Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea

Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea

MUUMBAJI wetu amewapa wanadamu zawadi ya lazima sana, ni kusema, uhuru wa kuchagua. Tena, anabariki sana wale wenye wanatumia uhuru wao wa kuchagua ili kutegemeza ibada ya kweli na ambao wanatimiza sehemu yao katika kutakasa jina lake na kuunga mukono kusudi lake kubwa. Yehova hapendi tumutii kwa sababu tu tunaona kwamba tunapaswa kufanya hivyo ili tusipatwe na jambo fulani mbaya. Lakini, anafurahi sana kuona watu wanajitoa kwake kwa sababu wanamupenda kwa moyo wote na wanataka kumuonyesha shukrani.

Kwa mufano, wakati Waisraeli walikuwa katika jangwa la Sinai, Yehova aliwaambia wajenge mahali pa ibada. Alisema hivi: ‘Kutoka katikati yenu mutoe muchango kwa ajili ya Yehova. Kila mutu mwenye moyo wenye nia na aulete ukiwa muchango wa Yehova.’ (Kut. 35:5) Kila Muisraeli alipaswa kuleta kile angeweza kutoa. Kila muchango wa kujipendea, iwe ni muchango gani, iwe ni mukubwa ao mudogo, ungeweza kutumiwa kwa njia yenye kufaa ili kutimiza kusudi la Mungu. Waisraeli walitenda namna gani?

‘Kila mutu ambaye moyo wake ulimusukuma’ na ‘kila mutu ambaye roho yake ilimuchochea’ alitoa zawadi ya kujipendea, ‘kila mutu mwenye moyo wenye nia.’ Wanaume na wanawake walitoa kwa kujipendea vitu mbalimbali kwa ajili ya kazi ya Yehova. Walitoa vipini, pete za masikio, pete, zahabu, feza, shaba, uzi ya rangi ya bluu (bleu), manyoya ya wanyama yenye rangi ya zambarau, kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kitani bora, manyoya ya mbuzi, ngozi za kondoo-dume zenye zilitiwa rangi nyekundu, ngozi ya sili, mbao za mushita (ao acacia), majiwe yenye bei kubwa, zeri, na mafuta. Mwishowe, ‘vitu hivyo vikakuwa vya kutosha kwa ajili ya kazi yote iliyopaswa kufanywa, na kuzidi.’—Kut. 35:21-24, 27-29; 36:7.

Jambo lenye Yehova alifurahia sana, haikuwa tu vitu vyenye watu walitoa, lakini roho ya kujitolea ya wale wenye walitegemeza ibada safi. Walikuwa pia tayari kutoa wakati wao na nguvu yao. Biblia inasema kwamba ‘wanawake wote waliokuwa wenye hekima ya moyo walisokota (ao walisuka) kwa mikono yao.’ Kwa kweli, ‘wanawake wote ambao mioyo yao iliwasukuma kwa hekima walisokota manyoya ya mbuzi.’ Zaidi ya hilo, Yehova alimupatia Bezaleli “hekima katika uelewaji na katika ujuzi na katika kila aina ya ufundi.” Mungu aliwapatia Bezaleli na Oholiabu uwezo wenye walihitaji ili kufanya kazi yote yenye aliwaomba.—Kut. 35:25, 26, 30-35.

Wakati Yehova aliwaomba Waisraeli watoe michango, alijua kabisa kwamba ‘kila mutu mwenye moyo wenye nia’ atategemeza ibada ya kweli. Kisha, Yehova alibariki sana wale wenye walikuwa tayari kutoa; aliwatolea muongozo na aliwasaidia kupata furaha kubwa sana. Kwa njia hiyo, Yehova alionyesha kwamba wakati anabariki watumishi wake wenye kuonyesha roho ya kujitolea, anaweza kuhakikisha kwamba hakuna kitu kinakosa ili kutimiza mapenzi yake. (Zab. 34:9) Yehova hatakosa kubariki roho yako ya kujitolea ambayo unaonyesha kwa kumutumikia kwa moyo wote.