo kutamusaidia asianze kuvutiwa kimapenzi na mutu huyo asiyekuwa bibi ao bwana yake.

Ndugu na dada zetu ambao ndoa zao zimevunjika wanaweza kupatwa na matatizo mengi ya moyoni kama vile kuwa na wasiwasi kuhusu wakati wao ujao, kujisikia kuwa peke yao, ao kutengwa na wengine. Tunapoelewa kwamba ni kawaida kujisikia hivyo na wakati huohuo pia ni vigumu kupambana na hali hiyo, tunapaswa kumuiga Yehova kwa kuwategemeza kwa uaminifu ndugu na dada hao. (Zab. 55:22; 1 Pet. 5:6, 7) Tunaweza kuwa hakika kwamba watapendezwa sana na musaada wowote ambao tutawatolea. Bila shaka, watapata marafiki wazuri katika kutaniko wanaoweza kuwasaidia!—Met. 17:17; 18:24.

^ fu. 6 Majina fulani yamebadilishwa.