Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kupambana na Mwisho wa Ulimwengu huu kwa Umoja

Namna ya Kupambana na Mwisho wa Ulimwengu huu kwa Umoja

‘Sisi ni viungo vya mutu na mwenzake.’ EFE. 4:25.

1, 2. Mungu anapenda waabudu wake wote wafanye nini?

JE, WEWE ni kijana? Ikiwa jibu ni ndiyo, ukuwe hakika kwamba, wewe ni mutu wa lazima katika kutaniko la Yehova la duniani pote. Katika inchi nyingi, vijana ndio wengi zaidi kati ya wale wenye wanabatizwa. Inatia moyo sana kuona vijana wengi sana wanajiunga na wale wenye wameamua kumutumikia Yehova.

2 Kwa kuwa wewe ni kijana, je, unafurahia kuwa pamoja na vijana wengine? Bila shaka jibu ni ndiyo. Kwa kawaida, tunapata furaha kwa kupitisha wakati pamoja na watu wa miaka yetu. Hata hivyo, iwe sisi ni vijana ao hapana, ao iwe tumetoka wapi, Mungu anapenda tumuabudu kwa umoja. Mutume Paulo aliandika kwamba Mungu anataka “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:3, 4) Andiko la Ufunuo 7:9 linasema kwamba waabudu wa Mungu wanatoka katika ‘mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.’

3, 4. (a) Ni roho gani imeenea sana kati ya vijana wengi leo? (b) Namna gani tunaweza kutenda kulingana na andiko la Waefeso 4:25?

3 Vijana wenye wanamutumikia Yehova wako tofauti sana na  vijana wa ulimwengu huu. Vijana wengi wenye hawamutumikie Yehova wanaishi maisha ya kujipenda wenyewe, ni kusema, wanafanya tu mambo yenye wanapenda. Wachunguzi fulani wamesema kwamba leo, kuliko wakati mwingine wowote, vijana wanaishi maisha ya kujipenda wenyewe. Kupitia maneno yao na namna yao ya kuvaa, vijana wanaonyesha kwamba wanazarau watu wakubwa, na wanawaona kuwa hawajipatanishe na wakati wa leo.

4 Tunajionea mambo hayo. Kwa hiyo, vijana wenye wanamutumikia Yehova wanatambua kwamba inaomba kujikaza sana ili kuepuka tabia hizo na kufanya mambo yenye Mungu anatuomba. Hata wakati wa mitume, Paulo alitambua kwamba ilikuwa lazima kushauri waamini wenzake waepuke ‘roho ambayo sasa inatenda katika wana wa kutotii’ na ambayo ‘wakati fulani walitembea ndani yake.’ (Soma Waefeso 2:1-3.) Vijana wenye wanatambua kwamba ni lazima waepuke roho hiyo na wamutumikie Yehova kwa umoja pamoja na ndugu na dada zao wanastahili kupongezwa. Kwa kufanya hivyo, wanatenda kulingana na maneno ya mutume Paulo yenye inaonyesha kwamba tuko “viungo vya mutu na mwenzake.” (Efe. 4:25) Kadiri tunakaribia mwisho wa ulimwengu huu, ni lazima sana tutumike kwa umoja. Tuchunguze sasa mifano fulani iliyo katika Biblia yenye itatusaidia kutambua kwamba ni lazima tutumike kwa umoja.

WALITENDA KWA UMOJA

5, 6. Habari ya Loti na binti zake inatufundisha nini kuhusu kutenda kwa umoja?

5 Zamani, Yehova alilinda watu wake wakati walitenda kwa umoja ili kusaidiana wakati wa magumu. Leo, watumishi wa Mungu, iwe ni vijana ao hapana, wanaweza kufaidika sana na mifano yenye kupatikana katika Biblia. Tufikirie kwanza mufano wa Loti na familia yake.

