Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani Unaamini Kabisa Kwamba Uko Katika Kweli?

Sababu Gani Unaamini Kabisa Kwamba Uko Katika Kweli?

‘Mujihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.’ROM. 12:2.

1. Viongozi wa dini zinazojiita kuwa za Kikristo wametenda namna gani wakati wa vita?

JE, MUNGU anataka Wakristo wapigane vita na kuua watu wa inchi zingine? Watu wanaojiita kuwa Wakristo wamefanya jambo hilo katika miaka 100 ambayo imepita. Viongozi wa dini ya Katoliki wamebariki maaskari na silaha zao ili waende kupigana vita na Wakatoliki wa inchi zingine. Hata viongozi wa kanisa la Kiprotestanti wamefanya hivyo. Hilo lilitokeza mauaji makubwa wakati wa Vita ya 2 ya Dunia.

2, 3. Mashahidi wa Yehova walikuwa na musimamo gani wakati wa Vita ya 2 ya Dunia na wakati wa vita zingine, na sababu gani?

2 Mashahidi wa Yehova walitenda namna gani wakati huo? Historia inaonyesha kwamba hawakuunga mukono upande wowote. Sababu gani walitenda hivyo? Sababu kubwa ni kwamba walifuata mufano wa Yesu na mafundisho yake. Yesu alisema hivi: ‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukiwa na upendo kati yenu wenyewe.’ (Yoh. 13:35) Walichukua kwa uzito kanuni inayopatikana katika maneno ambayo mutume Paulo aliandikia kutaniko la Korintho.—Soma 2 Wakorintho 10:3, 4.

3 Kwa sababu Wakristo wa kweli wanafuata mafundisho ya Biblia, hawajifunze vita, wala hawakubali kupigana wakati wa  vita. Maelfu ya Mashahidi wa Yehova, iwe ni wakubwa ao vijana wadogo, wanaume ao wanawake, wamepata mateso makubwa kwa sababu ya musimamo wao wa kikristo. Wengi wameteswa katika kambi za kazi ya kulazimishwa ao katika magereza. Wengine hata waliuawa wakati wa utawala wa Wanazi katika inchi ya Ujerumani. Hata kama walipata mateso hayo makali katika Ulaya, Mashahidi wa Yehova hawakuacha kazi yao ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Yehova. Waliendelea kuhubiri katika magereza, katika makambi ya mateso, ao walipopelekwa katika inchi za kigeni. * Pia, hawakuunga mukono upande wowote wakati wa mauaji ya kikabila yaliyofanyika katika inchi ya Rwanda, katika mwaka wa 1994. Wala hawakuunga mukono upande wowote katika vita iliyotokea katika eneo la Balkans, wakati utawala wa Yugoslavia ya zamani ulianguka.

4. Kwa sababu Mashahidi wa Yehova hawajiingize katika mambo ya vita, hilo limekuwa na matokeo gani juu ya watu wanaotutazama?

4 Kwa sababu Mashahidi wa Yehova hawajiingize katika mambo ya vita, watu wengi sana wameamini kwamba Mashahidi wanapenda kabisa Mungu, na wanapenda pia wanadamu wenzao. Jambo hilo linaonyesha kwamba wao ni Wakristo wa kweli. Kuna mambo mengine ambayo yanaonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli.

KAZI KUBWA ZAIDI YA KUFUNDISHA

5. Ni jambo gani ambalo Wanafunzi wa kwanza-kwanza wa Yesu waliona kuwa jipya?

5 Wakati Yesu alianza kuhubiri duniani, alionyesha kwamba ni lazima sana habari njema ya Ufalme wa Mungu ihubiriwe. Alichagua wanafunzi 12 ili kuanzisha kazi ya kuhubiri ambayo ingeenea katika dunia yote; kisha, alizoeza wanafunzi wengine 70. (Lu. 6:13; 10:1) Wanafunzi hao walizoezwa ili wahubirie kwanza Wayahudi, kisha wahubirie watu wengine. Lakini jambo la kushangaza ni kwamba baadaye, wangeenda kuhubiria hata watu wa mataifa wasiotahiriwa. Ni kweli kwamba wanafunzi wa Yesu ambao walikuwa Wayahudi waliona hilo kuwa jambo jipya.—Mdo. 1:8.

