Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unajitahidi “Kufikia” Madaraka?

Unajitahidi “Kufikia” Madaraka?

NDUGU Fernando * alikuwa na wasiwasi. Wazee wawili walimuita ili wazungumuze naye. Kila mara, kisha mwangalizi wa muzunguko kutembelea kutaniko lao, wazee walimuambia mambo ambayo alipaswa kufanya ili akuwe muzee wa kutaniko. Kisha, Fernando alianza kujiuliza kama siku fulani atakuwa muzee. Mwangalizi wa muzunguko alitembelea tena kutaniko lao. Wazee walimuambia tena Fernando nini?

Fernando alisikiliza kwa hamu wakati wazee waliongea tena naye. Muzee mumoja alitumia andiko la 1 Timotheo 3:1 na kusema kwamba baraza la wazee lilipokea barua ya kukubali Fernando kuwa muzee wa kutaniko. Mara moja Fernando alisimama na kuuliza hivi: “Unasema nini?” Muzee huyo akarudilia yale ambayo alisema; mara moja Fernando akaonekana kuwa na sura yenye furaha. Kisha, wakati kutaniko lilijulishwa, ndugu na dada wote walifurahi.

Je, ni mubaya ikiwa ndugu anapenda kupata madaraka katika kutaniko? Hapana. Andiko la 1 Timotheo 3:1 linasema hivi: ‘Ikiwa mwanaume yeyote anajitahidi [ao anajikaza] kufikia cheo cha [ao kazi ya] mwangalizi, yeye anatamani kazi njema.’ Maneno hayo yanatia ndugu wengi moyo na wanafanya kabisa maendeleo ya kiroho ili wastahili kupewa mapendeleo katika kutaniko. Jambo hilo linakuwa na matokeo mazuri, kwa sababu tunakuwa na wazee na watumishi wa huduma wengi sana wenye uwezo. Lakini, kwa sababu makutaniko yanaendelea kuongezeka, kuna lazima ya ndugu wengi wanaopaswa kujikaza ili kuwa wazee ao watumishi wa huduma. Namna gani ndugu wanaweza kujikaza kufikia madaraka? Je, wale wanaotaka kuwa wazee, wanapaswa kuogopa, kama ndugu Fernando?

‘KUJITAHIDI’ KUNAMAANISHA NINI?

Neno ‘kujitahidi [ao kujikaza] linatokana na neno la Kigiriki ambalo linamaanisha kutamani sana, kunyorosha mukono ili kukamata kitu fulani. Pengine hilo linafanya ufikirie  mutu anayenyorosha mukono ili kuchuma tunda lenye kumuvutia lililo kwenye muti. Lakini kujikaza kufikia madaraka hakumaanishe kuwa na tamaa isiyofaa ya kutafuta kuwa muzee. Sababu gani? Kwa sababu wale wanaotaka kuwa wazee wanapaswa kuwa na nia ya kufanya ‘kazi njema,’ ni kusema, kutumikia wengine, lakini hawapaswe kuona kama kupata madaraka kunawafanya kuwa wa maana sana kuliko wengine.

Mambo ambayo mutu anapaswa kutimiza ili kuwa muzee, yanapatikana katika andiko la 1 Timotheo 3:2-7 na Tito 1:5-9. Kuhusu kanuni zinazopatikana katika maandiko hayo, ndugu mumoja ambaye amekuwa muzee kwa miaka mingi alisema hivi: “Ninaona kwamba, jambo la maana zaidi ni kuwa na sifa nzuri. Kujua kusema na kufundisha ni mambo ya maana, lakini kuna sifa zingine za lazima sana; kwa mufano, muzee anapaswa kuwa mutu asiyelaumika, mwenye kiasi katika mazoea, mwenye utimamu wa akili ao akili nzuri, mwenye utaratibu, mukaribishaji-wageni, na mwenye usawaziko.”

