Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakumbuka?

Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari zilizozungumuziwa hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Basi, jaribu kujibu maulizo yanayofuata:

Mwana-kondoo wa Pasaka alipaswa kuchinjwa wakati gani wa siku 14 Nisani?

Tafsiri fulani za Biblia zinaonyesha kwamba mwana-kondoo alipaswa kuchinjwa “katikati ya zile jioni mbili,” ni kusema, wakati ambapo jua lilikuwa limeshuka lakini mwangaza kidogo ulikuwa ungali. (Kut. 12:6)—15/12, ukurasa wa 18-19.

Ni kanuni gani za Biblia ambazo vijana wanaweza kutumia ili kuchukua maamuzi yenye hekima?

Ni kanuni tatu. Kanuni ya (1) Tafuta kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake. (Mt. 6:19-34) (2) Pata furaha kwa kuwatumikia wengine. (Mdo. 20:35) (3) Mutumikie Yehova wakati ungali kijana. (Mhu. 12:1)—15/1, ukurasa wa 19-20.

Ni wapandaji wa farasi gani waine ambao wako katika mwendo tangu 1914?

Yesu, ndiye mupandaji wa farasi nyeupe, kazi yake ya kwanza ilikuwa kumutosha Shetani mbinguni pamoja na mashetani wake. Mupandaji wa farasi ya rangi ya moto anafananisha vita ambavyo vimetesa wanadamu. Mupandaji wa farasi mweusi anafananisha njaa. Mupandaji wa farasi wa rangi ya majivu anatokeza kifo kupitia pigo lenye kuua, na anaua mamilioni ya watu. (Ufu. 6:2-8)—1/2, ukurasa wa 6-7.

“Ndoa ya Mwana-Kondoo” itafanywa wakati gani? (Ufu. 19:7)

“Ndoa ya Mwana-Kondoo” itafanywa kisha Mufalme, Yesu Kristo, kukamilisha ushindi wake, ni kusema, kisha kuharibiwa kwa Babiloni Mukubwa na kisha kupiganwa kwa vita ya Har-magedoni.—15/2, ukurasa wa 10.

Sababu gani Wayahudi wa siku za Yesu walimungojea Masiya? (Luka 3:15)

Hatuwezi kuhakikisha kwamba Wayahudi wa siku za Yesu walielewa unabii wa Danieli kuhusu Masiya kama vile tunavyouelewa. (Dan. 9:24-27) Lakini, pengine, walisikia kuhusu tangazo la malaika kwa wachungaji ao maneno ya nabii mwanamuke Ana aliyosema juu ya mutoto Yesu kwenye hekalu. Tena, wanajimu walikuja kumutafuta ‘yule mufalme wa Wayahudi aliyezaliwa.’ (Mt. 2:1, 2) Baadaye, Yohana Mubatizaji alionyesha kwamba Kristo angetokea karibuni.—15/2, ukurasa wa 26-27.

Tunaweza kufanya nini ili Ndiyo yetu isimaanishe Siyo? (2 Kor. 1:18)

Ni kweli kwamba, kwa sababu ya hali fulani ambazo hatukutazamia, tunaweza kushindwa kutimiza ahadi yetu. Lakini, tukitoa ahadi ao kufanya mapatano, tunapaswa kufanya yote tunayoweza ili kuyatimiza.—15/3, ukurasa wa 32.

Namna gani tunaweza kushinda kishawishi cha kutazama ponografia?

Kuna hatua tatu zenye kusaidia (1) Tenda bila kukawia na kuepuka kukazia macho picha zinazoamusha tamaa ya ngono. (2) Linda mawazo yako kwa kukaza akili juu ya mambo yanayofaa na kusali. (3) Linda hatua zako kwa kuepuka filme ao programe za Internete zinazoonyesha ponografia.—1/4, ukurasa wa 10-12.

Mukristo akiacha familia yake ili kwenda kutafuta feza katika inchi nyingine, hilo linaweza kuwa na matokeo gani yasiyotazamiwa?

Wakati wazazi na watoto hawaishi pamoja katika familia, wanaweza kuteseka moyoni na kuwa na mwenendo mubaya. Watoto wanaweza kuchukia wazazi wao. Na bibi ao bwana aliyeachwa anaweza kuangukia katika uzinifu.—15/4, ukurasa wa 19-20.

Sababu gani watenda-maovu waliouawa walivunjwa pia miguu?

Waroma waliwaua watenda-maovu fulani kwenye muti. Wayahudi waliomba miguu ya watenda-maovu pamoja na ile ya Yesu ivunjwe. Hilo lingefanya wasongwe pumuzi ao washindwe kupumua ili wakufe haraka. Kwa hiyo, hawangebaki usiku kucha juu ya muti. (Kum. 21:22, 23)—1/5, ukurasa wa 11.

Tunapaswa kukumbuka maulizo gani ine tunapohubiri?

Nitazungumuza na watu wa namna gani? Nitawapata wapi? Ni wakati gani ulio muzuri wa kuwapata watu? Nitazungumuza nao namna gani?—15/5, ukurasa wa 12-15.

Kuvuta tumbako kumetokeza hatari gani?

Katika miaka mia moja iliyopita, watu 100000000 walikufa kwa sababu ya kuvuta tumbako. Sasa ni watu karibu 6000000 wanaokufa kila mwaka kwa sababu ya kitendo hicho.—1/6, ukurasa wa 3.