6 Maisha ya Loti na familia yake ilikuwa katika hatari kwa sababu muji wa Sodoma, ambamo walikuwa wanaishi, ulikuwa karibu kuharibiwa. Malaika wa Mungu walimuambia Loti akimbilie katika eneo la milima; walisema hivi: “Kimbia kwa ajili ya nafsi yako.” (Mwa. 19:12-22) Loti alitii, na binti zake wawili walijiunga naye kwa kuondoka katika muji. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu wengine wa familia ya Loti walikataa kujiunga nao. Vijana wanaume wenye walipaswa kuoa binti za Loti walimuona ‘kama mutu aliyekuwa anafanya muzaha.’ Kwa hiyo walipoteza uzima wao. (Mwa. 19:14) Ni Loti tu pamoja na binti zake, wenye walijiunga naye, ndio walipona.

7. Wakati Waisraeli waliondoka katika inchi ya Misri, namna gani Yehova alisaidia wale wenye walitenda kwa umoja?

7 Tufikirie mufano mwengine. Wakati Waisraeli waliondoka katika inchi ya Misri, hawakujigawanya katika vikundi tofauti-tofauti, na kila kikundi kujichagulia njia. Na wakati Yehova aliachanisha maji ya Bahari Nyekundu kisha Musa ‘kunyoosha mukono wake juu ya bahari,’ Musa hakuingia peke yake katikati ya maji hayo wala hakuenda tu na Waisraeli fulani. Lakini, kwa sababu Yehova aliwalinda, Waisraeli walivuka pamoja Bahari Nyekundu. (Kut. 14:21, 22, 29, 30) Walitenda kwa umoja, na “jamii kubwa iliyochangamana” ya watu wasio Waisraeli ilijiunga na kuvuka pamoja nao. (Kut. 12:38) Ingekuwa vibaya sana ikiwa watu fulani, pengine kikundi fulani cha vijana, wangejitenga na wengine, na kuchagua njia yao wenyewe. Hauone kwamba kufanya hivyo ingekuwa kukosa akili, na kungewafanya wakose ulinzi wa Yehova?—1 Kor. 10:1.

8. Katika siku za Yehoshafati, namna gani watu wa Mungu walitenda kwa umoja?

8 Katika siku za Mufalme Yehoshafati, watu wa Mungu walipambana na ‘umati mukubwa’ wa maadui wenye kuogopesha kutoka katika maeneo yenye ilikuwa inawazunguka. (2 Nya. 20:1, 2) Jambo la kufurahisha ni kwamba, watu wa Mungu hawakujaribu kupiganisha maadui wao kwa nguvu zao wenyewe. Lakini, walimutegemea Yehova. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 20:3, 4.) Na Waisraeli  hawakufanya hivyo wakiwa mumoja-mumoja, lakini walitenda kwa umoja. Biblia inasema kwamba “watu wote wa Yuda walikuwa wamesimama mbele za Yehova, hata watoto wao, wake zao na wana wao.” (2 Nya. 20:13) Wote pamoja, iwe ni vijana ao hapana, walijikaza kufuata muongozo wa Yehova, na Yehova aliwalinda. (2 Nya. 20:20-27) Mufano huo muzuri unaonyesha namna watu wa Mungu wanapaswa kupambana na magumu kwa umoja.

9. Wakristo wa kwanza-kwanza walitenda kwa umoja. Mufano wao unaweza kutufundisha nini?

9 Wakristo wa kwanza-kwanza walitenda pia kwa umoja. Kwa mufano, wakati Wayahudi na watu wasio Wayahudi walikuwa Wakristo, walijitoa wenyewe “kwa fundisho la mitume na kushirikiana, katika kula milo na katika sala.” (Mdo. 2:42) Umoja huo ulionekana zaidi sana wakati wa mateso; wakati huo walihitaji sana kusaidiana. (Mdo. 4:23, 24) Hauone kwamba ni lazima sana kutenda kwa umoja wakati wa magumu?

