Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tuwasaidie Wengine Watumie Uwezo Wao Wote

Tuwasaidie Wengine Watumie Uwezo Wao Wote

“Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.” ZAB. 32:8.

1, 2. Namna gani Yehova anawaona watumishi wake walio duniani?

WAZAZI wanapotazama watoto wao wakicheza michezo fulani, mara nyingi wanashangazwa na uwezo mbalimbali wa watoto wao. Wewe pia umejionea jambo hilo? Mutoto mumoja anaweza kujua vizuri michezo mbalimbali kama vile kuogelea ao kukimbia lakini ndugu yake anaweza kujua kuchapa ao kutengeneza vitu fulani. Ijapokuwa watoto hao wana uwezo fulani, wazazi wanapendezwa wanapovumbua uwezo mbalimbali wa watoto wao.

2 Yehova pia anapendezwa sana na watoto wake walio hapa duniani. Anawaona watumishi wake wa siku zetu kuwa “vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote.” (Hag. 2:7) Anapendezwa nao zaidi sana kwa sababu ya imani na ushikaminifu wao. Hata hivyo, pengine umetambua kwamba Mashahidi wenzako wana uwezo mbalimbali. Ndugu fulani wana uwezo wa kutoa hotuba nzuri lakini wengine wana uwezo wa kupanga mambo vizuri sana. Dada wengi wana uwezo wa kujifunza kwa urahisi luga za kigeni na kuzitumia katika mahubiri. Lakini wengine ni mifano mizuri katika kuwategemeza wale wanaohitaji kutiwa moyo na kuwahangaikia wagonjwa. (Rom. 16:1, 12) Tunafurahi sana kuwa na ndugu na dada hao katika kutaniko la Kikristo, sivyo?

3. Tutazungumuzia maulizo gani katika habari hii?

 3 Hata hivyo, ndugu na dada zetu fulani, kutia ndani vijana ao wale waliobatizwa hivi karibuni, wanaweza kuona kwamba hawajapata kazi fulani ya kufanya katika kutaniko. Namna gani tunaweza kuwasaidia watumie uwezo wao wote? Sababu gani tunapaswa kujikaza kutambua sifa zao nzuri, na kuwaona namna Yehova anavyowaona?

YEHOVA ANATAMBUA SIFA NZURI ZA WATUMISHI WAKE

4, 5. Namna gani habari iliyo kwenye Waamuzi 6:11-16 inaonyesha kwamba Yehova anatambua uwezo wa watumishi wake?

4 Habari nyingi katika Biblia zinaonyesha wazi kwamba Yehova haone tu sifa nzuri za watumishi wake, lakini pia anatambua uwezo wao mbalimbali. Kwa mufano, wakati Gideoni alichaguliwa ili kuwaokoa watu wa Mungu katika mikono ya Wamidiani adui zao, ni wazi kwamba alishangaa wakati malaika alimusalimia hivi: ‘Yehova yupo pamoja nawe, Ee mwanaume shujaa na mwenye nguvu.’ Ni wazi kwamba wakati huo, Gideoni hakujiwazia kuwa “mwenye nguvu.” Alikuwa na mashaka juu yake na alijiona kuwa mutu ambaye hastahili. Lakini, kama vile habari hiyo inaonyesha, ijapokuwa Gideoni aliona kuwa hastahili, bila shaka, Yehova aliona kabisa kwamba anastahili.—Soma Waamuzi 6:11-16.

5 Yehova alimutumikisha Gideoni ili kuwaokoa Waisraeli kwa sababu aliona ufundi mbalimbali aliotumia. Kwanza, malaika wa Yehova alimuona akipiga-piga ngano kwa nguvu zake zote. Kuna jambo lingine ambalo malaika huyo aliona. Zamani, ilikuwa jambo la kawaida kwa walimaji kupigia-pigia ngano mahali penye kuwa wazi ili upepo uweze kusukuma mbali uchafu wote uliotoka katika ngano. Jambo la kushangaza ni kwamba Gideoni alikuwa akipiga-piga ngano kwa siri mahali pa kukamulia divai ili aweze kuzificha Wamidiani. Huo ulikuwa ufundi wa akili kabisa. Kwa kweli, Yehova hakumuona Gideoni kuwa mulimaji tu mwenye akili, lakini pia alimuona kuwa mwanaume mwenye hekima. Bila shaka, Yehova aliona uwezo wake na alimutumikisha.

6, 7. (a) Namna gani maoni ya Yehova juu ya nabii Amosi yalikuwa tofauti na maoni ya Waisraeli fulani? (b) Ni nini inaonyesha kwamba nabii Amosi alijua mambo mengi?

