Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unapaswa Kubadilisha Mawazo Yako?

Unapaswa Kubadilisha Mawazo Yako?

VIJANA fulani Wakristo wanaamua kuenda kuangalia filme. Wamesikia kwamba vijana wengine wengi kwenye masomo waliifurahia sana. Wakati wanafika kwenye chumba cha kuonyeshea filme hiyo, wanaona kwenye vibao vya matangazo picha za silaha na za wanawake wenye kuvaa vibaya. Watafanya nini? Wataamua tu kuingia ili kuangalia filme hiyo?

Hali hiyo inaonyesha kwamba maamuzi yenye tunafanya inaweza kuwa na matokeo mazuri ao mabaya juu ya hali yetu ya kiroho na pia juu ya urafiki wetu pamoja na Yehova. Wakati fulani, unaweza kupanga kufanya jambo fulani, lakini kisha kufikiria tena jambo hilo, unaamua kubadilisha mawazo yako. Je, kufanya hivyo kutaonyesha kwamba hauna musimamo, ao je, ni lazima wakati fulani kubadilisha mawazo yako?

Wakati Haifae Kubadilisha Mawazo Yako

Upendo wetu kwa Yehova ndio ulituchochea kujitoa kwake na kubatizwa. Tunatamani sana kuendelea kuwa waaminifu kwa Mungu. Hata hivyo, adui yetu Shetani Ibilisi ameazimia kuvunja uaminifu wetu. (Ufu. 12:17) Tumeamua kumutumikia Yehova na kushika amri zake. Kwa kuwa tumeamua kujitoa kwa Yehova, itakuwa vibaya sana ikiwa tunabadilisha mawazo yetu! Hilo linaweza kufanya tupoteze uzima wetu.

Zaidi ya miaka 2600 iliyopita, Mufalme Nebukadneza wa Babiloni alifanya sanamu kubwa ya zahabu na akaamuru watu wote waiinamie na kuiabudu. Mutu yeyote mwenye angekataa kufanya hivyo angetupwa katika tanuru la moto. Lakini, Shadraki, Meshaki, na Abednego, vijana watatu ambao walikuwa waabudu wa Yehova, walikataa kufanya hivyo. Kwa sababu hawakuinamia sanamu hiyo, walitupwa katika tanuru la moto. Yehova aliwaokoa kwa njia ya muujiza, lakini walikuwa tayari kutia uzima wao katika hatari kuliko kuvunja uamuzi wao wa kumutumikia Mungu.—Dan. 3:1-27.

 Baadaye, nabii Danieli aliambiwa kwamba ikiwa anaendelea kusali kwa Yehova, atatupwa katika shimo la simba. Lakini kama kawaida, aliendelea kusali kwa Yehova mara tatu kwa siku. Danieli hakuvunja uamuzi wake wa kumuabudu Mungu wa kweli. Baadaye, nabii Danieli aliokolewa “kutoka katika makucha ya simba.”—Dan. 6:1-27.

Leo pia, watumishi wa Yehova wanaishi kulingana na uamuzi wao wa kujitoa kwake. Katika inchi moja ya Afrika, wanafunzi fulani ambao ni Mashahidi wa Yehova walikataa kuabudu alama ya taifa. Waliambiwa kwamba watafukuzwa kwenye masomo ikiwa wanakataa kujiunga na wanafunzi wengine ili kuabudu alama hiyo. Muda mufupi kisha hapo, waziri anayesimamia mambo ya masomo alitembelea muji wao na akazungumuza na wanafunzi fulani Mashahidi. Vijana hao Mashahidi walieleza musimamo wao kwa heshima na bila kuogopa. Kuanzia wakati huo, jambo hilo halikutokea tena. Sasa, ndugu na dada vijana wanaenda kwenye masomo bila kuogopa kwamba watashawishiwa kuvunja urafiki wao pamoja na Yehova.

