Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unapata Chakula “kwa Wakati Unaofaa”?

Unapata Chakula “kwa Wakati Unaofaa”?

TUNAISHI nyakati ngumu zaidi kuliko wanadamu wengine wote ambao waliishi mbele yetu. (2 Tim. 3:1-5) Kila siku, upendo wetu kwa Yehova na nia yetu ya kuendelea kumutii inajaribiwa. Yesu alijua mbele ya wakati kwamba siku hizi zingekuwa ngumu, lakini alihakikishia wanafunzi wake kwamba wangepata vitia-moyo ili waweze kuvumilia mupaka mwisho. (Mt. 24:3, 13; 28:20) Ili kuwatia nguvu, alichagua mutumwa mwaminifu ili awatolee chakula cha kiroho “kwa wakati unaofaa.”—Mt. 24:45, 46.

Tangu kuwekwa kwa mutumwa mwaminifu katika mwaka wa 1919, mamilioni ya “watumishi wa nyumbani” kutoka mataifa yote wamekusanywa katika tengenezo la Mungu na wanalishwa kiroho. (Mt. 24:14; Ufu. 22:17) Lakini, chakula hicho hakipatikane katika luga zote, na si watu wote wanaoweza kupata vichapo vilivyo kwenye adresi yetu ya Internete. Kwa mufano, watu wengi hawana namna ya kupata video na habari zilizo kwenye adresi yetu ya Internete jw.org. Je, hilo linamaanisha kwamba watu fulani wanakosa chakula ambacho wanahitaji ili kuendelea kuwa na afya nzuri ya kiroho? Tutafute majibu ya maulizo ine ya lazima.

 1 Ni jambo gani la kwanza kabisa katika chakula ambacho Yehova anatutolea?

Wakati Shetani alimujaribu Yesu kwa kumuambia ageuze majiwe kuwa mikate, Yesu alimuambia hivi: ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mukate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’ (Mt. 4:3, 4) Maneno ya Yehova yanapatikana katika Biblia. (2 Pet. 1:20, 21) Kwa hiyo, jambo la kwanza kabisa katika chakula ambacho Yehova anatutolea ni Biblia.—2 Tim. 3:16, 17.

Tengenezo la Yehova limefanya Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ipatikane ikiwa nzima ao sehemu katika luga zaidi ya 120, na luga nyingi zinaongezwa kila mwaka. Zaidi ya tafsiri hiyo, kuna mamilioni ya tafsiri zingine za Biblia katika maelfu ya luga zikiwa nzima ao sehemu. Kazi hiyo kubwa inapatana na mapenzi ya Yehova ambaye anapenda “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:3, 4) Na kwa sababu “hakuna kiumbe kisichokuwa wazi machoni [pa Yehova],” tunaweza kuwa na uhakika kwamba atavuta katika tengenezo lake watu “wanaotambua uhitaji wao wa kiroho,” na atawatolea chakula cha kiroho.—Ebr. 4:13; Mt. 5:3, 6; Yoh. 6:44; 10:14.

2 Vichapo vyetu vinatimiza kazi gani katika kutolea watu chakula cha kiroho?

Ili mutu akuwe na imani yenye nguvu, anapaswa kufanya mengi zaidi kuliko kusoma tu Biblia. Anapaswa kuelewa mambo ambayo anasoma na kutumikisha yale anayojifunza. (Yak. 1:22-25) Wakati wa mitume, towashi Muethiopia alifanya hivyo. Alikuwa anasoma Neno la Mungu; kisha Filipo akamuuliza hivi: “Je, wewe kwa kweli unaelewa unayoyasoma?” Towashi alimujibu: ‘Kwa kweli, ninawezaje kuelewa, mutu fulani asiponiongoza?’ (Mdo. 8:26-31) Filipo alimusaidia towashi huyo kupata ujuzi sahihi wa Neno la Mungu. Mambo ambayo towashi huyo alijifunza yalimugusa sana moyo, kwa hiyo akaamua kubatizwa. (Mdo. 8:32-38) Vilevile, vichapo vyetu vinavyotegemea Biblia vimetusaidia tupate ujuzi sahihi wa kweli. Vinatuchochea kutumikisha mambo ambayo tunajifunza.—Kol. 1:9, 10.

Tunapokea chakula cha kiroho kwa uwingi kupitia vichapo vyetu. (Isa. 65:13) Kwa mufano, gazeti Munara wa Mulinzi, ambalo linapatikana katika luga zaidi ya 210, linafasiria unabii wa Biblia, linatusaidia tuelewe vizuri zaidi mambo mazito, na linatusaidia kuishi kulingana na kanuni za Biblia. Gazeti Amuka!, ambalo linachapishwa katika luga 100 hivi, linaongeza ujuzi wetu juu ya vitu ambavyo Yehova aliumba na linatuonyesha namna ya kutumia mashauri ya Biblia. (Met. 3:21-23; Rom. 1:20) Mutumwa mwaminifu anatutolea vichapo katika luga zaidi ya 680! Je, kila siku unajiwekea wakati ili kusoma Biblia? Je, unasoma kila gazeti, na vichapo vingine ambavyo vinatolewa kila mwaka katika luga yako?

