Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maoni ya Yehova Juu Uzaifu wa Wanadamu

Maoni ya Yehova Juu Uzaifu wa Wanadamu

‘Viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa zaifu zaidi ni vya lazima.’1 KOR. 12:22.

1, 2. Sababu gani mutume Paulo aliwaelewa vizuri wale waliokuwa zaifu?

WAKATI fulani kila mutu anajisikia kuwa muzaifu. Magonjwa kama vile homa ao mambo mengine yanayosumbua afya, yanaweza kutufanya tuwe wazaifu na kukosa nguvu za kufanya kazi zetu za kila siku. Wazia sasa kwamba wewe unajisikia kuwa muzaifu, si kwa muda mufupi tu, lakini kwa muda murefu. Unapokuwa katika hali hiyo, utafurahi ikiwa wengine wanakuelewa na kujitia pa nafasi yako, sivyo?

2 Mutume Paulo pia alijisikia kuwa zaifu wakati fulani kwa sababu ya matatizo kutoka inje na ndani ya kutaniko. Mara nyingi, mutume Paulo alifikiri kwamba alikuwa amefikia mwisho. (2 Kor. 1:8; 7:5) Alipofikiria maisha yake na magumu mengi aliyopata kwa sababu ya kumutumikia Mungu kwa uaminifu, alisema hivi: ‘Ni nani aliye zaifu, nami si zaifu?’ (2 Kor. 11:29) Tena, mutume Paulo alilinganisha ndugu na dada katika kutaniko la Kikristo na viungo vya mwili wa mutu aliposema kwamba viungo ‘vinavyoonekana kuwa zaifu zaidi ni vya lazima.’ (1 Kor. 12:22) Maneno hayo yanamaanisha nini? Sababu gani tunapaswa kuwa na maoni ya Yehova kuhusu wale wanaoonekana kuwa zaifu? Na tutapata faida gani ikiwa tunakuwa na maoni kama hayo?

 MAONI YA YEHOVA KUHUSU UZAIFU WA WANADAMU

3. Ni nini inaweza kufanya tuwe na maoni yasiyofaa kuelekea ndugu na dada wanaohitaji musaada?

3 Tunaishi katika ulimwengu wa watu wanaoonyesha roho ya kushindana na ya kujivuna kwa sababu wana nguvu ao ni vijana. Wengi wanafanya yote wanayoweza ili kufanikiwa bila kuhangaikia wale walio wazaifu. Sisi hatuwezi kuunga mukono tabia hiyo. Lakini, bila kujua, tunaweza kuanza kuwa na mawazo mabaya kuelekea wale wanaohitaji musaada wa kawaida, hata katika kutaniko. Namna gani tunaweza kuona kila ndugu na dada kama vile Yehova anavyomuona?

4, 5. (a) Namna gani mufano ulio kwenye 1 Wakorintho 12:21-23 unatusaidia kuelewa maoni ya Yehova kuhusu uzaifu wa wanadamu? (b) Tunaweza kupata faida gani kwa kuwasaidia wale walio zaifu?

4 Mufano unaopatikana katika barua ya kwanza ya mutume Paulo kwa Wakorintho, unaweza kutusaidia tuelewe maoni ya Yehova kuhusu uzaifu wa wanadamu. Katika sura ya 12, mutume Paulo anatukumbusha kwamba hata viungo vya mwili ambavyo vinaonekana kuwa zaifu sana ao ambavyo havivutie sana ni vya lazima katika mwili wetu. (Soma 1 Wakorintho 12:12, 18, 21-23.) Watu fulani wanaoamini fundisho la mageuzi wamesema kwamba viungo fulani vya mwili wetu havina lazima yoyote. Hata hivyo, Anatomia ao elimu ya miili ya viumbe inaonyesha kwamba viungo vya mwili vilivyoonwa kuwa si vya lazima vinafanya kazi ya maana sana katika mwili wetu. * Kwa mufano, watu fulani wanaoamini fundisho la mageuzi walifikiri kwamba kidole kidogo cha mwisho kwenye muguu wetu hakina kazi, lakini wamevumbua sasa kwamba kidole hicho kinafanya mwili wetu usimame wima bila kuyumba-yumba.

5 Mufano wa mutume Paulo unaonyesha kwamba kila ndugu na dada katika kutaniko la Kikristo ni wa lazima. Tofauti na Shetani anayetaka watu wajione kuwa hawafae kitu, Yehova anawaona watumishi wake wote kuwa “wa lazima” kutia ndani wale wanaoonekana kuwa zaifu. (Ayu. 4:18, 19) Kujua hivyo kunapaswa kutuchochea tufurahie nafasi yetu katika kutaniko letu na kati ya watu wa Mungu walio katika dunia yote. Kwa mufano, fikiria wakati fulani ulipomusaidia mutu mwenye kuzeeka na ambaye alikuwa na lazima ya musaada. Pengine alifurahi, lakini wewe pia ulifurahi, sivyo? Kuwasaidia wengine, kunatuletea furaha, kunatusaidia tukomalishe uvumilivu, upendo na sifa zingine za Kikristo. (Efe. 4:15, 16) Yehova, Baba yetu mwenye upendo, anataka tuwaone ndugu na dada wote kuwa wa lazima, hata wale wanaoonekana kuwa zaifu.

