MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 8, 2014

Gazeti hili lina habari za kujifunza za tarehe 29 Mwezi wa 9, mupaka tarehe 26 Mwezi wa 10, 2014.

Unapata Chakula “kwa Wakati Unaofaa”?

Ili mutu aendelee kuwa nguvu kiroho, je, anapaswa kuwa na vichapo vyote ambavyo mutumwa mwaminifu anatutolea?

Daraka la Wanawake Katika Mupango wa Yehova

Ujifunze matokeo ya kumuasi Mungu juu ya wanaume na wanawake. Chunguza habari ya wanawake waaminifu wa zamani. Ona pia sehemu ambayo wanawake Wakristo wanatimiza leo katika kazi ya kuhubiri.

Neno la Mungu Liko Hai!—Ulitumie

Kila Shahidi wa Yehova anataka kupata matokeo mazuri anapohubiri. Chunguza mapendekezo fulani kuhusu namna ya kutumia Neno la Mungu lenye nguvu pamoja na trakte zetu mupya ili kuanzisha mazungumuzo.

Yehova Anatukaribia Namna Gani?

Tunahitaji kuwa marafiki wa karibu wa Yehova. Ona namna zabihu ya ukombozi na Biblia inaonyesha kwamba Yehova anatuvuta kwake.

Sikiliza Sauti ya Yehova Popote Ulipo

Ujifunze sababu gani ni lazima kusikiliza sauti ya Yehova na kuzungumuza naye. Habari hii itatusaidia kuona mambo ambayo tunapaswa kufanya ili Shetani na mielekeo yetu mibaya visitufanye tukose kumusikiliza Yehova.

‘Rudi na Uwatie Nguvu Ndugu Zako’

Ikiwa ndugu alikuwa muzee, je, anaweza tena ‘kufikia cheo cha kuwa mwangalizi?

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati Yesu alisema kwamba wale watakaofufuliwa ‘hawataoa wala kuolewa,’ alikuwa akizungumuzia ufufuo utakaofanyika duniani?

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

“Eureka-Drama” Ilisaidia Watu Wengi Kupata Kweli ya Biblia

Eureka-Drama ilifanana na “Foto-Drama ya Uumbaji” lakini ilifupishwa na, ingeweza kuonyeshwa katika maeneo ya vijiji, bila hata kutumia umeme (courant).