Zaidi ya vichapo, tengenezo la Yehova linatayarisha hotuba zinazotegemea Biblia ambazo zinatolewa kwenye mikutano na kwenye mikusanyiko. Je, unafurahia hotuba, michezo inayotegemea Biblia, maonyesho, na sehemu za kuuliza watu maulizo ambazo zinafanywa kwenye mikutano hiyo? Bila shaka Yehova anatutolea karamu ya kiroho.—Isa. 25:6.

 3 Ikiwa vichapo fulani havipatikane katika luga yako, je, utakosa kabisa chakula cha kiroho?

Hapana. Haishangaze kuona kwamba watumishi fulani wa Yehova wanapata chakula kingi cha kiroho kuliko wengine. Sababu gani? Tufikirie hali ya mitume. Walipata maagizo mengi zaidi kuliko wanafunzi wengine wa wakati wao. (Mk. 4:10; 9:35-37) Hata hivyo, wanafunzi hao wengine hawakukosa kabisa chakula cha kiroho ambacho walihitaji.—Efe. 4:20-24; 1 Pet. 1:8.

Pia, ni vizuri kukumbuka kwamba mambo mengi ambayo Yesu alisema na kufanya wakati alikuwa duniani hayakuandikwa katika Injili. Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Kwa kweli, kuna mambo mengine mengi pia aliyofanya Yesu, ambayo, kama yangeandikwa kirefu, nazani ulimwengu wenyewe haungeweza kuwa na nafasi ya kuviweka vitabu vya kukunjwa ambavyo vingeandikwa.’ (Yoh. 21:25) Hata kama wafuasi wa Yesu wa wakati wa mitume walijua habari nyingi juu yake, sisi pia tuna habari za lazima. Yehova amefanya yote ili tujue mambo ya lazima juu ya Yesu, na tufuate mufano wa Yesu.—1 Pet. 2:21.

Pia, fikiria barua ambazo mitume waliandikia makutaniko ya wakati wao. Inaonekana kuna barua fulani ambayo Paulo aliandika lakini barua hiyo haipatikane katika Biblia. (Kol. 4:16) Je, tunakosewa na kitu fulani kwa sababu hatuna barua hiyo? Hapana. Yehova anajua mahitaji yetu na anatutolea mambo ya lazima ili tuendelee kuwa na afya nzuri ya kiroho.—Mt. 6:8.

Yehova anajua mahitaji yetu na anatutolea mambo ya lazima ili tuendelee kuwa na afya nzuri ya kiroho

Leo, watumishi fulani wa Yehova wana chakula kingi cha kiroho kuliko wengine. Je, kuna vichapo vichache tu ambavyo vinapatikana katika luga yako? Ikiwa jibu ni ndiyo, ujue kwamba Yehova anakupenda. Ujifunze vichapo hivyo, na ikiwezekana, huzuria mikutano katika luga ambayo unaelewa. Pia, ujue kwamba Yehova ataendelea kukupatia nguvu ya kiroho.—Zab. 1:2; Ebr. 10:24, 25.

4 Je, utakuwa muzaifu kiroho ikiwa hauna uwezo wa kupata vichapo vinavyopatikana kwenye adresi yetu ya Internete jw.org?

Kwenye adresi yetu ya Internete, kuna magazeti na vichapo vingine vinavyosaidia watu kujifunza Biblia. Kwenye adresi hiyo kuna pia habari zinazosaidia bibi na bwana, vijana, na wazazi walio na watoto wadogo. Familia zinafaidika kwa kujifunza habari hizo wakati wa Ibada yao ya Familia. Tena, adresi yetu ya Internete inatoa habari za pekee; kwa mufano inatoa habari juu ya wanafunzi wanaomaliza masomo ya Gileadi, mukutano wa kila mwaka, na inajulisha ndugu duniani pote kuhusu misiba ya asili na mambo ya kisheria ambayo watu wa Yehova wanapambana nayo. (1 Pet. 5:8, 9) Tena, adresi yetu ya Internete inatusaidia katika kazi ya kuhubiri; inafanya habari njema ipatikane hata katika maeneo ambamo kazi yetu imekatazwa.

Lakini, unaweza kuendelea kuwa nguvu kiroho hata kama hauna namna ya kupata habari zilizo kwenye adresi yetu ya Internete. Mutumwa mwaminifu anafanya yote ili kuchapisha vichapo vingi ambavyo vitasaidia watumishi wote wa nyumbani kulishwa vizuri kiroho. Kwa hiyo, usiwaze kwamba unapaswa tu kununua telefone ao ordinatere inayoweza kufungua adresi yetu ya Internete. Ndugu na dada fulani wanaweza kufanya mipango ili kuchapisha habari fulani zinazopatikana kwenye adresi yetu ya Internete na kuzipatia wale ambao hawana uwezo wa kutumia Internete; lakini makutaniko hayalazimishwe kufanya hivyo.

Sisi ni wenye shukrani kwa Yesu kwa sababu anatimiza ahadi yake ya kuendelea kutuhangaikia kiroho. Kwa sababu siku hizi za mwisho zilizo ngumu zinakaribia sana kumalizika, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova ataendelea kututolea chakula cha kiroho “kwa wakati unaofaa.”