Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Aliijua Njia’

‘Aliijua Njia’

GUY HOLLIS PIERCE, ndugu wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova alifikia mwisho wa maisha yake hapa duniani Siku ya Pili, tarehe 18 Mwezi wa 3, 2014. Tumaini lake la kufufuliwa kama mumoja wa ndugu za Yesu lilitimia wakati alikufa akiwa na miaka 79.—Ebr. 2:10-12; 1 Pet. 3:18.

Ndugu Guy Pierce alizaliwa tarehe 6 Mwezi wa 11, 1934 katika muji wa Auburn, Californie, États-Unis na akabatizwa katika mwaka wa 1955. Katika mwaka wa 1977, alimuoa dada Penny, mwanamuke mwenye alipenda sana, na wakazaa watoto. Kwa sababu alikuwa na uzoefu wa kutunza familia, Ndugu Guy Pierce aliwatendea watu kama baba yao. Katika mwaka wa 1982 yeye pamoja na dada Penny wakakuwa mapainia wenye bidii, na kuanzia mwaka wa 1986 akakuwa mwangalizi wa muzunguko katika États-Unis; alifanya kazi hiyo kwa muda wa miaka 11.

Katika mwaka wa 1997, Ndugu Guy Pierce pamoja na dada Penny walianza kutumikia kwenye Beteli ya États-Unis. Ndugu Pierce alitumika kwenye Biro ya Utumishi, na katika mwaka wa 1998 aliwekwa kuwa musaidizi kwenye Halmashauri ya Wafanyakazi ya Baraza Linaloongoza. Ndugu Guy Pierce alitangazwa kuwa ndugu wa Baraza Linaloongoza tarehe 2 Mwezi wa 10, 1999 kwenye mukutano wa kila mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Katika miaka ya hivi karibuni alitumika katika Halmashauri ya Wafanyakazi, Halmashauri ya Uandikaji, Halmashauri ya Utangazaji, na katika Halmashauri ya Waratibu.

Watu kutoka mahali mbalimbali na wenye asili na desturi mbalimbali walivutiwa na Ndugu Pierce kwa sababu alikuwa na sura yenye furaha na alipenda kuchekesha watu. Hata hivyo, watu walivutiwa sana naye kwa sababu alikuwa mwenye upendo, munyenyekevu, na aliheshimu sheria na kanuni za Yehova zenye haki, pia alikuwa na imani yenye nguvu katika Yehova. Ndugu Guy Pierce aliamini kabisa kwamba ahadi za Yehova haziwezi kukosa kutimia, na alipenda kujulisha watu wote kweli hiyo.

Ndugu Pierce alikuwa anamutumikia Yehova bila kuchoka; alikuwa anaamuka asubuhi sana na mara nyingi alitumika mupaka usiku sana. Alisafiri katika maeneo mengi duniani ili kutia moyo ndugu na dada zake Wakristo. Alijiwekea wakati wa kuzungumuza na ndugu ao dada mumoja-mumoja kwenye Beteli na pia wengine wenye walipenda kuwa pamoja naye, kumuomba mashauri ao musaada. Hata kisha miaka mingi kupita, Wakristo wenzake wanaendelea kukumbuka namna alikuwa tayari kukaribisha watu, alikuwa rafiki muzuri, na namna alitia wengine moyo kwa kutumia Maandiko.

Ndugu na rafiki yetu huyo mupendwa ameacha bibi na watoto sita. Ameacha pia wajukuu (ao wankana) na watoto wa wajukuu wake. Alikuwa pia na watoto wengi sana wa kiroho. Hotuba ya maziko ya ndugu Pierce ilitolewa Siku ya Posho, tarehe 22 Mwezi wa 3, 2014 kwenye Beteli ya Brooklyn; ilitolewa na ndugu Mark Sanderson ambaye pia ni ndugu wa Baraza Linaloongoza. Kati ya mambo yenye alizungumuzia, alisema kwamba Ndugu Pierce alikuwa na tumaini la kuishi mbinguni. Pia, ndugu Sanderson alisoma maneno haya ya Yesu: ‘Katika nyumba ya Baba yangu muna makao mengi. . . . Nikienda na kuwatayarishia ninyi mahali, nitakuja tena nami nitawapokea ninyi nyumbani kwangu mwenyewe, ili mahali nilipo mimi, ninyi pia muwe hapo. Na mahali ninakoenda ninyi munaijua njia.’—Yoh. 14:2-4.

Kwa kweli, tunamukosa sana Ndugu Pierce. Lakini, tunafurahi kwa sababu ‘aliijua njia’ ya kuenda kwenye ‘makao’ yake ya milele.