Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anatukaribia Namna Gani?

Yehova Anatukaribia Namna Gani?

‘Mukaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ YAK. 4:8.

1. Wanadamu wote wanahitaji nini, na ni nani anaweza kutimiza mahitaji hayo?

WANADAMU wana uhitaji mukubwa wa kujisikia kuwa karibu na watu wengine. Tunaweza kusema kwamba watu wanakaribiana ikiwa “wanapendana sana na wanajuana vizuri kabisa.” Kwa kawaida tunafurahi kuwa karibu na watu wa familia na marafiki ambao wanatupenda, wanatufurahia, na wanatuelewa. Lakini, Muumbaji wetu Mukubwa ndiye anapaswa kuwa rafiki yetu wa karibu zaidi.—Mhu. 12:1.

2. Yehova anatuahidi nini, lakini sababu gani watu wengi hawaamini ahadi hiyo?

2 Katika Neno lake, Yehova anatuambia ‘tumukaribie,’ na anaahidi kwamba tukimukaribia, ‘yeye pia atatukaribia.’ (Yak. 4:8) Hilo ni wazo lenye kupendeza sana. Lakini, watu wengi wanawaza kwamba haiwezekane Mungu awakaribie; wanajisikia kuwa hawastahili kumukaribia ao kwamba Mungu iko mbali sana na haiwezekane kumukaribia. Je, kweli inawezekana kumukaribia Yehova?

3. Tunapaswa kujua nini juu ya Yehova?

3 Tunapaswa kujua kwamba Yehova “hayuko mbali sana” na wale wanaotaka kumukaribia; inawezekana wanadamu wamujue Mungu. (Soma  Matendo 17:26, 27; Zaburi 145:18.) Mungu alikusudia kwamba hata wanadamu wasio wakamilifu wamukaribie; yeye iko tayari na anataka wanadamu wakuwe marafiki wake. (Isa. 41:8; 55:6) Mutunga-zaburi alijionea jambo hilo; kwa hiyo aliandika hivi: ‘Ee musikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja. Mwenye furaha ni yule unayemuchagua na kumufanya akaribie.’ (Zab. 65:2, 4) Biblia inaeleza namna Asa, mufalme wa Yuda, alimukaribia Yehova na namna Yehova alimutendea. *

MUFANO WA ZAMANI UNAOTUFUNDISHA

4. Mufano wa Asa uliwafundisha nini watu wa Yuda?

4 Mufalme Asa alionyesha bidii kubwa kwa ajili ya ibada safi kwa kuondoa ukahaba uliofanywa kwenye hekalu na ibada ya sanamu ambayo ilienea sana katika inchi. (1 Fal. 15:9-13) Aliambia watu waziwazi ‘wamutafute Yehova Mungu wa mababu zao na kutenda sheria na amri.’ Yehova alimubariki Asa, na watu waliishi kwa amani katika miaka kumi ya kwanza ya utawala wake. Mufalme Asa alijua ni nani aliwapatia amani hiyo. Aliwaambia watu hivi: ‘Inchi bado inapatikana kwa ajili yetu, kwa sababu tumemutafuta Yehova Mungu wetu. Tumemutafuta, naye anatupa pumuziko kuzunguka pande zote.’ (2 Nya. 14:1-7) Tuone namna mambo yalikuwa.

5. Ni hali gani iliyojaribu imani ya Asa, lakini alitenda namna gani?

5 Ujitie pa nafasi ya Asa. Zera, Muethiopia alikuja kushambulia Yuda akiwa na wanaume milioni moja na magari ya vita 300. (2 Nya. 14:8-10) Ingekuwa wewe ungefanya nini wakati ungeona jeshi kubwa kama hilo likishambulia ufalme wako? Jeshi lako lina maaskari 580000 tu. Unapoona kwamba hesabu ya maaskari wako ni karibu nusu ya hesabu ya maadui, ungeanza kujiuliza sababu gani Mungu aliruhusu maadui hao washambulie ufalme wako. Katika hali kama hiyo, je, ungejitumainia? Namna Asa alitenda ilionyesha kwamba alimutumainia Yehova, na kwamba alikuwa rafiki yake. Alimulilia hivi: “Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana sisi tunakuegemea wewe, nasi kwa jina lako tumekuja kupigana na umati huu. Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu. Usiache mwanadamu anayeweza kufa apate nguvu juu yako.” Mungu alijibu namna gani sala ya Asa? “Yehova akawashinda Waethiopia.” Hakuna hata mumoja kati ya maadui hao aliyeponyoka vita iliyofuata.—2 Nya. 14:11-13.