6 Pia, Yehova alitambua uwezo wa mutumishi wake Amosi, hata kama wengi walimuona kuwa hafae kitu ao hastahili. Nabii Amosi mwenyewe alisema kwamba alikuwa muchungaji wa kondoo na muminyaji wa tini za mikuyu, chakula kilichoonwa kuwa cha maskini. Yehova alipomutuma Amosi atoe ujumbe wa hukumu juu ya ufalme wa Israeli wenye makabila kumi kwa sababu ya ibada yao ya sanamu, Waisraeli fulani walifikiri kwamba Yehova hakufanya uamuzi muzuri.—Soma Amosi 7:14, 15.

7 Amosi alitoka katika kijiji cha mbali sana. Lakini alijua desturi za watu na watawala fulani wa wakati wake na hilo lilionyesha kwamba alijua mambo mengi. Pengine alielewa vizuri hali zilizokuwa katika Israeli na alijua habari fulani kuhusu mataifa jirani kupitia wafanya-biashara wenye kusafiri. (Amo. 1:6, 9, 11, 13; 2:8; 6:4-6) Leo, watu fulani wenye elimu ya Biblia wanasema kwamba nabii Amosi alikuwa mwandikaji muzuri. Si kwa sababu tu alitumia maneno rahisi na yenye nguvu lakini pia alitumia vizuri ulinganifu na maneno yenye kupendeza. Nabii Amosi alimujibia bila woga kuhani muovu Amazia; hilo lilionyesha kwamba Yehova alichagua mutu aliyefaa ili atoe ujumbe wake na ambaye angetumia uwezo ambao watu hawakuona hapo mbele.—Amo. 7:12, 13, 16, 17.

8. (a) Yehova alimuhakikishia Daudi jambo gani? (b) Sababu gani maneno yaliyo kwenye Zaburi 32:8 yanawatia moyo wale wanaojisikia kwamba hawastahili ao hawana uwezo?

8 Bila shaka, Yehova anatambua uwezo wa kila mutumishi wake. Alimuhakikishia Mufalme Daudi kwamba angemuongoza  siku zote ‘jicho lake likiwa likimutazama.’ (Soma Zaburi 32:8.) Hauone kwamba jambo hilo linapaswa kututia moyo? Hata kama tunaweza kujiona kuwa hatustahili, Yehova anaweza kutusaidia tutimize mambo yanayopita uwezo wetu na kufikia miradi ambayo hatukuwazia hata siku moja kwamba tungefikia. Kama vile mwalimu anavyomuongoza polepole mwanafunzi ambaye hana uzoefu, Yehova iko tayari kutuongoza tunapoendelea kufanya maendeleo ya kiroho. Pia, Yehova anaweza kutumia ndugu zetu watusaidie tutumikishe uwezo wetu wote. Namna gani?

TAMBUA SIFA NZURI ZA WENGINE

9. Namna gani tunaweza kutumia shauri la mutume Paulo la “kuangalia” faida za wengine?

9 Mutume Paulo aliwashauri Wakristo wote ‘waangalie’ faida za waamini wenzao. (Soma Wafilipi 2:3, 4.) Shauri la mutume Paulo linamaanisha kwamba tunapaswa kutambua uwezo wa wengine na kupendezwa nao. Tunajisikia namna gani wakati ndugu ao dada anapendezwa na maendeleo fulani ambayo tumefanya? Mara nyingi, jambo hilo linatuchochea tufanye maendeleo zaidi. Vivyo hivyo, tunapotambua jitihada ambazo ndugu zetu wanafanya, hilo litawachochea waendelee kumutumikia Yehova kwa bidii.

10. Ni nani ambao tunapaswa kusaidia sana?

10 Ni nani ambao tunapaswa kuhangaikia sana? Bila shaka, sisi wote tunahitaji musaada wa pekee mara kwa mara, zaidi sana vijana ao wale waliobatizwa hivi karibuni. Tunapaswa kuwasaidia waone kwamba wanahusika katika utendaji mbalimbali wa kutaniko. Hilo litawasaidia waelewe kwamba wao pia ni wa maana katika kutaniko. Lakini ikiwa hatuhangaikie ndugu hao wanaweza kupoteza tamaa yao ya kutafuta kufikia mapendeleo fulani, kama vile Neno la Mungu linawatia moyo wafanye.—1 Tim. 3:1.

11. (a) Namna gani muzee mumoja alimusaidia kijana fulani afanye maendeleo? (b) Mufano wa Julien unakufundisha somo gani?