6. Ni jambo gani lilimusaidia Petro atambue kwamba Mungu hana ubaguzi?

6 Mutume Petro alitumwa kwa Kornelio ambaye alikuwa Mutu wa Mataifa asiyetahiriwa. Petro alitambua kwamba Mungu hana ubaguzi. Kornelio na watu wa familia yake walibatizwa. Ukristo ulikuwa umeanza kuenea katika maeneo mapya. Watu wa mataifa yote wangeweza kusikia kweli na kuikubali. (Mdo. 10:9-48) Sasa, habari njema ilipaswa kuhubiriwa katika dunia yote.

7, 8. Tengenezo la Yehova limefanya mipango gani inayosaidia watu? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

7 Wale ambao leo wanaongoza kazi ya Mashahidi wa Yehova wamefanya yao yote ili habari njema ya Ufalme ifikie watu katika dunia yote. Leo, Mashahidi wa Yehova karibu milioni 8 wanajikaza sana ili kujulisha watu ujumbe wa Kristo katika luga zaidi ya 600, na hesabu hiyo inaendelea kuongezeka. Mashahidi wa Yehova wanajulikana sana kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, ao katika barabara; wakati fulani wanatia vichapo kwenye meza ao katika kitu fulani cha kukokota.

8 Mashahidi wa Yehova zaidi ya 2900 wamezoezwa ili kutafsiri Biblia na vichapo vinavyosaidia watu kuelewa Biblia. Hawatafsiri tu katika luga kubwa-kubwa. Wanatafsiri pia katika luga ambazo hazijulikane  sana, lakini ambazo zinasemwa na watu wengi. Kwa mufano, katika inchi ya Uhispania, kuna watu wengi wanaosema luga ya Catalan, luga yao ya kizalikio. Katika miaka ya hivi karibuni, watu wengi walianza tena kusema luga ya Catalan; lakini katika maeneo ya Andorra, Alicante, visiwa vya Balearic, na Valencia, ilikuwa inasemwa tofauti kidogo. Mashahidi wa Yehova wanatoa vichapo katika luga ya Catalan, wanafanya pia mikutano ya Kikristo katika luga hiyo, na jambo hilo linafurahisha sana watu wanaosema luga hiyo.

9, 10. Ni jambo gani linaloonyesha kwamba tengenezo la Yehova linapenda kabisa kusaidia watu kiroho?

9 Mipango hiyo imefanywa pia katika sehemu zingine za dunia. Katika inchi ya Meksiko, watu wanazungumuza Kihispania (Espagnol), lakini kuna vikundi vikubwa vya watu wanaosema luga zingine. Kikundi kimoja ni cha Wamaya. Biro ya tawi ya Meksiko ilihamishia watafsiri wa luga ya Maya katika eneo ambamo wangeweza kusema luga hiyo, na kusikia namna watu wanaiongea. Mufano mwengine ni juu ya luga ya Nepali, ambayo inazungumuzwa katika inchi ya Nepali, iliyo na wakaaji zaidi ya milioni 29. Watu katika inchi hiyo wanasema luga karibu 120, lakini kuna watu zaidi ya milioni 10 wanaosema luga ya Nepali, na wengine wengi wanatumia luga hiyo, hata kama wanazungumuza luga ingine. Vichapo vyetu vinatolewa pia katika luga hiyo.

10 Tengenezo la Yehova linachukua kwa uzito kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme katika dunia yote. Hilo linaonekana wazi kupitia kazi kubwa ambayo watafsiri wanatimiza. Katika dunia yote, watu wanapewa mamilioni ya trakte, broshua, na magazeti bila kuwalipisha feza. Feza za kusaidia kazi hiyo iendelee ni michango ya kujipendea ambayo Mashahidi wa Yehova wanatoa. Wanatenda kulingana na maneno haya ya Yesu: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’—Mt. 10:8.

Watafsiri hawa wanatayarisha vichapo katika luga ya Bas-Allemand(Ona fungu la 10)

Vichapo vya luga ya Bas-Allemand vinasaidia sana katika inchi ya Paraguay(Ona pia picha mwanzoni mwa habari hii)

11, 12. Kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri katika dunia yote, imekuwa na matokeo gani mazuri juu ya watu wengine?