‘Ujikaze’ kufikia madaraka kwa kusaidia kutaniko kwa njia mbalimbali

Ndugu ambaye anapenda kufikia madaraka, anajikaza kuwa mutu asiyelaumika kwa kuepuka kila namna ya udanganyifu na mwenendo muchafu. Ni mwenye kiasi katika mazoea, anatumia akili nzuri, ni mwenye utaratibu na usawaziko; kwa hiyo, ndugu na dada wanatumaini kwamba anaweza kusimamia vizuri kutaniko na kutoa musaada unaofaa wakati wa magumu. Kwa sababu ni mukaribishaji-wageni, anaweza kutia moyo vijana, na wapya katika kweli. Anafariji na kusaidia wagonjwa na wazee-wazee kwa sababu anapenda wema. Anaonyesha sifa hizo katika maisha yake; hafanye hivyo kwa sababu tu anataka kupata madaraka, lakini kwa sababu anapenda kusaidia wengine. *

Wazee wako tayari kutoa mashauri na vitia-moyo, lakini ni ndugu ambaye anataka kufikia madaraka ndiye anapaswa kujikaza kutimiza mambo yanayoombwa. Ndugu Henry, muzee mwenye uzoefu, anasema hivi: “Ikiwa unataka kufikia madaraka, tumika kwa bidii ili kuonyesha kwamba unastahili.” Anataja andiko la Mhubiri 9:10, ambalo linasema hivi: “‘Yote ambayo mukono wako unapata kufanya, uyafanye kwa nguvu zako zote.’ Kazi yoyote ambayo wazee wanakuomba ufanye, ujikaze kuifanya kwa moyo wote. Furahia kila kazi ambayo unapewa katika kutaniko, hata kama ni ya kusafisha Jumba la Ufalme. Kisha muda fulani, kazi yako na bidii yako vitaonekana wazi.” Ikiwa unapenda kuwa muzee, tumika kwa bidii, ujikaze kuwa mutu mwenye kutumainika katika kila kazi ambayo unapewa katika kutaniko. Ujikaze pia kuwa munyenyekevu  na kuepuka tamaa isiyofaa ya kupata mamlaka.—Mt. 23:8-12.

EPUKA KABISA MAWAZO NA MATENDO YASIYOFAA

Ndugu fulani wanaotaka kupata madaraka wanaweza kuanza kujionyesha kwamba wanastahili, ao kujaribu kushawishi wazee ili wawapendekeze. Wengine hawafurahi wakati wazee wanawashauria. Ndugu hao wanapaswa kujiuliza hivi: ‘Je, ninatafuta faida zangu, ao ninaona kwamba ni pendeleo kubwa sana kuchunga kondoo za Yehova?’

Wale wanaojikaza kufikia madaraka, hawapaswe kusahau jambo lingine linaloombwa kwa wazee, ni kusema, “kuwa vielelezo [ao mifano] kwa kundi.” (1 Pet. 5:1-3) Ndugu ambaye ni mufano kwa kutaniko anaepuka mawazo yasiyofaa na matendo ya udanganyifu. Anajikaza kuwa muvumilivu iwe amepewa madaraka ao hapana. Kuwa muzee hakumaanishe kwamba mutu hawezi tena kufanya makosa. (Hes. 12:3; Zab. 106:32, 33) Hata ikiwa ndugu ‘hafahamu chochote juu yake mwenyewe,’ wengine wanaweza kuwa na sababu zinazowafanya wakuwe na maoni yasiyofaa juu yake. (1 Kor. 4:4) Kwa hiyo, ikiwa wazee wanakutolea mashauri ya Biblia, usisirike, lakini ujikaze kusikiliza. Kisha ujikaze kutumikisha mashauri waliyokutolea.

UTAFANYA NINI IKIWA MADARAKA YANAKAWIA?

Ndugu fulani wanangojea muda murefu sana mbele ya kupata madaraka. Ikiwa umengojea kwa miaka mingi ili ‘ufikie kazi ya mwangalizi’, je, wakati fulani hilo linakusumbua? Ikiwa ni hivyo, kumbuka maneno haya yaliyoongozwa na roho ya Mungu: ‘Tarajio lililocheleweshwa linafanya moyo kuwa mugonjwa, lakini kitu kinachotamaniwa kinapokuja ni muti wa uzima.’—Met. 13:12.

Mutu anaweza kuvunjika moyo sana ikiwa anaona kwamba muradi wake unakawia kutimia. Abrahamu alijisikia hivyo. Yehova aliahidi kumupatia mutoto, lakini miaka mingi ilipita mbele Yehova atimize ahadi hiyo. (Mwa. 12:1-3, 7) Wakati alikuwa muzee sana, Abrahamu alimulilia Yehova hivi: ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, utanipa nini, kwa sababu mimi ninaenda zangu bila mutoto. Haukunipa uzao wowote.’ Yehova alimuhakikishia kwamba atatimiza ahadi hiyo. Lakini kulipita tena miaka 14 hivi mbele Mungu atimize ahadi yake.—Mwa. 15:2-4; 16:16; 21:5.