6. Mufano wa Asa unatufundisha nini?

6 Ni nini ilimusaidia Asa amutumainie kabisa Yehova na atafute muongozo na ulinzi kwake? Biblia inasema kwamba ‘Asa alifanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova’ na kwamba ‘moyo wake ulikuwa mukamilifu kwa Yehova.’ (1 Fal. 15:11, 14) Ni lazima sisi pia tumutumikie Mungu kwa moyo mukamilifu. Ni jambo la lazima sana tufanye hivyo ili tukuwe marafiki wake sasa na wakati unaokuja. Sisi ni wenye shukrani kwamba Yehova alifanya hatua ya kwanza ili kutuvuta kwake na kutusaidia tuendelee kuwa marafiki wake. Tuchunguze njia mbili ambazo Yehova ametumia ili kufanya hivyo.

YEHOVA AMETUVUTA KUPITIA ZABIHU YA UKOMBOZI

7. (a) Yehova amefanya nini ili kutuvuta kwake? (b) Ni njia gani kubwa zaidi ambayo Mungu anatumia ili kutuvuta kwake?

7 Yehova alionyesha kwamba anapenda wanadamu kwa kuwatayarishia makao mazuri, ni kusema, dunia. Anaendelea kutuonyesha upendo kwa kututimizia mahitaji yetu ya kimwili; kwa kufanya hivyo anategemeza uzima wetu. (Mdo. 17:28;  Ufu. 4:11) Jambo la lazima zaidi, Yehova anatutimizia mahitaji yetu ya kiroho. (Lu. 12:42) Anatuhakikishia pia kwamba wakati tunasali anatusikiliza. (1 Yoh. 5:14) Lakini, njia kubwa zaidi ambayo Mungu anatumia ili kutukaribia na ili tumukaribie, ni upendo ambao anatuonyesha kupitia zabihu ya ukombozi. (Soma 1 Yohana 4:9, 10, 19.) Yehova alimutuma ‘Mwana wake muzaliwa-pekee’ duniani ili tukombolewe kutoka utumwa wa zambi na kifo.—Yoh. 3:16.

8, 9. Yesu ana daraka gani katika kusudi la Yehova?

8 Yehova amefanya iwezekane hata kwa watu ambao waliishi mbele ya Kristo wafaidike na zabihu ya ukombozi. Kuanzia wakati Yehova alitabiri juu ya yule ambaye angekomboa wanadamu, kwa maoni yake, ni kama vile zabihu ya ukombozi ilikuwa imekwisha kutolewa, kwa sababu anajua kwamba kusudi lake halikose kutimia. (Mwa. 3:15) Miaka mingi baadaye, mutume Paulo alionyesha shukrani yake kwa Mungu kwa sababu ya “kuachiliwa huru kwa njia ya fidia [ao zabihu ya ukombozi] ambayo Kristo Yesu alilipa.” Paulo aliongeza hivi: Mungu ‘alikuwa akizisamehe zambi zilizotokea wakati uliopita alipokuwa akivumilia kwa subira.’ (Rom. 3:21-26) Kwa kweli, Yesu anatimiza daraka kubwa ili tuweze kumukaribia Yehova.

9 Ni kupitia Yesu tu ndiyo watu wanyenyekevu wanaweza kumujua Yehova na wanafurahia kuwa na urafiki wa karibu pamoja naye. Namna gani Maandiko yanakazia jambo hilo? Paulo aliandika hivi: ‘Mungu anapendekeza upendo wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.’ (Rom. 5:6-8) Hatukustahili kukombolewa kupitia Zabihu ya Yesu, lakini Mungu alitukomboa kwa sababu alitupenda. Yesu alisema hivi: ‘Hakuna mutu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amuvute.’ Alisema tena hivi: “Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yoh. 6:44; 14:6) Yehova anatumia roho yake takatifu ili kuvuta watu kwake kupitia Yesu, na anawasaidia wabaki katika upendo Wake ili wapate uzima wa milele. (Soma Yuda 20, 21.) Tuchunguze njia ingine ambayo Yehova anatumia ili kutuvuta kwake.