11 Kwa kuwa wanajitoa katika kazi ya kuhubiri na kufundisha watu, Mashahidi wa Yehova wanaamini kabisa kwamba wako katika kweli, na wanafanya yao yote ili kuhubiria watu wa mataifa mengine. Mashahidi wengi wanaishi maisha mepesi, wamejifunza luga zingine, ao wanajifunza kuishi maisha ambayo hawakuzoea, ili tu waweze kufanya kazi hiyo ya maana sana. Kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri katika dunia yote  imesaidia watu wengi waamini kwamba Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli.

12 Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi hiyo yote kwa sababu wanaamini kabisa kwamba wako katika kweli. Lakini ni mambo gani mengine ambayo yanasadikisha watu kwamba Mashahidi wa Yehova wako katika kweli?—Soma Waroma 14:17, 18.

MAMBO AMBAYO YAMEWASADIKISHA

13. Namna gani Mashahidi wa Yehova wanajikaza ili tengenezo liendelee kuwa safi?

13 Tunaweza kufaidika sana kwa kusikia maelezo ya Wakristo fulani wa siku zetu ambao wanaamini kabisa kwamba wako katika kweli. Ndugu mumoja ambaye ametumikia Yehova kwa miaka mingi alisema hivi: “Mambo yote ya lazima yanafanywa ili tengenezo la Yehova liendelee kuwa safi, hata kama inafaa kushauria mutu ao kumurekebisha.” Ni nini inawezesha jambo hilo? Ni kufuata kanuni zilizo katika Neno la Mungu, na mufano muzuri ambao Yesu na wanafunzi wake walituachia. Kwa hiyo, katika siku hizi, ni watu wachache sana ndio wanatengwa na kutaniko kwa sababu wanakataa kuishi kulingana na kanuni za Mungu. Hesabu kubwa sana ya Mashahidi wa Yehova, hata wale ambao zamani walikuwa na maisha yasiyopendeza Mungu, wanaendelea kuishi wakiwa na mwenendo muzuri sana.—Soma 1 Wakorintho 6:9-11.

14. Watu wengi ambao walitengwa wamefanya mabadiliko gani, na hilo limekuwa na matokeo gani?

14 Biblia inasema kwamba wale wanaokataa kumutii Mungu wanapaswa kutengwa na kutaniko. Jambo la kufurahisha ni kwamba wengi kati yao wametubu, wameacha matendo yao mabaya na wamerudishwa katika kutaniko. (Soma 2 Wakorintho 2:6-8.) Kufuata kanuni za Biblia kunasaidia tengenezo letu likuwe safi, na hilo linafanya watu wengine watutumainie. Kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanafuata kanuni za Mungu, wako tofauti kabisa na dini zingine ambazo zinaacha watu wafanye mambo mabaya; na jambo hilo limesadikisha watu wengi kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wanaoishi kulingana na mafundisho ya Biblia.

15. Ni nini inamusadikisha ndugu mumoja kwamba iko katika kweli?

15 Sababu gani Mashahidi wenye uzoefu wanaamini kwamba wako katika kweli? Ndugu mumoja aliye na miaka 54 anaeleza hivi: “Tangu ujana wangu, imani yangu imetegemea mambo tatu ya musingi, ni kusema, (1) Mungu iko; (2) ni yeye aliongoza watu ambao waliandika Biblia; na (3) leo, anatumia kutaniko la Kikristo la Mashahidi wa Yehova, na analibariki. Ninapoendelea kujifunza, sikuzote ninachunguza mambo hayo tatu na kujiuliza ikiwa ni ya kweli. Ninapoendelea kuchunguza mambo hayo kila siku, imani yangu inakuwa nguvu zaidi na ninasadiki kabisa kwamba tuko katika kweli.”