TUTENDE KWA UMOJA KADIRI SIKU YA YEHOVA INAKARIBIA

10. Ni wakati gani watu wa Mungu watahitaji zaidi kutenda kwa umoja?

10 Tunakaribia kipindi kigumu sana katika historia. Nabii Yoeli anaita kipindi hicho “siku yenye giza na weusi.” (Yoe. 2:1, 2; Sef. 1:14) Wakati huo, watu wa Mungu watahitaji zaidi kutenda kwa umoja. Kumbuka maneno haya ya Yesu: “Kila ufalme uliogawanyika na kupingana wenyewe unaangamia.”—Mt. 12:25.

11. Andiko la Zaburi 122:3, 4 linaweza kufundisha nini watu wa Mungu leo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

11 Wakati wa kipindi kigumu chenye kitapata ulimwengu huu, tutahitaji kabisa kutenda kwa umoja. Tunaweza kulinganisha umoja huo wa kiroho na namna nyumba zilikaribiana katika muji wa zamani wa Yerusalemu. Nyumba hizo zilijengwa karibu-karibu sana; ndio maana mutunga-zaburi aliita Yerusalemu kuwa ‘muji ambao umeunganishwa pamoja kwa umoja.’ Hilo liliwawezesha wakaaji wasaidiane na kutoleana ulinzi. Tena, jambo hilo lilifananisha umoja wa kiroho wa taifa nzima wakati “makabila [yote] ya Yah” ilikusanyika kwa ajili ya ibada. (Soma Zaburi 122:3, 4.) Leo, sisi pia tunahitaji kuendelea ‘kuunganishwa pamoja kwa umoja.’ Itakuwa hivyo pia wakati wa kipindi kigumu ambacho kinakuja.

12. Ni nini itatusaidia kuokoka wakati watu wa Mungu watashambuliwa?

12 Sababu gani wakati huo itakuwa jambo la lazima sana ‘tuunganishwe pamoja kwa umoja’? Unabii wenye kupatikana katika Ezekieli sura ya 38 unasema kwamba ‘Gogu wa inchi ya Magogu’ atashambulia watu wa Mungu. Wakati huo hatutaruhusu jambo lolote litutenganishe. Hatutajaribu kutegemea ulimwengu ili kupata musaada. Lakini, itakuwa lazima tukuwe karibu sana na ndugu na dada zetu. Hilo halimaanishe kwamba tutaokolewa kwa sababu tu tuko pamoja na wengine. Katika kipindi hicho kigumu, Yehova na Mwana wake watawaokoa tu wale wanaoliitia jina la Yehova. (Yoe. 2:32; Mt. 28:20) Unafikiri kwamba Yehova ataokoa wale wenye wanajitenga na kundi lake?—Mika 2:12.

13. Mambo yenye tumejifunza katika habari hii inaweza kufundisha nini vijana wenye kumuogopa Mungu?

13 Sasa tumeelewa vizuri zaidi kwamba si jambo la hekima kuiga vijana wenye wanajitenga na Wakristo wenzao. Tunakaribia wakati wenye tutahitaji sana musaada wa Wakristo wenzetu. Jambo hilo linahusu Wakristo wote, iwe vijana ao hapana! Kwa kweli, sasa ndio wakati wa kujifunza kutenda kwa umoja, kwa sababu umoja huo utatusaidia sana katika siku zenye zinakuja.

 ‘VIUNGO VYA MUTU NA MWENZAKE’

14, 15. (a) Sababu gani Yehova anatufundisha kuishi kwa umoja? (b) Yehova anatutolea mashauri gani ili tuendelee kuwa na umoja?