Tufikirie pia mufano wa ndugu Joseph, ambaye bibi yake aligonjwa kansere na akakufa bila kukawia. Watu wa familia ya ndugu Joseph walimuelewa na walikubali bibi yake azikwe kulingana na imani yake. Lakini, watu wa familia ya bibi yake hawakuwa Mashahidi, na walitaka kufuata desturi zenye kumuchukiza Mungu. Ndugu Joseph anasema hivi: “Kwa sababu nilikataa kubadilisha mawazo yangu, walijaribu kushawishi watoto wangu; lakini wao pia walikataa kabisa. Watu wa jamaa walipenda pia kufanya makesha nyumbani kwangu kulingana na desturi zao; lakini niliwaambia kwamba ikiwa wanapenda tu kufanya makesha, wanapaswa kutafuta mahali pengine pa kuifanyia. Walijua vizuri kwamba kufanya makesha hakulingane na imani yetu; kwa hiyo, kisha kubishana sana nao waliamua kufanya makesha hayo mahali pengine.

“Wakati huo mugumu, nilimuomba sana Yehova asaidie familia yetu ili tusivunje sheria zake. Alisikiliza sala zangu na alitusaidia tubaki waaminifu ijapokuwa mikazo.” Kwa sababu jambo hilo lilihusu ibada yao kwa Yehova, ndugu Joseph na watoto wake walikataa kubadilisha mawazo yao.

Wakati Unaweza Kubadilisha Mawazo Yako

Muda mufupi kisha Pasaka ya mwaka wa 32, mwanamuke mumoja wa taifa la Sirofoinike alimuendea Yesu Kristo katika eneo la Sidoni. Aliendelea kumuomba Yesu afukuze roho muovu ambaye alikuwa anamusumbua binti yake. Kwanza, Yesu hakumuambia neno lolote. Yesu akawaambia wanafunzi wake hivi: “Sikutumwa kwa wowote ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” Wakati mwanamuke huyo aliendelea kumuomba, Yesu alimuambia hivi: ‘Si sawa kuuchukua mukate wa watoto na kuwatupia imbwa wadogo.’ Kwa sababu mwanamuke huyo alionyesha imani kubwa, alimujibu Yesu hivi: ‘Ndiyo, Bwana; lakini kwa kweli hao imbwa wadogo wanakula sehemu ya makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza ya mabwana zao.’ Yesu alijibia ombi la mwanamuke huyo na akamuponyesha binti yake.—Mt. 15:21-28.

Kwa kufanya hivyo, Yesu alimuiga Yehova kwa kuwa tayari kubadilika kulingana na hali. Kwa mufano, wakati Waisraeli walifanya ndama ya zahabu, Mungu alipanga kuwaangamiza kabisa; lakini wakati Musa alimusihi afikirie uamuzi Wake, Yehova alikubali.—Kut. 32:7-14.

Mutume Paulo alimuiga Yehova na Yesu. Kwa muda fulani, mutume Paulo aliona kwamba hangeweza kuenda pamoja na Yohana Marko katika safari zake za umisionere kwa sababu, katika safari ya kwanza ya umisionere Marko alimuacha Paulo na Barnaba. Lakini kisha hapo, mutume Paulo alitambua kwamba Marko alijitoa mwenyewe na kwamba atakuwa wa lazima sana kwake. Ndio maana mutume Paulo alimuambia Timotheo hivi: ‘Umuchukue Marko na ukuje pamoja naye, kwa maana yeye ni mwenye faida kwangu kwa ajili ya huduma.’—2 Tim. 4:11.

Halafu sisi? Tukimuiga Baba yetu wa mbinguni mwenye rehema, subira, na upendo,  tunaweza kuona kwamba ni jambo lenye kufaa kubadilisha mawazo yetu. Kwa mufano, tunaweza kubadilisha mawazo yetu kuelekea watu wengine. Yehova na Yesu ni wakamilifu, lakini sisi hatukamilike. Wao walikuwa tayari kubadilisha mawazo yao; hauone kwamba sisi pia tunapaswa kufikiria mambo yenye ilifanya wengine watende kwa njia fulani na pengine kubadilisha mawazo yetu?