16. Ni jambo gani limemusadikisha dada mumoja kwamba iko katika kweli?

 16 Dada mumoja aliyeolewa, na ambaye anatumikia kwenye makao makubwa huko New York, anasema kwamba ni tengenezo la Yehova tu ndilo linaendelea kutangaza jina la Yehova ambalo linapatikana mara 7000 hivi katika Biblia. Dada huyo anasema hivi: “Ninatiwa moyo na andiko la 2 Mambo ya Nyakati 16:9 ambalo linasema hivi: ‘Macho ya Yehova yanaenda huku na huku duniani kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo wao ni mukamilifu kumuelekea yeye.’” Dada huyo anaendelea kusema hivi: “Kweli imenisaidia kujua namna ya kuwa na moyo kamili ili Yehova aweze kunionyesha nguvu zake. Ninaona urafiki wangu pamoja na Yehova kuwa jambo la maana zaidi katika maisha yangu. Tena ninapendezwa na daraka la Yesu la kutusaidia tumujue vizuri Mungu, na hilo linanitegemeza sana.”

17. Mutu mumoja ambaye zamani aliamini kwamba hakuna Mungu, amefikia kuamini nini leo, na sababu gani?

17 Mutu fulani, ambaye hapo zamani aliamini kwamba hakuna Mungu, anasema hivi: “Uumbaji unanihakikishia kwamba Mungu anataka watu wafurahie maisha; kwa hiyo, hataruhusu mateso yaendelee milele. Watu wa ulimwengu wanapoendelea kuzama katika mabaya, watumishi wa Yehova wanaendelea kuonyesha imani, bidii, na upendo. Ni roho ya Yehova ndiyo inafanya jambo hilo lenye kushangaza sana liwezekane.”—Soma 1 Petro 4:1-4.

18. Sababu gani ndugu wawili wameamini kwamba wako katika kweli, na wewe unajisikia namna gani unapofikiria maneno yao?

18 Shahidi mwengine ambaye amemutumikia Yehova kwa miaka mingi anatoa sababu zinazomufanya aamini kwamba iko katika kweli; anasema hivi: “Kujifunza kwa muda wa miaka mingi kumenisadikisha kwamba Mashahidi wa Yehova wamejikaza sana ili kufuata mufano wa Wakristo wa wakati wa mitume. Niliposafiri katika inchi mbalimbali, nilijionea umoja wa Mashahidi wa Yehova wa duniani pote. Kweli ya Biblia imenifanya nitosheke na nikuwe na furaha.” Wakati ndugu mumoja aliye na miaka zaidi ya 60 aliulizwa sababu gani anaamini kwamba iko katika kweli, alitia mukazo juu ya Yesu Kristo, kwa kusema: “Tumejifunza kwa uangalifu maisha ya Yesu na mambo aliyotimiza alipokuwa duniani, na tunafurahia mufano wake. Tumefanya mabadiliko katika maisha yetu ili tumukaribie Yehova kupitia Yesu Kristo. Tumetambua kwamba watu watakombolewa kupitia zabihu ya ukombozi ya Kristo. Na tunajua kwamba alifufuliwa kutoka kwa wafu. Tuko na ushuhuda wa watu wengi waliojionea jambo hilo.”—Soma 1 Wakorintho 15:3-8.

TUWASAIDIE WENGINE WAJUE KWELI

19, 20. (a) Mutume Paulo alikazia jambo gani ili kusaidia Wakristo wa kutaniko la Roma wafikiri? (b) Sisi Mashahidi wa Yehova tuko na pendeleo gani?

19 Sisi Mashahidi wa Yehova tunapenda wanadamu wenzetu; kwa hiyo, tunapenda wao pia wajue kweli. Ili kuwasaidia Wakristo wa kutaniko la Roma wafikiri, mutume Paulo alisema hivi: ‘Ukitangaza waziwazi lile neno lililo katika kinywa chako mwenyewe, kwamba Yesu ni Bwana, na kuonyesha imani moyoni mwako kwamba Mungu alimufufua kutoka kwa wafu, utaokolewa. Kwa maana kwa moyo mutu anaonyesha imani kwa ajili ya uadilifu, lakini kwa kinywa mutu anafanya tangazo la waziwazi kwa ajili ya wokovu.’—Rom. 10:9, 10.

20 Sisi Mashahidi wa Yehova tunaamini kabisa kwamba tuko katika kweli, na tuko na pendeleo la kuhubiria wengine habari njema ya Ufalme wa Mungu. Tunapoendelea kufanya kazi hiyo, tunataka wengine wapendezwe na mambo ambayo tunawafundisha, lakini pia wajionee kwamba tunaamini kabisa mambo hayo.

^ fu. 3 Ona kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu, ukurasa wa 190-198, na 448-454.