14 Yehova anatusaidia tumutumikie “bega kwa bega.” (Sef. 3:8, 9) Anatutayarisha kwa ajili ya wakati unaokuja wa milele. Anafanya hivyo namna gani? Yehova ana kusudi la ‘kukusanya pamoja vitu vyote katika Kristo.’ (Soma Waefeso 1:9, 10.) Anapenda kuunganisha viumbe wote wenye kuwa mbinguni na duniani ambao wanapenda, na bila shaka atatimiza jambo hilo. Kwa kuwa wewe ni kijana, hauone kama ni jambo la lazima kabisa kutumika kwa umoja pamoja na tengenezo la Yehova?

15 Leo, Yehova anatufundisha kuishi kwa umoja, kwa sababu anapenda tuweze pia kuishi kwa umoja katika Ulimwengu mupya. Mara kwa mara, Maandiko yanakazia kwamba tunapaswa ‘kutunzana,’ ‘kuwa na upendo mwororo kwa mutu na mwenzake,’ ‘kuendelea kufarijiana,’ na “kujengana.” (1 Kor. 12:25; Rom. 12:10; 1 Tes. 4:18; 5:11) Yehova anajua kwamba Wakristo hawakamilike, na hilo linafanya ikuwe vigumu sana kutenda kwa umoja. Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza sana ili tuweze ‘kusameheana kwa hiari.’—Efe. 4:32.

16, 17. (a) Taja kusudi moja la mikutano yetu. (b) Mufano wa Yesu wakati alikuwa kijana unaweza kufundisha nini vijana leo?

16 Pia, Yehova anatufundisha namna tunaweza kuishi kwa umoja kupitia mikutano ya Kikristo. Mara nyingi andiko la Waebrania 10:24, 25 linatutia moyo kukusanyika. Kusudi moja la mikutano yetu ni kutusaidia ‘tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.’ Ni jambo la maana kujua kwamba mikutano yetu imetayarishwa ili itupatie nafasi ya ‘kutiana moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri tunavyoona siku ile kuwa inakaribia.’

17 Yesu ni mufano muzuri kwetu kwa sababu, wakati alikuwa kijana, aliona mikutano kuwa ya lazima sana. Wakati alikuwa na miaka 12, alienda pamoja na wazazi wake kwenye mukusanyiko mukubwa ili kumuabudu Yehova. Wakati fulani, wazazi wake walimukosa; haikuwa kwa sababu alienda kutembea-tembea na vijana wengine. Lakini, wakati Yosefu na Maria walimupata kwenye hekalu, alikuwa anazungumuza pamoja na walimu kuhusu Maandiko.—Lu. 2:45-47.

18. Namna gani sala zetu zinaweza kutusaidia kuwa katika umoja?

18 Tunapaswa kuonyesha wengine upendo na kutumia mikutano yetu ya Kikristo  ili kufanya umoja wetu ukuwe wenye nguvu. Lakini, tunapaswa pia kusali kwa ajili ya wengine. Tunaonyesha kwamba tunahangaikia wengine, wakati tunawataja katika sala zetu. Wakristo wote wanapaswa kufanya mambo hayo, iwe ni vijana ao hapana. Ikiwa wewe ni kijana, unatumia nafasi hizo ili kuwa karibu sana na familia yako ya kiroho? Kufanya hivyo kunaweza kukusaidia uhakikishe kwamba umejitenga na ulimwengu huu ambao unakaribia kuharibiwa.

Kila mumoja wetu anaweza kusali kwa ajili ya ndugu na dada zetu(Ona fungu la 18)

TUONYESHE KWAMBA TUKO ‘VIUNGO VYA MUTU NA MWENZAKE’

19-21. (a) Ni katika njia gani kubwa tunaonyesha kwamba ‘sisi ni viungo vya mutu na mwenzake’? Toa mifano. (b) Namna ndugu na dada fulani walitenda wakati wa misiba inaweza kutufundisha nini?