YEHOVA ANATUVUTA KUPITIA NENO LAKE

10. Namna gani mafundisho ya Biblia yanatusaidia tumukaribie Mungu?

10 Kufikia hapa, tumekwisha kurudilia ao kutaja maandiko katika vitabu 14 tofauti vya Biblia. Hatungekuwa na Biblia, namna gani tungejua kwamba tunaweza kumukaribia Muumbaji wetu? Bila Biblia, namna gani tungejifunza juu ya zabihu ya ukombozi na namna gani tungejua kwamba Yehova ametuvuta kwake kupitia Yesu? Kupitia roho yake takatifu, Yehova aliongoza kazi ya kuandika Biblia, ambayo inatuonyesha sifa zake zenye kuvutia na mambo makubwa ambayo anakusudia kufanya. Kwa mufano, katika andiko la Kutoka 34:6, 7, Yehova alijitambulisha kwa Musa kuwa ‘Mungu mwenye rehema na neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fazili zenye upendo na kweli, anayehifazi fazili zenye upendo kwa ajili ya maelfu, anayesamehe kosa na ubaya na zambi.’ Ni nani ambaye hangependa kumukaribia Mutu kama huyo? Yehova anajua kwamba tunapoendelea kujifunza juu yake kupitia Biblia, tutamuona kuwa mutu wa kweli na tutamukaribia zaidi.

11. Sababu gani tunapaswa kujikaza kujifunza sifa za Mungu na njia zake? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

11 Maneno ya utangulizi ya kitabu Mkaribie Yehova yanaeleza vizuri namna tunaweza kumukaribia Yehova Mungu; yanasema hivi: ‘Ili kuwa na urafiki na mutu yeyote, ni lazima tumujue mutu huyo, tuvutiwe na sifa zake za pekee na kuzisamini. Hivyo basi, ni jambo la maana sana kwetu kujifunza sifa na njia za Mungu za kutenda mambo, kama zinavyofunuliwa na Biblia.’ Sisi ni wenye shukrani sana kwa Yehova, kwa sababu amefanya Neno lake liandikwe kwa namna inayoeleweka wazi.

12. Sababu gani Yehova alitumia wanadamu ili kuandika Biblia?

 12 Yehova angependa, angewaomba malaika waandike Biblia. Kwa kweli, malaika wanapendezwa sana na mambo ya wanadamu. (1 Pet. 1:12) Bila shaka, malaika wangeweza kuandika ujumbe wa Mungu kwa wanadamu. Lakini, je, malaika wangeweza kabisa kuwa na maoni ya wanadamu? Je, wangeweza kuelewa mahitaji yetu, uzaifu wetu, na mambo ambayo tunapenda? Hapana; Yehova alijua kwamba kuna mambo ambayo hawangeweza kufanya. Kwa sababu Yehova alitumia wanadamu ili waandike Biblia, tunaona kuwa iliandikwa kwa ajili yetu. Tunaweza kuelewa mawazo ya waandikaji wa Biblia na ya watu wengine wanaotajwa katika Biblia, na namna walijisikia. Tunaweza kuelewa mambo yaliyowavunja moyo, yaliyowatia katika mashaka, yaliyowaogopesha; tunaweza pia kuelewa makosa yao, kufurahia mambo yaliyowafurahisha na yale waliyotimiza. Eliya, na waandikaji wa Biblia walikuwa na “hisia kama zetu [walijisikia kama sisi].”—Yak. 5:17.

Namna gani unaweza kumukaribia Mungu kwa kutafakari juu ya namna aliwatendea Yona na Petro?(Ona fungu la 13 na la 15)

13 Kwa mufano, je, malaika angeandika vizuri namna nabii Yona alijisikia wakati alikimbia mugawo ambao Yehova alimupatia? Ni jambo lenye kufaa kwamba Yehova alimuomba Yona aandike habari yake mwenyewe, vilevile sala ya kutoka moyoni ambayo alitoa alipokuwa ndani ya bahari. Yona alisali hivi: ‘Nafsi yangu ilipozimia ndani yangu, Yehova Ndiye nilikumbuka.’—Yona 1:3, 10; 2:1-9.

14. Sababu gani unapendezwa na maneno ambayo Isaya aliandika?

14 Ona pia mambo ambayo Yehova alimuambia Isaya aandike juu yake mwenyewe. Kisha kuona utukufu wa Mungu kwa njia ya muujiza, nabii Isaya alichochewa kusema hivi juu ya hali yake ya kutokamilika: ‘Ole wangu! Kwa maana ni kama nimenyamazishwa, kwa sababu mimi ni mutu asiye na midomo safi, nami ninakaa  katikati ya watu wasio na midomo safi; kwa maana macho yangu yamemuona Mufalme, Yehova wa majeshi, mwenyewe.’ (Isa. 6:5) Ni malaika gani ambaye angeweza kusema maneno hayo? Lakini Isaya aliweza kuyasema, na tunaweza kujisikia namna alijisikia.