11 Ludovic, muzee wa kutaniko ambaye alisaidiwa alipokuwa kijana, anasema hivi: “Wakati ninapendezwa kwelikweli na ndugu fulani, hilo linamuchochea afanye maendeleo bila kukawia.” Kuhusu kijana Julien aliyekuwa mwenye haya, ndugu Ludovic anasema hivi: “Kwa sababu wakati fulani Julien alijiona kwamba hastahili na kwa kuwa alikuwa mutu mwenye haya, alikuwa na tabia ambayo haikuwapendeza wengine. Lakini nilitambua kwamba alikuwa mutu muzuri na alipenda kabisa kusaidia wengine katika kutaniko. Kwa hiyo, kuliko kumuchambua kwa sababu ya uzaifu wake, nilifikiria sana sifa nzuri zake na nilijaribu kumutia moyo.” Kisha muda fulani, Julien aliwekwa kuwa mutumishi wa huduma, na leo ni painia wa kawaida.

MUWASAIDIE WATUMIE UWEZO WAO WOTE

12. Tunapaswa kufanya nini ili kumusaidia ndugu atumie uwezo wake wote? Toa mufano.

12 Bila shaka, ikiwa tunataka kuwasaidia wengine watumie uwezo wao wote, tunapaswa kuwa watazamaji wazuri. Kama vile mufano wa Julien unavyoonyesha, hatupaswe kuona tu uzaifu wa mutu, lakini tunapaswa kutambua sifa nzuri na uwezo wake ambao anaweza kukomalisha baadaye. Jambo hilo linapatana kabisa na namna Yesu alimuona mutume Petro. Wakati fulani, mutume Petro alionekana kuwa mwenye kuyumba-yumba, lakini Yesu alitabiri kwamba angekuwa imara kama vile mwamba.—Yoh. 1:42.

13, 14. (a) Namna gani Barnaba alimuona kijana Marko? (b) Kijana mumoja alipata musaada gani? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

13 Barnaba alitumia njia hiyo kumuelekea Yohana aliyeitwa pia kwa jina la Marko. (Mdo. 12:25) Katika safari ya kwanza ya umisionere ya mutume Paulo pamoja na Barnaba, Marko alienda pamoja nao kama ‘mutumishi.’ Pengine Marko aliwatimizia  mahitaji yao ya kimwili. Hata hivyo, walipofika huko Pamfilia, Marko aliwaacha mara moja. Walipaswa kusafiri kuelekea kaskazini bila yeye kwa kupitia katika eneo ambamo mulikuwa wanyanganyi wengi. (Mdo. 13:5, 13) Barnaba hakufikiria uzaifu wa Marko lakini baadaye alipata nafasi nzuri ili kumuzoeza. (Mdo. 15:37-39) Hilo lilimusaidia kijana huyo awe Mukristo mwenye kukomaa kiroho. Jambo la kupendeza ni kwamba, Marko alikuwa huko Roma pamoja na mutume Paulo aliyekuwa mufungwa; naye pia alituma salamu zake kwa kutaniko la Wakolosai, na mutume Paulo alizungumuza vizuri kumuhusu. (Kol. 4:10) Fikiria furaha ambayo Barnaba alipaswa kuwa nayo wakati mutume Paulo alisema kwamba alihitaji Marko ili amusaidie.—2 Tim. 4:11.

14 Ndugu Alexandre ambaye aliwekwa kuwa muzee hivi karibuni anakumbuka namna ndugu mumoja alimusaidia. Anasema hivi: “Nilipokuwa kijana, ilikuwa vigumu kwangu kusali mbele ya watu wengi. Muzee mumoja alinionyesha namna ya kujitayarisha na kuwa mwenye kutulia wakati wa kusali. Kuliko kuachia pale, alinitolea nafasi ya kusali kila mara kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri. Kisha muda mufupi, nilishinda tatizo hilo.”

15. Namna gani mutume Paulo alionyesha kwamba alipendezwa na waamini wenzake?

15 Unapoona sifa nzuri za ndugu ao dada, je, unamuambia kwamba unapendezwa na sifa zake? Katika sura ya 16 ya barua ya mutume Paulo kwa Waroma, anataja ndugu na dada zaidi ya 20 ambao sifa zao nzuri zilizomuchochea awapende sana. (Rom. 16:3-7, 13) Kwa mufano, mutume Paulo anakubali kwamba Androniko na Yunia walikuwa wamemutumikia Kristo kwa muda murefu kuliko yeye, na alikazia sana uvumilivu wao. Mutume Paulo alizungumuzia pia mama yake na Rufo aliyemuhangaikia kwa upendo.