6. Namna gani mutume Paulo alitumia maneno ‘zaifu’ na “nguvu”?

6 Ni jambo lenye kupendeza, kuona kwamba katika barua ambayo mutume Paulo aliwaandikia Wakorintho, alitumia maneno, ‘zaifu’ na ‘uzaifu’ alipozungumuzia namna watu wasioamini walikuwa wakiwaona Wakristo na pia alitumia maneno hayo ili kuonyesha namna alijisikia yeye mwenyewe. (1 Kor. 1:26, 27; 2:3) Wakati mutume Paulo alizungumuzia wale waliokuwa na “nguvu,” nia yake haikuwa kuwachochea Wakristo fulani wajisikie kuwa wa lazima sana kuliko wengine. (Rom. 15:1) Alipenda tu kuonyesha kwamba Wakristo waliokuwa na uzoefu mwingi walipaswa kuvumilia wale waliokuwa wapya katika kweli.

UNAHITAJI KUBADILI MAONI YAKO?

7. Ni jambo gani linaweza kutuzuia tusiwasaidie wale walio katika uhitaji?

7 Tunaposaidia ‘mutu wa hali ya chini’ tunamuiga Yehova, na hilo linafanya tukubaliwenaye. (Zab. 41:1; Efe. 5:1) Bila shaka, kuwa na maoni mabaya wakati fulani kuelekea wale walio katika uhitaji, kunaweza kutuzuia tusiwasaidie. Ao kwa sababu ya  kukosa maneno ya kusema, tunaweza kuondoka na kumuacha yule anayepambana na magumu fulani. Dada Cynthia, * ambaye bwana yake alimuacha, alisema hivi: “Ikiwa ndugu ao dada wanakuepuka ao hawakutendee namna marafiki wa karibu wanapaswa kufanya, hilo linaweza kuumiza. Unapopambana na magumu fulani, unahitaji sana watu wakukaribie zaidi.” Mufalme Daudi pia alipatwa na hali hiyo.—Zab. 31:12.

8. Nini itatusaidia tuendelee kujitia pa nafasi ya wengine?

8 Pengine tunaweza kujitia pa nafasi ya wengine ikiwa tunakumbuka kwamba ndugu na dada zetu wapendwa wamekuwa zaifu kwa sababu ya hali mbalimbali, kama vile magonjwa, kuishi na bibi ao bwana ambaye si Shahidi, ao kushuka moyo. Sisi pia tunaweza kujikuta katika hali kama hizo siku moja. Mbele waingie katika Inchi ya Ahadi, Waisraeli ambao walikuwa maskini na zaifu katika inchi ya Misri, waliambiwa kwamba hawangepaswa ‘kufanya moyo [wao] kuwa mugumu’ kuelekea ndugu zao waliokuwa maskini. Yehova alitaka Waisraeli waelewe kwamba maskini alipaswa kusaidiwa.—Kum. 15:7, 11; Law. 25:35-38.

9. Ni jambo gani tunalopaswa kufanya kwanza ili kusaidia ndugu ao dada anayepambana na magumu fulani? Toa mufano.

9 Kuliko kuchambua ao kushakia ndugu na dada wanaopambana na magumu, tunapaswa kuwasaidia na kuwafariji kiroho. (Ayu. 33:6, 7; Mt. 7:1) Kwa mufano, wazia kwamba mutu fulani anayetembeza pikipiki anafanya aksidenti; anaumia sana na anapelekwa haraka kwenye hospitali. Anapofika kwenye hospitali, je, waganga watapoteza wakati ili kutafuta kujua kwanza ni nani aliyemugonga? Hapana, wanapaswa kwanza kumutunza mutu huyo haraka sana. Vivyo hivyo, ikiwa ndugu ao dada amekuwa muzaifu kwa sababu ya magumu fulani ya pekee, tunapaswa kwanza kumutolea musaada wa kiroho.—Soma 1 Wathesalonike 5:14.