Inaweza kuwa jambo lenye kufaa kubadilisha mawazo yetu kuhusiana na miradi ya kiroho. Pengine watu fulani wenye tunajifunza nao Biblia na wenye wameanza kuhuzuria mikutano tangu wakati fulani wanaweza kusita kubatizwa. Ao pengine ndugu na dada fulani wanaweza kusita kufanya kazi ya upainia, hata kama wako na uwezo wa kupanua utumishi wao kwa njia hiyo. Pengine tena ndugu fulani hawapendi kujikaza kufikia madaraka katika kutaniko. (1 Tim. 3:1) Wewe pia uko katika hali kama hizo? Yehova anakualika kwa upendo uonje mapendeleo kama hayo. Hauone kwamba unapaswa kubadilisha mawazo yako ili kujionea furaha ya kujitoa kwa Mungu na kutumikia wengine?

Kubadilisha mawazo kunaweza kukuletea baraka

Dada Ella anasema hivi juu ya utumishi wake kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika inchi fulani ya Afrika: “Wakati nilifika kwenye Beteli, sikufikiri kwamba ningebaki huko muda murefu. Nilitamani kumutumikia Yehova kwa nafsi yangu yote, lakini pia nilipenda kuwa karibu na watu wa familia yangu. Mwanzoni, nilikumbuka sana watu wa familia yangu. Lakini, dada mwenye tulikuwa naye katika chumba kimoja alinitia moyo; kwa hiyo, nikaamua kubaki kwenye Beteli. Kisha kufanya miaka kumi kwenye Beteli, ninajisikia kwamba ninapaswa kusaidia ndugu na dada kwa kuendelea kutumikia huko muda murefu zaidi.”

Wakati Unapaswa Kubadilisha Mawazo Yako

Unakumbuka jambo lenye lilimupata Kaini wakati alikuwa na wivu juu ya  ndugu yake na kukasirika sana? Mungu alimuambia mutu huyo mwenye kukasirika sana kwamba angemukubali ikiwa angebadilika na kufanya mambo mazuri. Mungu alimushauri Kaini azuie zambi yenye ‘ilimuvizia katika mwingilio.’ Kaini alipaswa kubadilisha mutazamo wake na mawazo yake, lakini hakufuata shauri la Mungu. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, Kaini alimuua ndugu yake na kwa hiyo akakuwa mutu wa kwanza kuua mwanadamu mwenzake.—Mwa. 4:2-8.

Kaini alipaswa kubadilisha mawazo yake

Fikiria pia mufano wa Mufalme Uzia. Mwanzoni, alifanya mambo mazuri machoni pa Yehova na aliendelea kumutafuta. Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba Uzia akakuwa mwenye kiburi na kwa hiyo akaharibisha sifa yake. Aliingia katika hekalu ili kutoa uvumba, hata kama hakuwa kuhani. Wakati makuhani walimushauri asifanye jambo hilo lenye kuonyesha kiburi, je, alibadilisha mawazo yake? Hapana. Uzia akakasirika sana na akazarau shauri lao. Ndio sababu, Yehova alimupiga ugonjwa wa ukoma.—2 Nya. 26:3-5, 16-20.

Kwa kweli, kuna wakati tunapaswa kabisa kubadilisha mawazo yetu. Tufikirie mufano mumoja wa wakati wetu. Joachim alibatizwa katika mwaka wa 1955, lakini katika mwaka wa 1978 alitengwa na kutaniko. Kisha miaka zaidi ya 20, alitubu na akarudishwa katika kutaniko. Muzee mumoja alimuuliza sababu gani alikawia kuandikia wazee ili arudishwe katika kutaniko. Joachim alijibu hivi: “Ni kwa sababu nilikuwa na hasira na kiburi. Ninasikitika kwa sababu nilikawia sana. Hata kama nilitengwa, nilijua kwamba Mashahidi wa Yehova wanafundisha kweli.” Alihitaji kubadilisha mawazo yake na kutubu.

Tunaweza pia kujikuta katika hali zenye zinatuomba tubadilishe mawazo na mwenendo wetu. Katika hali kama hizo, sisi wote tuazimie basi kufanya hivyo ili tumupendeze Yehova.—Zab. 34:8.