Frédéric (kushoto) alimutia moyo Rico aendelee kumutumikia Yehova(Ona fungu la 16

16. Kumupongeza kijana kunaweza kuwa na matokeo gani?

16 Tunaweza kupata matokeo mazuri tunapotolea ndugu zetu pongezi ya kweli. Fikiria kijana Rico wa huko Ufaransa, ambaye alivunjika moyo kwa sababu baba yake asiye kuwa Shahidi alikataa abatizwe. Rico alifikiri kwamba alipaswa kungojea mupaka afikie miaka kumi 18 ili ajitoe kwa Yehova. Tena alihuzunika kwa kuwa wanafunzi wenzake walimucheka kwa sababu ya imani yake. Ndugu Frédéric, ambaye ni muzee wa kutaniko, aliyejifunza Biblia pamoja na kijana huyo, anasema hivi: “Nilimupongeza Rico kwa sababu ya musimamo wake ulionyesha kwamba amekuwa mwenye bidii sana ili kutetea imani yake.” Maneno hayo yalimutia moyo Rico aendelee kuwa mufano muzuri na yalimusaidia kuwa na urafiki muzuri pamoja na baba yake. Rico alibatizwa akiwa na miaka 12.

Jérôme (kuume) alimusaidia Ryan kuwa misionere(Ona fungu la 17)

17. (a) Namna gani tunaweza kusaidia ndugu zetu wafanye maendeleo? (b) Namna gani misionere mumoja aliwasaidia ndugu vijana, na matokeo yalikuwa nini?

17 Mara nyingi tunapongeza ndugu wanapotimiza vizuri migawo yao ao kwa sababu ya  jitihada zao. Tunapofurahia mambo ambayo wametimiza, tunawachochea Wakristo wenzetu wamutumikie Yehova kwa uwezo wao wote. Dada Sylvie, * ambaye ametumikia kwenye Beteli ya Ufaransa kwa miaka mingi, alisema kwamba dada pia wanaweza kupongeza ndugu zao. Alitambua kwamba dada wanapendezwa na mambo fulani ambayo ndugu hawatambue. Kwa hiyo, “maneno yao ya pongezi yanaweza kuongezea yale ambayo ndugu wenye uzoefu wanaweza kusema.” Aliongezea hivi: “Kwangu mimi, kuwapongeza wengine ni jambo ambalo ninapaswa kufanya.” (Met. 3:27) Ndugu Jérôme, ambaye ni misionere katika Guiana ya Ufaransa, amesaidia vijana wengi wanaume kuwa wa misionere. Ndugu Jérôme anasema hivi: “Nimetambua kwamba wakati ninapongeza vijana juu ya mambo fulani wanayotimiza katika mahubiri ao wanapotoa maelezo mazuri, wanafanya maendeleo na kutumia uwezo wao wote.”

18. Sababu gani ni vizuri kutumika pamoja na ndugu vijana?

18 Tunaweza pia kuwachochea Wakristo wenzetu wafanye maendeleo kwa kutumika pamoja nao. Muzee wa kutaniko anaweza kumuomba kijana anayejua kutumia ordinatere amusaidie kuchukua habari fulani kwenye adresi yetu ya Internete jw.org. Habari hizo zinaweza kuwasaidia ndugu na dada fulani wenye kuzeeka wasio na ordinatere. Ao ikiwa unaombwa kufanya kazi fulani kwenye Jumba la Ufalme, sababu gani usimualike ndugu kijana fulani atumike pamoja nawe? Kufanya hivyo kutakutolea nafasi nzuri ya kuona uwezo wa vijana, kuwapongeza na kuona matokeo.—Met. 15:23.

FANYA MIPANGO KWA AJILI YA WAKATI UJAO

19, 20. Sababu gani tunapaswa kuwasaidia wengine wafanye maendeleo?

19 Wakati Yehova alichagua Yoshua aongoze Waisraeli, alimuagiza pia Musa ‘amutie moyo’ na ‘kumuimarisha [ao kumutia nguvu].’ (Soma Kumbukumbu la Torati 3:28.) Leo, watu wengi wanajiunga nasi ili kumuabudu Yehova. Wakristo wote wenye uzoefu, ni kusema, wazee wa kutaniko na wengine, wanaweza kuwasaidia vijana na wale waliobatizwa hivi karibuni watumie uwezo wao wote. Kwa kufanya hivyo, wengi kati yao wanaweza kuanza utumishi wa wakati wote, na wengine wengi watakuwa wenye ‘kustahili kufundisha wengine.’—2 Tim. 2:2.

20 Hata iwe sisi tunapatikana katika kutaniko lenye kuwa na ndugu wenye uzoefu ao katika sehemu itakayokuwa kutaniko hivi karibuni, acheni tuendelee kufanya mipango kwa ajili ya wakati ujao. Siri ni kumuiga Yehova, ambaye siku zote anatambua sifa nzuri za watumishi wake.

^ fu. 17 Jina limebadilishwa.