10. Namna gani wale wanaoonekana kuwa zaifu wanaweza kabisa kuwa “matajiri katika imani”?

10 Ikiwa hatufikirie tu uzaifu fulani wa ndugu ao dada, tunaweza kuona kwamba wao si wazaifu kabisa. Fikiria dada ambao wamekuwa wakivumilia upinzani katika familia kwa miaka mingi. Wamoja kati yao wanaweza kuonekana kuwa wenye sura ya huruma na zaifu, lakini wanaendelea kuwa na imani yenye nguvu. Wakati unamuona dada ambaye analea watoto peke yake akiwaleta kwa ukawaida kwenye mikutano, je, haufurahie bidii na imani yake? Na tuseme nini kuhusu vijana wanaoendelea kushikamana na kweli hata kama wanatatizwa sana kwenye masomo? Tunakubali kwamba wale wanaoonekana kuwa zaifu sana wanaweza kuwa “matajiri katika imani” kama wale wengine walio kati yetu na ambao wana hali nzuri sana.—Yak. 2:5.

UWAONE WENGINE KAMA YEHOVA ANAVYOWAONA

11, 12. (a) Ni nini itatusaidia tubadili maoni yetu juu ya uzaifu wa wanadamu? (b) Namna Yehova alimutendea Haruni, inatufundisha nini?

11 Tunapochunguza namna Yehova alivyoshugulikia watumishi wake fulani, hilo linatusaidia kubadili maoni yetu kuhusu uzaifu wa wanadamu. (Soma Zaburi 130:3.) Kwa mufano, ikiwa ungekuwa pamoja na Musa, wakati Haruni alitengeneza ndama ya zahabu, ungemuona Haruni namna gani alipokuwa akitetea uzaifu wake? (Kut. 32:21-24) Ao ungekuwa na maoni gani juu ya mutazamo wa Haruni wakati Miriamu dada yake alimuchochea amuchambue Musa kwa sababu alioa mwanamuke asiye Mwisraeli? (Hes. 12:1, 2) Ungefanya nini wakati Musa na Haruni walikosa kumuheshimu Yehova, wakati alitoa maji kwa njia ya muujiza huko Meriba?—Hes. 20:10-13.

 12 Katika hali hizo zote, Yehova alipaswa kumupatia Haruni malipizi mara moja. Lakini alielewa kwamba Haruni hakuwa mutu mubaya. Inaonekana kwamba Haruni alifanya makosa kwa sababu alikuwa katika hali ngumu na alichochewa na watu wabaya. Lakini, Haruni alikubali makosa yake na alikuwa tayari kukubali malipizi ya Yehova. (Kut. 32:26; Hes. 12:11; 20:23-27) Yehova alikazia imani ya Haruni na nia yake ya kutubu. Miaka mingi baadaye, Haruni na watoto wake waliendelea kukumbukwa kuwa watu waliomuogopa Yehova.—Zab. 115:10-12; 135:19, 20.

13. Namna gani tunaweza kubadili maoni yetu juu ya uzaifu wa wanadamu?

13 Ili tuwaone wengine kama Yehova anavyowaona, tunapaswa kuchunguza maoni yetu juu wale ambao wanaonekana kuwa zaifu. (1 Sam. 16:7) Kwa mufano, tunatenda namna gani wakati kijana fulani hachague vizuri mambo ya kujifurahisha ao wakati anatenda bila kufikiri? Kuliko kumuchambua sana, sababu gani hatuwezi kufikiria jambo la kufanya ili kumusaidia akomae kiroho? Tunaweza kuchukua hatua ya kumusaidia mutu fulani aliye katika uhitaji. Tukifanya hivyo, tutaendelea kukomaa katika uelewaji na upendo.

14, 15. (a) Yehova alifanya nini Eliya aliposhuka moyo wakati fulani? (b) Hali iliyomupata Eliya inaweza kutufundisha somo gani?

14 Jambo lingine linaloweza kutusaidia tuwe na maoni ya Yehova kuhusu uzaifu wa wengine, ni kuchunguza namna alivyowatendea watumishi wake fulani walioshuka moyo. Mumoja kati ya watumishi hao alikuwa nabii Eliya. Hata kama alikuwa amewaua bila woga manabii 450 wa Baali, Eliya alikimbia aliposikia kwamba Malkia Yezebeli alikuwa amepanga kumuua. Kisha kutembea kilometre 150 kuelekea Beer-sheba, Eliya alienda mbali katika jangwa.  Akiwa mwenye kuchoka sana kwa sababu ya kutembea katika jua kali, nabii huyo alikaa chini ya muti na ‘aliomba kwamba akufe.’—1 Fal. 18:19; 19:1-4.

Yehova alielewa uzaifu wa nabii Eliya na alituma malaika ili amusaidie(Ona fungu la 14, 15)

15 Yehova alijisikia namna gani huko mbinguni alipomuona nabii wake mwaminifu ambaye alikuwa ameshuka moyo? Je, alimukataa mutumishi wake kwa sababu alishuka moyo wakati fulani na kupoteza bidii yake? Bila shaka, hapana! Yehova alielewa uzaifu wa nabii Eliya na alituma malaika ili amusaidie. Mara mbili malaika alimubembeleza Eliya akule. Kwa hiyo, safari iliyofuata haingekuwa “ndefu mno [ao sana] kwake.” (Soma 1 Wafalme 19:5-8.) Bila shaka, mbele hata amupatie maagizo fulani, Yehova alimusikiliza kwanza nabii wake na kumutolea musaada ambao alihitaji.