19 Leo, watu wa Yehova wanaishi kulingana na kanuni iliyo katika andiko la Waroma 12:5 lenye kusema hivi: ‘Sisi ni viungo ambavyo kila kimoja ni cha kile kingine.’ Tunajionea jambo hilo wakati misiba inatokea. Katika Mwezi wa 12, 2011, upepo mukali ulileta mafuriko makubwa katika kisiwa cha Mindanao katika inchi ya Ufilipino. Katika usiku moja, nyumba zaidi ya 40000 ziliingiliwa na maji, kutia pia nyumba nyingi za ndugu na dada zetu. Lakini, biro ya tawi ya inchi hiyo ilitoa ripoti kwamba “mbele hata halmashauri za kutoa misaada zianze kufanya kazi, ndugu na dada zetu wa inchi zingine walikuwa wanatuma misaada.”

20 Tena, wakati tetemeko kubwa la dunia lilitokeza mafuriko makubwa (ao tsunami) mashariki mwa Japani, ndugu na dada wengi walipoteza vitu vyao. Wamoja kati yao walipoteza karibu vitu vyao vyote. Dada Yoshiko, ambaye alipoteza nyumba yake, alikuwa anaishi kwenye kilometre 40 mbali na Jumba la Ufalme. Anasema hivi: “Siku moja kisha tetemeko la dunia, tulishangaa kuona mwangalizi wa muzunguko pamoja na ndugu mwengine wanakuja kututafuta.” Anaongeza hivi kwa sura yenye furaha: “Tulifurahi kabisa kuona namna kutaniko lilishugulikia kabisa mahitaji yetu ya kiroho. Zaidi ya hilo tulipewa koti, viatu, sakoshi, na manguo ya kulala nayo.” Ndugu mumoja wa halmashauri ya kutoa misaada anasema hivi: “Ndugu na dada wa sehemu zingine za inchi ya Japani walitumika kwa umoja, na walisaidiana. Hata ndugu na dada wa États-Unis walikuja kutusaidia. Wakati ndugu na dada hao waliulizwa sababu gani walisafiri kutoka mbali, walisema hivi: ‘Sisi pamoja na ndugu na dada wa inchi ya Japani ni mutu mumoja, na wanahitaji musaada.’” Hauone kwamba ni pendeleo kubwa sana kuwa katika tengenezo lenye kuhangaikia watu wake? Ukuwe hakika kwamba Yehova anafurahi sana wakati anaona tunatenda kwa umoja.

21 Ikiwa tunaonyesha roho hiyo tangu sasa, hilo litatusaidia kupambana na kipindi kigumu cha wakati unaokuja hata kama hatutakuwa pamoja na ndugu na dada wa sehemu zingine za dunia. Kwa kweli, kutenda kwa umoja kunatutayarisha kwa ajili ya nyakati ngumu zenye zitatokea kadiri ulimwengu huu unakaribia mwisho wake. Dada Fumiko, ni mumoja kati ya watu wenye waliteseka kwa sababu ya upepo mukali sana (ao typhon) wenye ulipiga inchi ya Japani. Anasema hivi: “Mwisho unakaribia sana. Kwa hiyo, tunahitaji kuendelea kusaidia waamini wenzetu kadiri tunangojea wakati ambapo hakutakuwa tena misiba.”

22. Umoja wa Kikristo unaweza kutuletea baraka gani za milele?

22 Wakristo wote, iwe vijana ao hapana, wanajikaza kuishi katika umoja tangu sasa. Kwa kufanya hivyo, wanajitayarisha ili kuokoka mwisho wa ulimwengu huu muovu ambao hauna umoja. Mungu wetu atatuokoa kama vile aliokoa watu wake zamani. (Isa. 52:9, 10) Kumbuka kwamba, ikiwa unaendelea kujiunga na watu wa Mungu, unaweza kuwa kati ya watu wenye wataokolewa. Jambo lingine lenye litatusaidia ni kuona uriti wetu wa kiroho kuwa wa lazima sana. Tutazungumuzia jambo hilo katika habari yenye kufuata.