Je, wakati Abrahamu alikuwa anangojea, alipoteza furaha yake ya kumutumikia Yehova? Hapana. Hakuwa na mashaka hata kidogo juu ya ahadi ya Mungu. Aliendelea tu kungojea. Mutume Paulo aliandika hivi: “Baada ya Abrahamu kuonyesha subira [ao uvumilivu], aliipata ahadi hiyo.” (Ebr. 6:15) Mwishowe, Mungu Mweza-yote alimubariki mwanaume huyo mwenye imani kwa njia ambayo hakutazamia. Mufano wa Abrahamu unaweza kukufundisha nini?

Ikiwa unapenda kuwa muzee wa kutaniko lakini kumepita sasa miaka mingi, endelea tu kumutumainia Yehova. Usipoteze furaha yako ya kumutumikia. Ndugu Warren, ambaye amesaidia ndugu wengi wafanye maendeleo ya kiroho, anasema hivi: “Mutu anatimiza hatua kwa hatua sifa za kustahili kupata madaraka. Inafaa wakati upite ili uwezo wa ndugu na sifa zake vionekane. Mambo hayo yanaonekana kupitia namna  ndugu huyo anajiendesha na namna anatimiza migawo yake. Ndugu fulani wanawaza kama wanapaswa tu kupata madaraka katika kutaniko ili wakuwe na furaha. Kufikiri hivyo ni kujidanganya na kunafanya mutu afikirie madaraka kupita kiasi. Iwe unatimiza mugawo gani unapomutumikia Yehova, ukitimiza mugawo huo kwa uaminifu, utakuwa na furaha.”

Ndugu mumoja alingojea miaka zaidi ya kumi mbele akubaliwe kuwa muzee. Anasema kwamba Ezekieli sura ya 1 ilimufundisha kwamba “Yehova anaongoza gari lake, ni kusema, tengenezo lake, kwa mwendo anaochagua. Jambo la lazima ni namna Yehova anapanga wakati, lakini si namna sisi tunapanga wakati. Kwa hiyo, ninaweza kuwa muzee ao hapana; haitegemee tu mapenzi yangu, kwa sababu inawezekana mimi nipende jambo fulani, lakini Yehova anaona kwamba sihitaji kabisa jambo hilo.”

Ukipenda kuwa muzee siku fulani, ujikaze kufikia daraka hilo kwa kusaidia kutaniko lenu likuwe na furaha. Ukiona kwamba madaraka yanakawia, usisumbuke; endelea tu kuvumilia. Ndugu Raymond, ambaye tumetaja katika habari hii, anasema hivi: “Tamaa isiyofaa ya kupata mamlaka inazuia mutu kuwa na furaha. Wale ambao siku zote wanajisumbua-sumbua kwa sababu madaraka yanakawia, wanapoteza furaha ya kumutumikia Yehova.” Onyesha sehemu zote za tunda la roho ya Mungu katika maisha yako, zaidi sana uvumilivu. Ujikaze kutengeneza hali yako ya kiroho kupitia funzo lako la Biblia. Endelea kuhubiri kwa bidii na kujifunza Biblia na watu wanaopendezwa. Saidia familia yako ipendezwe na utendaji mbalimbali wa kiroho, na ibada ya familia. Tumia kila nafasi uliyo nayo ili kuwa pamoja na ndugu na dada. Unapojikaza kufikia daraka lako, utaendelea kumutumikia Yehova kwa furaha.

Kujikaza kufikia madaraka katika kutaniko ni jambo lenye kuleta furaha. Yehova na tengenezo lake hawapendi kuwaona wale wanaojikaza kufikia madaraka wapoteze furaha yao ya kumutumikia. Mungu anategemeza na kubariki wale wote wanaomutumikia kwa nia njema. Bila shaka, Yehova, ‘haongeze maumivu pamoja [na baraka yake].’—Met. 10:22.

Hata kama unajikaza tangu zamani kufikia madaraka, endelea kufanya maendeleo ya kiroho. Kwa sababu unajikaza kuonyesha sifa za kiroho, unatumika kwa bidii katika kutaniko na unashugulikia familia yako, Yehova hatasahau yote ambayo unafanya. Iwe umepewa mugawo gani katika kutaniko, endelea kumutumikia Yehova kwa furaha.

^ fu. 2 Majina fulani yamebadilishwa.

^ fu. 8 Kanuni ambazo zinazungumuziwa katika habari hii zinahusu pia wale wanaotaka kuwa watumishi wa huduma. Mambo yenye wanapaswa kutimiza inapatikana katika andiko la 1 Timotheo 3:8-10, 12, 13.