16, 17. Namna Yehova alivyomuhangaikia nabii Eliya inatufundisha nini?

16 Namna gani tunaweza kumuiga Mungu wetu mwenye kutuhangaikia? Tunapaswa kuepuka kutoa mashauri haraka-haraka. (Met. 18:13) Ni vizuri zaidi kwanza tuwe na wakati wa kuwasikiliza wale ambao wanaweza kujisikia kuwa ‘wana heshima ndogo’ kwa sababu ya hali zao. (1 Kor. 12:23) Ndipo tunaweza kujua mambo wanayohitaji kabisa na tutakuwa tayari kuwasaidia.

17 Kwa mufano, fikiria dada Cynthia tuliyezungumuzia hapo mbele, ambaye bwana yake alimuacha yeye na binti zake wawili. Walibakia peke yao. Mashahidi wenzao walitenda namna gani? Dada Cynthia anasema hivi: “Tuliwaambia kupitia telefone mambo yaliyotupata, na kisha dakika 45 walifika nyumbani kwetu. Walikuwa wakilia. Walibakia pamoja nasi kwa muda wa siku mbili ao tatu za kwanza-kwanza. Kwa kuwa hatukuwa tunakula tena muzuri na tulijisikia vibaya moyoni, walitubeba nyumbani kwao kwa muda fulani.” Mufano huyo unatukumbusha yale ambayo mutume Yakobo aliandika: “Ikiwa ndugu ao dada yuko uchi naye hana chakula cha kutosha kwa ajili ya siku, na mumoja wenu amwambie: ‘Nenda kwa amani, jipashe moto na kula vizuri,’ lakini ninyi mukose kumupa mahitaji ya mwili wake, ina faida gani? Vivyo hivyo, pia, imani, ikiwa haina matendo, imekufa yenyewe.” (Yak. 2:15-17) Kwa sababu ndugu na dada wa kutaniko lake walisaidia kwa wakati unaofaa, dada Cynthia na binti zake walipata nguvu za kuwa mapainia wasaidizi miezi sita tu kisha kupatwa na hali hiyo yenye kuhuzunisha.—2 Kor. 12:10.

FAIDA NYINGI

18, 19. (a) Namna gani tunaweza kuwasaidia wale walio zaifu wakati fulani? (b) Ni nani wanaofaidika tunaposaidia wale wanaojisikia kuwa zaifu?

18 Pengine umejionea kwamba kisha kugonjwa kwa muda murefu inaweza kuchukua wakati ili kupata tena nguvu. Vivyo hivyo, Mukristo ambaye amekuwa zaifu kwa sababu ya magumu yake ao hali mbaya mbalimbali, anahitaji wakati ili awe tena nguvu kiroho. Bila shaka, ndugu ao dada huyo anapaswa kutia nguvu imani yake kupitia funzo la pekee, sala na kuhuzuria mikutano. Lakini, je, tutaendelea kumuvumilia mupaka awe tena nguvu kiroho? Anapopata nguvu polepole, je, tutaendelea kumuonyesha upendo? Je, tutajikaza kusaidia kwa muda fulani wale walio zaifu wajisikie kuwa wa maana na waone kwamba tunawapenda?—2 Kor. 8:8.

19 Tusisahau hata kidogo kwamba tunaposaidia ndugu na dada zetu, tunapata furaha inayotokana tu na kutoa. Pia tunaonyesha sifa yetu ya kujitia pa nafasi ya wengine na kuwa wenye kuvumilia. Lakini tunaweza kufanya mengi zaidi. Ndugu na dada wanakuwa wenye kuchangamuka na wenye upendo zaidi. Zaidi ya hilo, tunamuiga Yehova ambaye anamuona kila mutumishi wake kuwa wa lazima. Bila shaka sisi wote tuna sababu nzuri za kukubali shauri la ‘kuwasaidia wale walio zaifu.’—Mdo. 20:35.

^ fu. 4 Katika kitabu chake La Lignée Humaine, Charles Darwin anazungumuzia viungo fulani vya mwili kuwa “si vya lazima.” Mutetezi wake mumoja alisema kwamba kuna viungo kumi na mbili hivi katika miwili wa mwanadamu ambavyo “havina kazi,” kutia ndani sehemu inayopatikana chini ya utumbo mukubwa (ao appendice) na kiungo fulani kinachopatikana ndani ya shingo yetu (ao thymus).

^ fu. 7 Jina limebadilishwa.