15, 16. (a) Sababu gani tunaelewa kabisa namna wanadamu wenzetu wanajisikia? Toa mifano. (b) Ni nini itatusaidia kumukaribia Yehova?

15 Je, malaika wangeweza kusema kama Yakobo kwamba wao ‘hawastahili,’ ao wangeweza kujisikia kuwa ‘wenye zambi,’ kama Petro? (Mwa. 32:10; Lu. 5:8) Je, ‘wangeogopa,’ kama wanafunzi wa Yesu, ao je, ikiwa wangepambana na upinzani katika mahubiri, wangehitaji ‘kujipa ujasiri,’ kama vile Paulo na wenzake walifanya? (Yoh. 6:19; 1 Tes. 2:2) Hapana, malaika ni wakamilifu kabisa na wana uwezo mwingi kuliko wanadamu. Wakati wanadamu ambao hawakamilike wanajisikia namna hiyo, tunawaelewa mara moja kwa sababu sisi pia ni wanadamu. Wakati tunasoma Neno la Mungu, kwa kweli tunaweza ‘kushangilia pamoja na watu wanaoshangilia, na kulia pamoja na watu wanaolia.’—Rom. 12:15.

16 Tukifikiri sana juu ya yale ambayo Biblia inasema kuhusu namna Yehova aliwatendea watumishi wake waaminifu wa zamani, tutajifunza mambo mengi mazuri juu ya Mungu wetu, ambaye kwa uvumilivu na upendo aliwakaribia wanadamu hao wasio wakamilifu. Tukifanya hivyo, tutafikia kumujua Yehova vizuri kabisa, tutamupenda sana, na zaidi ya yote tutamukaribia.—Soma Zaburi 25:14.

KUWA RAFIKI YA MUNGU MILELE

17. (a) Azaria alimutolea Asa shauri gani nzuri? (b) Namna gani Asa alikosa kufuata shauri la Azaria, na hilo lilikuwa na matokeo gani?

17 Kisha Mufalme Asa kupata ushindi juu ya jeshi la Waethiopia, nabii Azaria alimuambia yeye na watu wake maneno fulani ya hekima. Azaria aliwaambia hivi: ‘Yehova yuko pamoja nanyi ikiwa ninyi muko pamoja naye; nanyi mukimutafuta, atawaruhusu mumupate, lakini mukimuacha yeye atawaacha ninyi.’ (2 Nya. 15:1, 2) Lakini baadaye, Asa hakufuata shauri hilo nzuri. Aliposhambuliwa na ufalme wa kaskazini wa Israeli, alitafuta musaada kwa Wasiria. Kuliko kumutumainia tena Yehova, alifanya mapatano na wapagani. Ndiyo maana, Asa aliambiwa hivi: “Umetenda kwa upumbavu kwa habari hii, kwa maana tangu sasa na kuendelea kutakuwa na vita juu yako.” Miaka iliyobaki ya utawala wa Asa ilikuwa yenye kujaa vita. (2 Nya. 16:1-9) Tunapata somo gani?

18, 19. (a) Tutafanya nini ikiwa tunatambua kwamba tumeanza kujitenga na Mungu? (b) Namna gani tunaweza kumukaribia Yehova zaidi?

18 Hatupaswe hata kidogo kujitenga na Yehova. Ikiwa tunatambua kwamba tumeanza kujitenga na Yehova, tunapaswa kutenda kupatana na andiko la Hosea 12:6, ambalo linasema: ‘Rudi kwa Mungu wako, ushike fazili zenye upendo na haki; nawe umutumaini Mungu wako sikuzote.’ Kwa hiyo, tuendelee kumukaribia Yehova zaidi kwa kufikiri sana juu ya zabihu ya ukombozi, na kujifunza kwa uangalifu Neno lake Biblia.—Soma Kumbukumbu la Torati 13:4.

19 Mutunga-zaburi aliandika hivi: ‘Kumukaribia Mungu ni kwema kwangu.’ (Zab. 73:28) Tuendelee basi kujifunza mambo mengi zaidi juu ya Yehova na kufikiria zaidi sababu zinazofanya tumupende. Tunapenda kabisa Yehova aendelee kutukaribia tangu sasa na hata milele.

^ fu. 3 Kuhusu mufalme Asa, soma habari yenye kichwa “Kuna Sawabu kwa Ajili ya Kazi Yenu,” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 8, 2012.