MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 9, 2014

Gazeti hili lina habari za kujifunza za tarehe 27 Mwezi wa 10, mupaka tarehe 30 Mwezi wa 11, 2014.

Unajitahidi “Kufikia” Madaraka?

Namna gani unaweza kufanya hivyo kwa njia inayofaa?

Sababu Gani Unaamini Kabisa Kwamba Uko Katika Kweli?

Habari hii itazungumuzia sababu zinazofanya watu fulani wakubali kwamba Mashahidi wa Yehova wako katika kweli. Inazungumuzia pia sababu zinazofanya Mashahidi wa Yehova waamini kwamba wako katika kweli.

Umutumikie Mungu kwa Uaminifu Ijapokuwa ‘Mateso Mengi’

Kila mutu anapata mateso katika ulimwengu huu unaotawaliwa na shetani. Shetani anatumia njia gani ili kutushambulia? Tunaweza kujitayarisha namna gani ili kupambana na mashambulizi hayo?

Wazazi, Muwe Wachungaji wa Watoto Wenu

Wazazi wana daraka la kuchunga watoto wao ‘katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’ (Waefeso 6:4) Habari hii inazungumuzia njia tatu zinazoweza kusaidia wazazi wawachunge watoto wao na kuwasaidia wamupende Yehova.

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maneno ya Biblia kwenye Zaburi 37:25 na yale ya Yesu kwenye Mathayo 6:33 yanamaanisha kwamba Yehova hawezi kuruhusu hata kidogo Mukristo akose chakula?

Kifo—Adui wa Mwisho Atakayeangamizwa

Kifo na mambo yanayotokeza kifo vinatesa sana wanadamu. Sababu gani wanadamu wanakufa? ‘Kifo, adui wetu wa mwisho, ataangamizwa’ namna gani? (1 Wakorintho 15:26) Majibu ya maulizo hayo yanakazia haki, hekima, na zaidi sana upendo wa Yehova.

Tusisahau Wale Wanaofanya Utumishi wa Wakati Wote

Watumishi wengi wa Yehova wanafanya kwa bidii utumishi wa wakati wote. Tunaweza kufanya nini ili kukumbuka ‘kazi yao ya uaminifu’ na ‘kazi yao ya jasho yenye upendo’?—1 Wathesalonike 1:3.